Madudu ukaguzi maalum wa CAG upande wa REA 2015-2020

Madudu ukaguzi maalum wa CAG upande wa REA 2015-2020

UKAGUZI wa Ufanisi wa Mamlaka ya Nishati Vijijini (REA) uliofanywa na CAG umeimulika REA kuanzia mwaka 2015/2016 mpaka 2019/2020.

Ukaguzi umefanyika kwa maombi ya wafadhili; Shirika la Kimataifa la Maendeleo Sweden (Sida).

Kwamba Machi 2016, Tanzania na Sida waliingia mkataba wa ufadhili wa kutandaza umeme vijijini. Fedha zilitoka SEK 600 milioni (Sh133 bilioni).

Uzembe wa kuchelewa kupakua malighafi Bandari ya Dar, ulisababisha REA watumie Sh775.76 milioni kulipa tozo ya uchelewaji (demurrage charge). Fedha za ufadhili zikatumika ndivyo sivyo kwa uzembe.

CAG amebaini kuwa transfoma zilizofungwa uwezo wake ni 50KV, wakati bajeti ilikuwa 100KV. Fedha za wafadhili zilipigwa cha juu.

Upembuzi yakinifu haukufanyika. Hata udongo haukupimwa. Nguzo zimewekwa pasipo vipimo. Pesa ya upembuzi yakinifu (feasibility study), imepigwa.

Wateja 51,425 tu kati ya 98,689 walioomba kuunganishiwa umeme, ndio wameungabishiwa. Hiyo ni sawa na asilimia 52.1.

CAG ameandika; nyaraka za Sida zinaonesha REA walitakiwa kusambaza umeme kwenye nyumba 86,000, hivyo kuhudumia watu 430,000 kupitia gridi ndogo (Green Min and Micro Grid). Wameishia nyumba 17,302, yaani asilimia 20.

Uzembe wa kutohuisha taarifa za utafiti wa mradi, ulisababisha REA kuingia gharama za ziada Sh160 milioni.

Kuna jumla ya Sh5.94 bilioni, ambazo REA wamekuwa wakizitenga kama bajeti ya matangazo na elimu lakini hakuna maelezo ya zilivyotumika.

Mwaka 2018/2019, REA walitengeneza bajeti ya kununua transfoma na kuunganishia wateja umeme Sh254.8 bilioni. CAG akagundua, gharama halisi ilikuwa Sh117 bilioni. Kwa hiyo kulikuwa na udanganyifu wa Sh137.8 bilioni. Ufisadi.

Lingine, REA wilitumia Sh125.57 milioni, kununua transfoma 12 zilizo chini ya kiwango.

Siasa zikaingia. Tozo ya umeme kwa mwezi ikapitishwa Sh11,000. Serikali ikasema tozo Sh1,000. Gharama za uendeshaji zikawa kubwa kuliko mapato. Umeme ukazima vijijini.

Sehemu kubwa, CAG ameeleza tatizo la uchelewaji. Miradi ambayo ilipaswa kukamilika mwaka 2019/2020, mpaka sasa bado.

Hayo yalitokea Waziri wa Nishati akiwa Kalemani, aliyempokea Simbachawene kutoka kwa Muhongo. Rais simtaji. Hamkawii kusema namchukia John.

Ndimi Luqman MALOTO
Walinda Legasi ngoja kama nawaona hv [emoji12][emoji12][emoji12]
 
Katika miaka 6 ya Magufuli amesambaza vijiji vingi na umeme wa bei nafuu kuliko marais wote tanganyika mpaka nyumba za nyasi ziliwekewa umeme, wakati kabla ya Magufuli ulikuwa ukiwasha umeme unaoneka bonge la tajiri, Sasahivi tumerudi kulekule kama una kuanzia sh,350,000 hauwezi pata umeme kutoka elfu 29.Magufuli amuwezi kimchafua kizembezembe kazi zake alizozifanya bado zinamtangaza, kipindi cha Magufuli hadi dawasco walikuwa unafungiwa maji bure unaanza kulipa taratibu, Sasahivi kajaribu uone.Magufuli hata hatungiwe riport namna hipi tulioshudia tawala zilizopita hatuelewi hayo maripoti.
Hachafuliwi weee [emoji1][emoji23][emoji23] acha uoga
 
Inasikitisha sana... Mambo ya serikali ndivyo yalivyo...
 
