Madhara ya Awamu ya Tano yanayofumbiwa Macho

Madhara ya Awamu ya Tano yanayofumbiwa Macho

Heshima kwako pia Mkuu 🙏🏾. Ngoja tusubiri lakini alipokula kiapo huku akiwa ameshika kitabu kitakatifu cha dini yake na kutamka atailinda na kuitetea Katiba ya nchi halafu huu mwezi wa tatu sasa anajua fika kwamba kuwepo Bungeni kwa COVID-19 ni uvunjwaji wa katiba kwa Wabunge FAKE kuendelea kulipwa billions of taxpayers money na yeye yuko kimya ni UNAFIKI wa hali ya juu kuhusu kwenda kinyume na kiapo chake.
Na wahenga walisema siku njema huonekana asubuhi na asubuhi inazidi kuyoyoma ni 11:00am now she is fast approaching 12 noon.
Tusubiri ila mimi machale YAMESHANICHEZA pamoja na kuwa baadhi ya mambo aliyoyafanya hadi sasa nayafurahia na kuyaunga mkono.



Mkuu BAK heshima kwako tena. Covid 19 bungeni ni ukakasi mkubwa. Ila kumtegemea mama kuwa angelivalia hili njuga dhidi ya Jobo na mhimili wake, itakuwa ni kusubiri dodo kwenye mnazi.

Hili labda tusubiri Chadema itakapokutana naye angalau kusikia maoni yake pamoja na mengi mengine yaliyo fyongo na hata muhimu zaidi.

Wapongezwe Chadema kwa msimamo wao kuhusu wabunge wale. Kwa Chadema wale wamefukuzwa. Si wanachama tena na Chadema haipokei ruzuku kuwahusu wala michango ya wasiokuwa wanachama wake. Kwa hili, kwa mujibu wa Chadema - this is a closed case.

Mawili yafuatayo ni ya muhimu zaidi kwetu kama watanzania:

1. Kushughulikia UVIKO kisayansi - hili ni dharura kweli kweli. Mzee Kaunda ndiyo hivyo tena.
2. Kuhitaji haki kurejelewa - hili lahitaji uwepo wa katiba mpya.

#1 Mama aliteua tume ya wataalamu wabobezi. Na sasa tuko njiani kupata chanjo.

#2. Lisemwalo lipo kama halipo laja. Tumpe mama muda wakati as we reserve our right to push.

Au nasema uongo ndugu zangu?
 
Ila hili la Magufuli na Corona ndio kubwa zaidi,,,kuli dilute itachukua muda sana

Hapa kuna shughuli pevu. Binadamu mjinga brainwashed ni hatari kuliko mbwa:

IMG_20210618_002640_205.jpg
 
Sasa kama si Mama wa kukemea huo uvunjwaji wa Katiba Bungeni na hao COVID-19 na kuusimamisha mara moja ni nani wa kufanya hivyo? Atapiga kimya kwa miaka mitano huku mabilioni ya walipa kodi yakilipwa kwa watu ambao si Wabunge!? Ukimya wake ni ushahidi tosha kwamba na yeye anaufagilia huo uvunjwaji wa katiba.
Mkuu BAK heshima kwako tena. Covid 19 bungeni ni ukakasi mkubwa. Ila kumtegemea mama kuwa angelivalia hili njuga dhidi ya Jobo na mhimili wake, itakuwa ni kusubiri dodo kwenye mnazi.

Hili labda tusubiri Chadema itakapokutana naye angalau kusikia maoni yake pamoja na mengi mengine yaliyofuata na umuhimu zaidi.

Wapongezwe Chadema kwa msimamo wao kuhusu wabunge wale. Kwa Chadema wale wamefukuzwa. Si wanachama tena na Chadema haipokei ruzuku kuwahusu wala michango ya wasiokuwa wanachama wake. Kwa hili, kwa mujibu wa Chadema - this is a closed case.

Mawili yafuatayo ni ya muhimu zaidi kwetu kama watanzania:

1. Kushughulikia UVIKO kisayansi - hili ni dharura kweli kweli. Mzee Kaunda ndiyo hivyo tena.
2. Kuhitaji haki kurejelewa - hili lahitaji uwepo wa katiba mpya.

#1 Mama aliteua tume ya wataalamu wabobezi. Na sasa tuko njiani kupata chanjo.

