Madhara ya Kuwadharau Watumishi wa Mungu

Madhara ya Kuwadharau Watumishi wa Mungu

Kufa kupo lakini inategemea unakufaje
Heri wafu wafao katika Bwana tangu sasa
Mkuu, unaamini wote walimokuwepo kwenye meli ya titanic wote walimtukana Mungu? kuna wengine walikuwa wafuasi wa Mungu wako ila mbona walikufa? nini kiliwafanya wafe katika makosa ambayo si yao,na kwa mtizamo wako ni kwamba wote waliokuwemo ndani ya titanic walimtukana Mungu wako jambo ambalo si kweli.
 
holoholo
wananchi wa kule Brazil walipigwa mafuriko baada ya kufanya tamasha la kumdhihaki na kumtukana Mungu.

Chadwick Boseman wa Black Panther aliigiza movie ambayo ndani yake alimtukana Mungu kwa dakika kadhaa matusi mazitomazito yuko wapi leo.

Marilyn Monroe aliugua akafatwa na watumishi wa Mungu amkubali kristo na aiponye nafsi yake akasema hata huyo Mungu wenu hawezi kunisaidia yu wapi leo.

Wataalamu wa Titanic walijinadi kuwa kwa uimara wa meli yao hata Mungu hawezi kuizamisha iko wapi leo.
wanasiasa wa afrika wanaofuja mali za umma hawamdhihaki mungu?

kunyanyasa wanyonge sio kumdhihaki mungu? mbona hawafi?

mnaokota visa tu, na vingi ni vya kutunga.

na inashangaza sana huyo mungu anajali kuhusu jina lake tu, hajali watu wake.

"hofu ya mungu" eti ni kitu kizuri.
 
Kuwadharau Watumishi wa Mungu ni kosa linaloweza kuleta madhara makubwa kwa mtu binafsi na jamii. Biblia inatufundisha kwamba Watumishi wa Mungu wameteuliwa kutangaza Habari Njema na kuwaongoza watu katika njia ya haki. Kuwadharau ni sawa na kupinga kazi ya Mungu, jambo linaloweza kuleta laana badala ya baraka.

Katika historia ya Biblia, wale waliowadharau Watumishi wa Mungu walikumbwa na matatizo makubwa. Mfano mzuri ni Waisraeli waliopuuza maonyo ya manabii na hatimaye wakaangukia katika adhabu.

Hii hapa ni mifano mingine ya watu waliowadharau watumishi wa Mungu na kupata madhara:
  • Miriam na Haruni (Hesabu 12:1-10). Miriam na Haruni walimdhihaki Musa kwa sababu ya mke wake Mkushi na kuhoji “Je! Ni kweli BWANA amenena na Musa tu?” Mungu aliwakasirikia, na Miriam alipatwa na ukoma hadi Musa alipomuombea.

  • Vijana waliomdhihaki Elisha (2 Wafalme 2:23-24). Kuna vijana walimdhihaki nabii Elisha wakimwita "kipara." Elisha aliwalaani kwa jina la Bwana, na dubu wawili wakatoka msituni na kuwaua vijana arobaini na wawili.

  • Kora, Dathani na Abiramu (Hesabu 16:1-35). Watu hawa walimwasi Musa na Haruni wakidai kwamba kila mtu alikuwa mtakatifu na kwamba Musa hakustahili kuwaongoza. Mungu aliifunua ardhi, ikawameza Kora na wafuasi wake, na moto kutoka mbinguni ukawateketeza wengine.

  • Gehazi (2 Wafalme 5:20-27). Gehazi, mtumishi wa nabii Elisha, alimdanganya Naamani kwa tamaa ya mali, kinyume na maagizo ya bwana wake. Kwa sababu hiyo, alilaaniwa na akapigwa na ukoma uliokuwa juu ya Naamani.

  • Mfalme Uzia (2 Mambo ya Nyakati 26:16-21). Mfalme Uzia alikosa heshima kwa Mungu na makuhani kwa kuingia hekaluni kufukiza uvumba, jambo lililokuwa jukumu la makuhani pekee. Mungu alimwadhibu papo hapo kwa kumpiga kwa ukoma, na alitengwa hadi kifo chake.

