Mada ya wanyama

Mada ya wanyama

FB_IMG_1636613784103.jpg
 
KUNA DHANA MIONGONI MWA WATU WANASEMA KUA :Nyoka hana uadui na mwanadamu,ila mwanadamu ndiye mwenye uadui na nyoka,kama hujamuona nyoka anaweza kuja hadi kwenye miguu yako ila ukimuona tu hata kama hutakimbia yeye lazima akimbia au atakugonga,kwamba ukimuona mwili wako unatoa kiashiria kwa nyoka kua wewe ni adui..


Hii imekaaje
Ni kweli, nyoka tunapishana nao tu mara nyingi bila kujua na wala hawatufanyi kitu kwa kuwa tunapopishana nao bila kujua wao wanapata taarifa kwamba hatujamuona ila ukijua tu wanapata taarifa kwamba umeshajua au ukimkanyaga wanapata taarifa kwamba umemuona hivyo huchukua tahadhari kwa kukung'ata.
 
tulikuwa tunaamini zamai kwamba mbuni akifkuzwa na mnyama ili awe kitoweo basi huzamisha kichwa chake ardhini akijua amejifiiichaaa...
ila ukweli ni huwa anaangalia mayai yake kama yameanza kutotoa na kuyageuza geuza yazidi kupata joto.
huyo ni mbuni dume pichani.
Hivi hawa ndege wanaliwa? Mana nyama yake c itakuwa kama umechinja ng'ombe.
 
Siku zote najua Komodo wanapatikana Indonesia na maeneo mengine ya Asia pekee, sikujua kama wapo Australia.

Afrika na Asia lazima tuwe na death toll kubwa kutokana na umbali wa vituo vya afya, upatikanaji wa anti venom na gharama yake.

Kuna ndege anaitwa Cassowary, yupo Australia pia, picha yake ukimuona ni kacute kumbe kakiller.
Screenshot_20211202-075733.jpg
 
WAJUE WANYAMA KWA SIFA ZAO ZA KIPEKEE.

1. Nyangumi.
Huyu ndio mnyama mkubwa kuliko wanyama wote, ukimuweka katika kiwanja cha mpira wa miguu, hubakiza mita chache ili kufikia nusu ya kiwanja hicho, mbali na ukubwa huo lakini ni mnyama mwenye macho madogo sana, ila sehemu za siri noma sana dume huwa na uume wenye futi 12.

2. Twiga.
Huyu ndiye mnyama mrefu kwenda juu kuliko wanyama wote unaowafahamu, anapenda amani, ni mpole lakini hapendi mizaha, miguu yake ndio silaha pindi anapovamiwa na hilo teke usiombe.

3. Kozi
Huyu ndiye kiumbe mwenye uwezo wa kukimbia kuliko mnyama yoyote, ni ndege mwenye ufanano sana na tai, ukimshitua akakimbia kama upo Dar es salaam usiendelee kumtafuta dar, wapigie ndugu zako moro kuuliza kama ametua huko au lah.

4. Nyegere.
Ndio anavunja rekodi kwa wivu alishawashangaza watalii hapo Serengeti baada ya jike wake kujikwaa, alichimba shimo refu kidogo kuhakiki kama ile ilikuwa ni ajali kweli, au kuna faulo alitaka kuchezewa kwa bae wake.

5. Kobe
Ndiye mnyama anayeishi miaka mingi duniani, pengine kuliko wanyama wengine wote hufikia miaka hadi 350, kwa Tanzania tunao wenye miaka 200+, kama nakuona raha za dunia zinavyokufanya utamani kuwa Kobe.

6. Kicheche.
Ndiye mnyama anayependa ngono kuliko kiumbe yoyote, wanapokutana jinsia tofauti kabla ya salamu huanza kusasambua kwanza, yaani hawa katika jamii zao hata msibani hukutana kwa mapenzi pia, inakadiriwa kwa siku ili walale usingizini mwororo auheni wapitiane mara 60 na zaidi ! Na ndio sababu hata mtu akiwa kiwembe huitwa kicheche.

7. Konokono.
Ndio kiumbe anayesafiri taratibu sana na hii ni kwa sababu hujitengenezea njia ya kupita kwanza ndipo apite.

8. Tai
Ndio kiumbe mkorofi kupita kiasi ni kawaida kunyang'anya watalii chakula, ni kawaida kusumbua ndege wenzie wanapoatamia, kupigana nk ili mradi fujo.

