Mafanikio ya Rais Magufuli: Viva Rais Magufuli, viva Tanzania

Tuna rais kichaa na mawaziri vichaa.

Dah! Tanzania ya viwanda.
 
Mkuu kumbuka ufisadi uliofanyika katika kipindi cha awamu ya tatu na nne ulikuwa wa kutisha na CCM iligeuka kuwa chama cha watu wenye maslahi maalum binafsi. Makundi yenye nia mbaya yalijengeka hata kufukia kutaka kuingia Ikulu kwa njia yeyote. Rais Magufuli kama binadamu anaweza kukosea lakini tuangalie mazuri mangapi anayoyafanya.
 
Well said Mkuu
 
Wapi baadhi ya watu katika mtandao huo wa Jf kazi yao ni kutafuta vikasoro kasoro kwenye kila analolifanya Mh.Rais na watumishi wenzake, akisaidia kuichangia shule, utasikia mtu anapost upumbavu humu eti shule zote ziko hivyo, lakini upumbavu wa wabunge flani wanaoibuka hadharani kudai wakurugenzi ni wezi bila kutoa vithibitisho, cha ajabu hakuna anayekemea hiyo tabia chafu. Mtu anayediriki bila aibu kuchafua taswira na Juhudi zinazofanywa na Serikali hii hakika ni Shetani na anadhambi kubwa. Lakini kama mtu huyo ni Chadema binafsi namsamehe bure, kwani Chadema wanajulikana kwa mapungufu yao, mioyo yao ni makazi ya Ibilisi, hata wakipinga hatuoni ajabu, Shetani alipinga hata mema ambayo Mungu wa mbinguni aliyapanga, Chadema ni wakala wa Shetani.
 
Ccm isiogope kupingwa maana hata wale wanaoamini Vitabu vitakatifu YESU na Uungu wake alipingwa. Hata Mungu alipata upinzani kutoka kwa Lucifer.

Upinzani ni kitu kipo tangu ulimwengu usimikwe.
 
Shetani ni wewe unayeacha kutumia akili zako kwa maslahi ya tumbo lako. Ninyi ndio mko radhi kuliuza Taifa kwa maslahi yenu kwa sababu ya kutothamini mustakabali wa Taifa letu.

Kuna mdau kakwambia upinzani upo enzi na enzi na hata hapa tulipitisha rasmi 1992. Sasa kwa nini wapinzani waonekane maadui na wakose haki ndani ya Taifa lao. Mnawafunga, mnawapiga, mnawabambikia kesi, wengine mpaka mnawauwa. Mnajenga mustakabali gani wa Taifa huko baadae? Hali hii itaenda mpama lini umewahi kukaa kujiuliza hilo au unawaza tumbo lako. Mnadai mnapendwa lakini uchaguzi ukija tume na polis ndio waokozi wenu

Uzalendo ni kuweka Taifa lako mbele. Litizama Taifa kwa ukubwa wake hivi vyama vitakuja na kuondoka. Na pia uelewe sio mkosoaji ni Chadema au CUF wengine hatuna vyama

Sasa unataka Tusifie kitu gani wakati maovu ni mengi.

NIKUULIZE, UKIPEWA JUICE KWENYE GLASS YA NUSU LITA HALAFU MTU AKAWEKA KIPANDE KIDOGO CHA KINYESI UTAKUNYWA? .

Hakuna demokrasia, hakuna utawala wa sheria, bunge liko mfukoni hata wabunge wenzenu huko wakitetea maslahi ya wananchi wanatishwa wanaambiwa watapigwa mpaka shangazi zao.

Mitandao haumuipendi kwa sababu huku angalau watu wanaona kuna nafasi ya kutoa maoni yao. Ndio maana mnajitahidi kuidhibiti. Mmeanza kuwabana bloggers na sasa mmeenda kwa vituo vya runinga. Yote haya mnajua hampendwi na hamuungwi mkono. Akija asiweza kulazimisha namna hii ndio mwisho wenu.

