Madawa ya Kulevya: Aisha Bui (mke mwenza na Amina chifupa) nae akamatwa Brazil

Madawa ya Kulevya: Aisha Bui (mke mwenza na Amina chifupa) nae akamatwa Brazil

Taratibu ndugu usiwaingize waliofariki kwa sababu hawapo nasi na hawawezi kujitetea dhidi ya tuhuma zako.

Kitu kingine ni kwamba, Mimi binafsi sifagilii matumizi, mauzo/manunuzi na wala usafirishaji wa madawa ya kulevya. Lakini hali kadhalika, sielewi hii hali ha furaha sana kwa baadhi yetu kufurahia kusikia mtanzania mwenzetu amepatwa na matatizo kama haya. Nadhani ni vyema kutazama athari zinazosababishwa kwa jamii yetu sisi watanzania kabla ya kufikiria athari zinazosababishwa kwa "mabwana zenu" wa huko Ulaya. Mimi binafsi ningefurahi sana kama Joseph Kaniki au Matumla yoyote angekamatwa akiingiza unga/sembe nchini mwetu, Tanzania. Sababu ya furaha yangu ingekuwa ni kuokolewa/ kuepushwa kwa vijana wetu na madawa ya kulevya. Lakini kama Joseph Kaniki au Matumla amekamatwa akiingiza madawa ya Kulevya nchi za Ulaya kwa wazungu, basi mimi sioni sababu yoyote ya kusherehekea kukamatwa kwao. Kwa sababu hilo ni tatizo la wazungu na wazungu wana nyenzo zote za kukabiliana na matatizo yao.

Najua kuna wajinga humu, narudia kwa herufi kubwa pasipo kuomba msamaha, (KUNA WAJINGA NA WAPUMBAVU HUMU JAMII FORUM) wenye hoja hafifu kwamba; eti wabeba sembe wanalichafua jina la Tanzania. Wabeba sembe wanachafua majina yao binafsi, na siyo jina la Tanzania. Kwa mfano. Mimi binafsi nimeishi ughaibuni kwa miaka mingi na Wa-Nigeria wanajulika kwa miaka mingi sana katika fani ya kusafirisha madawa ya kulevya, kusafirisha malaya "prostitute", kusafirisha mipesa mingi haramu "money laundering" na kadhalika. Na baadhi ya nchi nyingine zinazojulikana kwa tabia hii ni Senegal na Jamaica. Lakini wananchi wa Tanzania au Malawi hawapewi umuhimu wowote ambao wananchi wa Senegal, Nigeria na Jamaica hawapewi. Na kwa wale ambao wanaangalia TV za ughaibuni vipindi kama "UK Border" au "Nothing to declare"; kila siku kwenye vipindi vile huonyesha kukamatwa kwa wabeba sembe "drug mules" na mataifa yao huwa ni Uingereza (wazungu); Wachina, Nigeria na kadhalika. Sijawahi kuona Mtanzania kakamatwa kwenye kipindi kile.

Kwa ufupi, Watanzania ni "wachezaji wapya" katika mchezo huu haramu na hawajulikani kabisa katika fani hii.
Waingereza ni miongoni mwa wabeba sembe wakuu duniani. Najua wengi wenu humu pale kwenye neno "Mzungu" ile herufi "z" huwa hamuioni na akili zenu katika neno Mzungu inasoma neno Mungu. Kwa hiyo haingingii akilini mwenu kwamba wazungu (waungu wenu) ni wabeba sembe.

Kwa mfano hapa chini kuna link mbili ambazo zinaonyesha wabeba sembe wa kizungu, na wahalifu hawa hupewa msaada wote wa kidiplomasia na nchi yao Uingereza kwa sababu Waingereza wanatambua kwamba watu wa aina hii wapo.


1. Peru 'drugs mules' Melissa Reid and Michaella McCollum 'had a good offer' - Home News - UK - The Independent

2. Lindsay Sandiford loses final appeal against drug trafficking death sentence in Bali - Telegraph

Lakini hata siku moja hutosikia watu wakisema kwamba eti watu hawa wanachafua jina la Uingereza.

