kigumu twawala
Member
- Nov 23, 2010
- 50
- 2
Mh huyu anasema, hakuna hitaji la lazima la katiba mpya ambayo kupatikana kwake ni gharama, mbali ya changamoto nyingine za ujenzi wa taifa. Tunamuuliza kazi za ujenzi wa taifa kwake na serikali yake wananazo zionaz ni muhimu kuliko hii ya katiba ni kununua mashangingi ya billioni 9? Na wamesha sahau kuwa kabla ya uchaguzi walituambia magari ya gharama sasa basi wataelekeza matumizi ya serikali serikali katika kuwahudumia walalalahoi wa nchi hii na tukaona matrekta ya kilimo kwanza, wamerudi kulekule kwenye matumizi ya anasa kazi ipo.
Anasema serikali haiko tayari kuanzisha mchakato wa kupata katiba mpya kwani hawaja pokea maombi kwa kufuata utaratibu kwa wenye madai (wananchi). Hivi hii ni serikali ya aina gani ya wananchi au serikali ya watawala? kwa maana anatuambia kuwa hawaoni kilio cha wananchi wao.
Anasema serikali isilazimishwe kushuhulikia suala hili nyeti kwa kupitia magazeti(sina hakika kama vyombo vingine vya habari anavichukulia je hapa?). Kama serikali inajua kuwa ni suala nyeti. kwanini inachezea suala nyeti?
Anasema kwamba shauku ya mabadiliko ya jumla ya katiba hayako kwa maslahi ya wananch na serikali, ila hasemi ni wapi, lini na vipimo vipi wametumia kujua kutokuwepo kwa shauku hiyo. Sasa kwa hili tunamuabia Waziri huyu kuwa awe mkweli wa nafsi yake na serikali, asiwa semee wananchi. Atuambie hivi mabadiliko hayatakuwa na maslahi kwa watawala, mafisadi na wachakachuaji maslahi ya watanzani. Kwani kwao wao katiba mpya ni kujitengenezea anguko lao kwa mikono yao wenyewe.
Kwa kauli za aina hii za viongozi wa serikali kunakila sabaubu ya wananchi walio wengi ambao ndio watanufaika kwa kupatikana katiba mpya, kuamini kuwa katiba mpya haitakuja bila ya kutumika nguvu ya umma.
Anasema serikali haiko tayari kuanzisha mchakato wa kupata katiba mpya kwani hawaja pokea maombi kwa kufuata utaratibu kwa wenye madai (wananchi). Hivi hii ni serikali ya aina gani ya wananchi au serikali ya watawala? kwa maana anatuambia kuwa hawaoni kilio cha wananchi wao.
Anasema serikali isilazimishwe kushuhulikia suala hili nyeti kwa kupitia magazeti(sina hakika kama vyombo vingine vya habari anavichukulia je hapa?). Kama serikali inajua kuwa ni suala nyeti. kwanini inachezea suala nyeti?
Anasema kwamba shauku ya mabadiliko ya jumla ya katiba hayako kwa maslahi ya wananch na serikali, ila hasemi ni wapi, lini na vipimo vipi wametumia kujua kutokuwepo kwa shauku hiyo. Sasa kwa hili tunamuabia Waziri huyu kuwa awe mkweli wa nafsi yake na serikali, asiwa semee wananchi. Atuambie hivi mabadiliko hayatakuwa na maslahi kwa watawala, mafisadi na wachakachuaji maslahi ya watanzani. Kwani kwao wao katiba mpya ni kujitengenezea anguko lao kwa mikono yao wenyewe.
Kwa kauli za aina hii za viongozi wa serikali kunakila sabaubu ya wananchi walio wengi ambao ndio watanufaika kwa kupatikana katiba mpya, kuamini kuwa katiba mpya haitakuja bila ya kutumika nguvu ya umma.