Maduka ya dawa Tanzania yanatumika kutuibia, kututesa, kuharibu afya zetu na kutuua?

Maduka ya dawa Tanzania yanatumika kutuibia, kututesa, kuharibu afya zetu na kutuua?

Kwa siku za karibuni hapa JF kuna mjadala mkali sana unaendelea kuhusu taaluma ya ufamasia na maduka ya dawa hapa Tanzania. Kupitia mijadala hiyo, nimejifunza mambo kadhaa ambayo hapo kabla sikuyajua kwa kina. Nimegundua mambo haya:

1. Mtu ili kuanzisha na kuendesha biashara ya duka la dawa, huihitaji uwe ni mfamasia kitaaluma bali unahitaji kukodisha cheti cha mfamasia yoyote na kukitundika kwenye duka lako la dawa, na kuanzia hapo utauza dawa yoyote hata kama elimu yako ni darasa la saba! Hii ni sawa na rubani mwenye leseni ya kurusha ndege za abiria kuikodisha leseni yake kwa kampuni ya ndege ili itundikwe ndani ya ndege, halafu mtu yoyote anaweza kushika usukani wa ndege na kuamua kuirusha ndege!

2. Kumbe wafamasia kitaaluma hawajui (hawakufunzwa) na hawapaswi kumpima mgonjwa (examination), kugundua ugonjwa (diagnosis), kuidhinisha dawa za kutumia (Prescription) au kumtibu mgonjwa kwa dawa (drug administration). Mfamasia anapaswa tu kumgawia mgonjwa dawa (drug dispensing) kwa mujibu wa kibali cha Daktari. Ajabu ni kuwa huku mitaani maduka ya dawa ndio hospitali zisizo rasmi, tukiumwa tunaenda na pesa kwenye duka la dawa na kutibiwa faster!

3. Kiujumla karibu dawa zote hazipaswi kuuzwa na duka lolote la dawa mpaka kibali rasmi cha dawa kutoka kwa Daktari (Prescription). Ajabu ni kuwa huku mtaani dawa yoyote unaweza ukauziwa na duka lolote la dawa ukienda na pesa tu!


Baada ya kupitia hayo yote nimegundua wazi kubwa, kiujumla maduka ya dawa hapa Tanzania huenda kwa sehemu kubwa yanatuibia, kutuumiza, kuharibu afya zetu na kutuua!

Unatakiwa kujifunza zaidi. Inaonekana knowledge gap kwako ni Kubwa Sana Yaani.
 
Kuanzisha pharmacy ni jambo moja na kuendesha pharmacy ni jambo lingine. Mimi mgonjwa ninayefika duka la dawa kununua dawa, cheti cha mfamasia kilichotundikwa kinanisaidia nini?
Umeisoma hiyo Pharmacy ACT ?
 
Kuanzisha pharmacy ni jambo moja na kuendesha pharmacy ni jambo lingine. Mimi mgonjwa ninayefika duka la dawa kununua dawa, cheti cha mfamasia kilichotundikwa kinanisaidia nini?
Wewe ukienda Dukani kununua Bidhaa leseni ya biasharaa inakusaidia nini???
 
1. Mtu ili kuanzisha na kuendesha biashara ya duka la dawa, huihitaji uwe ni mfamasia kitaaluma bali unahitaji kukodisha cheti cha mfamasia yoyote na kukitundika kwenye duka lako la dawa, na kuanzia hapo utauza dawa yoyote hata kama elimu yako ni darasa la saba! Hii ni sawa na rubani mwenye leseni ya kurusha ndege za abiria kuikodisha leseni yake kwa kampuni ya ndege ili itundikwe ndani ya ndege, halafu mtu yoyote anaweza kushika usukani wa ndege na kuamua kuirusha ndege!
Mkuu 'Zanzibar ASP', Samahani, naona hujajifunza chochote hapa bali umekubali kupotoshwa au kuimarisha mawazo potofu uliyokuwa nayo toka mwanzo.

Chukulia mfano wa hilo hapo uliloandika hapo juu.
Niambie, ni sheria gani Tanzania inayoruhusu maduka ya dawa kutumia vyeti vya Famasia bila Famasia kuwa mwangalizi/msimamizi wa shughuli zinazoendelea dukani humo.

Nieleze kwa uhakika ni wapi katika jukwaa hili palipoelezwa hayo uliyoweka hapo juu!

