Madhaifu ya wanyakyusa nilichogundua baada ya kupeleka posa/barua kwa binti wa kinyakyusa

Kuoa sio lele mama vijana, kuna makabila
Mama ndo ana sauti utaenda kila familia ila ndo hivo hivo. Sasa kuoa sio lele mama nenda na mshenga wa hilo kabila usilete ujuaji kwenye ndoa hutaoa. Mimi nilioa mpare posa ilikubaliwa mahari ikakatiliwa na ikapandishwa hapo hapo kwenye tukio. Mama akalia baba akasusa. Mshenga ndio alikaa nao kujadili. Siku hiyo haikufanywa sherehe ilibidi turudi tena siku nyingine mahari ilikataliwa na baba na mashangazi wa binti wamekaza mbele ya familia yangu yote.. wewe ungeweza? Bado kidogo kidume nitoe chozi utoe wapi 2.5 million hapo hapo familia yenyewe Me ndo naitunza unaweza kuanza kuchangisha hapo hela itimie? Ililuwa fedheha. Nenda na mshenga wa hilo
Kabila, mshenga akawakemea kikwao kabisa na kuwashirikisha maisha yetu me na huyo dada ( nilimgharamia sana) baadaye wakaona aibu tukarudi tena hio pesa hatukuitoa. Nenda na mshenga
 
Kwa guu lile kule kwenye uzi ule wala huhitaji kujipigia promo maana we Pisi Kali uliyenona [emoji847]

Ubinadamu ni kazi/Humanity is a work.
Sent from my CPH2387 using JamiiForums mobile app
Siyo guu langu lile mkuu😃😃 acha nijipigie promo mkuu mimi hata siyo pisi kali 🏃‍♀️🏃‍♀️
 
Hebu yataje hayo Makabila yanayopokea mahali ya 30,000/= hadi 50,000/=.

Sent from my V1901A using JamiiForums mobile app
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…