9. Nyati
Mnyama mwenye hasira na kisasi kuliko wanyama wengine wote, simba wanamwelewa vyema sana huyu kiumbe, wakithubutu kuua mtoto wake na wao huenda kukanyaga watoto wake vile vile au vipi bwana jicho kwa jicho, jino kwa jino tuone sasa.

10. Kipepeo.
Ndiye kiumbe mpenda amani pasina mfano, ukipita msituni umenuna usitegemee watakusogelea, ila mkipita na mwenza wako, mnacheka mna furaha, ahaa utashangaa wanawapamba !

11. Simba.
Pengine sababu ya kuitwa Mfalme ni ubabe, Dume la simba ndio mnyama pekee anayejijua kwamba anaogopwa na hata majike wake wanapopata dhahama, akipata taarifa hujitokeza mara moja na ukiona madume yameongozana mawili basi jua huo mziki mwamuzi ni Mungu.

12. Mbu
Ndio kiumbe aliyeweza kuua binadamu wengi sana kuliko mnyama yoyote yule unayemfahamu wewe, utapokaona tafadhari Katie kitasa.

13. Komba
Ndiye mnyama mlevi kuliko wanyama wote na akilewa hulia pasina sababu ya msingi, hata ukibahatika kumuona sura yake imekaa kilevi levi, hupendelea pombe za kienyeji kuliko bia, we watege kwa mnazi au ulanzi sio misosi hapo utawapata.

14. Popo
Pamoja kwamba mchoro wake hupendeza sana katika michoro, ila ni miongoni mwa viumbe wenye sura mbaya sana kuliko wengine wote.

15. Tembo
Ndiye mnyama mwenye uwezo wa kuhifadhi sana kumbukumbu katika kichwa chake, kama ulipojenga walihawi kupita tegemea kuna siku watakuwa wageni wako, wakati tunakazana kusema tembo wamevamia sehemu fulani tukae tukijua maeneo hayo wana historia nayo, sasa siku mpige jiwe mkutane baada ya miaka kumi ndio utajua ule mkonga ni bakora au pua.

16. Pomboo
Ndiye mnyama mwenye huruma sana kiasi kwamba akikuona una tatizo, huacha mambo yake na kutaka kukusaidia
Itaendelea...
Mkuu;
1.Kinyonga:
Kinyonga ni mnyama mwenye Upendo wa hali ya juu. Anapofikia hatua ya kuzaa, hupanda juu ya mti mrefu sana na hujiachia/hujidondosha na akifika chini hupasuka/husambaratika ili watoto watoke. Anakufa kwa ajili ya watoto kuishi. Anajifanyia caesarian section Binafsi
2. Mbwa koko:
Mbwa mwenye watoto hubangaiza na akirejea /akirudi pale kwenye kundi la watoto huwatapikia chakula alichookoteza na maisha yanasonga. Usipolielewa hilo utakereka na kuona kinyaa sana kwa Tabia hii.
3.Binadamu:
Binadamu hapendi kuambiwa UKWELI kwamba yeye ni mmojawapo wa WANYAMA tena mnyama hatari zaidi Duniani. Bora Ukutane na kundi la Simba kuliko kukutana na Binadamu mmoja hususan adui yako!
 
Mkuu;
1.Kinyonga:
Kinyonga ni mnyama mwenye Upendo wa hali ya juu. Anapofikia hatua ya kuzaa, hupanda juu ya mti mrefu sana na hujiachia/hujidondosha na akifika chini hupasuka/husambaratika ili watoto watoke. Anakufa kwa ajili ya watoto kuishi. Anajifanyia caesarian section Binafsi
2. Mbwa koko:
Mbwa mwenye watoto hubangaiza na akirejea /akirudi pale kwenye kundi la watoto huwatapikia chakula alichookoteza na maisha yanasonga. Usipolielewa hilo utakereka na kuona kinyaa sana kwa Tabia hii.
3.Binadamu:
Binadamu hapendi kuambiwa UKWELI kwamba yeye ni mmojawapo wa WANYAMA tena mnyama hatari zaidi Duniani. Bora Ukutane na kundi la Simba kuliko kukutana na Binadamu mmoja hususan adui yako!
Binadamu hapendi kuambiwa UKWELI kwamba yeye ni mmojawapo wa WANYAMA tena mnyama hatari zaidi Duniani. Bora Ukutane na kundi la Simba kuliko kukutana na Binadamu mmoja hususan adui yako
 