Kama wewe uliona au kusikia kuwa hayo yanafanyika, umejiridhisha kwamba ndio utaratibu ulioruhusiwa na sheria na mamlaka inayosimamia taaluma ya Famasia? Kwa nini ulalamike na kujiapiza kabisa hili "umejifunza" jukwaani hapa? Ni nani katika wachangiaji aliyesema kuwa hivyo ndivyo inavyotakiwa kuwa ndani ya Famasi?
2. Kumbe wafamasia kitaaluma hawajui (hawakufunzwa) na hawapaswi kumpima mgonjwa (examination), kugundua ugonjwa (diagnosis), kuidhinisha dawa za kutumia (Prescription) au kumtibu mgonjwa kwa dawa (drug administration). Mfamasia anapaswa tu kumgawia mgonjwa dawa (drug dispensing) kwa mujibu wa kibali cha Daktari. Ajabu ni kuwa huku mitaani maduka ya dawa ndio hospitali zisizo rasmi, tukiumwa tunaenda na pesa kwenye duka la dawa na kutibiwa faster!
Hili nalo umepotoka, pamoja na kuwa kweli kwamba siyo kazi ya MFamasia kutambua matatizo yanayomhusu mgonjwa. Hii ni kazi ya taaluma nyingine, na hili siku zote linajulikana. Nashanga sana kwamba wewe ndio leo umelifahamu. Wewe tokea utotoni mwako umekuwa huendi kutibiwa hospitali? Uliwahi hata siku moja kwenda Famasi moja kwa moja kupata dawa kabla ya kumwona daktari? Huu ni uongo ulio wazi kabisa kwa malengo uliyonayo mwenyewe, na kujaribu kuhalalisha jambo ambalo hata kama hukulijua, bado hulijui na unajiapiza umejifunza hapa JF.

Hili swala la "Drug administration" linatumika kuwachanganya tu watu.
Drg administration inahusu mgonjwa kumeza, kupaka, kudunga sindano, kuweka machoni au sikioni au sehemu za siri, n.k.

Katika njia zote hizo za kumpa mgonjwa dawa, ni njia chache sana, kama ya kudunga sindano inayohitaji NESI (na kiukweli si daktari), amdunge sindano mgonjwa.
Dawa nyingi nyingine, anayehusika katika ku'administer' dawa ni mgonjwa mwenyewe, baada ya kufahamishwa namna ya matumizi ya dawa aliyopewa, kama vidonge. Kama mgonjwa ni mahututi yupo hospitali, atapewa dawa hizo na nesi. Au kama ni mtoto nyumbani, mama anachukua jukumu la kumpa mtoto dawa kama ilivyoelekezwa.

Sasa hili unalosema Famasia hawezi ku'administer' dawa ni jambo ambalo sio la ukweli, bali ni upotoshaji. Kwa sababu dawa nyingi zaidi ni mgonjwa mwenyewe anaye'administer' na wala siyo daktari.

Lakini tusiishie hapo. Unaposema Famasia hajui ku'adminster' dawa, huo ni uongo, kwa sababu kati ya Daktari, nesi na Famasia, ni Famasia pekee anayejua kwa undani zaidi njia sahihi inayofaa kwa mgonjwa kutumia dawa, kwa kumeza, au kuweka machoni, au kuweka kwenye ngozi, n.k., kwa sababu yeye anaifahamu vizuri zaidi dawa

Kuepuka kuandika kirefu sana, ngoja nikwambie hili la mwisho:

Unapoona daktari akiandika dawa, usidhani daktari huyo kila kitu kipo kichwani mwake. Katika kutibu kuna "GUIDELINES", taratibu zinazotakiwa kufuatwa, na katika kila ugonjwa kuna dawa zake maalum zilizoainishwa zitumike. Kwa hiyo usidhani daktari anajua kila nittygritty ya kila kitu katika matibabu hayo. Katika upande wa dawwa, ukimchuka Famasia na Daktari kawaweka uwanjani na kuwapa maswali nje ya "GUIDELINES" utakuta daktari haendi mbali..

Hayo mengine ya huko chini ya upotoshaji bado sijayasoma.
Lakini bandiko lako hapa ni mwendelezo ule ule wa watu wenye maslahi, maslahi ambayo yameguswa, sasa wanageukia taaluma husika na kuanza kuwatupia lawama.
Ndiyo, kuna lawama stahiki, kama hizo za kutumia vyeti kwenye Famasi bila Famasia mwenyewe kuwepo hapo mahala. Lakini hili ni kosa, kama makosa mengine yanayofanywa, tena zaidi upande huo unaolilia kwamba ni wajuaji zaidi wa dawa kuliko watu waliosomea fani wenyewe.