#2. Lisemwalo lipo kama halipo laja. Tumpe mama muda wakati tu reserve our right to push.

Au nasema uongo ndugu zangu?
 
Kigogo ni vipande gani cha mti unachokiongelea wewe?

Umeona uzi una neno Magufuli ndani yake?

Elimu ni ufunguo wa maisha jombi someni mada na mawazo yaliyo wazi. Siyo kuja na wagombea wenu mifukoni. Hizi si chaguzi za mabwana dhwalimu!
Wote mna Magufulimania siku sio siku kwenu hadi mumtaje. Hata hivyo unaona hamu ya watu kuchangia mashambulizi kwa Magufuli inashuka kila siku ipitayo. Zamani hapa uzi ungekuwa ushakimbia sana. Uzi wako hapa umesogea sababu ya watu wanaokuchalenji sio wanaosapoti ulichoandika.
 
Mama yuko Ikulu miezi mitatu pamoja na kuwa si kipindi kirefu lakini kuna mengi ambayo angestahili kuyamaliza ndani ya kipindi hiki cha miezi mitatu. Kuendelea kwake KUDEMKA kunaonyesha hana nia ya kuleta demokrasi ya kweli nchini. Atagusa gusa hapa na pale na kukutana na makundi ya Watanzania yasiyohusu kitu kwani hayamwambii ukweli husika kisha atachanja mbuga kuelekea 2025 kufanya mwizi mwingine wa kura. Mimi na magufuli ni KITU KIMOJA. Katiba mpya mtasubiri sanaas. I rest my case.
Mpaka sasa hata yeye hajui anafanya nini?
 
Sasa kama si Mama wa kukemea huo uvunjwaji wa Katiba Bungeni na hao COVID-19 na kuusimamisha mara moja ni nani wa kufanya hivyo? Atapiga kimya kwa miaka mitano huku mabilioni ya walipa kodi yakilipwa kwa watu ambao si Wabunge!? Ukimya wake ni ushahidi tosha kwamba na yeye anaufagilia huo uvunjwaji wa katiba.
Ndugai ni mhujumu uchumi no moja
 
Ungekuwa fair japo nusu hekta kama ungejaribu kubaini walau faida moja tu ya awamu ya 5, ambayo kimsingi, kwa yenyewe tu ni bora sana zaidi ya mapokoto ambayo umeyaandika hapa.
Mleta mada ameweka wazi kwamba mada hii ni ya kuangazia madhara hasi (akimaanisha mapungufu) ya awamu ya tano. Kuhusu faida aka misifa anzisha uzi wako.
 
Mleta mada ameweka wazi kwamba mada hii ni ya kuangazia madhara hasi (akimaanisha mapungufu) ya awamu ya tano. Kuhusu faida aka misifa anzisha uzi wako.

Mkuu kwani unadhani ile misungu sungu, boda boda, mipiga debe nk humu haipo?

Hilo jamaa ni moja ya hiyo mijamaa. Mijinga iliyo brainwashed. Haijui inataka nini au haitaki nini. Mama Samia ana kazi kubwa sana ya kuya accommodate pia haya.
 
Wote mna Magufulimania siku sio siku kwenu hadi mumtaje. Hata hivyo unaona hamu ya watu kuchangia mashambulizi kwa Magufuli inashuka kila siku ipitayo. Zamani hapa uzi ungekuwa ushakimbia sana. Uzi wako hapa umesogea sababu ya watu wanaokuchalenji sio wanaosapoti ulichoandika.

Labda kama utakuwa umekuja na mgombea wako mfukoni. Wapi mwendazake katajwa kwenye huu uzi?

Huu uzi uko wazi unahusu madhara ya awamu ya tano kwa awamu ya sita yanayojulikana kuwa ni yote: chanya na hasi.

Huu uzi unaangazia yaliyo hasi kama ambavyo mwingine ungeweza kuangazia yaliyo chanya. Hali kadhalika uzi huu ungeweza kuangazia yaliyo chanya na ukaacha mwingine kuangazia yaliyo hasi.

Kwamba uzi haukimbii? Mafanikio ya nyuzi halisi au zenye maslahi ya taifa, hazipimwi kwa kukimbia. Vinginevyo labda ungejikita zaidi kwenye ule uzi pendwa wa kula matunda kimasikhara wake rikiboy.