Ukitaka kujua kuwa huyu CAG ni jipu basi ni pale anapoongelea vitu unavyovifahamu kwa undani, watu wataonewa bure kwakua ripoti ya huyu bwana inachukuliwa kama msahafu wakati imejaa utumbo kibao. Kwamba ufunge transfoma za 100 kVA kila mahali regardless ya idadi ya watumiaji?? Alafu distribution lines ziwe na urefu kiasi gani?
Sasa kwa nini kwenye makadirio wa quote tuu za 100kVa wakati walijua na ndogo zitahitajika.
 
UKAGUZI wa Ufanisi wa Mamlaka ya Nishati Vijijini (REA) uliofanywa na CAG umeimulika REA kuanzia mwaka 2015/2016 mpaka 2019/2020.

Ukaguzi umefanyika kwa maombi ya wafadhili; Shirika la Kimataifa la Maendeleo Sweden (Sida).

Kwamba Machi 2016, Tanzania na Sida waliingia mkataba wa ufadhili wa kutandaza umeme vijijini. Fedha zilitoka SEK 600 milioni (Sh133 bilioni).

Uzembe wa kuchelewa kupakua malighafi Bandari ya Dar, ulisababisha REA watumie Sh775.76 milioni kulipa tozo ya uchelewaji (demurrage charge). Fedha za ufadhili zikatumika ndivyo sivyo kwa uzembe.

CAG amebaini kuwa transfoma zilizofungwa uwezo wake ni 50KV, wakati bajeti ilikuwa 100KV. Fedha za wafadhili zilipigwa cha juu.

Upembuzi yakinifu haukufanyika. Hata udongo haukupimwa. Nguzo zimewekwa pasipo vipimo. Pesa ya upembuzi yakinifu (feasibility study), imepigwa.

Wateja 51,425 tu kati ya 98,689 walioomba kuunganishiwa umeme, ndio wameungabishiwa. Hiyo ni sawa na asilimia 52.1.

CAG ameandika; nyaraka za Sida zinaonesha REA walitakiwa kusambaza umeme kwenye nyumba 86,000, hivyo kuhudumia watu 430,000 kupitia gridi ndogo (Green Min and Micro Grid). Wameishia nyumba 17,302, yaani asilimia 20.

Uzembe wa kutohuisha taarifa za utafiti wa mradi, ulisababisha REA kuingia gharama za ziada Sh160 milioni.

Kuna jumla ya Sh5.94 bilioni, ambazo REA wamekuwa wakizitenga kama bajeti ya matangazo na elimu lakini hakuna maelezo ya zilivyotumika.

Mwaka 2018/2019, REA walitengeneza bajeti ya kununua transfoma na kuunganishia wateja umeme Sh254.8 bilioni. CAG akagundua, gharama halisi ilikuwa Sh117 bilioni. Kwa hiyo kulikuwa na udanganyifu wa Sh137.8 bilioni. Ufisadi.

Lingine, REA wilitumia Sh125.57 milioni, kununua transfoma 12 zilizo chini ya kiwango.

Siasa zikaingia. Tozo ya umeme kwa mwezi ikapitishwa Sh11,000. Serikali ikasema tozo Sh1,000. Gharama za uendeshaji zikawa kubwa kuliko mapato. Umeme ukazima vijijini.

Sehemu kubwa, CAG ameeleza tatizo la uchelewaji. Miradi ambayo ilipaswa kukamilika mwaka 2019/2020, mpaka sasa bado.