Sikuhakiki andiko hili, kama kuna makosa, kunradhi.
 
Kiufupi hizo ndio tiba tunazopata huku Mtaani kwetu, na kwenda kwa mbele kwa "Wataalamu" ni kujilipua tu....kwa hiyo kufunga maduka labda mtatusaidia kukimbilia kwa kina Mwampesa, GwaJuma and co...wao Magonjwa yote wanatutibu kwa kutoa tu sadaka elfu kumi au ishirini.
LOooh,
Hili la mkasa ulioueleza hapa lilikuwa halijaingia akilini mwangu kabisa.

Ahsante sana kwa kunifungua macho.

Sasa nimeelewa vizuri maana ya kampeni hii dhidi ya Famasi.

Ahsante sana mkuu 'May Day', kwa kuueleza mkasa huu.

Hii ni vita ya kibiashara, tena biashara haramu?
 
Ilikuwa hadi wapate mafunzo ya ADDO kwanza ndipo wanaruhusiwa kuyamiliki na kuuza.

Pia watu ambao walikuwa hawana elimu ya afya walikuwa wanapatiwa mafunzo ya ADDO ya umiliki wa DLDM na walipaswa kuweka mtu anayeweza kuuza ambaye anazitambua dawa.

Sasa ADDO imesinamishwa ndio unaona kelele zote hizi.

Hata hivyo hizi kelele ni kama njia tu, agenda kubwa hapa ni suala la maslahi tu kwenye hii Business of Pharmacy. Imeonekana Wafamasia wanafaidi sana kwenye hii business yao
Nilihisi tu kuna jambo juu ya kelele hizi nyingi na za ajabu sana.

Now I know.
 
Kule
Tuanze kwanza, kuna wangapi wameherabiwa afya na kuuwawa na hayo maduka ya dawa unayoyaongelea? Kuna takwimu zilizokusanywa? Serikali ikikurupuka na kuyabana maduka ya dawa inaweza kuleta matatizo tena haswa kwa wale watu wenye kipato cha chini. Gharama zitaongezeka kwa sababu urasimu unaongozeka.
Maeneo ya kijijini kwetu kuna mtu amefariki ndo amezikwa jana Mungu amlaze mahali pema peponi. Kisa tu alienda duka la dawa wakamuuzia dawa akarudi home kumbe tatizo lake ilibidi akae wodini hata siku mbili coz Sugar ilikua juu na Bp ilikua juu
 
Kwa siku za karibuni hapa JF kuna mjadala mkali sana unaendelea kuhusu taaluma ya ufamasia na maduka ya dawa hapa Tanzania. Kupitia mijadala hiyo, nimejifunza mambo kadhaa ambayo hapo kabla sikuyajua kwa kina. Nimegundua mambo haya:

1. Mtu ili kuanzisha na kuendesha biashara ya duka la dawa, huihitaji uwe ni mfamasia kitaaluma bali unahitaji kukodisha cheti cha mfamasia yoyote na kukitundika kwenye duka lako la dawa, na kuanzia hapo utauza dawa yoyote hata kama elimu yako ni darasa la saba! Hii ni sawa na rubani mwenye leseni ya kurusha ndege za abiria kuikodisha leseni yake kwa kampuni ya ndege ili itundikwe ndani ya ndege, halafu mtu yoyote anaweza kushika usukani wa ndege na kuamua kuirusha ndege!

2. Kumbe wafamasia kitaaluma hawajui (hawakufunzwa) na hawapaswi kumpima mgonjwa (examination), kugundua ugonjwa (diagnosis), kuidhinisha dawa za kutumia (Prescription) au kumtibu mgonjwa kwa dawa (drug administration). Mfamasia anapaswa tu kumgawia mgonjwa dawa (drug dispensing) kwa mujibu wa kibali cha Daktari. Ajabu ni kuwa huku mitaani maduka ya dawa ndio hospitali zisizo rasmi, tukiumwa tunaenda na pesa kwenye duka la dawa na kutibiwa faster!

3. Kiujumla karibu dawa zote hazipaswi kuuzwa na duka lolote la dawa mpaka kibali rasmi cha dawa kutoka kwa Daktari (Prescription). Ajabu ni kuwa huku mtaani dawa yoyote unaweza ukauziwa na duka lolote la dawa ukienda na pesa tu!


