Madhara ya Kuwadharau Watumishi wa Mungu

Madhara ya Kuwadharau Watumishi wa Mungu

Setfree

JF-Expert Member
Joined
Dec 25, 2024
Posts
1,679
Reaction score
2,123
Kuwadharau Watumishi wa Mungu ni kosa linaloweza kuleta madhara makubwa kwa mtu binafsi na jamii. Biblia inatufundisha kwamba Watumishi wa Mungu wameteuliwa kutangaza Habari Njema na kuwaongoza watu katika njia ya haki. Kuwadharau ni sawa na kupinga kazi ya Mungu, jambo linaloweza kuleta laana badala ya baraka.

Katika historia ya Biblia, wale waliowadharau Watumishi wa Mungu walikumbwa na matatizo makubwa. Mfano mzuri ni Waisraeli waliopuuza maonyo ya manabii na hatimaye wakaangukia katika adhabu.

Hii hapa ni mifano mingine ya watu waliowadharau watumishi wa Mungu na kupata madhara:
  • Miriam na Haruni (Hesabu 12:1-10). Miriam na Haruni walimdhihaki Musa kwa sababu ya mke wake Mkushi na kuhoji “Je! Ni kweli BWANA amenena na Musa tu?” Mungu aliwakasirikia, na Miriam alipatwa na ukoma hadi Musa alipomuombea.

  • Vijana waliomdhihaki Elisha (2 Wafalme 2:23-24). Kuna vijana walimdhihaki nabii Elisha wakimwita "kipara." Elisha aliwalaani kwa jina la Bwana, na dubu wawili wakatoka msituni na kuwaua vijana arobaini na wawili.

  • Kora, Dathani na Abiramu (Hesabu 16:1-35). Watu hawa walimwasi Musa na Haruni wakidai kwamba kila mtu alikuwa mtakatifu na kwamba Musa hakustahili kuwaongoza. Mungu aliifunua ardhi, ikawameza Kora na wafuasi wake, na moto kutoka mbinguni ukawateketeza wengine.

  • Gehazi (2 Wafalme 5:20-27). Gehazi, mtumishi wa nabii Elisha, alimdanganya Naamani kwa tamaa ya mali, kinyume na maagizo ya bwana wake. Kwa sababu hiyo, alilaaniwa na akapigwa na ukoma uliokuwa juu ya Naamani.

  • Mfalme Uzia (2 Mambo ya Nyakati 26:16-21). Mfalme Uzia alikosa heshima kwa Mungu na makuhani kwa kuingia hekaluni kufukiza uvumba, jambo lililokuwa jukumu la makuhani pekee. Mungu alimwadhibu papo hapo kwa kumpiga kwa ukoma, na alitengwa hadi kifo chake.

  • Anania na Safira(Matendo ya Mitume 5:1-11). Kisa cha Anania na Safira ni mfano mwingine wa madhara ya kuwadharau watumishi wa Mungu. Anania na mke wake Safira walimdanganya Mtume Petro kuhusu kiasi cha fedha walichopata baada ya kuuza shamba. Walimdanganya si Petro tu, bali Roho Mtakatifu. Kwa dharau yao dhidi ya mamlaka ya Mtumishi wa Mungu na uongo wao mbele za Mungu, wote wawili walianguka chini na kufa mara moja.

  • Namkumbuka ndugu mmoja katika nchi fulani aliyemdharau Mtumishi wa Mungu. Akawa anapanga kwenda Mahakamani kumfungulia kesi. Alipatwa na ajali mbaya sana na mipango yake haikuendelea.
Biblia inatufundisha kwamba hata kumdharau tu mwenzako ni dhambi(Mithali 11:12). Kwa mantiki hiyo, ni hatari zaidi kuwadharau Watumishi wa Mungu.

“Mpeni kila mtu haki yake; mtu wa ushuru, ushuru; wa kodi, kodi; na astahiliye heshima, heshima.”( Warumi 13:7 BHN).

Let those who immerse themselves in the message of this thread apprehend its profound and weighty significance, that they may not be ensnared by the subtle machinations of folly, thereby precipitating upon themselves the inescapable and irrevocable consequences of their deliberate and reckless disregard
.
 
Mtumishi Naomba tenda niwatengenee hii sanamu mnaloliomba toba na baraka nitatengenezea kwa bei rahisi mtalipia tu mifuko miwili ya cement na kokoto kidogo
downloadfile.png
 