Mkuu;
1.Kinyonga:
Kinyonga ni mnyama mwenye Upendo wa hali ya juu. Anapofikia hatua ya kuzaa, hupanda juu ya mti mrefu sana na hujiachia/hujidondosha na akifika chini hupasuka/husambaratika ili watoto watoke. Anakufa kwa ajili ya watoto kuishi. Anajifanyia caesarian section Binafsi
2. Mbwa koko:
Mbwa mwenye watoto hubangaiza na akirejea /akirudi pale kwenye kundi la watoto huwatapikia chakula alichookoteza na maisha yanasonga. Usipolielewa hilo utakereka na kuona kinyaa sana kwa Tabia hii.
3.Binadamu:
Binadamu hapendi kuambiwa UKWELI kwamba yeye ni mmojawapo wa WANYAMA tena mnyama hatari zaidi Duniani. Bora Ukutane na kundi la Simba kuliko kukutana na Binadamu mmoja hususan adui yako!
Binadamu hapendi kuambiwa UKWELI kwamba yeye ni mmojawapo wa WANYAMA tena mnyama hatari zaidi Duniani. Bora Ukutane na kundi la Simba kuliko kukutana na Binadamu mmoja hususan adui yako[emoji1545]
 
Hili dude wabongo wanaliita chunusi,wanaamini kwenye maji kuna jini linalofyonza damu,kumbe ni huyo electric eel anakugonga shoti unakufa halafu tukikupata tunakukuta umepungukiwa damu sababu ya ile shoti,hapo wabongo ndio wanasema jini lilikunyonya damu[emoji16][emoji16][emoji16]
Dah! Huwezi amini ndy nimejua leo basi hawa samaki kigoma wako wengi
 
Tasmanian Devil,
Tasmanian-Devils-hero.jpg
Miongoni mwa wanyama wakorofi sana, usidanganyike na kisura chake kicute ukakutana nacho mtaani uende kukipetipeti. Wanaishi kibabe na hawana hofu na hupigana hata na mbwa wakubwa bila kujali size yao.

Ubabe unaanza tangu siku wanapozaliwa. Jike anaweza kuzaa vitoto 20-30 au zaidi ila ana chuchu nne tu hivyo vitoto vinapozaliwa tu vinaanza kushindana na kupigania chuchu vinyonye. Kwa hali hii asilimia kubwa ya vitoto vinakufa vinapozaliwa tu na vingine havitaishi kufika ukubwani.

Ukubwani nako ni ubabe. Jike atapandwa na dume mbabe tu hivyo madume watapigana na kushindana kupata mke. mshindi atapata nafasi ya kuongeza kizazi chake and the cycle continues.
bG9jYWw6Ly8vcHVibGlzaGVycy81NDk5MS8yMDIxMDUyOTAzMzYtbWFpbi5jcm9wcGVkXzE2MjIyMzQxOTUuanBn.jpg
 
Bull Shark

Papa mkorofi na aggressive kuliko wote. Inasemekana huyu ndo shark hatari kuliko hata Great White Shark ambaye wengi wanamchukulia kama mfalme wa bahari. Probability ya kung'atwa na bull shark ni kubwa kuliko kung'atwa na Great White. Hawa wanaishi karibia maeneo yote,

Bull shark anaweza kuishi baharini na pia kwenye mito na maziwa (saltwater na freshwater kote anatamba) tofauti na shark wengine.

Kama shark wengine wengi wanaozaa watoto na sio wale wanaotaga mayai, embryo wa shark wakiwa tumboni huwa hawana source ya chakula kingine hivyo wanakulana wenyewe kwa wenyewe mpaka wachache tu ndo wanabaki wakati wa kuzaliwa. Mara nyingine wanakulana mpaka wanabaki wawili tu au hata mmoja tu ndo anafanikiwa kuzaliwa.

Hawalelewi na wazazi. Anapozaliwa tu anaanza kujitegemea (tena anabidi asepe fasta tu akizaliwa maana kama mama yake ana njaa anaweza kumgeuza chakula 😁😁).

1280px-Bullshark.JPG
 
Back
Top Bottom