Madaktari kuchati kazini: Ongezeko la machekibobu

Madaktari kuchati kazini: Ongezeko la machekibobu

Siku hizi mimi nawaita waganga wa kienyeji
Yaani kabla hujamaliza sentence yeye ameishaandika na anakuambia kachukue dawa
Hawa makanjanja sijui wanafundishwa nini maana hata nidhamu hawana na manesi wafuata mkumbo wao ndio serial killers waliojificha nyuma ya nguo hizo nyeupe
Wanauwa kama nini
 
Japo madaktari wote ni makasuku wanaomeza madesa ya shule na kuyakariri jinsi yalivyo, lakini mnyonge mnyongeni, nchi hii walikuwepo madaktari bwana!

Kuna madaktari ukiwaambia naumwa kichwa anakimbilia kukudunga chanjo ya FANSIDA, sijui ni kukariri ama ndivyo walivyofundishwa huko mashuleni?

Mimi mzee wangu alikuwa daktari, tena daktari nguli aliyeheshimika haswa kutokana na huduma zake. Hawa ni wale madaktari wa zamani ambao akikuhudumia unasema kweli hapa nimehudumiwa na DOKTA HASWA!

Madaktari wa enzi hizo ukiwafuata hadi unahisi raha kuhudumiwa. Utakaguliwa, utabonyezwa bonyezwa vimashavu vyako, unaachama mdomo unamulikwa koromelo na kitochi, yaani hadi raha!!!

Baadaye unawekewa la kupimia moyo, huku daktari anakuhoji kitaalamu na kwa ufanisi.

Lakini siku hizi kumezuka wimbi la MACHEKIBOBU wanaojiita madaktari. Hawawezi kukuhudumia wana mapepe na mawenge muda wote.

Unashtukia daktari amerukia kipima moyo, mara amekitupa mezani, anakurupuka nduki anawahi kuchungulia meseji ya Instagram. Akikuhurumia sana anakudunga chanjo la KOVIDI.

Akikuhoji wala hakuangalii usoni, kaweka EARPHONES anasikiliza singeli ati! Ni mwendo wa Unasemaaaa!!!??? Eeeeh, unasemajeee!!??? Eeeeeeeh?? sijasikia umesemaaa??? Eeeh nasemajeeee!

MY TAKE: Hili nalo mkalitizame.
Anhaaa BICHWA KOMWE - leo umetufikia sasa .

Shida ni hizi division one za mchongo ambazo zinatuletea masharobaro kazini eti daktari .

Ninayo mengi rafiki ila wacha nikae kimya ila jua vijana ndiyo wazinguzi ila ni mwendo wa kuwapiga makofi matatu heshima inachukua mkondo wake .

Sent from my SM-J410F using JamiiForums mobile app
 
Siku hizi mimi nawaita waganga wa kienyeji
Yaani kabla hujamaliza sentence yeye ameishaandika na anakuambia kachukue dawa
Hawa makanjanja sijui wanafundishwa nini maana hata nidhamu hawana na manesi wafuata mkumbo wao ndio serial killers waliojificha nyuma ya nguo hizo nyeupe
Wanauwa kama nini
Hatari sana
 
Mim nimeenda kupima U.T.I ila vipimo na Cha ukimwi wakaweka ila mi nikajikausha kimya ,nikamuuliza sasa hicho kingine Cha nin akasema malaria sasa wakati hapo ashanichoma kwenye kidole na akaweka damu kwenye ki glass ili apeleke [emoji436],alafu damu nyingine akaweka kwenye kile kidude Cha kupimia ukimwi ....majibu hata hakunipa kama yakoje ndo nashindwa kuwaelewa kwanini anakupima alafu majibu hatoi

Sent from my Infinix X652C using JamiiForums mobile app
Wachawi wale.
 