  • Anania na Safira(Matendo ya Mitume 5:1-11). Kisa cha Anania na Safira ni mfano mwingine wa madhara ya kuwadharau watumishi wa Mungu. Anania na mke wake Safira walimdanganya Mtume Petro kuhusu kiasi cha fedha walichopata baada ya kuuza shamba. Walimdanganya si Petro tu, bali Roho Mtakatifu. Kwa dharau yao dhidi ya mamlaka ya Mtumishi wa Mungu na uongo wao mbele za Mungu, wote wawili walianguka chini na kufa mara moja.

  • Namkumbuka ndugu mmoja katika nchi fulani aliyemdharau Mtumishi wa Mungu. Akawa anapanga kwenda Mahakamani kumfungulia kesi. Alipatwa na ajali mbaya sana na mipango yake haikuendelea.
Biblia inatufundisha kwamba hata kumdharau tu mwenzako ni dhambi(Mithali 11:12). Kwa mantiki hiyo, ni hatari zaidi kuwadharau Watumishi wa Mungu.

“Mpeni kila mtu haki yake; mtu wa ushuru, ushuru; wa kodi, kodi; na astahiliye heshima, heshima.”( Warumi 13:7 BHN).

Let those who immerse themselves in the message of this thread apprehend its profound and weighty significance, that they may not be ensnared by the subtle machinations of folly, thereby precipitating upon themselves the inescapable and irrevocable consequences of their deliberate and reckless disregard
.
Watumishi gani hao? Nabii Tito
 
Adhabu ya kumtega na kumuangusha kwenye dhambi ya uzinzi baba mchungaji ni ipi?
Sijui kama nimeelewa vizuri swali lako.
Kama unamaanisha mwanamke anayeweka mtego ili Mchungaji aanguke na kuzini na huyo mwanamke, basi adhabu ya huyo mwanamke ni ile ile watakayopata wazinzi:
Ufunuo 21:8 BHN
"Lakini waoga, wasioamini, wapotovu, wauaji, wazinzi, wachawi, waabudu sanamu, na waongo wote, mahali pao patakuwa ndani ya lile ziwa linalowaka moto na madini ya kiberiti; hicho ndicho kifo cha pili.”

Kama ni mwanaume ameweka mtego huo ili Mchungaji anaswe kwenye uzinzi, adhabu ya mwanaume huyo inaweza pia kuwa kubwa kuliko hii wanayostahili wanaowakosesha wadogo wanaoamini:
Lakini mtu yeyote atakayemkosesha mmoja wa hawa wadogo wanaoniamini, ingekuwa afadhali afungiwe shingoni jiwe kubwa la kusagia, akatupwe katika kilindi cha bahari." (Mathayo 18:6).
 
Watumishi gani hao? Nabii Tito
Watumishi wa Mungu ni wale wanaozifuata nyayo za Yesu Kristo.

Paulo anasema katika 1 Kor 11:1
Mnifuate mimi kama mimi ninavyomfuata Kristo.

Ni rahisi kuwatambua Watumishi wanaomfuata Yesu Kristo.
Mathayo 7:16-20 BHN
"Mtawatambua kwa matendo yao. Je, watu huchuma zabibu katika miti ya miiba, au tini katika mbigili? La! Basi, mti mzuri huzaa matunda mazuri, na mti mbaya huzaa matunda mabaya. Mti mzuri hauwezi kuzaa matunda mabaya, wala mti mbaya hauwezi kuzaa matunda mazuri."
 
kudharau si ndio kutokutii? au mimi sijaelewa
mfano kuna mtumishi wa Mungu huko daslam aliwaambia mhame maana kuna mafuriko yataizamisha daslam yote
mbona hamkumtii? maana mlimdharau mtumishi wa Mungu
 
kudharau si ndio kutokutii? au mimi sijaelewa
mfano kuna mtumishi wa Mungu huko daslam aliwaambia mhame maana kuna mafuriko yataizamisha daslam yote
mbona hamkumtii? maana mlimdharau mtumishi wa Mungu
Duh, hapo tena inabidi turudi darasa la kwanza tujifunze Kiswahili:

Kudharau na kutokutii ni maneno yenye maana zinazokaribiana lakini maana hizo hazifanani:
  • Kudharau ni hali ya kutoonyesha heshima au kutojali thamani ya kitu au mtu. Ni hali ya kuona jambo fulani au mtu sio wa maana au sio muhimu. Mfano: Anawadharau wazazi wake.
  • Kutokutii ni hali ya kukosa kutii amri, maagizo, au sheria. Ni kufanya kinyume cha kile unachoamriwa au kuelezwa. Mfano: Mtoto alikataa kutii agizo la wazazi wake.
Mtu anaweza kutokutii bila kudharau, yaani kama hatimizi maagizo lakini bado ana heshima kwa anayemwamuru. Vilevile, mtu anaweza kudharau bila kutokutii, yaani, anaweza kutekeleza amri, maagizo, au sheria sio kwa sababu anamheshimu aliyetoa maagizo, bali kwa sababu analazimika kufanya hivyo kwa sababu fulani, kama vile hofu ya adhabu, matarajio ya faida, au kushinikizwa na mazingira. Tuko pamoja?
 