sahihi kabisa ulichosema
tujikumbushe haya
afrika kabla ya ukoloni haikuwa na dini isipokuwa dini ilikuwa wanahubiri mizimu ya kwao na walifanikiwa
baada ya nchi nyingi za ulaya kuanza kutafuta malighafi ndio wakaja huku afrika wakawakuta babu zetu wakiwa na shida na wakaleta dini.
baada ya kuleta dini ndio tukaanza kuona makanisa makubwa makubwa huku wachungaji wakiwa matajiri kupindukia waumini wakiwa maskini kupindukia wanauziwa mafuta.maji,mchanga na kokote pamoja na kuwekewa kiwango cha sadaka huku makanisa yakifanya biashara kubwa wakati waumini hawafaidiki na biashara hizo japo sadaka wanatoa wamejengewa shule huku ada zikiwa kubwa hata hawawezi kusomesha hizo shule hofu na sheria kali zikiwa zimewekwa kwa kanisa upande wa sadaka na zaka
je ulaya ambako dini imetokea kuna haya mpaka majina yakaletwa unashindwa kuita jina la ukoo unaita jina la uzungu wakati wao huwezi ukasikia mtu anaitwa majina yetu
 
sahihi kabisa ulichosema
tujikumbushe haya
afrika kabla ya ukoloni haikuwa na dini isipokuwa dini ilikuwa wanahubiri mizimu ya kwao na walifanikiwa
baada ya nchi nyingi za ulaya kuanza kutafuta malighafi ndio wakaja huku afrika wakawakuta babu zetu wakiwa na shida na wakaleta dini.
baada ya kuleta dini ndio tukaanza kuona makanisa makubwa makubwa huku wachungaji wakiwa matajiri kupindukia waumini wakiwa maskini kupindukia wanauziwa mafuta.maji,mchanga na kokote pamoja na kuwekewa kiwango cha sadaka huku makanisa yakifanya biashara kubwa wakati waumini hawafaidiki na biashara hizo japo sadaka wanatoa wamejengewa shule huku ada zikiwa kubwa hata hawawezi kusomesha hizo shule hofu na sheria kali zikiwa zimewekwa kwa kanisa upande wa sadaka na zaka
je ulaya ambako dini imetokea kuna haya mpaka majina yakaletwa unashindwa kuita jina la ukoo unaita jina la uzungu wakati wao huwezi ukasikia mtu anaitwa majina yetu
Duh, comment yako ina "points" kama tatu, lakini zote hazihusiani na uzi huu. Unaonaje uki-post uzi maalum wa hayo uliyoongea?
 
Kazi ya mjoli wa Mungu akidharauliwa ni moja tu nayo ni kukung'uta mavumbi miguuni pake.... Kinachofuata ni kilio na kusaga meno
 
Hapo unazungumzia watumishi halali wa Mungu Sio hawa wanaouza mafuta na udongo na wanaohamasisha kupanda mbegu kwa kutumia pesa.
Ikiwa kuwatukana hawa matapeli waliotapakaa kila mahali wakigawa wokovu kwa kuuza,kuwatukana tu haitoshi inatakiwa wakatwe vichwa.
 
Kuwadharau Watumishi wa Mungu ni kosa linaloweza kuleta madhara makubwa kwa mtu binafsi na jamii. Biblia inatufundisha kwamba Watumishi wa Mungu wameteuliwa kutangaza Habari Njema na kuwaongoza watu katika njia ya haki. Kuwadharau ni sawa na kupinga kazi ya Mungu, jambo linaloweza kuleta laana badala ya baraka.

Katika historia ya Biblia, wale waliowadharau Watumishi wa Mungu walikumbwa na matatizo makubwa. Mfano mzuri ni Waisraeli waliopuuza maonyo ya manabii na hatimaye wakaangukia katika adhabu.

Hii hapa ni mifano mingine ya watu waliowadharau watumishi wa Mungu na kupata madhara:
  • Miriam na Haruni (Hesabu 12:1-10). Miriam na Haruni walimdhihaki Musa kwa sababu ya mke wake Mkushi na kuhoji “Je! Ni kweli BWANA amenena na Musa tu?” Mungu aliwakasirikia, na Miriam alipatwa na ukoma hadi Musa alipomuombea.

  • Vijana waliomdhihaki Elisha (2 Wafalme 2:23-24). Kuna vijana walimdhihaki nabii Elisha wakimwita "kipara." Elisha aliwalaani kwa jina la Bwana, na dubu wawili wakatoka msituni na kuwaua vijana arobaini na wawili.

  • Kora, Dathani na Abiramu (Hesabu 16:1-35). Watu hawa walimwasi Musa na Haruni wakidai kwamba kila mtu alikuwa mtakatifu na kwamba Musa hakustahili kuwaongoza. Mungu aliifunua ardhi, ikawameza Kora na wafuasi wake, na moto kutoka mbinguni ukawateketeza wengine.

  • Gehazi (2 Wafalme 5:20-27). Gehazi, mtumishi wa nabii Elisha, alimdanganya Naamani kwa tamaa ya mali, kinyume na maagizo ya bwana wake. Kwa sababu hiyo, alilaaniwa na akapigwa na ukoma uliokuwa juu ya Naamani.

  • Mfalme Uzia (2 Mambo ya Nyakati 26:16-21). Mfalme Uzia alikosa heshima kwa Mungu na makuhani kwa kuingia hekaluni kufukiza uvumba, jambo lililokuwa jukumu la makuhani pekee. Mungu alimwadhibu papo hapo kwa kumpiga kwa ukoma, na alitengwa hadi kifo chake.

