Mafanikio ya Rais Magufuli: Viva Rais Magufuli, viva Tanzania

Mafanikio ya Rais Magufuli: Viva Rais Magufuli, viva Tanzania

[HASHTAG]#RipotiYaKwanza[/HASHTAG]

Lissu: Tusihangaike na udongo, tuhangaike na mikataba na sheria mbovu za madini zilizotufikisha hapa. Tuangalie tulipojikwaa, tusiangalie tulipoangukia.

CCM: Lissu analinda wezi. Mikataba na sheria za madini hazina shida. Shida ipo kwenye udongo wenye makinikia. Tumeibiwa sana kwenye udongo. Hatukubali.

[HASHTAG]#RipotiYaPili[/HASHTAG]

JPM: Tumelogwa na nani? Watanzania tumeibiwa sana. Naagiza mikataba yote na sheria zote za madini zipitiwe upya.

CCM: Rais wetu mzalendo. Amefanya kazi kubwa sana. Tumuombee.!!

[HASHTAG]#MyTake[/HASHTAG]:
Lugha ileile aliyoongea Lissu akaambiwa amehongwa, ndiyo aliyoongea JPM leo akaitwa mzalendo. Akili za CCM kama kifurushi cha jaza ujazwe [emoji23][emoji23].!
NDO MLICHOPEWA KUPOST UKO UFIPA NINI? NAONA KILA UZI MNAPEST HII TAKATAKA TU. CAN YOU FLY TO KIA
 
Vita ni vita tuu haijalishi ni ya nini, lakini kwa Tanzania tuna bahati hatujapata kupigina vita ya ndani yaani wenyewe kwa wenyewe tofauti na nchi nyingine tulizopakana nazo. Lakini kwa sasa kuna kila dalili ya vita tena hatalishi kwa maisha ya watu na Mali zao . Nadhani kwa mtazamo wangu tunaweza kupigana vita ya kiuchumi au matabaka ya kipamapato toka upande mmoja mpaka mwingine, sioni hali hiyo tukiikwepa kwa kila namna kuna mgawanyiko mkubwa wa maisha na maendeleo ya watu, kuna pengo kubwa kati ya walionacho na wasionacho tena kuna kibri toka kwa wenye nacho hawataki kusikia watu wakilalamika njaa ama ugumu wa maisha kwa namna yeyote ile labda kwa kudhani wote wanakula na kusaza kama wao walivyo. Kuna rasimali nyingi zinapatikana kwenye mazingira ya wananchi lakini hawanufaiki nazo kamwe, Kuna unyanyasaji wa wananchi hasa waliopo maeneo yenye rasilimali zinazonufaisha watu wachache, tena hata inapotokea wananchi kuomba namna nzuri ya kunufaika nazo hubezwa na kupigwa ama kuhamishwa kwa nguvu . Binadamu sio wajinga wakati wote hata kama hawana silaha za kupigana vita. Huu ni mtizamo tuu unaweza kupingana nami ama kukubaliana kwa hoja MUHIMU KUJUA,
(UNAWEZA KUWADANGANYA WATU MARA MOJA LAKINI HUWEZI KUDANGANYA WATU WOTE SIKU ZOTE.)
Nawakilisha...
 
(UNAWEZA KUWADANGANYA WATU MARA MOJA LAKINI HUWEZI KUDANGANYA WATU WOTE SIKU ZOTE.)

Hii ingenoga kama ungesema, "UNAWEZA KUDANGANYA WATU WOTE MARA MOJA NA UNAWEZA KUDANGANYA WATU WACHACHE MARA ZOTE, LAKINI HUWEZI KUDANGANYA WATU WOTE SIKU ZOTE"
 
Hii ingenoga kama ungesema, "UNAWEZA KUDANGANYA WATU WOTE MARA MOJA NA UNAWEZA KUDANGANYA WATU WACHACHE MARA ZOTE, LAKINI HUWEZI KUDANGANYA WATU WOTE SIKU ZOTE"
Ni vyema pia kama umeelewa nawe umeongezea ili inoge, bado vita ya kiuchumi ipo mbioni
 
Ni wazi sasa vilio vya watanzania kuhusu rasilimali zao sasa kimepata mtu wa kuvisikiliza, haijalishi ni njia ipi JPM anatumia, ingawa kwangu naona yuko sahihi kabisa, ni lazima sasa wote tuungane, hata kama kuna makosa katika utekelezaji wa hatua zake, tuungane pamoja kurekebisha kasoro hizo na tupambane pamoja, si wakati wa kusikiliza wasomi wasio jasiri, wasomi ambao kwa muda wote wametumia usomi wao na madaraka waliyopewa kutudanganya na kuwa sehemu ya wizi wa rasilimali zetu.

