Madudu ya ajabu ya ubatili wa Katiba yetu, mabadiliko "fake" ya sheria na Tume ya Uchaguzi. Rais Samia asilaumiwe kwasababu yeye sio mwanasheria!

Pascal Mayalla

Platinum Member
Joined
Sep 22, 2008
Posts
53,857
Reaction score
121,995
Wanabodi,

Kama kawaida yangu kila nipatapo fursa, huja na makala zangu za kwa maslahi ya taifa. Makala ya leo ni kuhusu fursa ya kuufanya uchaguzi Mkuu ujao wa Rais, Wabunge, Madiwani na serikali za mitaa utakuwa ni uchaguzi huru na wa haki.

Kwanza tukubaliane katika uendeshaji wa nchi, katiba, sheria, taratibu na kanuni ndio kila kitu.

Tangu tumepata uhuru wetu, nchi yetu Tanzania haijawahi kubahatika kupata rais ambaye ni mwanasheria, hivyo marais wetu wote wanawategemea wanasheria kwenye utengenezaji wa katiba, sheria, taratibu na kanuni, hivyo kukitokea madudu ya ajabu ya kisheria kama ubatili kwenye katiba yetu, rais ambaye sio mwanasheria, hawezi kujua kwasababu anawategemea washauri wake ambao ni wanasheria.

Mtu ambaye sii mwanasheria, hawezi kuujua ubatili wa sheria, atawategemea washauri wake wamwambie kuhusu issues zozote za kikatiba na kisheria, ikitokea hao washauri nao japo ni wanasheria lakini hawajui sheria kikamilifu, ndio wanampotosha rais wetu, ndio maana bandiko hili ni utetezi kwa rais wa JMT Asilaumiwe kwa yanayotokea kwenye issues zote za katiba na sheria kwasababu yeye sio mwanasheria.

Japo kuna huu msemo wa Kiswahili usemao "Mkubwa ni jalala" na "aliyekutwa na ngozi ndiye aliyekula nyama" maadam rais ndio kipo chetu na macho yetu yote tumeyaelekeza kwake, lakini kuna mengine tutakuwa tunamuonea bure!, ndio maana niliwahi kushauri Rais Samia, sio malaika ni binadamu anaweza kukosea. Tusimlaumu, kumshutumu na kumponda kwa makosa ya kukoseshwa. Tumvumilie tumpe muda

Mfano mzuri na mfano hai ni katiba ya Tanzania ya 1977, imenajisiwa kwa kuchomekewa kifungu fulani batili, waliokichomekea kifungu hicho ni Bunge la JMT, aliyeubaini ubatili huo ni Mahakama Kuu ya Tanzania, aliyeulinda ubatili huo ni Mahakama ya Rufani ya JMT, hivyo mpaka hapa ninapozungumza, usikute Rais wa JMT, she is an innocent victim, hajui kuwa katiba ya JMT imenajisiwa kwa ubatili fulani kwasababu wanasheria washauri wake rasmi ni ama hawaujui ubatili huo ama wanaojua lakini hawamwambii ukweli rais wetu, hivyo ikitokea tukaenda kwenye uchaguzi Mkuu wa 2025 bila kuuondoa ubatili huu, mtu wa kulaumiwa sio Rais Samia, kwasababu yeye sio mwanasheria, and after all, tumekuwa tukiendesha chaguzi zetu zote kwa ubatili huu, hivyo taifa letu kujikuta linalaanika kwa adhabu za karma bila kujijua!.

Kwenye ubatili huu ninao uzungumzia hapa, kiukweli kabisa mhimili wa Serikali, Bunge na Mahakama, umetukosea sana Watanzania!.
Katika mihimili hiyo mitatu, ni mhimili wa serikali tuu ndio pekee unapowakosea Watanzania, unaweza kuushitaki mahakamani lakini mhimili wa Bunge na mhimili wa Mahakama, unapowakosea Watanzania, hakuna mahali popote pa kuwashitaki zaidi ya kutegemea huruma ya rais wa JMT pekee. Madudu haya ya ajabu ya kisheria yaliweza kufanyika vipi wakati tuna Wanasheria?

Kama hao wanasheria manguli wabobezi na wabobevu wa sheria ambao rais wa JMT anawategemea wamshauri, ndio hao hao waliotunga sheria batili inayokwenda kinyume cha katiba, na wakaipeleka Bungeni kutungwa kuwa sheria, sasa kunapotokea madudu ya ajabu ya marekebisho ya sheria kama haya yaliyoletwa jana Bungeni, unategemea nini?. Kumlaumu Rais Samia ambaye sii mwanasheria, ni kumuonea bure!.

