Mafanikio ya Rais Magufuli: Viva Rais Magufuli, viva Tanzania

Huwa wanatafuta sifa sasa mwakahuu pagum hawana jipya
 
mpaka sasa Dk. Magufuli anaonyesha uhai labda aje kuharibu badae
kwani hata Dk.Jakaya alianza hivo hivo
Rais Magufuli siyo Rais Kikwete.

Dhama za utawala wa Rais Magufuli ni tofauti na Rais Kikwete.

Jaribu kuangalia utendaji wa Rais Magufuli kuanzia siku aliyoteuliwa kuwa Naibu Waziri.

Angalia jinsi alivyoweza kupitia mchakato wa kuteuliwa kuwa mgombea Urais.

Rais Magufuli hakuwaahidi watu mbali mbali vyeo kabla ya kuchaguliwa kuwa Rais. Hana makundi ndani ya CCM na serikalini. Makundi ni sumu katika utendaji na mafanikio katika kufikia malengo.
 
Nakumbuka UKAWA walisema wakipunguza Safari tu watoto wanaweza kusoma bure hadi Chuo kikuu.Halafu acheni utahahira bila upinzani msingekuwa na Magufuli.Na ameanza Kweli kushughulikia vile vitu vilivyokuwa vikipigiwa kelele na UKAWA.Hii ni mafanikio kwa UKAWA na sasa kibao kimebadilika CCM ndo WATAISOMA no make ndo walikuwa wafaidika wa hizi Safari. Nia ya ukawa Pamoja na Elimiu,ilikuwa ni kuhakikisha serikali inapunguza matumizi yake,huduma Za afya,Maji n,k.Sasa Magufuli kaanza navyo.Watu walikuwa wakiwa beza sasa wanaamini UKAWA kelele zao hazikuwa Za bure.
 
Hamna jk hakuanza hivi,jk akuanza kwa kupunguza matumizi na wachapakaz,af hyu hyo ndo tabia yake,wala hagezi,nadhani mnamjua

Mkuu ni kweli usemacho Mhe JK alipolizinduwa Bunge la tisa hotuba yake ya kwanza kuhutubia Bunge alisema "watu wanasema Mimi mpole nasema nitakuwa mkali" lakini hakuwa mkali mpaka tumemsikia Mhe Mnyika alisema Rais ni dhaifu na Serikali dhaifu.
# SASA KAZI TUU #
 
Mimi cjaona ni wap UkAWA wamemkubl magufuli....
alaf naamin kama isingekua nguvu na uwepo wa upinzani magufuli asingekua rais mpaka xaxa
 
Thibtsha ni wap ukawa wamemkubli magufuli.....au kutokumtambua ndo kumkubali
 
Magufuli kawaweka UKAWA kwenye wakati mgumu sana, kwa sasa hawajua washikie ajenda gani, ya ufisadi isharudi CCM siku nyingi, i kama wamekata tamaa hivi, mie sioni hata haja ya uchaguzi wa Raisi 2020, soon CHADEMA itakuwa kama NCCR na Lowassa kuwa kama Mrema
 
kwa kauli za maghufuli kiujumla zinatia moyo. tunasubiri matendo zaidi...
Matendo gani unasubiri wakati kuna viongpzo muhimbili hospital kwa sasa wamekuwa demoted. Wale waliokuwa wanasafiri kwenda nje ya nchi mara nyingi zaidi kuliko kwenda kuwasalimia mama zao kwa sasa safari zimeota mbawa. Kuna panga amelipitisha kwa wale waliokuwa wanajiandaa kwenda kwenye mkutano wa jumuiya ya madola.
 
Una haki na uhuru wa kufikiria chochote kama takwa la Katiba yetu!

Hoja iliyo mezani ni viongozi wa UKAWA kuanza kukubali utendaji wa Rais Magufuli.

We unaongea hakuna tofauti na mlevi, inamaana magufuli atakuwa na ubavu wa kumpeleka mahakamani kikwete kwa matumizi mabaya ya ofisi kuhusu richmond au umeamua tu kutoa ushuzi humu.
 
Mwachenu magufuli afanye kazi ya wananchi kama wewe no ccm basi najuwa 2020 I'll vote no 4 magufuli na kama we we ni ukawa na mwananchi wa kawaida watamchagua lea kishindo Jana atatekeleza wajibu wake lea wananchi.
 




Kama Magufuli ataendelea hivyo basi watakaoumia ni CCM na sio wapinzani.
CCM miaka yote inawekwa madarakani kwa rushwa na pesa za rushwa zinapatikana kupitia mikataba feki na kufanya manunuzi kwa bei ya kuruka.
Pesa nyingi zinazoiweka CCM madarakani ni zile za kuchota kwenye mashirika ya umma kinyemela.

