Mafanikio ya kielimu yamekuwa kikwazo watoto kupenda kuajiriwa na kukacha biashara za wazazi, wewe mfanyabiashara umejipangaje??

Mafanikio ya kielimu yamekuwa kikwazo watoto kupenda kuajiriwa na kukacha biashara za wazazi, wewe mfanyabiashara umejipangaje??

sky soldier

JF-Expert Member
Joined
Mar 30, 2020
Posts
5,407
Reaction score
19,264
Kuna jirani hapa nilishangaa sana alipomuachisha chuo kijana wake akiwa mwaka wa pili, Huyu kijana alikuwa anasomea degree ya procurement, mzee wake akamwachisha kinguvu.

Nikaja kujua kwamba mzee alikuwa anahofia sana mtoto wake anaweza kutekwa na maisha ya kuajiriwa na kuacha kabisa biashara ya mzee wake ikiwa haina mrithi hasa ikija kutokea kijana kapata ajira mkoa mwengine.

Unaweza leo hii ukawa na biashara na ukapanga kuirithisha kwa watoto lakini elimu yao ikaingilia kidogo huku kwenye biashara tofauti na mtoto ambae shule aliishia au mlifanya aishie huku chini ili mumfundishe biashara.

Mfano leo hii unaweza ukawa una biashara nzuri ina faida ambayo ni mara 5 ya mshahara wa kazi anayoitaka mtoto wako, ila bado mtoto akapenda zaidi kuajiriwa na biashara ikakosa mrithi wa damu yako.

Kiukweli hii inauma, kijana anajazwa sumu huko na wenzake kwamba ajira hio haina risk atapokea mshahara kila mwezi huku biashara inaweza ikafilisika kwa hiyo akatawaliwa mawazo kwamba akomae na ajira, hii sumu ndio ambayo wahitimu wengi inawafanya kupenda ajira.

Je wewe una deal na hii hali vipi
 
Nashukuru kwa kunifumbua macho mkuu, kumbe ndivyo matoto ya wafanyabiashara yalivyo eeh!! Ok Mwanangu kusoma mwisho kidato cha 4, akimaliza hapo namfundisha umachinga.
 
Mkuu ,kwa biashara kumrithisha mtooto ni nzuri ,ila iwe imesimama au ina potential ya kusurvive .............biashara za familia zina mambo mengi, kwanini usimuache akaajiriwe hata miaka mitano alakifunze kazi aje kuzi implement kwenye biashara aliyoiacha..?

Mfano biashara inaingiza mil 10 faida kwa mwezi ,kwa mwaka mil 120 ,sasa hapo familia nzima inaangalia hapo.......labda familia zilebbiashara ya familia inaingiza faida mil 200 hadi bil. 1 kwenda mbele.......


Nahitimisha kusema , bora aanze na ajira kama tu ina maslahi au potential ya kupata sehemu nzuri au kupata uzoefu ili hata akishindwa biashara awe na uzoef wa kazi ,kama ndio taasisi ndogo mshahara mdogo bora akomae na biashara.......

Biashara mfano kipindi hiki zimekufa nyingi

Kuna jamaa biashara yao ya familia inaingiza bil 1 na zaidi faida kwa mwaka lakini kaajiriwa sehemu analamba mil 1.5 .huyu ndio ilibid aendelez biashara



Naongea kwa uzoefu
Kuna jirani hapa nilishangaa sana alipomuachisha chuo kijana wake akiwa mwaka wa pili, Huyu kijana alikuwa anasomea degree ya procurement, mzee wake akamwachisha kinguvu.

Nikaja kujua kwamba mzee alikuwa anahofia sana mtoto wake anaweza kutekwa na maisha ya kuajiriwa na kuacha kabisa biashara ya mzee wake ikiwa haina mrithi hasa ikija kutokea kijana kapata ajira mkoa mwengine.

Unaweza leo hii ukawa na biashara na ukapanga kuirithisha kwa watoto lakini elimu yao ikaingilia kidogo huku kwenye biashara tofauti na mtoto ambae shule aliishia au mlifanya aishie huku chini ili mumfundishe biashara.

Mfano leo hii unaweza ukawa una biashara nzuri ina faida ambayo ni mara 5 ya mshahara wa kazi anayoitaka mtoto wako, ila bado mtoto akapenda zaidi kuajiriwa na biashara ikakosa mrithi wa damu yako.

Kiukweli hii inauma, kijana anajazwa sumu huko na wenzake kwamba ajira hio haina risk atapokea mshahara kila mwezi huku biashara inaweza ikafilisika kwa hiyo akatawaliwa mawazo kwamba akomae na ajira, hii sumu ndio ambayo wahitimu wengi inawafanya kupenda ajira.

Je wewe una deal na hii hali vipi
 
Back
Top Bottom