Kwamba hatuachi kumtaja mwendazake? Sisi tuliopotezewa wapendwa? Sisi tuliouliwa wapendwa? Sisi tuliojeruhiliwa wapendwa? Nk, nk na bado yeye akiwa madarakani na hakutoa ushirikiano na wewe wataka tusimtaje? You must be kidding.

Kama unategemea kuwa labda karibu sasa tutaacha kumtaja, hakika utakuwa hujui ukisemacho mjomba!

Hiyo ndiyo habari yenyewe. Kama ulikuwa huijui bora ujifunze kuizowea tu.
 
Awamu ya sita imerithi kundi kubwa la wajinga na "the brainwashed to be catered for." Lenye mtizamo hasi katika elimu, sayansi na teknolojia. Kunatakikana jitihada kubwa za dhati na za pamoja katika kuyaweka mambo sawa.
Swadakta
 
Sasa kama si Mama wa kukemea huo uvunjwaji wa Katiba Bungeni na hao COVID-19 na kuusimamisha mara moja ni nani wa kufanya hivyo? Atapiga kimya kwa miaka mitano huku mabilioni ya walipa kodi yakilipwa kwa watu ambao si Wabunge!? Ukimya wake ni ushahidi tosha kwamba na yeye anaufagilia huo uvunjwaji wa katiba.

Mkuu BAK kwa mara nyingine heshima kwako tena.

Wabunge COVID 19 kama yalivyo mengine mengi yaliyo bado fyongo si haki hata kidogo.

Tusubiri Chadema kukutana na mama kupata kauli yake pia, huku tukiendelea kumsaidia kuwa na sauti zaidi, kwa kuwaongezea chagizo mitandaoni na hata kwa zomea zomea tu.

"Kwa hili pongezi kwao bawacha Geita ambao angalau walikabiliana na kipigo cha mbwa koko, japo kwa mkwara wao tu."

Tukumbuke haki na demokrasia hupiganiwa. Hivi havipewi na mtu kwa kupenda. Tusipovipigania hata mama hatatupa!

Kumtegemea Mama kulivalia njuga hili peke yake ndani ya yaliyoelezwa kwenye mada, labda kama tumeamua kusubiria dodo kwenye mnazi, au hata kumtaka naye kuendelea kujishasha kuwa mhimili wake nao, ni ule ule ambao ungali umejichimbia zaidi kuliko mingine.

Au nasema uongo ndugu zangu?
 
  • Nzuri
Reactions: BAK
Kauli mbili za Mama zinafikirisha sana Mkuu. Je, atazitengua kauli hizo kabla ya mwisho wa mwaka huu ili afanye kile Watanzania wengi tunakitaka cha kuwa na chaguzi huru na za haki.
1. Mimi na dhalimu magufuli ni kitu kimoja.
2. Mtasubiri sana Katiba mpya.
Mkuu BAK kwa mara nyingine heshima kwako tena.

Wabunge COVID 19 kama yalivyo mengine mengi yaliyo bado fyongo si haki hata kidogo.

Tusubiri Chadema kukutana na mama kupata kauli yake pia, huku tukiendelea kumsaidia kuwa na sauti zaidi, kwa kuwaongezea chagizo mitandaoni na hata kwa zomea zomea tu.

"Kwa hili pongezi kwao bawacha Geita ambao angalau walikabiliana na kipigo cha mbwa koko, japo kwa mkwara wao tu."

Tukumbuke haki na demokrasia hupiganiwa. Hivi havipewi na mtu kwa kupenda. Tusipovipigania hata mama hatatupa!

Kumtegemea Mama kulivalia njuga hili peke yake ndani ya yaliyoelezwa kwenye mada, labda kama tumeamua kusubiria dodo kwenye mnazi, au hata kumtaka naye kuendelea kujishasha kuwa mhimili wake nao, ni ule ule ambao ungali umejichimbia zaidi kuliko mingine.

Au nasema uongo ndugu zangu?

Cc: Sky Eclat
 
Kauli mbili za Mama zinafikirisha sana Mkuu. Je, atazitengua kauli hizo kabla ya mwisho wa mwaka huu ili afanye kile Watanzania wengi tunakitaka cha kuwa na chaguzi huru na za haki.
1. Mimi na dhalimu magufuli ni kitu kimoja.
2. Mtasubiri sana Katiba mpya.

