Mafanikio ya Rais Magufuli: Viva Rais Magufuli, viva Tanzania

Chadema, siku zote hufanya maamuzi ya kike, kukimbilia kwa Mwanaume (Muzungu) mwingine kushitaki!
ajabu huyo huyo muzungu akija kwenu ccm na na vipande vya pesa mnamuita mwanaume, na mnamnyenyekea na kumsifu
 
usishangae hivyo, ndio maana akitoka mtu chadema na kwenda ccm analamba uteuzi haraka. kama wanaweza kumshawishi meya/diwani kwa ahadi ya milioni 200 unategemea kuwa huko ccm kuna watu wenye akili kweli?
 
Mh mkubwa akosei kaka akikosea lejea kauli kwamba
 
WB yazungumzia mkopo kwa Tanzania


SUNDAY NOVEMBER 18 2018






Kwa ufupi
  • Akizungumza na waandishi wa habari jana, Dk Ghanem amesema benki hiyo itatoa fedha kwa ajili ya wasichana wote bila kujali hali zao, hivyo kuwatenganisha kwa kigezo chochote cha ujauzito au kingine chochote ni kwenda kinyume na mkakati wa elimu jumuishi.
ADVERTISEMENT

By Mwandishi Wetu, Mwananchi
Dar es Salaam. Baada ya kuzungumza na Serikali, makamu wa Rais wa Benki ya Dunia (WB) Kanda ya Afrika, Dk Hafez Ghanem amesema kuna masharti wamekubaliana kabla Tanzania haijapewa mkopo wa Dola 300 milioni za Marekani (Sh680.5 bilioni) kwa ajili ya kuboresha elimu nchini.
Akizungumza na waandishi wa habari jana, Dk Ghanem alisema benki hiyo inatoa fedha kwa ajili ya wasichana wote bila kujali hali zao, hivyo kuwatenganisha kwa kigezo cha ujauzito au kingine chochote ni kwenda kinyume na mkakati wa elimu jumuishi.
“Wataalamu wetu watashirikiana na Serikali kuona ilivyojiandaa kutoa elimu kwa wasichana wote. Tutakapojiridhisha bodi ya wakurugenzi itaidhinisha mkopo husika. Kuchelewa kwake kutategemea lini Serikali itatekeleza masharti tuliyokubaliana,” alisema.
Mkopo huo ilikuwa ujadiliwe na kuidhinishwa Oktoba 30, lakini kutokana na msimamo wa Serikali kutotoa fursa ya kuendelea na masomo wasichana wanaopata mimba, bodi ya benki hiyo ilisitisha kuujadili. Kwa utaratibu wa benki hiyo, kabla mradi wowote haujaidhinishiwa fedha zinazohitajika, huujadili kwanza. “Mradi wa Tanzania haujajadiliwa. Lakini kwa mazungumzo tuliyofanya, utajadiliwa Serikali itakapotimiza masharti tuliyokubaliana,” alisema Dk Ghanem.
Baada ya mazungumzo yaliyofanyika Ikulu jijini Dar es Salaam juzi, Rais John Magufuli alisema benki imekubali kutoa fedha hizo kwa ajili ya ujenzi wa madarasa, mabweni, maabara, nyumba za walimu na vifaa vya kufundishia.
“Kwa hiyo, (Dk Hafez) amekuja kututhibitishia kuwa Benki ya Dunia haitatuacha,” alisema Rais Magufuli.
Vilevile, Dk Ghanem alisema walizungumzia mabadiliko ya Sheria ya Takwimu na wameishauri Serikali kuhakikisha wadau wake wanakuwa huru kukusanya na kutumia takwimu.
Alisema WB haiwezi kufanyakazi bila takwimu ambazo zitakusanywa kwa uhuru, lakini masharti yaliyomo kwenye muswada, huenda yakazorotesha ufanisi wake.
Mabadiliko ya Muswada wa Takwimu yaliyofanyika mwaka huu na kuridhiwa na Bunge, yanazuia mtu au taasisi yoyote kukusanya, kutafsiri au kutumia takwimu lazima zithibitishwe na Ofisi ya Taifa ya Takwimu (NBS).
 
Magufuli rais wetu inabidi awekewe ulinzi mkubwa na mkali. wako watu wamekaa mkao wa kutaka kuhujumu kila kitu..
hakuna mwenye shida naye
wazungu wakitaka kumu-eliminate ni dakika sifuri tu
zile drones zao zina accuracy ya ajabu
 
Tuwe makini jaman km mtu kaifanya poa lazima tumsifie na sio kwamba kua mpinzan kila kitu unapinga, binafsi hongera sana Raisi wetu kwa hii spid "MOTO PAMBA PASI"
spidi gani wakati taifa limejaa woga
ukimkosoa rais kidogo unafungwa au unapotezwa
inflation bado ipo juu
biashara zinafungwa
mnavutaga nini nyinyi!!!!!
 
Eti Viva, mijitu ya ovyo imesababisa uchumi kwenda harijojo sasa ivi iko bize inakwapua mafao ya wafanyakazi na kutengeneza sheria kandamizi. Idiots
 
Angalia mafisadi wanavtotapatapa walikuwa wameshageuza nchi kama kijiwe. Money laundering ilikuwa kama ibada.
Yaani siamini mpaka akina kimei wamebanwa mpaka eanatumia pesa walizoiba au walizopata kimagumashi angalau kuwanusulu wenziwe.
Aise kikwete alitaka kuiuza nchi kabisa wala alikuwa hajali ilimradi rafiki zake wanafaidi tu.
Mpaka akina hawa ghasia walifikia hatua ya kudhani hili ni shamba lao peke yao ndo mana hata mme wao alifanya namna yoyote jk amteu kuw barozi nje akale kama ndugu zake wengine walivyokuwa wanakuala.
Angalia akina nape walivyokuwa wanafaidi korosho kupitia migogo ya wakulima na hakuna aliyekuwa anajali

Budyanhulu wachimbaji adogowadogo walikuwa wanafunikwa na kufia shimoni mamia kwa maelfu wala hakuna aliyekuwa anajali hata jk mwenyewe vilikuwa havimuhusu. Saaa amepatikana wa kuwatetea.
Ilifika mpaka kagame anakuja kuua hapahapa nchini lakini hakuna aliyekuwa anajali mfano ni mauaji ya prof mwaikusa wa udam kagame alimfata hukuhuku akamuua. Sasa hivi thubutu uone jeshi liko imara kwelikweli na rais yuko imara
 
Umetoroka Milembe hospital
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…