Maelfu ya mateka ya majeshi ya Ethiopia yalitekwa na Tigray Defense forces yafikishwa mji mkuu wa Tigray

Maghayo

JF-Expert Member
Joined
Oct 5, 2014
Posts
20,307
Reaction score
47,210
Inakuwaje WanaJF!

Tigray defense forces ni nouma. Serikali ya Ethiopia inaminya uhuru wa habari kuficha kinachoendelea Tigray lakini mkong'oto wanaoupokea huko ni wa Hatari. Hii imetokea jana. Hao ni washenajeshi wa Ethiopia walioshikwa mateka wakiwa paraded Mekelle mji mkuu wa Tigray
Your browser is not able to display this video.


mng'ato Jumbe Brown
 
Idadi ya kawaida kabisa ya wanajeshi mateka. Hawa hawafiki hata 6,000 kwa haraka haraka
 
... inaanza kunipa shaka uwezo wa Ethiopia kijeshi; kama wanamgambo wa Tigray wanawatoa jasho kiasi hiki ndio watapambana na Egypt kugombea maji ya Blue Nile "roho" ya Egypt? Ethiopia wajipange kweli kweli kama wanataka kulinda legacy ya haki ya kutumia maji ya Blue Nile bila "kuingiliwa" na foreign powers.
 
Hahah historia ya hao jamaa ni very interesting.

Majuzi naona serikali ilisitisha mapambano ili kupisha huduma za kimsaada kwa wananchi lkn waasi wakagoma,wakasema tuendelee kuchapana tu.

Wakikaa vibaya Hawa wa tigray watajitenga na kua na nchi yao,Ila watauwawa Sana aisee.

Na US inatoa kauli kuishutumu Serikali kuu huku Russia wakitoa kauli kuipongeza Serikali,huku nako Egypt na Sudani wako kiuchochezi kwny mgogoro huo.
 
Kwani tulisemaje tangu nyuzi za zamani huu mgogoro unaanza. Yani kuna watu humu walikuwa wanadai eti Egypt itapigwa na Ethiopia, Ethiopia hii yenye migogoro kibao ndani wala haina utengamano. Yani nchi iliyopigwa na ka-Elitrea eti ikaipige nchi iliyokomaa na Israel
 
Mkuu dudus wale siyo wanamgambo. Wale ni jeshi kamili. Wengi wao walikuwa makamanda kwenye jeshi la Ethiopia. Na wengi wao ndo walimng'oa dikteta mengistu haile mariam.
Huyu Ahmed Abiy wakati huo alikuwa kachalii naye aliungana nao huko maporini licha ya yeye kuwa half oromo Amharic.

Mwaka jana Abiy alitumia ujanja kuanzisha vita kwa kuwawahi TPDF kabla hawajavamia na kumili maghala ya silaha. Wangefankiwa tu sasa hivi Tigray ingekuwa nchi kamili.

Kingine kinachowasaidia TPDF kwenye hii vita ni Terrain. Tigray ni mountainous. Ngoja niingie chimboniwawekee video ya majeshi ya Tigray wakimatch ambayo iliipa Ethiopia government a wake up call. Muda siyo naibuka kutoka chimbohizi video ni nadra ha youtube.
 
Hizi video ndo ziliifanya serikali Addis Abeba ishtuke nakuchukua hatua haraka sana. Yani hawa wanaume wangefanikiwa kuchukua silaha sasa hivi Tigray ingekuwa nchi kamili. Na Tigray ingekuwa nchi kamili Oromia nao wangetaka taifa lao pia Amhara kwa iyo Ahmed Abiy ilibidi tu kuwa bomb marafiki zake wa muda mrefu kunusuru Ethiopia kuzidi kugawanyika.
Your browser is not able to display this video.


dudus mng'ato
 
TPDF
 
Basi kwa hali ilivo utawala wa waziri mkuu wa Ethiopia Ahmed Abiay utakua na mwisho mbaya au hata miaka miwili ijayo atakua keshatolewa.
 
TDF , Tigray Defence Force , msisahau watigray ndio jamii ya watu ethiopia wanaojiita first class people kwa ufupi hao ndio wenye wasomi wengi na kwenye serikali kuu ndio wenye position nyingi lakini pia ndio watu walioshika uchumi yaani wanawafanyabiashara wakubwa na wenye ushawishi mkubwa pale ethiopia, hata mkurugenzi wa WHO nae ni mtigray hivo jamaa msiwachukulie poa
 
Hizi nchi za kimaskini ni shida tupu.
Kinachogombewa haswaa ni nini?
Kuna haja gani kuwepo kwa vita nchini Ethiopia?
Kwanini wasikae chini tu na kukubaliana ili mambo yaishe, ili watu wao wapone, pesa za kupigana vita ziende kwenye maendeleo na wajenge nchi yao?
 
Ethiopia hana ubavu wa kusimama na Egypt
hawafanani kabisaaaa
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…