Madaktari acheni kutuchanganya na hii kauli yenu tata ya Critical but Stable

Madaktari acheni kutuchanganya na hii kauli yenu tata ya Critical but Stable

Tasnia ya udaktari ni sawa na muuza ice cream.
Daima utapewa matumaini na kukufurahisha wewe unayemuuguza jamaa yako.

Hata Nyerere baba wa Taifa, Mwl. Nyerere, inajulikana alikata roho siku kama 7 kabla ya kutangaziwa kifo chake ili mipango yote iwekwe sawa kwa ajili ya kuhimili changamoto na mihemuko serikali na wananchi.

Ila hilo neno la critical but stable lilitumika sana. Though, kifo kikifika ndiyo hakuna zuio.

Nawapenda sana Watu kama Wewe Mkuu na unaonyesha hata uwezo wako wa akili nao ni mkubwa sana na ndiyo huwa tunaelewana na tunaenda sawa humu Jamvini. Ufafanuzi wako ni mzuri na nimeupenda Mkuu. Sasa taratibu naanza kuelewa maana halisi ya Kauli tata ya Critical but Stable.

Nyie ndiyo Watu ambao nataka mchangie sana huu uzi na siyo wale Wapumbavu wachache wanaodhani kila muda ni muda wa Siasa tu au wanadhani dunia nzima basi ni Wao tu pekee ndiyo wanauguza Mgonjwa wao wakati ukweli ni kwamba hata Sisi wengine tuliopo huku Nyumbani nasi tuna Wagonjwa wetu hivyo kukimbilia humu JF ili kupata ufafanuzi wa Kidaktari siyo dhambi au uhalifu.
 
Nadhani aliyekuhifadhi tumboni mwake kwa miezi Kenda / Tisa Yeye ndiyo anaweza akawa Punguani mkubwa wa kunizidi. Hivi katika uzi wangu nimetaja mahala popote jina la Tundu Lissu? Kwahiyo GENTAMYCINE sina uhuru wangu na haki yangu ya kuhoji Jambo la Kitaalam na kupata ufafanuzi wake? Kwani ni Wagonjwa wangapi humu Mahospitalini huwa tunaambiwa na Madaktari kuwa wapo Critical but Stable?

Utundu Lissu katika huu uzi wangu umekukaje? Umepimaje kama Mimi siuguzi huyo Mgonjwa wangu? Naona unanitafuta Mkuu hivyo endelea tu utakipata unachokitafuta kutoka Kwangu kwani unaonekana unajifanya Kunijua sana halafu unawashwawashwa na Mimi.

Na nilitaka ufafanuzi wa Kitaalam na Kiueledi kabisa kutoka kwa Madaktari humu JF na sikuhitaji maoni ya Wapumbavu wachache wa mfano wako ambao akili zenu zote na muda wote zimekaa tu Kiitikadi za Kisiasa. Nauguliwa je ni dhambi kuhoji juu ya jambo fulani ambalo linanitatiza?

Uvumilivu wangu Kwako unaanza kufikia Kikomo.
Acha kutisha watu wewe mama
 
Sijui ni kwanini Madaktari wanapenda sana kusema kuwa Mgonjwa fulani yupo Critical but Stable lakini baadae ukija kuchunguza zaidi utakuta tayari huyo Mgonjwa ameshaonyesha dalili zote za Kukata roho / Kufa na mara nyingi wale Wagonjwa wengi ambao huwa tunaambiwa na Madaktari wetu kuwa wapo Critical but Stable huwa wanafariki dunia ndani ya ama muda mchache au siku chache tu zijazo.

Na kuna Daktari mmoja alinipa Siri kubwa ya wao kupenda kuitumia hii Kauli ya Critical but Stable kwamba huwa wanaitumia sana ili kuwaandaa Kisaikolojia wenye Mgonjwa wao ili hata baadae wakiwaambia ameshafariki basi wasiwe na mshtuko mkubwa lakini ukweli ni kwamba Kitabibu duniani kote hakuna kitu cha fulani ni Critical but Stable ila ukweli ni kwamba tayari huyo Mgonjwa anakuwa ameshafikia hatua ya mwisho kabisa ya kukata roho.

