Macho yangu yananidanganya?

Macho yangu yananidanganya?

Kifo cha Magufuli kilikuwa habari ya dunia.

Kwa mtu aliyekuwa hasafiri sana nje ya nchi, sikujua kama watu wa mataifa mengine walikuwa wanamfuatilia kiasi hicho.

Kifo chake kilikuwa headline news kwenye vyombo vikubwa vya habari vya kimataifa!
Kwamba hakusafiri sana nje ya nchi haina maana kwamba hakuwa na impact kubwa katika jumuiya ya kimataifa. Siasa zake za pekee mara moja zilimtangaza. Misimamo yake ya pekee kuhusu covid pia ilimtangaza sana.

Kwamba msomi wa kiwango cha PhD, tena ya Chemistry, anadiriki kudisprove kipimo cha covid, kwa kutumia sample za mapapai na oil?

Kwamba anakejeli chanjo ambazo nchi za ulaya wametengeneza hasa kwa ajili ya raia zao, kwamba hazina utafiti wa kutosha, ambapo si kweli, halafu hapohapo anahimiza matumizi ya nyungu na madawa 'mbadala' ambayo hayajafanyiwa utafiti wa aina yoyote?

Rais ambaye anatangaza kuishinda covid, simply kwa kupiga marufuku utoaji takwimu za covid. Methali ya wazanaki ndio imemuumbua. Mfichaficha maradhi....

Kwa misimamo yake, analinganishwa na rais Trump wa USA na yule wa Brazil

Bila shaka Rais wa aina hiyo atakuwa maarufu saaana.

Bila shaka, atatangazwa sana ili kuonyesha kwa wengine wanaofikiria kufuata nyayo zake, mwisho wa kudharau na kuipuuza sayansi
 
UFIPA,mmebaki na aibu na sononi.

mtaambia nini watu[emoji23][emoji23][emoji23]
sisi wafuasi wake tumekubali mzee apumzike,halafu hali imekuwa mbaya zaidi kwenu.
Sidhani kama mama Samia ataendesha ule wizi wa kura wa 2019 na 2020, kuhonga wapinzani, na kuminya wapinzani ili ccm ishinde. Kwa maana hiyo nafurahia kutokuwepo kwa Magufuli uchaguzi wa 2025
 
Hiyo ya Fatma hata mimi nimeona!

Desperate menopausal little bitch.
Hizo chuki! Tatizo la matusi ya jumla kama hili kwa wanawake, ni kwamba wote tumezaliwa na wanawake. Mama zetu, dada zetu, shangazi, nk. Wote watapita hapo kwenye menopause, kama Mungu atawapa umri.
 
Nikuulize swali.....

Hivi Tundu alipoita maandamano baada ya uchaguzi mkuu mwaka jana hapakua na mitandao?? Au chadema hawakua na kamati kuu na wakazuiwa kufanya press?????

Kilichotokea leo ndio kilichofanyika kwenye kura za october 2020

Tujifunze:
Wanasiasa mmekumbushwa kwamba Kwenye ya nguvu ya umma.... hakuna anayenunuliwa viroba wala bangi. Ni mapenzi kwa mtu wao

Vyombo vya ulinzi na usalama tukio la leo pale taifa na airport limethibitisha nguvu ya wananchi
bila kushurtishwa haizuiliki na yoyote

Mungu ibariki Tanzania Mungu mbariki rais wetu Samia Suluhu Hassan[emoji1241]
Hayati John Pombe Joseph Magufuli apumzike kwa amani Amina [emoji120]
 
Binadamu tuko na udhaifu mwingi sana, hasa suala la kifo huwa tunarudi nyuma na kuzipuuza chuki zetu.
Sio kila aliyeandamana barabarani alikuwa anampenda kabla ya kifo chake.

 
Kukimbia na masanduku ya kura ndio demokrasia..?

Twaweza: ccm inapendwa na wajinga.
Simlijifanya mnalinda kura sasa na makamanda wenu sasa mnalalamika nini?

Nyinyi mnachotafuta ni domokras,inamaana kila eneo walikimbia na masanduku ya kura simliweka wawakilishi wenu

Njaa inawasumbua na kutaka kushiba pasipokufanya kazi mle kupitia majukwaa tu
 
Ulitaka kuwe na vurugu ili iweje?
Huwezi kupendwa ukiwa maiti.Wingi wa watu kwenye msiba,tena mjini kulikojaa majobless ni kitu cha kawaida sana.
Kumbuka kuwa gari la matangazo lilipita kila eneo kuhamasisha watu wajitokeze kwa wingi kwenye uwanjani na barabarani.
Msiba ukipigiwa debe ni dalili mbaya.
 
Nasoma huu uzi wako hata sielewi lengo lako, kwani watu kujaa huko uwanjani kunuaga Magufuli kuna shida gani?
Watu wanakwenda kwa sababu nyingi, kuaga, kushangaa ni kweli .....
 
Umesahau kwa miezi mitatu IGP Sirro alikuwa anatishia kuuwa watu watakaoandamana?
 
Mkuu kukaa kimya Ni hekima. Sasa kama watu wanapokea maagizo kirahisi Hivi Ni jambo Jema. La msingi usije pinga tena kuhusu kura za ndio. Mana nayo Ni maagizo Tena ya mtu aliye hai.

Upande wa pili wa Shilling, JPM alipendwa na wengi sana kuliko wewe na Wenzako wa mtandaoni. Na ninyi nanyi huwa mnaagizwa. Akkianza mmoja, utaona wengine wanakujaaaaa. Lakini bado hamtoshi.

Baba JPM rest in the Peace of God.
 
Back
Top Bottom