Madhara ya Kuwadharau Watumishi wa Mungu

Madhara ya Kuwadharau Watumishi wa Mungu

Kuwadharau Watumishi wa Mungu ni kosa linaloweza kuleta madhara makubwa kwa mtu binafsi na jamii. Biblia inatufundisha kwamba Watumishi wa Mungu wameteuliwa kutangaza Habari Njema na kuwaongoza watu katika njia ya haki. Kuwadharau ni sawa na kupinga kazi ya Mungu, jambo linaloweza kuleta laana badala ya baraka.

Katika historia ya Biblia, wale waliowadharau Watumishi wa Mungu walikumbwa na matatizo makubwa. Mfano mzuri ni Waisraeli waliopuuza maonyo ya manabii na hatimaye wakaangukia katika adhabu.

Hii hapa ni mifano mingine ya watu waliowadharau watumishi wa Mungu na kupata madhara:
  • Miriam na Haruni (Hesabu 12:1-10). Miriam na Haruni walimdhihaki Musa kwa sababu ya mke wake Mkushi na kuhoji “Je! Ni kweli BWANA amenena na Musa tu?” Mungu aliwakasirikia, na Miriam alipatwa na ukoma hadi Musa alipomuombea.

  • Vijana waliomdhihaki Elisha (2 Wafalme 2:23-24). Kuna vijana walimdhihaki nabii Elisha wakimwita "kipara." Elisha aliwalaani kwa jina la Bwana, na dubu wawili wakatoka msituni na kuwaua vijana arobaini na wawili.

  • Kora, Dathani na Abiramu (Hesabu 16:1-35). Watu hawa walimwasi Musa na Haruni wakidai kwamba kila mtu alikuwa mtakatifu na kwamba Musa hakustahili kuwaongoza. Mungu aliifunua ardhi, ikawameza Kora na wafuasi wake, na moto kutoka mbinguni ukawateketeza wengine.

  • Gehazi (2 Wafalme 5:20-27). Gehazi, mtumishi wa nabii Elisha, alimdanganya Naamani kwa tamaa ya mali, kinyume na maagizo ya bwana wake. Kwa sababu hiyo, alilaaniwa na akapigwa na ukoma uliokuwa juu ya Naamani.

  • Mfalme Uzia (2 Mambo ya Nyakati 26:16-21). Mfalme Uzia alikosa heshima kwa Mungu na makuhani kwa kuingia hekaluni kufukiza uvumba, jambo lililokuwa jukumu la makuhani pekee. Mungu alimwadhibu papo hapo kwa kumpiga kwa ukoma, na alitengwa hadi kifo chake.

  • Anania na Safira(Matendo ya Mitume 5:1-11). Kisa cha Anania na Safira ni mfano mwingine wa madhara ya kuwadharau watumishi wa Mungu. Anania na mke wake Safira walimdanganya Mtume Petro kuhusu kiasi cha fedha walichopata baada ya kuuza shamba. Walimdanganya si Petro tu, bali Roho Mtakatifu. Kwa dharau yao dhidi ya mamlaka ya Mtumishi wa Mungu na uongo wao mbele za Mungu, wote wawili walianguka chini na kufa mara moja.

  • Namkumbuka ndugu mmoja katika nchi fulani aliyemdharau Mtumishi wa Mungu. Akawa anapanga kwenda Mahakamani kumfungulia kesi. Alipatwa na ajali mbaya sana na mipango yake haikuendelea.
Biblia inatufundisha kwamba hata kumdharau tu mwenzako ni dhambi(Mithali 11:12). Kwa mantiki hiyo, ni hatari zaidi kuwadharau Watumishi wa Mungu.

“Mpeni kila mtu haki yake; mtu wa ushuru, ushuru; wa kodi, kodi; na astahiliye heshima, heshima.”( Warumi 13:7 BHN).

Let those who immerse themselves in the message of this thread apprehend its profound and weighty significance, that they may not be ensnared by the subtle machinations of folly, thereby precipitating upon themselves the inescapable and irrevocable consequences of their deliberate and reckless disregard
.
Mwampo naye yumo?
 
Ni lazima kuwadharau kwa kuwa wanawadanganya watu watoe sadaka ili wao washibishe matumbo yao. Tena wengine wanatumia nguvu za giza, kupata umati wa watu wanaokusikiliza ni lazima ushirikina utumike.
 
Kuwadharau Watumishi wa Mungu ni kosa linaloweza kuleta madhara makubwa kwa mtu binafsi na jamii. Biblia inatufundisha kwamba Watumishi wa Mungu wameteuliwa kutangaza Habari Njema na kuwaongoza watu katika njia ya haki. Kuwadharau ni sawa na kupinga kazi ya Mungu, jambo linaloweza kuleta laana badala ya baraka.

Katika historia ya Biblia, wale waliowadharau Watumishi wa Mungu walikumbwa na matatizo makubwa. Mfano mzuri ni Waisraeli waliopuuza maonyo ya manabii na hatimaye wakaangukia katika adhabu.

