Uchaguzi 2020 Madiwani wa CHADEMA waliohamia CCM ,wapukutishwa Arusha

Uchaguzi 2020 Madiwani wa CHADEMA waliohamia CCM ,wapukutishwa Arusha

Takribani madiwani 20 wa chadema waliojiunga ccm kuunga juhudi za Rais Magufuli wameangukia pua kwenye kura za maoni huku eti wakidai wamehujumiwa na wajumbe.

Hatua hiyo imedhihirisha wazi kwamba wenye ccm yao wapo na sio wahamiaji kama walivyopigwa mweleka kwenye kura za maoni na wengi wao wakiambulia kura moja na sifuri.
Wajumbe sio watu wazuri.
 
Takribani madiwani 20 wa chadema waliojiunga ccm kuunga juhudi za Rais Magufuli wameangukia pua kwenye kura za maoni huku eti wakidai wamehujumiwa na wajumbe.

Hatua hiyo imedhihirisha wazi kwamba wenye ccm yao wapo na sio wahamiaji kama walivyopigwa mweleka kwenye kura za maoni na wengi wao wakiambulia kura moja na sifuri.
Maaama yanguuu aliniambiyaaa utavuna ulichopandaaaa pararaaa papaaa[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]
 
Hili si lakucheka sana huo bado ni ushindi kwa ccm kwasababu majimbo hayo tunaweza kusema tayari yapo mikonini mwa ccm
Poa tu,ni heri ccm kuliko hawa wasaliti kushinda,kupigwa chini kwa wasaliti inapungua ari ya kuhama na kusaliti vyama vyao
 
Tamaa ya fisi...waache wajiambishe!! Wajumbe hongereni sana kwa kazi nzur kukomesha rushwa za waziwazi walizokula hawa jamaa!!
 
WAJUMBE SIYO WATU,NI NYOKA WA NDIMI TATU.Nashauri kwa Ngazi za maamuzi ziteue Mjumbe miongoni mwa waliopata sifuri ndo jina lirudi ili iwe fundisho kwa wimbi la WATOA RUSHWA na WALA RUSHWA WAO@wajumbe.Vinginevyo wenye pesa wataendelea na mchezo huu milele.
 
Takribani madiwani 20 wa chadema waliojiunga ccm kuunga juhudi za Rais Magufuli wameangukia pua kwenye kura za maoni huku eti wakidai wamehujumiwa na wajumbe.

Hatua hiyo imedhihirisha wazi kwamba wenye ccm yao wapo na sio wahamiaji kama walivyopigwa mweleka kwenye kura za maoni na wengi wao wakiambulia kura moja na sifuri.
Wajumbe wako sahihi .
Hawawezi kumpa kura mtu aliyewatukana na kikitukana Chama chao kwa miaka nenda rudi eti Leo wamerudi kwa sababu ya Rushwa ya fedha na madaraka ndio wapewe kura.

Wajumbe wamewatumbua majipu yanayopenda Rushwa ya madaraka.
Wamerudi CCM na kuacha Ubunge kwa ahadi ya kupewa majimbo au uteuzi.
Hii ni Rushwa ya ahadi ya madaraka.

Waliotoka upinzani kwa ahadi ya uteuzi hawafai kamwe mana ni wapenda Rushwa.
Mtu msafi kabisa anaweza kukaa ndani ya Chama bila Madaraka.
Kuhama Chama au kujiunga na Chama kwa sababu ya ahadi ya madaraka ni Rushwa.

Watanzania wote tuwaunge mkono wajumbe wa CCM kwa kukomesha vitendo vya Rushwa ya fedha na madaraka.

Hili suala la Rushwa ya madaraka limeharibu sio tu vyama kama taasisi Bali hata taasisi za umma zimekosa watu wenye maadili na kujikuta watu wanakiuka katina na sheria za utumishi wa umma kwa sababu ya kukimbila uteuzi na kuahidiwa kupitishwa kwa kupewa ushindi wa mezani.
Hii ikiacha italeta utendaji uliogubikwa na ubinafsi wa mtu kujipendekeza kwa malengo ya kupata uteuzi bila kufuata sheria.
Mtu anaajiriwa kama Mhandishi badala ya kufanya kazi yake ya uhandishi yeye anafanya kazi za Chama cha siasa wakati kila Chama kina watendaji wake wanaolipwa kwa kazi hiyo.

Naipongeza sana serikali kwa kuamua kukaa mbali na hao watu wanaojipendekeza kwa Rushwa ya madaraka na fedha. Huu ni ubinafsi bora wakatwe wakae pembeni ili watafutwe watu waliopigania Chama katika shida na raha. Sio waone Chama kinafanya vizuri ndio wanajiuza kwa kutamani uteuzi ambao ni kwa ajili ya wenye Chama na sio wavamizi ambao hawako tayari kukaa bila madaraka.
Kwao Umuhimu wa CCM sio Sera wala itikadi Bali ni madaraka na uteuzi
 
Waende wakafanye issue nyingine kama hawana waende Lumumba hawatakosa kazi hata za kusafisha choo.
Sio wanachama hao ni wasaka madaraka.
Hii nchi hatuwezi kutumia kodi za wananchi kuwalipa wanasiasa mamilioni halafu hawana hata shukrani zaidi ya kutamani madaraka makubwa tuu huku hospitali zikikosa madaktari na madawa. Walimu wana mishahara midogo na kazi ngumu lakini wanafanya kazi zao mwaka mzima sembuse hawa wasaka madaraka wanaohama hama vyama kutafuta nafasi zile zile walizoziacha kwa kutoa matusi na kuwatukana wapiga kura waliowachagua
 
Takribani madiwani 20 wa chadema waliojiunga ccm kuunga juhudi za Rais Magufuli wameangukia pua kwenye kura za maoni huku eti wakidai wamehujumiwa na wajumbe.