Kwenye za karne nyingi na biashara hii kama Uturuki, ugiriki na Pakistani; katika sheria zao wana adhabu tofauti kwa muhalifu anayetoa sembe au kuingiza sembe katika nchi zao. Wakikumata unaingiza sembe nchini mwao adhabu yake ni sawa na kubondwa bondwa na nyundo na wakikukamata unatoka na sembe adhabu yake ni sawa na kunaswa kibao tuu.

Kwa ufupi, tuangalie wabeba sembe wanaoliingiza nchini mwetu na tuachanane na wanaolisafirisha juu kwa juu. Kama m-beba sembe alitumia msuli wa walet lake akakupokonya demu; hilo ni kosa la demu wako na usilete nongwa zako hapa. Na kama tukiangalia katika "economic perspective"; kama mbeba sembe wa kibongo akibeba na kuuza sembe lake juu kwa juu (kwa mfano kutoka kwa pele kwenda sweden) kisha akaja kufanya matanuzi Bongo; ni wajinga tuu ndiyo wasioweza kuuona mchango wake katika uchumi wa bongo. Huyu mtu ameliingizia taifa fweza za kigeni, kama amejenga nyumba atakuwa ametoa ajira kwa mafundi adamu, na kadhalika.

Hitimisho. Mimi siyo mbeba unga na ninafanya kazi kama Engineering Consultant Ughaibuni (kwa wale mtakaosema, kwanini unawatetea bana, wewe ni mbeba sembe ninii?) Lakini maisha na wazungu wamenifundisha kuangalia yanayonihusu na kuachana na yasiyonihusu. Sitetei wabeba unga, lakini kama mtu haingizi unga bongo, mimi sioni sababu ya kuwashwa na pilipili. Lakini akikamatwa anaingiza unga bongo basi mimi binafsi nipo radhi kukata shingo yake afe.


Kwa herini.

Injinia,tunamhurumia mtu kwa matatizo ya kujitakia,awe anatoa au anaingiza,biashara hii haifai,na kuhusu kuchafuliwa,ni kadhia ambazo watz wanatoa ushuhuda wa kukumbana nazo kwenye viwanja vya ndege huko ughaibuni,pindi waoneshapo Pass za TANZANIA
 
Baada ya bondia na footballer sasa musichana ya movie (maana kila asiyekuwa na address mjini sasa anataka awe muigizaji ili atoke khaa ) na toto ya town imekwisha Brazil eeh wasichana nyie wadogo mna mambo makuu jamani hizi lace wig, peruvian, simu za bei ya juu, vitz mbona zitawapeleka pabayaa??

Ndugu kama hamjawasiliana na ndugu yenu huyu kaeni mkao wa kula kupokea bad news (sioni huruma maana kapenda mwenyewe kuwa punda) hivi kila siku hamuoni TV/News Paper na Blogs zikiandika kwamba hali ya hewa ni mbaya ?? mara meli, mara wengine wamekamatwa Ethiopia daah mnawapa wengine ugumu wanaosafiri na Passport za ki Tanzania full kuangaliwa mpaka sehemu zisitakiwa.

NB
wale wasichana wanaoshawishiwa kuwa mapunda na makontena na wengine wanathubutu kwenda kwa waganga kupewa dawa ili wasishikwe USIJARIBU hakuna cha mganga wala nini, tulizana na tafuta plan B ya maisha na nini cha kufanya please i beg nisiposisitiza hivi tutapoteza wengi.

SOURCE: sintah.com

..........Miaka 2 au 3 iliyopita....... ilikuwa rahisi sana kuamini habari za matukio ukizikuta hapa jamvini........lakini kadiri siku zinavyokwenda ndivyo imani inapozidi kutoweka......Ni vyema tukajaribu kuepuka habari za uzushi na kupakana matope hasa pale tusipokuwa na uhakika nazo.....tuwaachie wengine ambao wako kwa ajili ya habari za aina hiyo..... ni mawazo yangu tu.......