Kumuita binadamu mwenzio 'mtumishi wa mungu' ni dalili za matatizo ya afya ya akili, kwa sifa anazopewa mungu sidhani kama anahitaji mtumishi
Kuna tofauti kubwa kati ya Mtumishi wa Mungu na mtumishi wa mungu.
Unamzungumzia nani. Mungu au mungu? Tuanzie hapo kwanza.
 
Duh, hapo tena inabidi turudi darasa la kwanza tujifunze Kiswahili:

Kudharau na kutokutii ni maneno yenye maana zinazokaribiana lakini maana hizo hazifanani:
  • Kudharau ni hali ya kutoonyesha heshima au kutojali thamani ya kitu au mtu. Ni hali ya kuona jambo fulani au mtu sio wa maana au sio muhimu. Mfano: Anawadharau wazazi wake.
  • Kutokutii ni hali ya kukosa kutii amri, maagizo, au sheria. Ni kufanya kinyume cha kile unachoamriwa au kuelezwa. Mfano: Mtoto alikataa kutii agizo la wazazi wake.
Mtu anaweza kutokutii bila kudharau, yaani kama hatimizi maagizo lakini bado ana heshima kwa anayemwamuru. Vilevile, mtu anaweza kudharau bila kutokutii, yaani, anaweza kutekeleza amri, maagizo, au sheria sio kwa sababu anamheshimu aliyetoa maagizo, bali kwa sababu analazimika kufanya hivyo kwa sababu fulani, kama vile hofu ya adhabu, matarajio ya faida, au kushinikizwa na mazingira. Tuko pamoja?
Mtu hatii lakini hadharau 🤔🤔🤔
"Ole wenu Mafarisayo wanafiki"
mahala fulani Yesu aliwahi kusema hilo
 
Mtu hatii lakini hadharau 🤔🤔🤔
"Ole wenu Mafarisayo wanafiki"
mahala fulani Yesu aliwahi kusema hilo
Unashangaa kauli hiyo?
Yamkini hata wewe hutii maagizo ya Yesu lakini haumdharau Yesu, unakubali kuwa ni Mwokozi.
 
Wote kwa pamoja
Mimi nimezungumzia watumishi wa Mungu, sio wa mungu. Watumishi wa Mungu ndio wanaostahili kuheshimiwa.

Unashangaa mwanadamu mwenzako kuitwa Mtumishi wa Mungu? Ina maana hujasoma hata Andiko hili? Kutoka 14:31 SRUV
"Israeli akaiona ile kazi kubwa aliyoifanya BWANA juu ya Wamisri, ndipo hao watu wakamcha BWANA, wakamwamini BWANA, na Musa mtumishi wake."
 
  • Thanks
Reactions: Cyb
Mimi nimezungumzia watumishi wa Mungu, sio wa mungu. Watumishi wa Mungu ndio wanaostahili kuheshimiwa.

Unashangaa mwanadamu mwenzako kuitwa Mtumishi wa Mungu? Ina maana hujasoma hata Andiko hili? Kutoka 14:31 SRUV
"Israeli akaiona ile kazi kubwa aliyoifanya BWANA juu ya Wamisri, ndipo hao watu wakamcha BWANA, wakamwamini BWANA, na Musa mtumishi wake."
Mimi nimesema binadamu wanaoita binadamu wenzao ‘watumishi/mtumishi wa Mungu/mungu’ wana viashiria vya matatizo ya afya ya akili
 
Mimi nimesema binadamu wanaoita binadamu wenzao ‘watumishi/mtumishi wa Mungu/mungu’ wana viashiria vya matatizo ya afya ya akili
Kinachokushangaza ni nini hapo? Mtumishi wa Mungu ni mtu anayemtumikia Mungu. Unataka tumwiteje?
 
  • Thanks
Reactions: Cyb
Back
Top Bottom