Mafanikio ya Rais Magufuli: Viva Rais Magufuli, viva Tanzania

Mafanikio ya Rais Magufuli: Viva Rais Magufuli, viva Tanzania

Mnyonge mnyongeni lakini haki yake mpeni. Huyu mzee anajitahidi ingawa hali ya maisha ya wananchi haijabadilika bado.
Nilikuwa nampinga kila leo kwa miaka 3 au 4 mfululizo but now nimeona ngoja nimuunge mkono.
CCM siiungi mkono maana ndio iliyotuharibia nchi yetu kwa ufisadi na undugu.
Nilikuwa na sababu lukuki za kumpinga huyu mzee ila sasa nimepata sababu zenye nguvu za kumuunga mkono na mguu ikiwezekana.
Sasa nitaanza kumpigia kampeni kila kona na ikiwezekana atawale 15 yrs.
Najua nina nguvu ndogo ktk jamii ila ninauwezo wa kumwongezea kura mia moja 2020 kwa kampeni nitakayompigia kazini na mitaani.
Leo najisikia kumuheshimu sana hadi title yangu nimemwita kwa majina yake yote kamili. Kuna jambo kanifurahisha sana.
Simuhukumu asiyemuunga mkono ila ninamtaka achunguze na kuzipitia upya sababu zake zinazomfanya asimuunge mkono.
2014 nikiwa nafanya kazi BARICK sasa Acacia mgodini Bulyanhulu niliwahi kuwaambia wenzangu kuwa hii nchi tungempata Magufuli ingetulia. Ingawa alipoingia tu baada ya miezi michache 2016 aliposimamisha stahiki za watumishi kwaajili ya uhakiki ndipo nikaanza kumchukia. Sasa simchukii tena.
sawa Bashite tumekusikia. hii sasa itakuwa id yako ya 200 humu JF!

Lissu au Membe mmojawapo akishika nchi 2020, wakolomije jiandaeni kuanza kupiga mbizi kuelekea hapo Comoro ukimbizini!
 
sawa Bashite tumekusikia. hii sasa itakuwa id yako ya 200 humu JF!

Lissu au Membe mmojawapo akishika nchi 2020, wakolomije jiandaeni kuanza kupiga mbizi kuelekea hapo Comoro ukimbizini!
Kwa I'd hii ukisoma post zangu za nyuma huko utajua kuwa nilikuwa upande gani.
 
Sawa mkuu. Japo mimi simuungi mkono ila jitihada za maendeleo ninazikubali
 
Ukimuunga mkono usiwe kipofu wa kutoona mabaya pia, Ukibeba Akili yako itakuwa vema kwani utaweza kuelewa magufuli vizuri
 
Kweli wewe ni kiazi sasa ulikua unampinga kwasababu gani

Nyie ndio mnaojenga picha mbovu kwa vyama vyenye mawazo tofauti na ccm

Angalau ungesema unamkosoa au unampinga kwa baadhi ya mambo, eti unasema "unampinga kila leo"

Nyie ndio wale wale tuhuwa fata upepo.. unapoongea case yako ya kuunga mkono naelewa kama unajitambua au hujitambui, hamna alie mkamilifu kwa 100% sasa unapounga mkono na mguu kuwa makini mzee.
 
Ni haki yako kikatiba hakuna anayeweza kukukataza kumkataa au kumkubali na kuhusu kutawala miaka 15 katiba ya nchi yetu haipo na infact nchi zilizoendelea wenyew hawana muda mwingi hvyo kwa nin sisi watu wa ku copy na ku paste tufanye hivyo??? Na just imagine kama kikwete angekaa muda mwingi huyo mbora wako magu angepata muda wa kuingia madarakani na wew kuona hyo talanta yake katika uongozi. Cha msingi ambacho unatakiwa kujua ni kwamba kila kitu kina muda wake na maendeleo siku zote yanaletwa na mabadiliko, na huwez kujisifu unaweza kuishi na watu vizur wakati unaishi na watu wale wale ulio wazoea.
 
Wakuu nahisi ikitokea Raisi akaugua na akawa hawezi fanya ziara wala kuhutubia basi nahisi wafanyakazi hata kazini hawataenda.

Viongozi watakuwa wanalala hakuna kwenda kazini na hakuna kazi itakayo fanyoka. Kwa sasa hatuna mifumo bali anategemewa mtu mmoja mmoja.

Vipi huyo mtu asipo kuwepo kazi zitafanyika vipi? Nchi itaenda kweli? Kodi itakusanywa? Hayo Madarasa sijui Stend zitajengwa?

Sipati picha
 
Wakuu nahisi ikitokea Raisi akaugua na akawa hawezi fanya ziara wala kuhutubia basi nahisi wafanyakazi hata kazini hawataenda.

Viongozi watakuwa wanalala hakuna kwenda kazini na hakuna kazi itakayo fanyoka. Kwa sasa hatuna mifumo bali anategemewa mtu mmoja mmoja.

Vipi huyo mtu asipo kuwepo kazi zitafanyika vipi? Nchi itaenda kweli? Kodi itakusanywa? Hayo Madarasa sijui Stend zitajengwa?

Sipati picha
Ndiyo maana Barack Obama kwa mara ya kwanza alipotembelea Adrika akiwa Rais wa Marekani nchini Ghana alisema "Africa doesn't need strongmen, it needs strong institutions,”

Other wise it is tyranny!!
 
Stendi[emoji32][emoji32]
Wakuu nahisi ikitokea Raisi akaugua na akawa hawezi fanya ziara wala kuhutubia basi nahisi wafanyakazi hata kazini hawataenda.

Viongozi watakuwa wanalala hakuna kwenda kazini na hakuna kazi itakayo fanyoka. Kwa sasa hatuna mifumo bali anategemewa mtu mmoja mmoja.

Vipi huyo mtu asipo kuwepo kazi zitafanyika vipi? Nchi itaenda kweli? Kodi itakusanywa? Hayo Madarasa sijui Stend zitajengwa?

Sipati picha
 
Unalipwa kiasi gani wewe kwa siku na huyo magufuli wako? Maana muda wote unawaza kumsifia, kumsujudia, kumpamba na kumtukuza tu! Hivi huchoki?
Huyu arudie tena kusoma kitabu cha walenga wapya, wenzie wanajikomba wanapata vyeo, shairi la walamba nyayo, " wajikomba komba kusifia ili wapate tende na aluwa" mwenzetu kipi hapatacho?
 
Nampongeza Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe, John Pombe Magufuri kwa kazi nzuri inayoonekana machoni mwa watanzania tangu 2016 hadi leo.
 
Back
Top Bottom