Sasa kama kumbe Mgonjwa kuwa Critical but Stable ni sawasawa tu na tayari ameshakata roho / amekufa nyie Madaktari huwa mnaogopa nini kutuambia Sisi tunaouguza kuwa Mpendwa Mgonjwa wetu ameshafariki dunia? Je hamuoni kwamba kuendelea kutuambia hii Kauli yenu ya Mgonjwa yupo Critical but Stable wakati kumbe ameshafariki dunia tayari mnatupa mzigo mwingine tu wa gharama na huenda mngesema tu ukweli mapema basi tungeokoa Pesa?

Kwa mfano Mimi binafsi nina Mgonjwa wangu Hospitali moja hapa Jijini ambaye alishambuliwa vibaya mno na Majambazi huku akiwa ameumizwa vibaya sana mkononi, mguuni, tumboni, kichwani na hadi wakaathiri na ini lake huku akiwa anapumulia mashine, lakini tokea tumkimbize hapo Hospitali leo ni siku kama si ya 15 basi ya 16 yupo ICU na hata haturuhusiwi kuingia kumuona ila ni Madaktari tu pekee ndiyo hutoka nje na kutupa taarifa zake za neno lao kubwa Kwetu sisi Wauguliwaji ni kwamba Mgonjwa wetu yupo Critical but Stable.

Madaktari acheni kutuchanganya tafadhalini huyu Critical but Stable anatutesa sana Sisi tunaouguza Wagonjwa wetu. Nawaomba pia Madaktari mliotukuka na mliopo humu JamiiForums mnipe ufafanuzi wa hii Kauli kwani inatuchanganya sana na hadi kuwafanya Ndugu, Jamaa na Marafiki zetu wengi wasijue la kufanya na huku wengine wasite pia hata kutaka kutoa msaada wao wa michango na huduma zingine kwa huyu Mgonjwa wetu Mpendwa ambaye ni Ndugu yangu aliyejeruhiwa vibaya sana na Majambazi huko Tarime Mkoani Mara ( Musoma ) akiwa anatoka Kazini na anaingia Nyumbani Kwake.

Nawasilisha.
Kila doctor anatoa majibu based on the available evidence....sasa kama unataka kupangia madaktar cha kufanya sawa.
 
Hoja yangu ni hiyo Kauli ya Critical but Stable tu na hakuna jingine tafadhali. Kwahiyo unataka kumaanisha kuwa Mimi GENTAMYCINE nina hamu huyu Mgonjwa wangu afariki dunia? Mkuu hebu tengua upesi kauli yako na nitake radhi sasa hivi.
Doctor hatakiwi kukukatisha tamaa.
 
Mbona naona mnamjaji jamaa tofaut,, tusiwaze negative ila kama kuna daktar aeleze tu mana ya hiyo kaul ya critical but stable.

Asante kwa kunielewa Mkuu na hicho ulichokisema ndicho hasa nilichokuwa nakitaka na ndiyo maana unaona hata uzi wenyewe nimekuja kuuanzisha huku katika Forum ya Madaktari ila nashangaa Watu wamekuja huku na kutaka kulazimisha yao na kuulazimisha huu uzi uwe ni kama wa Kisiasa zaidi.

Hilo suala la Critical but Stable ni suala langu binafsi kwakuwa hata Mimi pia ninauguza hivyo nimewauliza Madaktari ili waweze kunielimisha na kunipa ufafanuzi wao wa Kitaaluma na Kiuweledi kabisa ili basi na Mimi niweze kuongeza maarifa fulani.

Kuugua kwa Mheshimiwa Tundu Lissu kusiwe ni Kifungo au Kikwazo kwa sisi wengine kuhoji na kupata ufafanuzi wa masuala ya tiba.
 
Rudi shule.

Tumia akili.

Ahaaa af atakua ni mstaafu et
6947e402c15d11a92207bbd565c407f9.jpg
 
Nimecheka sana yaani tatizo la watu Wa Jf hawasomi maelezo ya mwanzo kwa umakini wanakimbilia kutoa shiit yaani ndio Hawa mtihani anajibu bila kusoma maelekezo mngemuelewa huyu kaka msinge lopoka shiit
 
Critical ni kuwa mgonjwa clinically yuko very ill but stable ni kuwa vital sign is ok and no sign of deterioration...the death is not knocking the door but its near enough to hear the knocking..

Asante sana Mkuu kwa huu ufafanuzi wako wa Kidaktari kabisa na nazidi sasa Kuelimika. Nafurahi sasa kuona Watu wenye akili zao wanaanza kunielewa na wananipa ushirikiano wa Kimaelezo na wale Mapopoma / Wapumbavu sasa wameshaanza kujitenga na huu uzi na wamerudi katika ile Forum yao ya Siasa hasa zile zao za Majitaka walizozoea.
 