Utafiti wa Twaweza unaonesha wananchi hawawaungi mkono na ndio maana mnapita denge kuwanunua, kuwatisha na kuwarubuni wanasiasa ili wahamie kwenu mkiwaahidi nafasi zile zile tena mnavunja na taratibu za Chama chenu. Siasa za kishamba kabisa

Uchumi unayumba sasa hivi kila siku tunakopa, hadi bil 200 nazo tunakopa, na hapo ndio mnakamua kodi kila mahala na kubana matumizi lakini ajabu mishahara haipandishwi,Sekta binafsi zinakufa watu ajira wamepunguzwa.

Si ajabu hata wewe unajua hali halisi lakini kwa sababu unalipwa kutetea kama wenzako inakubidi ufanye hivyo maana msipotetea hakuna wananchi wa kawaida wa kuwatetea
 
Nimesoma kwa kina sana mawazo yako, nilichogundua ni kwamba elimu yako ni ndogo na imepelekea hata uelewa wako use finyu, kama kweli Watanzania wameichoka Serikali yao ya awamu ya 5, umefuatilia mikutano ya Mhemiwa Rais ? Watu wanajaa kupita kiasi, je watu yao wanalazimishwa ? Wanakamatwa na polisi na kuletwa kwenye hadhara? Kama hawampendi Rais na Serikali yake kwanini waje? Kuhusu kukopa ni jambo la kawaida, mwaka Jana Marekani ilikopa US $ 900 kutoka World bank, je ndiyo kusema ilichukiwa na Wamarekani? Huko Marekani jumbo moja walijaribu kumpinga Trump kwa kuendeleza maandamano, kilichotokea walipiga sana, na 3 wenye asili ya kiafrika na kiasia walipata ulemavu wa kudumu, 7 walifungwa miezi 3 kila mmoja, sasa ikifanyika Tanzania tena kwa mujibu wa sheria kwanini inakuwa nongwa? Chadema hamfai, na hii tabia ya kishetani itawapeleka kuzimu.
 
Mikutano ya kusomba wanachama wenu na Malori kuwaweka sehemu moja kwa nini wasijae. Na sio kila anayekuwepi mkutanoni anakuunga mkono. Hata mimi akiwepi ntaenda.

Kuhusu elimu yangu ukitaka unaweza ukafahamu kisha ukalinganisha na yako .

Wasomi wengi hawawaungi mkono poa. Ndio maana mfano wa wasomi wanasheria Tz nzima hawawaungi mkono wako radhi wawachague viongozi wanaikosoa sana Serikali ndio maana wanawachagua watu kama Karume. Huo ni mfano tu. Kwa ufupu mmechokwa sana mnalazimisha mambo. Kazi mnayo angalia hata humu mitandaobi hamupendwi.
 
Argument zenyewe chali, mistari miwili !!! Tena haina hata mawazo yenye tija, thibitisha Ccm imechokwaje? Wakati Wabunge na wanachama wa vyama vingine tena Wasomi na wanasheria wanatimukia Ccm? Huko Chadema mbona hawaendi? Kumchagua Karume kuongoza TLS hakumasnishi kuichukia Ccm, kwani TLS ni Chama cha Siasa? Sasa unalingaishaje Chama cha Wanasheria Tanzania na Chama cha Siasa? Nfdiyo maana nimesema Elimu yako na uelewa wako ni mashaka matupu, huenda wewe ni miongoni mwa watu wenye vyeti feki.
 
Ngoja nifanye mengine. Maana mwenzangu hapo unalipwa siwezi kuendelea kubishana na wewe Mkuu The Genius. Naona umehama kutoka kutokuwa na elimu, umehamia vyeti mwisho utasema na jina nililotumia nimenunua kwa mtu sio langu ukadhani ni kama Bashite. Siku njema😀
 
NJAA mbaya sana usije kuta huyu naye ni musomi mzuri tu ila kageuzwa msukule au anajifanya hayawani na watawala yuawatumikia
 
Rais yeyote anayependa luxury life huwa hathubutu wala kujihusisha na coplicated projects hata kama zinafaida kwa wananchi wake kwa sababu zitamnyima muda wa kula bata, kweye hili,, Rais Magufuli ni kama mbingu na ardhi ndio maana anathubutu.

Big 5 My President!
 
Rubbish! Glorifying a dictator!
 
Anathubutu kwasababu hera sio ya kwake na pia hana huruma na wa Tznia.....huwezi kucheza kamali na maisha ya wtznia
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…