MICHARAZO MITUPU: Aisha Bui akana kukamatwa na 'unga' Brazili, adai yu salama Afrika Kusini
 
kuwaalika hawa wabeba unga ikulu wakafuturu


Huyu mutu ni wa hajabu sana. Hospitali kakribia zote za wilaya hapa Dar haswa wodi za kina mama na watoto hazina vitanda huu sijuwi mwaka wa ngapi sasa hatulioni hili tatizo kutatuliwa, ila msanii wa bongo fleva akiathirika na unga unaouzwa na wabunge wa CCM Mh. Mtukufu Mungu rais anachukua madaraka ya kuwatibia na kuwauliza eti unga una radha gani pale wanapo pona. Huyu msanii naye pia inabidi ashitakiwe.
 
Hivi huyu mwanamke wa kwenye picha hii ni mzuri?
.....Mkuu Jimmy Santadio.... hakuna mwanamke mzuri au mbaya duniani.......uzuri/ubaya ni sifa....na katika sifa ni lazima kuwa na vigezo.......na vigezo kila mmoja yuko huru kujiwekea vyake.......hivyo ni vigumu sana kujadili kama mwanamke ni mzuri au mbaya hapa jamvini kabla kwanza hamjakubaliana katika vigezo.........ni mawazo yangu tu.......
 
Wasichana wadogo, warembo.
Shule walisomeshwa kwa gharama kubwa,
Wanaishia kuwa punda wabeba mizigo.

Na wamama watu wazima kama Mamndenyi
nao wanaamua kuwa punda wabeba mizigo, loooh.

Vijana wenye nguvu marijali nao wanaamua kuwa
punda wabeba mizigo.

Hivi ni kwanini hii yote.
 
Last edited by a moderator:
..........Miaka 2 au 3 iliyopita....... ilikuwa rahisi sana kuamini habari za matukio ukizikuta hapa jamvini........lakini kadiri siku zinavyokwenda ndivyo imani inapozidi kutoweka......Ni vyema tukajaribu kuepuka habari za uzushi na kupakana matope hasa pale tusipokuwa na uhakika nazo.....tuwaachie wengine ambao wako kwa ajili ya habari za aina hiyo..... ni mawazo yangu tu.......

MICHARAZO MITUPU: Aisha Bui akana kukamatwa na 'unga' Brazili, adai yu salama Afrika Kusini


Mkuu Mtanzania1 achana na hizi blog za udaku. Wazazi wake wamekiri ni kweli mtoto wao amekamatwa, pia taarifa zipo kwa Nzowa. Aisha hayupo SA kama unavyotaka kutuaminisha.
 
Last edited by a moderator:
hawa huwa hawakomi. akili zao sijui ziko sehem gani ya mwili. Pamoja na wote hawa kukamatwa bado kuna wengine wanapaki mzigo waanze safari. wengine tayar wapo airport na mzigo.

akili kama za nyumbu wakitaka kuvuka mto, japo wanaona wenzao wanaliwa na mamba ila wengine wataendelea kuingia kwenye maji ya mto ili wavuke. :A S angry:
 
Hizi ndizo akili za nyumbu, wengine wanakufa mtoni nao wanakimbilia hukohuko.
 
Kwa akili yako unadhani suala la madawa ya kulevya ni suala la vyama vya siasa, madawa ya kulenya hayana itikadi.

Well said but sometimes you are unpredictable Mkuu
 
Ndugai karibu anafanikiwa kutekeleza kazi ya kuiua CCM!hivi nyinyi CCM akili zenu zikoje?mbona ni akili ndogo tu kujua kwamba matendo ya Ndugai yanafanya upinzani kukua?hivi amuoni upinzani unavyozidi kupata umaarufu kutokana na matendo ya Ndugai bungeni?hivi nyinyi akili zetu zipo wapi?mbona inakuwa vigumu sana kufikiri!!!!huyu jamaa nadhani ametumwa sio bure!yaani hata hili imekuwa vigumu kuliona jamani?NDUGAI YUPO KAZINI SHAURI YENU
 
Vitumbua havipikwi...
Vitumbua vinachomwa, na siku hizi wanaochoma ni wanaume...


Nasikitika tunahama kwenye mada lakn vitumbua havichomwi...waweza choma mahindi, mihogo, viazi lakini vitumbua vyaweza 'kaangwa' lakini huwezi kuvichoma...ni sawa na wanaosema 'kuchoma' chips????
 
Back
Top Bottom