#1. Mkuu, JPM = Mama, hiyo ni kauli ya mama ambayo haiungwi mkono hata na akina Elitwege, Idugunde, johnthebaptist (hivi sasa hajulikani alipo tokea sabaya akamatwe 😂😂😂😂) nk, SABAYA, bashiri, chakubanga na wengi wengine.

Wote hawa hawako vibaya kwenye hili, kwani matendo huongea zaidi kuliko maneno.

Upewe nini mkuu? Kauli tu?

#2. Mkuu, "mtasubiri sana katiba mpya?!" Kwa hakika hii ni kumnukuu mama ndivyo sivyo. Mama kikamilifu alisema "hili la katiba mpya, hebu tupeane muda kwanza." Mwisho wa kumnukuu.

Roma haikujengwa kwa siku moja. Kupeana muda haina maana kuwa mamandiyo kalipiga chini moja kwa moja. Kwamba mama katamka mwenyewe kuwa "haki huinua taifa," katiba mpya ni sehemu ya haki hizo.

Pamoja na yote jukumu la kupatikana kwa katiba mpya li mikononi mwako, mwangu na kila mmoja anayeihitaji. Tukiamua kulifanya suala hili ni la kufa na kupona kwa vitendo, mbona tarehe ya kuuanza mchakato wake itapatikana kesho tu?

Au nasema uongo ndugu zangu?
 
Ulichoandika ni kweli kabisa Mkuu na Roma hakuijengwa siku moja lakini tayari ni miaka 60 ya Uhuru na miaka 30 ya mfumo ya vyama vingi. Kwanini jambo jema la kuwa na Katiba mpya na Tume huru ya Uchaguzi ambalo litahakikisha chaguzi huru na za haki mpaka tumwage damu? Kwanini tusifanye kwa kuongea tu na kukubaliana na rasimu ya Warioba iko tayari na Warioba na Butiku ambao ni maccm damu damu lakini bado wanapigia debe Katiba mpya na tume huru vilio vyao vidharauliwe ndani ya maccm na Serikali?
 
Ulichoandika ni kweli kabisa Mkuu na Roma hakuijengwa siku moja lakini tayari ni miaka 60 ya Uhuru na miaka 30 ya mfumo ya vyama vingi. Kwanini jambo jema la kuwa na Katiba mpya na Tume huru ya Uchaguzi ambalo litahakikisha chaguzi huru na za haki mpaka tumwage damu? Kwanini tusifanye kwa kuongea tu na kukubaliana na rasimu ya Warioba iko tayari na Warioba na Butiku ambao ni maccm damu damu lakini bado wanapigia debe Katiba mpya na tume huru vilio vyao vidharauliwe ndani ya maccm na Serikali?

Mkuu ninakubaliana nawe kuwa linalowezekana leo lisingoje kesho.

Hata hivyo natamani kuipata picha ya wale sungu sungu waliokuwa Mwanza ili kukupa uelewa halisi wa watu wenyewe na wa madhara hasi ya awamu ile kama yalivyoelezwa kwenye mada. Wa aina hiyo ndiyo walikuwa engine yenyewe ya utawala wa juu wa awamu ya tano.

Hiiiiii bagosha!

Kwa hakika kuyaweka sawa ya watu hawa ambao hata walijazwa ujinga zaidi, mama anauhitaji sana msaada wako vile vile.

Miaka sitini "yes" lakini ni Kikwette aliyeuanzisha single handedly mchakato wa katiba mpya kwenye awamu ya 4. Tusisahau pia kuwa njiani tulipata vyama vingi pia. Bado tusisahau kuna makosa yaliyofanyika kutokea UKAWA kuachia mchakato ule pale ulipokuwa umefikia.

Ikumbukwe UKAWA walikosea kutokutambua kuwa ilikuwa heri ya nusu shari kuliko shari kamili. Natumaini unafahamu mchakato ule ulikwamia wapi.

Hapa ndipo Kamanda mpambanaji anapoeleweka anapojitanabaisha. Tusipigane kijinga. Lazima kutumia akili kuliko wao.

Au nasema uongo ndugu zangu?
 