Tukubali tukatae, Tanzania tuna tatizo kubwa la wanasheria wa ajabu!. Sakata la IGA ya DPW na Bandari ndio limetufungua macho!. Kwa mujibu wa katiba yetu Ile IGA ya DPW na Bandari zetu ni batili!, lakini IGA hiyo, pamoja na ubatili wake wote, bado ilipitishwa na Bunge letu Tukufu hivyo hivyo ilivyo without any reservations!, Japo Bunge Limeridhia, DPW Kuendesha Bandari Zetu, ni Makubaliano Tu, Tukithibisha Kuna Matatizo, Tunarekebisha Mkataba wa HGA, Kazi Nzuri Iendelee! tukauliza "IGA ya DPW imetusaidia sana kujitambua. Tuna wanasheria wa Aina Gani!, Bunge na Serikali yetu, Ilipitishaje IGA Hii? mwisho wa siku hii IGA, iliwekwa pembeni HGA safi ikasainiwa. Sasa unapowategemea wanasheria wa type hii ndio washauri wa sheria na wasaidizi wa Rais Samia, unategemea nini?!. Tusimlaumu kabisa Rais Samia.

Unaweza kufuatilia baadhi ya madudu ya ajabu ya kisheria yaliyofanywa na wanasheria wetu!

Mpaka leo ninapoandika hapa, ubatili huo bado uko ndani ya katiba yetu!. Kwa vile Rais wa JMT sio mwanasheria, tulichofanya akina sisi, ni kumweleza Rais Samia kuwa baadhi ya wanasheria anaowategemea hawamsaidii, hivyo akina sisi tukajitolea kuwa bypass and reach out kumfikia Samia mwenyewe na kumweleza kupitia mitandao ya kijamii na makala magazetini kuwa katiba yetu ni batili!.

Kuhusu huu ubatili kwenye katiba yetu, kama ni kumweleza Rais Samia, tumemweleza sana!.

Kikosi kazi kilipomaliza kazi tumampongeza tukamkumbusha. Pongezi Rais Samia, Serikali, Kukubali Kubadili Sheria ya Uchaguzi, Tume Huru ya Uchaguzi!. Tuanze na Katiba Kwanza Ndipo Sheria Au?.

Wakati hayo yote yakiendelea, tukamsikia Rais Samia akizungumzia haki tukajiuliza Rais Samia ana nia njema Watanzania wapate haki, ila Watanzania hawajui Haki! Je, Tumsaidie kuelimisha umma Katiba, Sheria na Haki au?

Kisha watu tukajitolea kufanya uelimishaji umma kuhusu katiba kupitia vipindi vya TV, Redio, makala magazetini na kwenye mitandao ya kijamii.
View: https://youtu.be/ZJIKhnZCf04?si=ElCUzq4FKy4oiGxP
Nikazungumza na wanasisa mbalimbali wana mategemeo gani kuhusu hali ya siasa, nikatengeneza Vox Populi, kwenye Vox Populi, ukikusanya sauti za wengi, ukaziweka sauti hizo pamoja, sauti hizo haziwi tena ni Vox Populi, zinageuka ni Vox Dei!.

Baada ya Serikali yetu sikivu kukubali italeta mabadiliko ya sheria ya uchaguzi na mabadiliko ya tume ya uchaguzi, tukashauri tena na tena!. Mabadiliko ya Sheria Bila Mabadiliko ya Katiba,Sawa na Kula Bila Kunawa!. Je Watanzania Tuna Haraka Sana na Uchaguzi Hadi Tukimbilie Kula Bila Kunawa?

Hatimaye jana Ijumaa, hiki ndio tukaletewa!. Sisi wa kupongeza tukapongeza Lile fupa lililowashinda marais wanaume 4, rais mwanamke 1 aligegeda kama mlenda!. Miswada 3 ya ukombozi mpya wa taifa letu yatua bungeni asubuhi hii

Kuna watu watamlaumu Rais Samia kwa kuamini ni yeye!, kumbe masikini ya Mungu, sio Rais Samia, yeye sio mwanasheria, hiki kilicholetwa Bungeni jana yaani ile Miswada ni kazi ya washauri wake ambao ni wanasheria. Tujifunze kuwa na Shukrani kwa Madogo ili Tupatiwe Makubwa!. Japo Tulitaka Kikubwa, Tumepewa Kiduchu!, Tukipokee Tushukuru, au Tususe Kudai Kikubwa?.

Sasa kwa vile tunayo miezi 3, ya kujadili na kutoa mapendekezo yetu, nashauri na kuwasisitiza tusimlaumu Rais Samia, wala tusiwalaumu wasaidizi wake, bali tutoe mapendekezo yetu kama tulivyofanya kwenye ile IGA, tukapata HGA nzuri.

Tupendekeze sheria nzuri ya uchaguzi na Tume huru na Shirikishi ya uchaguzi, naamini kabisa Rais Samia ni Rais msikivu na tutasikilizwa na mwisho wa siku tutabadili kwanza katiba kuondoa ubatili, kisha tutaunda Tume Huru na Shirikishi ya Uchaguzi, Tutabadili sheria yetu ya uchaguzi kuleta sheria mzuri ya haki ya uchaguzi ambayo itasawazisha uwanja wa siasa, a level playing field, tutafanya uchaguzi wa Rais, Wabunge, Madiwani na serikali za mitaa, hivyo utafanyika kwa siku moja na utasimamiwa na Tume moja Huru ya Uchaguzi na uchaguzi Mkuu wa 2025 utakuwa ni uchaguzi huru na wa haki!.

