Macho yangu yananidanganya?

Macho yangu yananidanganya?

Misimamo yake ya kulipenda taifa na kusema ukweli. I don't believe kama hii is his natural death, rogue elements within and abroad might be behind this dire circumstance, completely a big blow kwa taifa

Are you saying he should have died when he wanted. This is a load of serious twaddle!!

Unless you have proof of your assertion, this remains death - a natural one!!

Like any human being, he did both good and bad. Dont try to make him a perfect human being!!
 
hata misiba ya wezi inakuwaga na watu mkuu tena wengi tu, ni kweli wapo wengi waliompenda na wewe ukiwepo lakini pia wapo wengi tu waliomchukia na katika marais wote waliotawala Tanzania marehemu aliongoza kwa kuchukiwa. Kafa Nyerere, Mkapa je uliona watu wakinywa bia kufurahia vifo vyao? uliona watu wakikamatwa kwa kosa la kufurahia vifo vyao?
Ww dish lako limeyumba sana I see!
Hajawahi tokea rais aliyependwa kama Magu Tz isipokuwa JK Nyerere!
Yup! Mi mwenyewe nimeganda kwenye runinga siku nzima.

View attachment 1730948
 

Attachments

  • 16163349558931602167281051591942.jpg
    16163349558931602167281051591942.jpg
    83.5 KB · Views: 1
Ww dish lako limeyumba sana I see!
Hajawahi tokea rais aliyependwa kama Magu Tz isipokuwa JK Nyerere!
na wengine tumekuwa wavivu kukaa nyumbani,tuone kupitia tv.hali ingekuwa mbaya zaidi kila mtu angeenda huko.
 
Watanzania chochote utakachowahamasish,hasa kisichotumia mtaji,wanahamasika. Hata aje Id Amini dada leo au Hitler na itangazwe na ihamasishwe kama hivyo,watajitokeza zaidi ya hapo.
Pumbavu! Mandamano ya mbeligiji je? Walihamasishwa hawakuhamasishwa?!

Walitokea hawakutoka
 
Magufuli akumbukwe kwa mazuri yake na siyo kwa mapungufu yake.

Sijawahi kuwa shabiki wa Magufuli lakini kuna mambo mengi aliyoyafanya yalikuwa sahihi. Na hayo mazuri aliyoyafanya, wengi wetu hatujawahi kuyafanya na hatutayafanya.

Mimi binafsi, lililokuwa baya kabisa wakati wa utawala wake, ambalo kwa kweli lilikuwa ni doa kubwa ni matendo ya watu wasiojulikana ya kuua, kuteka na kupoteza watu.

Sina shaka hata kidogo juu ya marehemu kutamani sana nchi iwe na maendeleo japo kuna wakati zile mbinu za kufikia dhamira zake, zilikuwa na walakini. Kasoro nyingine kwenye utawla wake ni kukosekana demokrasia, kukosekana uhuru wa vyama vya siasa, kukosekana uhuru wa maoni, kukosekana uhuru wa vyombo vya habari, kukosekana kwa utawala wa kisheria, mbinu mbaya za ukusanyaji mapato ya serikali, kuua uwekezaji kutokana na harassment kwa wawekezaji bila ya sababu za msingi, n.k.

Nani atasema miundombinu siyo muhimu? Nani atasema ukarabati na ujenzi wa hospitali na zahati siyo muhimu? Nani atasema ukarabati wa viwanja vya ndege, haukuwa muhimu? Nani atasema udhibiti wa matumizi ya Serikali siyo jambo jema?

Samia aangalie mazuri ya marehemu, ayalinde na kuyaendeleza. Mapungufu ya marehemu yaachwe.
 
Walio wengi hawajaamini kuwa Fascist kuwa kafa,wanaenda kuhakikisha hivi ni kweli maana wengi kwa yale majivuno yake ya kutesa watu na kuua watu hawakudhani kama angekufa tena mapema kiasi hiki.

naona jinsi LGBT PEOPLE MNAVYOMUANDAMA MWENDAZAKE.
 
Japo alikuwa na mapungufu ya hapa na pale, lakini alikuwa nia ya kutupa hatua moja zaidi katika maendeleo,
Sidhani kama kuna mtu kama yeye ndani ya ccm.
katika hayo mapungufu ya hapa na pale kuna watu wameuliwa kashindwa kuwapa hiyo nafasi ya kupiga hatua moja zaidi

Hata kama hakuna mtu kama yeye pale ccm ila kila mmoja atasemwa kwa nafasi yake kulingana na matendo yake
 
Baada ya uchaguzi CDM walivyoitisha maandamano, rafiki yangu aliniambia hawa wanawajua waTz vizuri hawa? kama wanataka watu waandamane basi machinga wazuiwe au waondolewe kwenye maeneo wanakofanyia biashara hapo ndipo watu wataandamana, hivi hivi waTz wanatafuta mlo tu mambo yaliyo mengi hawaelewi yanawasaidiaje wao, hapo ndio wanasiasa wa chama dola wanapojizolea mashabiki zao.

Anyways to me, magufuli alikuwa na nia nzuri sana na nchi, his approach kuyafikia hayo mazuri ndio ilikuwa changamoto, plus ana issues in person ndio ikafanya things kuwa worse. hata hivyo amefanya pakubwa, apumzike kwa amani.
 
acha ujinga bana id amini aliliwa na nani???
Alililiwa na watu ambao walikuwa wanahesabu mazuri yake. Kwani unafikiri iddi amin alikuwa katiri kwa kila mtu?

Wapo wanaomuona shujaa kama ambavyo osama anavyoonekana shujaa kwa watu wengine
 
Back
Top Bottom