Kuna midada anavaa nguo fupi inafika mapajani, na unakuta mapaja meupe huku yuko anachat na simu ya macho matatu, kavaa koti jeupe, eti daktari, najiuliza uyu ni daktari au malaya aliyechangamka
Aisee..
Makahaba
 
Kuna midada anavaa nguo fupi inafika mapajani, na unakuta mapaja meupe huku yuko anachat na simu ya macho matatu, kavaa koti jeupe, eti daktari, najiuliza uyu ni daktari au malaya aliyechangamka
Aisee..
Toa code ya hiyo Hospitali Mkuu...
 
Mim nimeenda kupima U.T.I ila vipimo na Cha ukimwi wakaweka ila mi nikajikausha kimya ,nikamuuliza sasa hicho kingine Cha nin akasema malaria sasa wakati hapo ashanichoma kwenye kidole na akaweka damu kwenye ki glass ili apeleke [emoji436],alafu damu nyingine akaweka kwenye kile kidude Cha kupimia ukimwi ....majibu hata hakunipa kama yakoje ndo nashindwa kuwaelewa kwanini anakupima alafu majibu hatoi

Sent from my Infinix X652C using JamiiForums mobile app
Kaa kwa kutulia kwa nn unaogopa kupima ukimwi?
Usipo pima kwa hiyari utapimwa kwa lazima bila kujua
 
Siku hizi mimi nawaita waganga wa kienyeji
Yaani kabla hujamaliza sentence yeye ameishaandika na anakuambia kachukue dawa
Hawa makanjanja sijui wanafundishwa nini maana hata nidhamu hawana na manesi wafuata mkumbo wao ndio serial killers waliojificha nyuma ya nguo hizo nyeupe
Wanauwa kama nini
We mzee si ulisema upo ulaya na unamiliki viwanda?
Kumbe unatibiwa na makanjanja bongo land
 
Wanachonikera mimi ni tabia yao mpya ya kupenda kupima watu ukimwi

Kuna siku nimeumwa kichwa nikaenda kupima Malaria, baada ya kipimo akasema malaria yangu ni ndogo kiasi kwamba sihitaji kutumia dawa bali nitumie muda mwingi kupumzika na kunywa maji

Cha ajabu akashauri eti unaonaje tukupime na ukimwi? Nikamwambia acha ufala, mimi nimekuja kupima malaria siyo ukimwi, nikaondoka
Labda wanachukua data za maambukizi kwa ajili ya mashirika lakini Wanasahau good rapport na consent.
 
We mzee si ulisema upo ulaya na unamiliki viwanda?
Kumbe unatibiwa na makanjanja bongo land
Sasa nikija kununua mbaazi badala ya MO halafu nikwame Nzega nani anitibu hapo zaidi ya hao hao
Usinichonganishe nao wakaja kunidunga sindano zisizoeleweka
 

Huwa nasema, hakuna taaluma ambayo watu wake wanapaswa kupikwa na kuiva vizuri kila kona kama udaktari na wote wanaohusiana na utabibu.

Madaktari na wauguzi wengine wanatakiwa waive vizuri kabisa kitaaluma na kinidhamu. Wakufunzi wakiona mwanafunzi wa udaktari anakosa utu au nidhamu ni vizuri kumshauri akasome kitu kingine kwa kumwambia wazi wazi wewe hatuwezi kukuacha ukamalize watu.


 
Wanachonikera mimi ni tabia yao mpya ya kupenda kupima watu ukimwi

Kuna siku nimeumwa kichwa nikaenda kupima Malaria, baada ya kipimo akasema malaria yangu ni ndogo kiasi kwamba sihitaji kutumia dawa bali nitumie muda mwingi kupumzika na kunywa maji

Cha ajabu akashauri eti unaonaje tukupime na ukimwi? Nikamwambia acha ufala, mimi nimekuja kupima malaria siyo ukimwi, nikaondoka
Shida wagonjwa wa siku hizi mmekuamadaktari
Mtu anakuja na list ya vitu anavyotaka kupimwa
Kwa ufupi ujuaji mwingi
 
Sasa kama daktari ni content creator wa tiktok utafanyaje sasa inakubidi tu uwe makini kuangalia asije akakuchoma sindano ambayo imeshatumika kwa sababu ya kusahau
 
Back
Top Bottom