Madai ya mkurugenzi mkuu wa TRC kuhusu watu kuhujumu treni ya SGR yanahitaji kushughulikiwa haraka

Madai ya mkurugenzi mkuu wa TRC kuhusu watu kuhujumu treni ya SGR yanahitaji kushughulikiwa haraka

Hismastersvoice

JF-Expert Member
Joined
Jan 26, 2013
Posts
21,741
Reaction score
26,735
Siku ya jana kuna madai toka kwa mkurugenzi mkuu wa TRC kuwa anayo majina ya watu wanaoihujumu treni ya SGR, madai haya ni mazito na TRC haina uwezo wa kuyashughurikia kwa sababu yanahusu jinai.

Kwenye madai hayo kuna taarifa ya kuwa wapo watu wanakata waya za umeme ambao ndiyo nishati ya hiyo treni hivho kusababisha ishindwe kutembea, uhalifu huu ni mkubwa kwani umeme huo unatoka kwenye gridi ya taifa hivyo kunaweza kusababisha uharibifu kwenye gridi hiyo.

Ninashauri waziri mkuu amtake mkurugenzi Kadogosa ampe ushahidi wa madai hayo ili avitake vyombo vya dola kama polisi na usalama wa taifa walishughurikie haraka kabla madhara makubwa hayajatokea.
 
Wafanye mpango wa kulinda hiyo SGR Watanzania hawana utaratibu wa kulinda mali zao hakuna hujuma wahuni wanaiba hivyo vyuma wakauze kila kitu hujuma hujuma ili iweje wekeni mazingira ya kulinda sio mnaweka nauli kubwa mnataka Reli ijilinde yenyewe bila hata kuweka post kadhaa kwa umbali fulani mpaka Dodoma...
 
Huyu mzee ameamua kuweka siasa pembeni hicho alichokisema kinaukweli sana.

Nastaajabika sana na utendaji wa teeth. Hivi hujuma kwamba hawazioni au.!?

Maana ni kweli juzi kati walikata nyaya na muhimu za umeme na sio hivo tu kuna makundi ya watu wamekuwa wakisubiri treni baadhi ya maeneo na kuipiga mawe hii balaa lake halielezeki.

Nastaajabika mno na huuu utendaji wa teeth. Sema changamoto yote ni kuwa familia ya watanzania tumekosa kiongozi aliena uthubutu wa kuchallenge watu wa chini yake ili waweze kuwajibika.


Wahusika nawaombeni mchukue hatua. Hii ni aibu sana.

Hongera sana Mkurugenzi kwa maamuzi uliyoyatoa.
 
Nilitegemea mpaka sasa watu wawe washakamatwa kabla ya mkurugenzi kutoa hiyo taarifa ninachokiona hapa Kadogosa anatafuta pa kutokea
 
Siku ya jana kuna madai toka kwa mkurugenzi mkuu wa TRC kuwa anayo majina ya watu wanaoihujumu treni ya SGR, madai haya ni mazito na TRC haina uwezo wa kuyashughurikia kwa sababu yanahusu jinai.

Kwenye madai hayo kuna taarifa ya kuwa wapo watu wanakata waya za umeme ambao ndiyo nishati ya hiyo treni hivho kusababisha ishindwe kutembea, uhalifu huu ni mkubwa kwani umeme huo unatoka kwenye gridi ya taifa hivyo kunaweza kusababisha uharibifu kwenye gridi hiyo.

Ninashauri waziri mkuu amtake mkurugenzi Kadogosa ampe ushahidi wa madai hayo ili avitake vyombo vya dola kama polisi na usalama wa taifa walishughurikie haraka kabla madhara makubwa hayajatokea.
Ni ngumu.
Walishaambiwa kuwa huo mzigo ni fake.
Na miaongoni mwa waliosababisha ni yeye.

Hivyo anataka ku escape kwa staili hiyo.
 
Siku ya jana kuna madai toka kwa mkurugenzi mkuu wa TRC kuwa anayo majina ya watu wanaoihujumu treni ya SGR, madai haya ni mazito na TRC haina uwezo wa kuyashughurikia kwa sababu yanahusu jinai.

Kwenye madai hayo kuna taarifa ya kuwa wapo watu wanakata waya za umeme ambao ndiyo nishati ya hiyo treni hivho kusababisha ishindwe kutembea, uhalifu huu ni mkubwa kwani umeme huo unatoka kwenye gridi ya taifa hivyo kunaweza kusababisha uharibifu kwenye gridi hiyo.

Ninashauri waziri mkuu amtake mkurugenzi Kadogosa ampe ushahidi wa madai hayo ili avitake vyombo vya dola kama polisi na usalama wa taifa walishughurikie haraka kabla madhara makubwa hayajatokea.
Hiyo ni dalili mhimu kuwa kiongozi hatoshi. Unasemaje una majina ya wahulifu, unasubiri mpaka watekeleze uhalifu kisha unasema unawajua. Basi wewe unakuwa mhalifu namba moja.
 
Siku ya jana kuna madai toka kwa mkurugenzi mkuu wa TRC kuwa anayo majina ya watu wanaoihujumu treni ya SGR, madai haya ni mazito na TRC haina uwezo wa kuyashughurikia kwa sababu yanahusu jinai.

Kwenye madai hayo kuna taarifa ya kuwa wapo watu wanakata waya za umeme ambao ndiyo nishati ya hiyo treni hivho kusababisha ishindwe kutembea, uhalifu huu ni mkubwa kwani umeme huo unatoka kwenye gridi ya taifa hivyo kunaweza kusababisha uharibifu kwenye gridi hiyo.

Ninashauri waziri mkuu amtake mkurugenzi Kadogosa ampe ushahidi wa madai hayo ili avitake vyombo vya dola kama polisi na usalama wa taifa walishughurikie haraka kabla madhara makubwa hayajatokea.
Kwa Maslahi ya Taifa angewataja wahalifu hao na little Tamko Zito kuhusu SGR kwamba iwe Marufuku mtu kukaribia SGR bila sababu ya msingi.
 
Huyu mzee ameamua kuweka siasa pembeni hicho alichokisema kinaukweli sana.

Nastaajabika sana na utendaji wa teeth. Hivi hujuma kwamba hawazioni au.!?

Maana ni kweli juzi kati walikata nyaya na muhimu za umeme na sio hivo tu kuna makundi ya watu wamekuwa wakisubiri treni baadhi ya maeneo na kuipiga mawe hii balaa lake halielezeki.

Nastaajabika mno na huuu utendaji wa teeth. Sema changamoto yote ni kuwa familia ya watanzania tumekosa kiongozi aliena uthubutu wa kuchallenge watu wa chini yake ili waweze kuwajibika.


Wahusika nawaombeni mchukue hatua. Hii ni aibu sana.

Hongera sana Mkurugenzi kwa maamuzi uliyoyatoa.
Utupiaji mawe vyombo vya abiria hutokea na hufanywa na watoto na hili si kwa Tanzania tu. Waya kukatika si lazima mtu ahusike, kuna wakati waya za Tanesco hukatika bila mtu kuhusika, kwa SGR tuliambiwa bundi na nyani wanahusika.
Jambo la kujiuliza ni vipi TRC wameyapata majina ya wahujumu lakini wameshindwa kuwakamata! Au nao ni mabosi vigogo?
 
 
Kwa undani soma kitabu cha Ujasusi wa kidola na kiuchumi.

Hao wakiwa confirmed wamefanya hujuma inabidi watiwe kitanzi uwanja wa taifa warushe live ili asije MBWEHA mwingine kuja kuhujumu.
 
Back
Top Bottom