MADA: Fahamu zaidi kuhusu mbinu za kilimo cha tikitimaji, faida na changamoto zake

MADA: Fahamu zaidi kuhusu mbinu za kilimo cha tikitimaji, faida na changamoto zake

pilato93, Anaweka pesa huko tu ili asije tumia.. au akiweza afungua account bank iwe fixed kisha baada ya muda akachukue akaanze mishe huko.

Afu inaelekea hujui faida inakokotolewa vipi katika makampuni. Anza kuuliza uelekezwe sio usingizi umekata nawe unaanza kuandika mashudu hapa..
 
Anaweka pesa huko tu ili asije tumia.. au akiweza afungua account bank iwe fixed kisha baada ya muda akachukue akaanze mishe huko..
Afu inaelekea hujui faida inakokotolewa vipi katika makampuni..
Anza kuuliza uelekezwe sio usingizi umekata nawe unaanza kuandika mashudu hapa..
Bora hiyo fixed lakini hayo ya DSE ni majanga hizo faida za kampuni kugawa gawio jua wewe tu
 
Habari yenu,
Nadhani hapa kuna wataalamu wa kilimo, nimepata sehem nataka nilime matikiti maji kwa kuangalia nimeona ndo biashara inayolipa haraka haraka,

Mtaji nilionao wa kuanzia ni 20,000,000 naomba ushauri wenu juu ya hatua za kufuata,
Nunua trekta ukapige vibarua, na utalima upendavyo wewe,
 
K
Hizi ndizo hesabu zinazowaliza wengi 9milioni upate 30 million ndani ya miezi minne tu faida 21miliion yaani emu niache kidogo
Kama hutaki acha. Hiyo ni hessbu ya kawaida isipokuwa inatakuwa ajipange. Sikazi rahisi kuipata kama unavyodhani
 
Nooooooop
Kaa chini tafuta wazo jipya
sikushauri investment katika kilimo
share na watu upate ideas hope unaweza fanya jambo kubwa zaidi
 
Habari wana JF, hodi humu, mgeni mie, naomba msaada wake msanifu wa kilimo cha kivurini "greenhouse cultivation" tuwasliane kwa text plz 0755958401
 
Tatzo letu kubwa sana watu wa mjini tunafanya vitu kwa mkumbo. Mara vitunguu, mara product (sabuni) mara tikiti, mara matango, nyanyachungu etc.

Wapo watu maisha yao wanayaendesha kwa tikiti na huwez kuwaambia kitu.
Yapo mambo mengi ikiwemo uzoefu ktk kilimo cha japo zao moja.

Sasa wengi wetu hatufanyi utafit tunaingia kichwa kichwa.

Lakn pia baada ya kilimo kuna kuuza bidhaa.
Lazma ulimie majira fulani ili uvune kipindi ambacho hakuna matunda mengi sokoni.

MFANO.
Nov na Dec ni miez mbayo inamatund mengi sana kma Nanasi, Machungw, Embe etc, ukipelek tikit sokoni haliwez kuuza vzuri man nanasi, embe, chungwa, bei yke ni chini mno kuliko tikiti, so si rahis kumshawishi eidha mfanya biashara au mlaji kununua tikiti, na nji pekee ya kumshawishi ni kushusha bei n si vinginevyo.

Pia unapoanguka ni vyem ukajua umeangukia wapi. Wengi wetu humu wanasema wlianguka lakn hawasemi nini kiliwaangusha, hii inaleta maana halisi kwmb hawajui wapi alikijikwa kufikia kuanguka.

Kilimo si secta rahisi km secta nyingne tu. Inahitaji kila kinachohitajik kufanikish mlengo.

Tusikate tamaa, tujifunz mara kadhaa kabla ya kukata tamaa.
 
Nililima eka moja yalianza vizuuri yakazaa Matunda vizuuri watu wakaanza kunisifia wengine kukadiria, mwingine utapata million 4, mwingin 6 mwingine 3, yalipofikisha siku 60 yalianza kuoza, kutobolewa na wadudu, mashina kukauka hovyo, na mengine kupasuka. Yaan niliishia kupokea pole kama mtu aliyefiwa. Kweli nilikuwa nayahudumia madawa mbolea na maji kwa kufuata utaalam, sasa nimejuta, nilitumia laki8 nikaambulia laki3.5 so usikurupuke changamoto ni nyingi sana
[emoji19] [emoji19] [emoji19] [emoji19]
 
Kilimo ubaya wake ni kuwa hakitabiriki na pia unaweza lima ukakutana na matikiti mengine sokoni
yes hii ndio hatari zaidi..........

kilimo hasa cha tikiti inatakiwa uvune may/june au uvune oktoba/novemba

hapo katikati matikiti yanakua mengi mno sokoni
 
Chukua wastani wa walioajiriwa na wakulima ni wapi wenye nafuu kimaisha? Ukipata jibu rudi hapa utoe mrejesho.
wakulima hasa kama una mtaji aisee akipiga anapiga kweli.......
 
Manasse,
mkuu wengi wa wapiga kelele humu wanalima kwa smartfone.


mimi mwaka huu nililima kitunguu, kila mwezi nilikua najitahidi nifike shamba angalau mara moja.

nilianza na ekari 2, nilitumia roughly 5m.... nilipovuna aisee yalikua majanga, nikavuna 3m kasoro hivi. that means nilikula hasara ya 2M.

nilichojifunza ni kwamba nilimwamini mno msimamzi, pili sikua na vitendea kazi vyote!

hivyo, sisi walikulima wa mitandaoni mara nyingi tunataka mafanikio bila kusota vya kutosha!

ukiingia site mwenyewe, siku ya kupiga dawa uwepo, kumwagilia uwepo, kuweka mbolea uwepo, kupanda uwepo, kuandaa mbegu uwepo aisee hasara huwezi pata UNLESS iwe ni hasara kwa watu wote (kwamba bei zimekua mbaya) napo mtaji huwezi kupoteza HATA IWEJE!!!!
 
Back
Top Bottom