Hii hapa ni mifano mingine ya watu waliowadharau watumishi wa Mungu na kupata madhara:
  • Miriam na Haruni (Hesabu 12:1-10). Miriam na Haruni walimdhihaki Musa kwa sababu ya mke wake Mkushi na kuhoji “Je! Ni kweli BWANA amenena na Musa tu?” Mungu aliwakasirikia, na Miriam alipatwa na ukoma hadi Musa alipomuombea.

  • Vijana waliomdhihaki Elisha (2 Wafalme 2:23-24). Kuna vijana walimdhihaki nabii Elisha wakimwita "kipara." Elisha aliwalaani kwa jina la Bwana, na dubu wawili wakatoka msituni na kuwaua vijana arobaini na wawili.

  • Kora, Dathani na Abiramu (Hesabu 16:1-35). Watu hawa walimwasi Musa na Haruni wakidai kwamba kila mtu alikuwa mtakatifu na kwamba Musa hakustahili kuwaongoza. Mungu aliifunua ardhi, ikawameza Kora na wafuasi wake, na moto kutoka mbinguni ukawateketeza wengine.

  • Gehazi (2 Wafalme 5:20-27). Gehazi, mtumishi wa nabii Elisha, alimdanganya Naamani kwa tamaa ya mali, kinyume na maagizo ya bwana wake. Kwa sababu hiyo, alilaaniwa na akapigwa na ukoma uliokuwa juu ya Naamani.

  • Mfalme Uzia (2 Mambo ya Nyakati 26:16-21). Mfalme Uzia alikosa heshima kwa Mungu na makuhani kwa kuingia hekaluni kufukiza uvumba, jambo lililokuwa jukumu la makuhani pekee. Mungu alimwadhibu papo hapo kwa kumpiga kwa ukoma, na alitengwa hadi kifo chake.

  • Anania na Safira(Matendo ya Mitume 5:1-11). Kisa cha Anania na Safira ni mfano mwingine wa madhara ya kuwadharau watumishi wa Mungu. Anania na mke wake Safira walimdanganya Mtume Petro kuhusu kiasi cha fedha walichopata baada ya kuuza shamba. Walimdanganya si Petro tu, bali Roho Mtakatifu. Kwa dharau yao dhidi ya mamlaka ya Mtumishi wa Mungu na uongo wao mbele za Mungu, wote wawili walianguka chini na kufa mara moja.

  • Namkumbuka ndugu mmoja katika nchi fulani aliyemdharau Mtumishi wa Mungu. Akawa anapanga kwenda Mahakamani kumfungulia kesi. Alipatwa na ajali mbaya sana na mipango yake haikuendelea.
Biblia inatufundisha kwamba hata kumdharau tu mwenzako ni dhambi(Mithali 11:12). Kwa mantiki hiyo, ni hatari zaidi kuwadharau Watumishi wa Mungu.

“Mpeni kila mtu haki yake; mtu wa ushuru, ushuru; wa kodi, kodi; na astahiliye heshima, heshima.”( Warumi 13:7 BHN).

Let those who immerse themselves in the message of this thread apprehend its profound and weighty significance, that they may not be ensnared by the subtle machinations of folly, thereby precipitating upon themselves the inescapable and irrevocable consequences of their deliberate and reckless disregard
.
wacha watukanwe wengi wamekuwa matapeli
 
Ni lazima kuwadharau kwa kuwa wanawadanganya watu watoe sadaka ili wao washibishe matumbo yao. Tena wengine wanatumia nguvu za giza, kupata umati wa watu wanaokusikiliza ni lazima ushirikina utumike.
Kimaandiko, sio sahihi kumdharau mtu yeyote, hata Mtumishi wa Mungu anayeenda kinyume na mapenzi ya Mungu(Mithali 14:21).

Daudi hakumdharau Mfalme Sauli hata wakati Sauli alipokuwa amepotoka na kumfuatilia kwa uovu.
1 Samweli 24:6 SRUV
"Daudi akawaambia watu wake, Hasha! Nisimtendee bwana wangu, masihi wa BWANA, neno hili, kuunyosha mkono wangu juu yake, kwa maana yeye ni masihi wa BWANA."

Mtume Paulo alipotambua Petro amekwenda kinyume na injili, hakumdharau bali alimkemea ana kwa ana (Wagalatia 2:11-14).

Maandiko hayo yanatufundisha kwamba kama Mtumishi wa Mungu anapotosha mafundisho au anaishi maisha yasiyompendeza Mungu, hatupaswi kumdharau bali tunapaswa kumuonya kwa staha, upendo na hekima ili kumrejesha kwenye njia sahihi.

Na kama ni Mtumishi wa Mungu mzee, yaani anayekuzidi umri, usimkemee bali umuonye kama baba (1 Timotheo 5:1-2).

Hayo ndiyo mapenzi ya Mungu katika eneo hilo.
 
wacha watukanwe wengi wamekuwa matapeli
Usiwaunge mkono wanaowatukana. Kutukana ni dhambi.
Wakolosai 3:8
"Bali sasa yawekeni haya yote mbali nanyi, hasira, ghadhabu, uovu, matukano, matusi vinywani mwenu."
 
Back
Top Bottom