Sasa kama Magufuli atagoma kufanya huo ushetani uliofanywa na watangulizi wake basi ni dhahiri CCM itaporomoka huku Magufuli akibakia na kura zake mkononi na UKAWA watapaa kwa kasi kwani wabunge wengi walioko CCM wanaingia madarakani kwa mahela ya wizi wanayochoteana huko juu. Ndio maana walinunua masanduku ya ziada ya kura na kupiga kura kabla na kuzigawia kila majimbo .

Hivi leo Magufuli akisema anataifisha Majumba waliyogawana huku serikalini watakaolia ni UKAWA CCM .
Leo Magufuli akisema anawatimua kazi hao wafanyakazi wenye Vyeti feki watakaoumia ni CCM mana watoto wao wengi ndio wamefoji vyeti na wameajiriwa kwenye mashirika na idara mbalimbali. UKAWA watashangilia kuona kuwa walichokua wanakipigania kinatekelezwa.

Amini usiamini baada ya miaka miwili maadui wakubwa wa Magufuli watakua wapo ndani ya CCM.

Vigogo wengi wa CCM ndio wanaomiliki majumba na biashara nyingi za malori.
Leo hii Magufuli akitengeneza Reli na kuboresha usafirishajo wa treni watakaolia na kufilisika ni wanachama na vigogo wa CCM na sio UKAWA.
Leo hii pakiwa na katiba na sheria bora watakaoumia ni CCM maana walishazoea ulaghai na uovu .

Jambo lolote jema litakalofanywa katika hili taifa litawaumiza sana CCM na mabosi wao waliokua wanawakuwadia mali za watanzania. UKAWA hawajawahi kunufaika na mikataba feki na wawekezaji.
Mirija ya unyonyaji ilikua inatumiawa na CCM na watoto wao.

Leo hii kuna wabunge,waandishi wa habari na wanachama wa CCM wanaojifanya sana kumuunga mkono Mh.Magufuli lakini wamelenga madaraka ya uwaziri na sio maemdeleo kwa wananch .Hawa ni wanafiki na wote wako CCM na sio UKAWA.
Hata Kikwete walimsifu na kutoa kila tamko jema juu yake huku wakilenga madaraka na walipopata wakageuza nchi kuwa shamba la bibi.
Baada ya kipindi hiki cha mgao wa vyeo ndani ya serikali ukipita basi hawa apambe watapukutika sana
 

Ipo siku Mungu atajibu maombi na ni yeye anayejua nini cha kuwafanya kwa unyonyaji unaofanywa na sisiemu. Roho nyingi za watu mmezikatisha, hakika Mungu atawalipa na ninyi mnaokishabikia.
 

Ukifahamu kuwa siasa sio uadui utachakuwa umeimarisha demokrasia ya kiafrika.
Wanaccm shida sana. UKAWA wakipinga mnawashangaa na kuwatukana.
Wakishadidia jambo jema(ingawa ni mapema mno kumsifu kiongozi yeyote kwa mwezi na nusu) mnawashambulia.
Uchaguzi ulishakwisha, Rais ni Magufuli
 

Kumbe ukawa walikuwa na ajenda nzito hadi ccm/magufuli kaamua kuzitumia ktk uongozi wake!
Bravo ukawa!
 
Magufuli atatusaidia kuufuta upinzani..
Sipendi upinzani ufutike, lakini ninapenda viongozi wa upinzani wanaofanya biashara ya kisiasa lazima wafutike.

Huwezi kutueleza kwa miaka zaidi ya nane kuwa mtu fulani ni mla rushwa na fisadi halafu baadaye ukarudi tena na kuanza kutuaminisha tumchague kuwa Rais wa Tanzania kwa sababu siyo mla rushwa na fisadi. Mbaya zaidi unatuambia hayo maneno uliyosema yalikuwa ni maneno ya kisiasa tu. Hukumaanisha kama kweli ni mla rushwa na fisadi.
 
upinzani wa tanzania ni pasua kichwa...ni bora uvunjike yaani ufutike kabisa ili uanze upya...

upinzani wa dj na mr zero na luwasa huo ni upinzani au usanii tu.
 
wanamtambua ila hawawezi sema.
wakimkubali waziwazi watawaeleza nini watanzania wakati awali walimkashfu.
Hizo ndizo siasa za kinafiki ambazo pia Rais Magufuli amewaambia wana CCM ambao mchana wako CCM lakini usiku wako upinzani.

Rais Magufuli amesema watu wa aina hii ni janga kwa taifa.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…