  • Nzuri
Reactions: BAK
Hakuna sababu ya kupigana kipumbavu lakini ujue kuna vyama njaa ambavyo havitaki kuona mabadiliko ya kweli wao wakinunuliwa kwa mabilioni au vyeo ndani ya Serikali FAKE ya mseto basi huwa upande mmoja na maccm. Nasemea watu kama Zitto na chama chale cha ACT Wazalendo, Mrema na TPL yakr na yule Cheyo. Watu hawa ni watu hatari sana kwani nao wanajifanya ni wapinzani lakini hawana upinzani wowote bali ni wachumia tumbo na waganga njaa na wako taari kufanya lolote lile ili kuikwamisha Chadema.
Mkuu ninakubaliana nawe kuwa linalowezekana leo lisingoje kesho.

Hata hivyo natamani kuipata picha ya wale sungu sungu waliokuwa Mwanza ili kukupa uelewa halisi wa watu wenyewe na wa madhara hasi ya awamu ile kama yalivyoelezwa kwenye mada. Wa aina hiyo ndiyo walikuwa engine yenyewe ya utawala wa juu wa awamu ya tano.

Hiiiiii bagosha!

Kwa hakika kuyaweka sawa ya watu hawa ambao hata walijazwa ujinga zaidi, mama anauhitaji sana msaada wako vile vile.

Miaka sitini "yes" lakini ni Kikwette aliyeuanzisha single handedly kwenye awamu ya 4. Tusisahau pia kuwa njiani tulipata vyama vingi pia. Bado tusisahau kuna makosa yaliyofanyika kutokea UKAWA kuachia mchakato ule pale.

Ikumbukwe UKAWA walikosea kutokutambua kuwa heri ya nusu shari kuliko shari kamili. Natumaini unamfahamu mchakato ule ulikwamia wapi.

Hapa ndipo Mbowe anapoeleweka kama mpambanaji. Tusipigane kijinga. Lazima kutumia akili kuliko wao.

Au nasema uongo ndugu zangu?
 
Hakuna sababu ya kupigana kipumbavu lakini ujue kuna vyama njaa ambavyo havitaki kuona mabadiliko ya kweli wao wakinunuliwa kwa mabilioni au vyeo ndani ya Serikali FAKE ya mseto basi huwa upande mmoja na maccm. Nasemea watu kama Zitto na chama chale cha ACT Wazalendo, Mrema na TPL yakr na yule Cheyo. Watu hawa ni watu hatari sana kwani nao wanajifanya ni wapinzani lakini hawana upinzani wowote bali ni wachumia tumbo na waganga njaa na wako taari kufanya lolote lile ili kuikwamisha Chadema.

Mkuu BAK, wasalitii wapo siku zote na kila mahali. Hawakumpa Mandela shida hao wasitupe taabu sisi pia.

Kamanda wapambanaji wanapoongelea utayari wa kuwasamehe wote watambuao kuwa walikengeuka huko sasa ndiyo kuyaona ipasavyo mapambano sahihi ya kudai haki.

Viongozi wa namna hiyo huwa wamewiva itakuwa kutojitendea haki kutokuwasikiliza makamanda kama hao katika mapambano.

Mandela aliwavumilia kina Buthelezi. Kumbuka hata kamanda mkuu wa majeshi ya ANC, hatari Chris Hani hakuwa kutoka ANC.

Kwenye struggle kuna watu wa aina mbalimbali na wapo mle kwa sababu zao. Kule Afrika Kidini, wengine hata walikuwa wakitaka mbususu za kizungu tu. Wengine wakitaka uhuru tu wa kufika walikokuwa wakitanua wazungu nk. Lakini wote hao wakiunganishwa na kuwa kuiondoa apartheid kwanza kwani ndiyo kilichokuwa msingi wa kila mmoja kupata hitaji la moyo wake.

Tujikite zaidi katika yanayotuunganisha kuliko katika yale yanayotutenganisha. Huo ndiyo ulio wito wa wapambanaji mahali siku zote.

Siku tukiwasoma wapambanaji mahili wa namna hiyo tukaaelewa kikamilifu na kwa vitendo, watasambaratika majahili mmoja baada ya mwingine.

Hiyo ndiyo habari yenyewe.
 
Back
Top Bottom