Mafanikio ya Rais Magufuli: Viva Rais Magufuli, viva Tanzania

Tumemchoka kilasiku ni yeyetu,amefanya nimechukia kuangalia taarifa ya habari.Taarifa za habari zote zimesheeni pombe aka,
 
Ripoti ya pili ya makinikia hiyoooooooo inakuja J3. Hapa kazi tu!!
 
Kama kila mara unavyotuomba sisi Watanzania KUKUOMBEA napenda kukuthibitishia kuwa mimi katika Familia yangu maombi yetu ya kila siku ya Kifamilia kuanzia saa tatu usiku jina lako halikosi katika maombi yetu ya familia. Pia hatuwasahau wasaidizi wako Makamu wa Rais, Waziri Mkuu, Mawaziri na wengine wote wanaokusaidia mpaka Mtendaji wa Kijiji kuliongoza Taifa. Pili, mimi ni Mkatoliki , katika Ibada yetu ya kila Jumapili inapofika kipindi cha maombi Mhe. Rais Jina lako halikosi katika kukuombea. Kwa hili la dhahabu Mhe. Rais itatubidi tuweke bidii kukuombea sana. Hii ni vita.Tumeibiwa vya kutosha inatakiwa mtu aliyejitoa muhanga kama wewe. Mungu akubariki sana.
 
tatizo ni kwamba muitikio wa wasaidizi wake hauonekani
yani yapo yapo tu kama mizimu
hapo ndo mtu unajiuliza hawa watendaji wengine wako kwa maslahi ya nani
 
kwanza nianze kwa kusema nifuraha yangu kubwa sana kuwa mtanzania na kuwa hai siku ya leo na naamini ntakuwa hai muda mrefu sana mbelen ukiacha mapenzi ya Mungu.
kwa sababu kila ninapo lala nataman kesho ifike maana saiz kuwa mtanzania najitanua kifua mbele jaman ni raha kuwa mtanzania maana mabadiliko yanayo tokea na yanayo endelea yananifanya nifurahi zaid na zaid.

sio siri ccm na ambao sasa ni wapinzan kwa miaka ilopita walitufumba sana na kufanya mambo mengi ya ajabu ambayo kila mtanzania aliyachukia na kama ulikuwa na upeo wakuyasikia naamin yalikuuma,
niwakumbushe kipindi kile anaingia bungen dk slaa na documents zinazo usu serikali alikuwa akisoma mpaka roho inauma na hakuna hata mmoja alie leta solution mpaka mimi binafsi niliacha kusoma magazet na kusikiliza bunge maana tunaoneshwa kila kitu kila kosa la serikali lakin hao watu wanadunda tu na hakuna hatua hata moja inayochukuliwa watu wakawa wanajua jinsi ya kutusahaulisha mara kikombe cha babu na mengine mengiiiiii

watanzania tulisha kosea sana sasa mda wakujirekebisha ndo huu tumepata mtu ambae anatoa majawabu yayaliyo tusibu nakutuudhi wengi wetu kipindi ki l e cha nyuma kwa nn tusishukuru kwa huyu tulie nae.najua kunahoja nyingi sana lakin ukiwa na kiongozi ambae anaweza kusafisha nyumba yake kwanza nakuanza kwenda pembeni ni kushukuru sana mm ungu.
my take naamin magufuli he is the best to us,tuache lawama maana haijengi.
tuanzia hapa it doesnt matter hasara tutakayo ingia so long as tutabadilisha its ok
 
Leo ndio nimejua Raisi wetu sio wa Mchezo Mchezo. Taratibu viongozi wote waliopita wanapata presha maana kwa kasi hii Marais wa awamu ya tatu na nne lazima waingie kitanzini.

Ongeza kasi baba tumeshikilia gari na kujifunga mkanda kwa umakini
 
Kuna siku katika Forum hii niliwahi sema, ikitokea leo hii rais dr. John Pombe Joseph Magufuli akafariki, Tanzania haitaweza kumpata rais wa aina yake na mzalendo wa kweli kwa taifa hili kwa pengine miaka hamsini ijayo tena.

Kauli yangu kwa mtu mwenye akili timamu na mzalendo wa taifa hili aliyeisikiliza report ya pili iliyoundwa na mheshimiwa rais kuhusiana na sakata linalotawala sura ya tanzania leo na dunia kuhusu usafirishaji wa mchanga nje ya nchi ataafikiana na kauli yangu

Kwa nchi za udikteta hii ingekuwa ni sababu ya msingi tosha kuamua kwamba rais huyu awe ni rais wa milele tanzania.