  • Anania na Safira(Matendo ya Mitume 5:1-11). Kisa cha Anania na Safira ni mfano mwingine wa madhara ya kuwadharau watumishi wa Mungu. Anania na mke wake Safira walimdanganya Mtume Petro kuhusu kiasi cha fedha walichopata baada ya kuuza shamba. Walimdanganya si Petro tu, bali Roho Mtakatifu. Kwa dharau yao dhidi ya mamlaka ya Mtumishi wa Mungu na uongo wao mbele za Mungu, wote wawili walianguka chini na kufa mara moja.

  • Namkumbuka ndugu mmoja katika nchi fulani aliyemdharau Mtumishi wa Mungu. Akawa anapanga kwenda Mahakamani kumfungulia kesi. Alipatwa na ajali mbaya sana na mipango yake haikuendelea.
Biblia inatufundisha kwamba hata kumdharau tu mwenzako ni dhambi(Mithali 11:12). Kwa mantiki hiyo, ni hatari zaidi kuwadharau Watumishi wa Mungu.

“Mpeni kila mtu haki yake; mtu wa ushuru, ushuru; wa kodi, kodi; na astahiliye heshima, heshima.”( Warumi 13:7 BHN).

Let those who immerse themselves in the message of this thread apprehend its profound and weighty significance, that they may not be ensnared by the subtle machinations of folly, thereby precipitating upon themselves the inescapable and irrevocable consequences of their deliberate and reckless disregard
.
Adhabu ya kumtega na kumuangusha kwenye dhambi ya uzinzi baba mchungaji ni ipi?
 
Sema siku hizi kuna watumishi wanaojiita watu wa Mungu ila matendo yao yanatia shaka na kupelekea kupungua kwa heshima kwa watumishi wa Mungu halisia.
 
Let those who immerse themselves in the message of this thread apprehend its profound and weighty significance, that they may not be ensnared by the subtle machinations of folly, thereby precipitating upon themselves the inescapable and irrevocable consequences of their deliberate and reckless disregard.
Vijana wenzangu, nasisitiza👆soma tena.
========


Well said

Mungu ni mkubwa siku zote.
 
Mbona mimi sijazungumzia hiyo sanamu? Acha uchokozi, mkuu
Mimi nimeizungumzia kwasababu nimeona fursa kuwa wewe ni mtumishi na unahitaji sanamu kwaajili ya kuombea toba
 
Sijasoma andiko lote mkuu,ila nataka unithibitishie madhara ya moja kwa moja na mfano hai kwa mtu aliyewadharau watumishi wa Mungu wako hapa duniani, usinitajie walioko biblia manake hao ni wakusadikika hata wewe hauwajui na hakuna uthibitisho wowote kuwa walikuwepo.

twende kazi.
 
holoholo
wananchi wa kule Brazil walipigwa mafuriko baada ya kufanya tamasha la kumdhihaki na kumtukana Mungu.

Chadwick Boseman wa Black Panther aliigiza movie ambayo ndani yake alimtukana Mungu kwa dakika kadhaa matusi mazitomazito yuko wapi leo.

Marilyn Monroe aliugua akafatwa na watumishi wa Mungu amkubali kristo na aiponye nafsi yake akasema hata huyo Mungu wenu hawezi kunisaidia yu wapi leo.

Wataalamu wa Titanic walijinadi kuwa kwa uimara wa meli yao hata Mungu hawezi kuizamisha iko wapi leo.
 
holoholo
wananchi wa kule Brazil walipigwa mafuriko baada ya kufanya tamasha la kumdhihaki na kumtukana Mungu.

Chadwick Boseman wa Black Panther aliigiza movie ambayo ndani yake alimtukana Mungu kwa dakika kadhaa matusi mazitomazito yuko wapi leo.

Marilyn Monroe aliugua akafatwa na watumishi wa Mungu amkubali kristo na aiponye nafsi yake akasema hata huyo Mungu wenu hawezi kunisaidia yu wapi leo.

Wataalamu wa Titanic walijinadi kuwa kwa uimara wa meli yao hata Mungu hawezi kuizamisha iko wapi leo.
mkuu unafikiria kuwa watu wa Titanic wasingemtukana Mungu wako wangekuwepo hadi leo? kama jibu ni hapana basi kumbe kufa kupo tu hata kama wewe ni mtumishi wa Mungu kiasi gani utakufa tu.
 
mkuu unafikiria kuwa watu wa Titanic wasingemtukana Mungu wako wangekuwepo hadi leo? kama jibu ni hapana basi kumbe kufa kupo tu hata kama wewe ni mtumishi wa Mungu kiasi gani utakufa tu.
Kufa kupo lakini inategemea unakufaje
Heri wafu wafao katika Bwana tangu sasa
 
Siwezi heshimu mtu wa aina hii mimi. Hizo laana acha zije tu.
 

Attachments

  • 820af33a57db4b439d2bca9197e012ad.mp4
    6.1 MB
Back
Top Bottom