Hatua hiyo imedhihirisha wazi kwamba wenye ccm yao wapo na sio wahamiaji kama walivyopigwa mweleka kwenye kura za maoni na wengi wao wakiambulia kura moja na sifuri.
Ndiyo matunda ya wanasiasa uchwara hununuliwa kirahisi nakuuzwa pia 'cheap politicians are easily bought and sold'
 
Kama watafuata maoni kama haya basi wanakwenda kujifelisha wenyewe kwa sababu wajumbe wanaopiga kura ni wakaazi wa maeneo husika, ni vipi chama kirudi tena kuwahoji wananchi? Demokrasia imeongea usipoikubali subiri sanduku la kura.
Hakuna anaesikitisha kama yule aliyekuwa Meya wa Jiji la Arusha Calisti Lazaro. Aibu tupu.
Tamaaaaa ni mbaya !!
Hasa tamaa ya madaraka!!
 
WAJUMBE SIYO WATU,NI NYOKA WA NDIMI TATU.Nashauri kwa Ngazi za maamuzi ziteue Mjumbe miongoni mwa waliopata sifuri ndo jina lirudi ili iwe fundisho kwa wimbi la WATOA RUSHWA na WALA RUSHWA WAO@wajumbe.Vinginevyo wenye pesa wataendelea na mchezo huu milele.
Kuna mawili,wapo waliotumia rushwa kupita na ambao hawajatumia,sasa wanapomchukua aliyepata ziro kama rushwa haikutumika ina maana hapendwi,heri rushwa kuzibitiwa kuliko kuwapitisha waliopata zero
 
Nyumbani ni nyumbani, wameshakatwa mikia inawapasa kuomba msamaha na kurudi ktk zizi walilokulia. Hii inadhihirisha jambo tu, ya kuwa nje ya CDM wao si chochote kile, walifikia mafanikio kwa kupitia nyota ya CDM, kitu ambacho Polepole alikitumia ktk kuiharibu kesho yao ya maisha yao ya kisiasa.

Bado wana muda wa kuweza ku "retaliate" na hata kupeleka "demage" kwa kuilipa ghiliba iliyofanyika kwao vilevile. Rudini kundini hata kwa kisingizio mlikwenda kimkakati na kufanya "intelligence" ndani ya mahasimu wenu wakuu wa kisiasa.
 
Hili si lakucheka sana huo bado ni ushindi kwa ccm kwasababu majimbo hayo tunaweza kusema tayari yapo mikonini mwa ccm
Sidhani kama ni hivyo. Tuseme hao Wapinzani waliounga juhudi au waliokatwa ndio awali walikua wakikubalika.

So Hawa waliopitishwa Sasa hawakukubalika awali ndio maana hawakuwa madiwani. Conclusively hawa waliopitishwa sasa kama ndio wale wa 2015 wataendelea kuangukia pua tu.
 
Hapo ndipo ninapoiipa CCM heko
Heko kwa kututilia adabu hawa vitimba kwiri na vizabi zabina wa siasa.
Wakafie mbele hukoooo.
Malaya wakubwa wa siasa , wakitafuta sifa na mlo.
Sas tuwaone kama kweli wanamuunga mkono Magu ,wabakie benchi wampigie makofi mpaka 2025 wakiwa chini ya chama wakishiriki harakati mbali mbali za kuijenga CCM itakayokuwa mahututi baada ya Uchaguzi wa 2020.
Wakibaki hadi 2025 ndani ya CCM tutawaaminikweli wanaunga mkono JUHUDI za JIWE
Ujumbe huu umfikie aliekua Mbunge wa Momba Bw. David Silinde
 
Kosa kubwa ni kutokujua kuwa; Mtu hawezi kuwa mkubwa kuliko chama chake. Waliupata udiwani wakiwa cdm iweje ugeuke njiani? Waliokuchagua ndo wamekuomba ugeuke?
 
Takribani madiwani 20 wa chadema waliojiunga ccm kuunga juhudi za Rais Magufuli wameangukia pua kwenye kura za maoni huku eti wakidai wamehujumiwa na wajumbe.

Hatua hiyo imedhihirisha wazi kwamba wenye ccm yao wapo na sio wahamiaji kama walivyopigwa mweleka kwenye kura za maoni na wengi wao wakiambulia kura moja na sifuri.
Ukila vya watuu ukumbuke pia kwamba iko siku utaliwaaa kwa hiyoo wameliwa wao siwalikula vilivyo haramu
CCM OYEEEEEEEEE CCM Oyeeeeeeeeee
Chama kikubwa hiki kuna wanamkakati kama sisi kama wanaweza warudi walikotokaaaaa
Chama Dume CCM
CHAMA KONGWE BARANI AFRIKA NA DUNIANI KOTEE
 
Back
Top Bottom