Baada ya kupitia hayo yote nimegundua wazi kubwa, kiujumla maduka ya dawa hapa Tanzania huenda kwa sehemu kubwa yanatuibia, kutuumiza, kuharibu afya zetu na kutuua!
Nani kakwambia maduka ya dawa ni hospitali? Ondoa ujinga huo kwanza. Ukiwa waharisha usiende duka la dawa kuuliza dawa, nenda hospitali kwanza, wakikuandikia dawa ndipo waweza nunua popote pale kwenye duka la dawa.
 
Gharama za hospital ni kubwa sana mkuu! Hadi kumuona daktari sio chini ya shilingi 5000, vipimo, foleni, na adha nyingi. Maduka ya dawa yanasaidia sana, japo wanatoa dawa kiholela ila inasaidia.
Umenigusa sana... kula 💕
Tatizo la hospitali si gharama peke yake... Kuna thamani ya mtu, muda na quality ya huduma.
Hospitali/zahanati/vituo vya afya vinachangia watu kutafuta shortcuts ikiwemo wenye smart phones kutumia google kujitafutia tiba!
 
Hii vita sijui mwisho wake lini..?mana madaktari njaa hawaamini wanachokiona...mafamasia tuendelee kushikiria hapo hapo.

Halafu mleta uzi hujui hata maana ya neno afya..rudi shule kajifunze mana ya neno afya.

#MaendeleoHayanaChama

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Nimeishia hapo kwenye 'usukani' wa ndege, wewe jamaa ni FUTUHI ila sikuwahi kudhani ni mweupe kiasi hiki…. ukiweza kumwamini koboko basi utaamini kila kitu.
 
Mengine unayotakiwa kuyajua juu ya taaluma ya ufamasia na maduka ya dawa


MAKUNDI YA DAWA ZA BINADAMU 👇👇

1. Prescription Only Medicines ..(Cheti cha daktari kinahitajika )..hizo zenye "Dose;As directed by Physician".
2. Pharmacy Only Medicines(Cheti cha daktari hakihitajiki).
3. General Sale Medicines(Cheti cha daktari hakihitajiki)..hizi utazikuta hata dukani kwa mangi/mpemba n.k. mfano DAWA TATU/ACTION/HEDEX/PANADOL & PANADOL EXTRA/GLUCOSE /COFTA/TUMBOCID/ MOSQUITO (spray and repperants),CASTROL OIL/GLYCERINE/MEDICATED SOAPS /TOOTH PASTE/CONDOMS n.k.

KUHUSU DAWA ZIAZOTOLEWA KWA CHETI CHA DAKTARI (Prescription Only Medicine);

Dawa hizi zinazotolewa kwa cheti cha daktari kwa sababu zinachukuliwa kuwa hatari ikiwa hazitatumiwa chini ya usimamizi wa mtaalamu wa afya aliyeidhinishwa.
Dawa hizo kwa ujumla zinakusudiwa kutibu matatizo makubwa zaidi ya kiafya. Hii inaweza kujumuisha kisukari, saratani,magojwa ya moyo,bakteria,virusi nk.

Baadhi ya nchi kama vile Uingereza wapo wafamasia na manesi ambao wameidhinishwa kutoa(TO PRESCRIBE) baadhi ya dawa hizo.👇👇👇👇👇Nurses and pharmacists can prescribe as effectively as doctors - NIHR Evidence
Mkuu ungelitoa na vijimifano kidogo kwa namba mbili(2).
 
Kitu pekee ambacho mnatakiwa Mkijueee ADDO ishazikwaa.
 
Kwanza tambua kuwa ADDO ilianzishwa kwa sababu Pharmaceutical Personell walikuwa wachache, kwa sasa wapo wengi. Hizo nafasi zinaenda kwa wahusika.

Angalia hata mahospitalini, manesi walikuwa wanafanya kazi pharmacy kutokana na uhaba wa watu wa famasi. Ila kwa sasa watu wa Famasi wameongezeka na ile namba ya manesi inazidi kupungua kadri wanavyostaafu(maana hawawezi kutolewa kwa nguvu) hatimaye itaisha na nafasi zichukuliwe na wahusika.
Unamaanisha huko mbeleni mahospitalini hakutokuwa na manesi? Watakuepo wafamasia na madaktari tu?
 
Kuna kitu kinaweza kuvuka gharama ya uhai au afya ya mtu?
Standard za msingi zinaweza zisiwe na gharama kubwa bali zinahitaji umakini tu.
Acha kujitoa ufahamu, hujaona mtu anaachwa kuhudumiwa hospitali kwasababu hana pesa?
 
Back
Top Bottom