Mungu Ibariki Tanzania

Paskali
 
Kaka nn kimetokea? Ni jn tu ulimpamba mh.Rais kwamba amelivunja fupa lililowashinda watangulizi wenzake.
 
Hata hivyo kaka rejea somo lako la state and law kuna kitu kipo mule kinachopelekea haya.
 
Nikushangaa sana jana ukaja unak8mbia kusifia kuwa lile fupa liliwashinda wengi Samia ameliweza. Leo tena unatuambia Samia asilaumiwe. Why?? Kwahiyo ungekuwa na mapendekezo mazuri tumpongeze Samia na ukiwa hovyo km ulivyosema walaumiwe wengine?
 
Ifike mahala tuzionee huruma fedha zetu na pia tujihurumie wenyewe! Hawa maprofesa njaa ambao wanalenga kushibisha matumbo yao tuwakatae kabisa, wanaiangamiza nchi!
 
Taifa hili hata ikaja tokea Rais akawa mwanasheria, bado tutashuhudia sheria za hovyo na aibu kwa taifa, umefika wakati mpaka ni aibu na fedhea kujinasibu kuwa na manguli wa sheria.

Kumpata mtu mwenye taalumu kuhusu jambo fulani hakutoi wasaa wa kufanya vizuri katika nafasi hiyo mfano Rais wa awamu ya tatu BWM(RIP), alikuwa mwandishi wa habari (journalist), lakini hakuwa rafiki wa vyombo vya habari na waandishi, nakumbuka baada ya kifo chake Generali Ulimwengu aliwahi sema kwamba BWM alikuwa akiwadharau waandishi wa habari wazi wazi kwa kadai hawajui Kuzungumza kiingereza.

Pia kipindi cha awamu ya Tano Cha Shujaa JPM(RIP), alikuwa mwanasayansi, lakini kipindi cha Corona au Covid 19, hakutumia kanuni za kisayansi, bali alisisitiza kupiga Nyungu na mtambo uliwekwa hospitali ya taifa ya Muhimbili tena akaenda mbali zaidi mpaka kudai kuwa Papai lina Corona.

Awamu hii ya Sita waziri wa fedha ni nguli katika uchumi na msomi mwenye PhD, lakini ulileta uzi humu kuomba hiyo nafasi wapewe wengine.

Mifano hiyo ni ushaidi kwamba sio kila mwenye taalumu fulani akipewa kitengo katika taaluma hiyo basi atakuwa na utendaji mzuri bali unaweza kuwa wa hovyo.

Kwa madai ya kusema kwamba Rais hapaswi kupewa lawama kwa kuvunja katiba au kusaini sheria zilizo kinyume na katiba kwa kuwa sio mwanasheria hoja hii haina mashiko, maana humu ndani hudai kwamba uraisi ni taasisi hivyo basi taasisi inapo fanya mambo ya hovyo lawama lazima iende kwa mkuu wa taasisi na hii haita jalisha ni nguli katika taalumu hiyo au laa.
 
"Rais asilaumiwe sababu siyo mwanasheria". Wewe jamaa haupo sawa kichwani. Unajua vizazi vyako watakuja kuona maandishi yako huko mbeleni.
 
Ifike mahala tuzionee huruma fedha zetu na pia tujihurumie wenyewe! Hawa maprofesa njaa ambao wanalenga kushibisha matumbo yao tuwakatae kabisa, wanaiangamiza nchi!
Mkuu Mungu yupo, haya nayo yatapita iko siku watalia kilio cha "MBWA" mdomo juu.... Kama Gwajiboy aliapa kwa mbingu na ardhi eti hataki ubunge wala uraisi, unawashangaa hao?!!!!!
 
Sasa Mtu Mwenye Mamlaka Ya Kutia Saini Fulani Anyongwe Yupo Halafu Useme Asilaumiwe
Mbona Asijiuzuru Endapo Anaona Wazi Wazi Mamlaka Ya Juu Kabisa Anayo
Paschal Acha Haya Mambo
 
Kuwa na msimamo basi .
 
Mkuu acha kumtetea huyu maza amekuwa bungeni tangu sijui mwaka 2000 awe hajui kutofautisha kati ya Katiba na Sheria? huyu ni mvivu wa kusoma ndiyo maana mambo mengi anadanganywa, wazanzibari 99% ni wavivu wa kusoma ni watu wa kuambiwa na kuamini pekee.
 
Mzee wa kungata na kupuliza

UchaguZi unaokuja,panapo majaliwa mahudhurio,ushiriki
Ya upigaji kura utakuwa mdogo sana

Ova
 
CCM ni janga la taifa namba moja.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…