Wabunge na Viongozi wetu wa upinzani, hayo ndio mliyaibua katika mijadala yenu Bungeni na katika majukwaa, tutawashangaa mkibaki nyuma katika vita hivi.

Wakili msomi Tundu Lissu, ungana kwa hiari na timu ya Raisi kuonyesha usomi wako na uzalendo wako kupigana vita upande wa JPM, wewe ni mtanzania, tambua katika mkataba wowote ule, kuna masuala kama Fraud, Misrepresentation, Unfair Enrichment na mengi tu hufanya mikataba kuvunjwa, mbona unaangalia MIGA tu na mikataba ya kinyonyaji ya kimataifa, tumia weledi wako na mikataba ya kimataifa yenye sura za kinyonyaji ibadilishwe pia, anza kuingia kwenye issues ambazo tunafikiri ndio za kiwango chako sasa, kesi za uchaguzi na uchochezi waachie vijana waanze kupractise.

Kwa hili la rasilimali zetu, tuko pamoja na Raisi wetu
 
Naweza kuwa wrong, ila Mimi naona Kwa siasa za Ushabiki, hujuma, hila na Kuzungukana Tanzania hivi sasa Kuna Watu au Mtu anamega Matonge kabambe mno yaliyomzidi Kimo! Ubaya ni Kuna Watu Tangu enzi za Mwalimu mfumo wa Serikali upo kwenye Viganja vyao!

Sijui Kama mashaka haya kwa wengine yapo?
 
Kila akipiga huwa zinasikika sauti za vilio vya wanaccm wakisema tunakufaaaaa! tuacheeeeee!

Kila likipigwa Bomu majeruhi au Vifo huwa ni vya wanaccm.

magufuli endeleza mashambulizi mpaka wanye damu tangu watudanganye kwa Miaka 50 sasa inatosha
 
Kama ugonjwa uko mwilini mwako, dawa lazima uinywe wewe. CCM ndio shida yetu.

Kama Rais Magufuli asingekuwa CCM, si ajabu miaka mi5 ijayo tungekuwa mbali sana. Shida ni kwamba, kila anapochanganya ya CCM na serikali anajikuta kajikanyaga mguu mmoja juu ya mwingine.
 
Licha ya maisha kuwa magumu hivi bado watu wanapiga vigelegele na kumshangilia. Watu hawajui wale nni unga umepanda bei na almost kila kitu.

Watu wanaona bora wafe tu waendelee kumshangilia. Hivi sisi watanzania aliyeturoga nani. Kuna mijitu inashangila as if imeshushiwa chakula. Hamuoni maisha yalivyomagumu? Mnadanganywa na mchanga Wa madini ili msahau shida zenu.
Jpm hana dira yoyote ya maendeleo zaidi ya visasi na kukomoa waliompinga. Mpaka mda wake uishe itakuwa kufoka na kuhuzunika tu na kuwatumbua ambao hawapendi.
 
Hivi tumerogwa?Mbona huwa tunaandamana kwa vitu vingine ambavyo hata faida havina!UVCCM imekufa??Ni muda wa kuitisha maandamano kila kona ya nchi kuonyesha tunamuunga mkono Rais JPM na kwamba ACACIA watutake radhi hadharani na kutulipa stahili yetu! Nchi zilizoendelea jambo kama hili lingewafanya wananchi waandamane wiki nzima kumpongeza jemedari wao!Hebu nasi tufanye ili kumpa faraja na kumwongezea ujasiri wa mapambano atambue kuwa hayuko peke yake!
Tanzania kwanza
 
Hivi Watanzani tunasubili nini kujenga Sanamu ya Rais Magufuli na kuiweka Posta.Tukichelewa kujenga Sanamu wenzetu Kenya watawahi na kusema anatoka nchini kwao.Naomba tuungane Katika hili Watanzani.
Nawasilisha
 
Sanamu ya Kazi Gani wakati mawazo yake huakisi
"Living Statue Status"
 
MAANDIKO YANASEMA USIJIFANYIE SANAMU YA KUCHONGA YA KITU CHOCHOTE KILICHO JUU AU CHINI ARDHINI
 
Aksante mkuu kwa mawazo ya kiajab sana. Tangu yule aliyetoa wazo kuwa kile kitanda alichofia yulee kule Landani kinunuliwe kije kuwekwa hapa nyumbani ka ukumbusho kwa gharama yeyote. (na huenda ukawa ni weye pia uliyetoa wazo) naona hajatokea mwingine ila wewe leo.
Haya mawazo ya kilumumba jamani yawekeni akiba
 
Back
Top Bottom