Acha kujishaua nani huko Tarime alivamiwa kiasi kama Lissu? nani kapigwa risasi za tumbo kama yeye? tunajua hata mnaingia kwenye maombi kwa ajili ya kumwombea mabaya... hamtasikia hilo Mungu yupo na hata Ayub aliharibiwa mwili wote lakini roho yake ilikuwa salama
 
GENTAMYCINE, mimi si daktari wala tibabu, ila mada yako imenisukuma kutafuta maana ya hiyo kauli yz Madaktari ya mgonjwa kuwa katika hali ya kutibiwa wanayoiita critical but stable.

A Critical but Stable condition, in hospitals, indicates that the patient is in bad state but not likely to get worse in the short-term. A patient in critical condition implies that vital signs are not stable and not within normal limits e.g. a patient may be unconscious or indicators are unfavourable[/COLOR].

Maneno yafuatayo hutumika pia, mara kwa mara:
Critical, Comfortable, Progressing well

Kwa hivyo basi, madaktari wanaomtibu mgonjwa hutumia maneno hayo kuelezea hali ya mgonjwa na si vinginevyo. Ni lugha inayotumika kuwaambia wahusika na mgonjwa, hali yake, na wala hayana tafsiri/maana yoyote kisayansi.
 
Swali nitakalokuja kujiuliza ni kwa vipi aliingia kwenye critical au commatose state ??
Habari mkuu. Sija kuona siku nyingi kwenye ili jukwaa. Napenda ku kwambia ww ni mmoja kati ya watu walio nipaga chachu yaku jiunga Jf haswa haswa na kutoa michango yangu Jf dr..
Heshima yako broh.
 
Msigwa amesema amemuona mwanzo hadi mwisho (Jana aliporudi nchini), kwahiyo ondoa shaka mtoa mada. Jemedali yupo hai na atapona tuendelee kumsihi Mungu.

Madaktari kumruhusu apelekwe Marekani kwa matibabu zaidi, hawawezi na wala hawataweza kuruhusu kutokana na sababu mbalimbali...nikizihisi baadhi;
1. Hawawezi kukubali kushindwa kwa urahisi hivyo
2. Wanalinda heshima ya hospitali yao, isijeikagundulika waonekane wameshindwa kutibu wagonjwa...bora mgonjwa limpate lolote akiwa hapo na si kukiri kushindwa
3. Wamepata fedha nyingi za dharula, kibiashara ni lazima uendelee kumshawishi mgonjwa aendelee kubaki kwako na ikiwezekana umtishe asipate mawazo ya kumhamisha mgonjwa wake
4. Endapo limetokea baya kwa mgonjwa na unapata kigugumizi kumjuza muuguzi wake, na ikaenda zaidi yule muuguzi wake anataka kumhamisha mgonjwa kumpeleka mbele zaidi...basi huweza kutumia busara zaidi za kumfanya asijaribu kufanya hivyo na kumuaminisha kwamba akijaribu kufanya hivyo anaweza akatengeneza madhara zaidi. Mda huohuo wakiwa wanaandaa mazingira psychologically ya kumjuza kuwa mgonjwa wake si riziki.....(nisieleweke vibaya kwa mgonjwa wetu)
5. Mgonjwa watu yu salama na Mungu anaendelea kumlinda, tuzidishe maombi kwa kila mmoja na imani yake. Mtoa mada usilete mada km hizi wakati km huu!!

Samahani Mkuu haya maelezo yako unadhani yanashabihiana kabisa 100% na kile ambacho nimetaka kukijua au kupata ufafanuzi wa Kitaaluma na Kiuweledi kabisa kutoka kwa Madaktari wabobezi wa JamiiForums? Siku nyingine si vibaya sana kama ukificha Upopoma / Upumbavu japo kwa muda.

Kuugua kwa Tundu Lissu kusiwe Kikwazo kwa sisi wengine katika Kuhoji mambo ya Kitabibu na bahati mbaya sana unaweza kukuta hao hao ambao wanajifanya kumlilia au kuhuzunika na Kuuguliwa Kwake hawajatoa hata Senti moja ya mchango wao Kwake ila juhudi zao ni Kujitutumua tu humu JF.
 
Back
Top Bottom