Tumeona ulianza na wasomi ,baraza la mawaziri ,ndani ya baraza ni kuanzia Dr na ma Professor, hapo ukawafunga midomo kila mmoja akabaki ana subiri kama vile fisi alivyo subiri mkono wa binadamu kuwa huwenda utadondoka ili autafune, zaidi ukawingizia kale kaujanja ka utumbuaji, ukawa unatumbua asubuhi Dr na jioni ameingia Pr, kwa hilo ndo ukawamaliza kweli kweli.
Ukaona bado , ukaja na uanzishaji watume mbali mbali za uchunguzi zilizo husu mali zetu hasa kwenye sekta ya madini ambayo mabeberu walikuwa wajichotea wanavyo taka.
Hizi tume zika jaa wasomi , lo hapo ndo kabisa ukamaliza mchezo, wote wakaamua kwa dhati kabisa kukutungia wimbo wa kukusifu ili waendane na kasi yako ya uteuzi.
Ulipo ona kawimbo kao kamechanganya ukawaandalia kongamano pale chuo kikuu , ili watanzania wote sasa tuusike huo wimbo, na kweli ulikuwa wakuvutia sana make ulijaa sifa mwanzo mwisho.
Kwa hili kwanini tusikupongeze ? Ukaenda mbali sana ukaona wengine kila siku wako kwenye vyombo vya habari kazi yao ni kukiongelea chama vibaya, hao nao ukawarushia chambo cha madaraka ndani ya chama, bila ya kujitambua wakakimeza, hao sasa ndio wamekuwa wapiga debe wazuri ndani ya chama.
Kwa nini tusikupongeze kwa hili pia ?
Huko umemaliza.
Majuzi tumeona viongozi wa dini nao tayari umesha washika tena wao sasa ni kwa kikombe tu cha kahawa .
Ile habari kila wakati kukicha wana waraka tena kwa kushindana hawa wakiandika huu kesho yake wengine nao wana amka na huu, lililo baki tunashuhudia wale walio kuambia ukatubu sasa wanatubu wao.
Kwa nini tusikupongeze kwa hili nalo?
Umewafanya kuwa na wimbo mmoja wa sifa.
Oooh nilitaka kusahau , kwenye vyama vya upinzani wale vihere here wote ukawavuta , na kuwapa nafasi za kuwa Ma DC, RC, Makatibu kwenye wizara, na hata Uwaziri kabisa, kwa madiwani na Wabunge ukaja na ile Sera ya kata mti panda mti.
Hongera sana kwanini tusikupongeze kwa hili pia ?
Kwa wale vichwa ngumu ndani ya upinzani wasio taka kukuimbia nyimbo za sifa wao ukaona ni vema wakajifunze kutunga nyimbo hizo wakiwa lupango, tena kabla uliwatumia ujumbe kupitia yule rafiki yako , ukimwambia awafikishie ujumbe kuwa waache vihere here wataishia kwenye vyuo vya mafunzo ,na ndivyo ulivyo Fanya ,sasa ni kwa nini tusikupongeze?
Asiye taka kukusifu na kukupongeza huyo ana lake jambo.
Nasema tena hongera Mr president umefaulu kwa hili.
Sent using
Jamii Forums mobile app