Hayo yalitokea Waziri wa Nishati akiwa Kalemani, aliyempokea Simbachawene kutoka kwa Muhongo. Rais simtaji. Hamkawii kusema namchukia John.

Ndimi Luqman MALOTO
Habithi laamal wewe, paper on table currently is 2021/2022
 
Ukitaka kujua kuwa huyu CAG ni jipu basi ni pale anapoongelea vitu unavyovifahamu kwa undani, watu wataonewa bure kwakua ripoti ya huyu bwana inachukuliwa kama msahafu wakati imejaa utumbo kibao. Kwamba ufunge transfoma za 100 kVA kila mahali regardless ya idadi ya watumiaji?? Alafu distribution lines ziwe na urefu kiasi gani?
Usijifanye mjuaji wakati umeandika pumba tu. Kama usemavyo ni kweli kwanini wapange bajeti ya transform za 100kv kisha wanunue za 50kv? Huoni hoja ya mleta mada hapo au umejitoa ufahamu kwa mapenzi yako kwa legacy?
 
Usijifanye mjuaji wakati umeandika pumba tu. Kama usemavyo ni kweli kwanini wapange bajeti ya transform za 100kv kisha wanunue za 50kv? Huoni hoja ya mleta mada hapo au umejitoa ufahamu kwa mapenzi yako kwa legacy?
Umewahi kufanya kazi ya kuandaa specifications za mradi wowote?? Acha kubisha vitu usivyovijua. Anayeandaa hizo specs hata mahali hizo transfoma zitafungwa hapajui, kwa kifupi ni makadirio matupu ili upate figures ya kuweka kwenye bajeti.
 
Usijifanye mjuaji wakati umeandika pumba tu. Kama usemavyo ni kweli kwanini wapange bajeti ya transform za 100kv kisha wanunue za 50kv? Huoni hoja ya mleta mada hapo au umejitoa ufahamu kwa mapenzi yako kwa legacy?
BTW ni 'kVA' sio 'kv' 🤣
 
Umewahi kufanya kazi ya kuandaa specifications za mradi wowote?? Acha kubisha vitu usivyovijua. Anayeandaa hizo specs hata mahali hizo transfoma zitafungwa hapajui, kwa kifupi ni makadirio matupu ili upate figures ya kuweka kwenye bajeti.
Usitetee ufisadi hapa. Kama fedha zilizotolewa ni za 100kv, badala yake zikanunuliwa za 50kv bila kuonesha salio, huo ni Ufisadi. Sijui unabisha nini hapa.
 
Usitetee ufisadi hapa. Kama fedha zilizotolewa ni za 100kv, badala yake zikanunuliwa za 50kv bila kuonesha salio, huo ni Ufisadi. Sijui unabisha nini hapa.
Unajua hizo za 50 kVA zilinunuliwa ngapi badala ya zile za 100 kVA??
 
Sasa tukuamini wewe au tumwamini CAG aliyeenda field kufanya ukaguzi?
Huyo ni mbishi tuu hana lolote eti anasema "yalikuwa ni makadirio matupu ili upate figures ya (za) kuweka kwenye budget".What a contradiction.
 
Tukianzia hapo tufanye na 2015-2010 ili tumkamate yule mwizi na genge lake.
 
UKAGUZI wa Ufanisi wa Mamlaka ya Nishati Vijijini (REA) uliofanywa na CAG umeimulika REA kuanzia mwaka 2015/2016 mpaka 2019/2020.

Ukaguzi umefanyika kwa maombi ya wafadhili; Shirika la Kimataifa la Maendeleo Sweden (Sida).

Kwamba Machi 2016, Tanzania na Sida waliingia mkataba wa ufadhili wa kutandaza umeme vijijini. Fedha zilitoka SEK 600 milioni (Sh133 bilioni).

Uzembe wa kuchelewa kupakua malighafi Bandari ya Dar, ulisababisha REA watumie Sh775.76 milioni kulipa tozo ya uchelewaji (demurrage charge). Fedha za ufadhili zikatumika ndivyo sivyo kwa uzembe.