Kauli yangu inajengwa na uzalendo wa dhati ambao anao rais huyu kwa taifa na watu wake.

Ningekuwa na uwezo wa kimungu basi ningeweza amuru kwamba rais huyu aishi milele ktk dunia hii na akiwezekana awe rais milele wa tanzania na pengine na africa kwa ujumla.

Ni ujinga na upumbavu mkubwa na uuwaji kwa mtu uliyekabidhiwa madaraka na watu wako ukawa chanzo cha kuwaibia watu wako.

Report inatoa majonzi na masikitiko makubwa sana.

Rais wangu, zawadi kubwa niliyonayo kwako ni kukuombea kila lililojema ktk maisha yako, kukuombea maisha marefu, afya njema na zaidi ya yote mungu akulinde na akuongoze kwa kila ulifanyalo ktk maisha yako.

By Lutengano Nkanda Mwakisalu
 
Ni kweli wakurupukaji kama yeye watakuwa wameisha, ikiwezekana asepe tu
 
Huu ni Uzi maalumu kwa watoto wa mama Tanzania kuweza kumpongeza na kumtia moyo Rais wetu mh Magufuli kwa namna anavyotutumikia kama Kiongozi mkuu wa taifa letu.

Bila kujali itikadi zetu tunapaswa kuwa pamoja kama taifa ktk vita hii ya kuzikomboa rasilimali zetu zilizoporwa na manyang'au.

Tangia kuasisiwa kwa CCM tarehe 5/2/1977 sijawahi kuona maamuzi magumu yakichukuliwa na mkuu wa nchi ktk kupigania rasilimali za taifa kama afanyavyo Rais wetu wa awamu ya 5.

Mwalimu Nyerere wakati wa Tanu alituletea azimio la Arusha, lakini wajanja wachache kwenye miaka ya 80 wakalibinafsisha na kuturejesha kulekule kwenye unyonyaji unaomzidi hata mkoloni yaani wametuletea ukoloni mambo Leo.

Sasa imekuwa ni neema ya Mungu ktk zama hizi za utandawazi kumpata Kiongozi aina ya Magufuli ambaye hayuko tayari kuburuzwa na mabwanyenye.

Hivyo niwaombe sana Watanzania wenzangu tuzidi kumuunga mkono na kumtia moyo ili lengo lake la kukomboa rasilimali zetu liweze kutimia.

Vilevile tuzidi kumuombea kila siku ili baraka za Mungu zikaambatane Nate ktk utendaji kazi wake wa kila siku.

Mungu ibariki Tanzania, Mungu mbariki sana Rais wetu Magufuli! Ahsante.
 
wanamuonea bure chenge. Yeye alikuwa anatekeleza ilani ya ccm ya kuliibia taifa...
Ccm akiwemo magufuli ni wapumbavu sana kwa sababu haya yote ni sababu yao wote kwa umoja wao dhidi ya rasilimali za watz. Alafu wanaunda mitume kwa kuwapa ulaji wa bure watu wkt walipitisha haya yote kwa mbwembwe huku wakiwatukana watz matusi ya nguoni.
Shame on them ccm + their corrupt leaders
 
Poapoa umesikika mkuu ila nafasi za teuzi nahisi zimeisha
 
Uache kumsakama Lissu sasa kama kweli huu nsimamo wako.
 
[HASHTAG]#RipotiYaKwanza[/HASHTAG]

Lissu: Tusihangaike na udongo, tuhangaike na mikataba na sheria mbovu za madini zilizotufikisha hapa. Tuangalie tulipojikwaa, tusiangalie tulipoangukia.

CCM: Lissu analinda wezi. Mikataba na sheria za madini hazina shida. Shida ipo kwenye udongo wenye makinikia. Tumeibiwa sana kwenye udongo. Hatukubali.

[HASHTAG]#RipotiYaPili[/HASHTAG]

JPM: Tumelogwa na nani? Watanzania tumeibiwa sana. Naagiza mikataba yote na sheria zote za madini zipitiwe upya.

CCM: Rais wetu mzalendo. Amefanya kazi kubwa sana. Tumuombee.!!

[HASHTAG]#MyTake[/HASHTAG]:
Lugha ileile aliyoongea Lissu akaambiwa amehongwa, ndiyo aliyoongea JPM leo akaitwa mzalendo. Akili za CCM kama kifurushi cha jaza ujazwe [emoji23][emoji23].!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…