Salamu kwenu ndugu!
Kwanza kabisa naomba nitoe pongezi zangu za dhati kabisa kwa mh. Rais John Pombe Magufuli.
Moja ya matamanio yangu ni kuona Tanzania inakuwa yetu sote. Huu ni mwanzo wa kuwa na serikali yenye sura ya utaifa zaidi badala ya uchama zaidi.
Kwa nini amekuja kutengua torati?
Sababu kubwa ni kujali matamanio ya watanzania kuona tunasonga mbele.
Amethubutu kufanya kile ambacho watangulizi wake walishindwa kabisa kufanya,ni mengi achilia mbali hizi teuzi.
Huku chamani nadhani shughuli mnaiona.
Kufanya kazi kwa mazoea sasa inaanza kuwa hadithi. Huu nao ni utenguzi wa torati.
Kuwawajibisha viongozi mara moja,ni utenguzi wa torati.
Kama bado hujakubaliana kaa mkao kabisa ushuhudie torati ikitenguliwa kadiri inavyobidi. Hizi katiba zetu ndio torati zenyewe,ambazo kimsingi zinamengi ya kurekebishwa. Acha Mkuu aendelee kuzitengua torati.
Huyi ndiye mtenguaji torati,Rais John Joseph Pombe Magufuli.