CAG amebaini kuwa transfoma zilizofungwa uwezo wake ni 50KV, wakati bajeti ilikuwa 100KV. Fedha za wafadhili zilipigwa cha juu.

Upembuzi yakinifu haukufanyika. Hata udongo haukupimwa. Nguzo zimewekwa pasipo vipimo. Pesa ya upembuzi yakinifu (feasibility study), imepigwa.

Wateja 51,425 tu kati ya 98,689 walioomba kuunganishiwa umeme, ndio wameungabishiwa. Hiyo ni sawa na asilimia 52.1.

CAG ameandika; nyaraka za Sida zinaonesha REA walitakiwa kusambaza umeme kwenye nyumba 86,000, hivyo kuhudumia watu 430,000 kupitia gridi ndogo (Green Min and Micro Grid). Wameishia nyumba 17,302, yaani asilimia 20.

Uzembe wa kutohuisha taarifa za utafiti wa mradi, ulisababisha REA kuingia gharama za ziada Sh160 milioni.

Kuna jumla ya Sh5.94 bilioni, ambazo REA wamekuwa wakizitenga kama bajeti ya matangazo na elimu lakini hakuna maelezo ya zilivyotumika.

Mwaka 2018/2019, REA walitengeneza bajeti ya kununua transfoma na kuunganishia wateja umeme Sh254.8 bilioni. CAG akagundua, gharama halisi ilikuwa Sh117 bilioni. Kwa hiyo kulikuwa na udanganyifu wa Sh137.8 bilioni. Ufisadi.

Lingine, REA wilitumia Sh125.57 milioni, kununua transfoma 12 zilizo chini ya kiwango.

Siasa zikaingia. Tozo ya umeme kwa mwezi ikapitishwa Sh11,000. Serikali ikasema tozo Sh1,000. Gharama za uendeshaji zikawa kubwa kuliko mapato. Umeme ukazima vijijini.

Sehemu kubwa, CAG ameeleza tatizo la uchelewaji. Miradi ambayo ilipaswa kukamilika mwaka 2019/2020, mpaka sasa bado.

Hayo yalitokea Waziri wa Nishati akiwa Kalemani, aliyempokea Simbachawene kutoka kwa Muhongo. Rais simtaji. Hamkawii kusema namchukia John.

Ndimi Luqman MALOTO
Kwenye wizara hiyo wakati wa Kalemani kulikuwa na ufisadi wa hali ya juu. Kuna watu walipelekewa umeme, mtu mmoja, umbali wa zaidi ya kilometer 20 kwa gharama ya REA, lakini unapelekwa kwenye kabiashara kwa ndugu yake Kalemani. Kabiashara kenyewe, uwekezaji wake haufiki hata shilingi milioni 500.

Waziri alikuwa anacheza na media ili aonekane anafanya kazi sana wakati kwenye uhalisia ilikuwa tofauti. Umeme unapelekwa kwenye kijiji fulani, zinaunganishwa nyumba 2 au 4, waziri anaenda hapo na wanahabari kibao kutangaza tukio la kuwasha umeme kijiji fulani, lakini nyumba zilizounganishwa ni 2 au 4. Halafu timu ya ujenzi inahamia kijiji kingine. Kuna vijiji vingine mpaka leo, licha ya umeme kufika kijijini kwao karibia miaka 5 iliyopita, waliounganishiwa umeme, hawafiki hata 5% japo wameomba muda mrefu.

Kati ya Wizara ambazo efficiency ni very poor, Wizara ya Nishati ni miongoni. Mpaka sasa, hii Wizara haijapata unafuu wowote. Na kati ya mashirika ya hovyo kabisa galiyojaza watu ambao hawafanyi kazi, TANESCO, nadhani ni shirika la kwanza. Muda mwingi wamejazana ofisini, na kubakia wanazungukazunguka lakini hakuna cha maana wanachokifanya.
 
Back
Top Bottom