Mafanikio ya Rais Magufuli: Viva Rais Magufuli, viva Tanzania

Uhai wa kiumbe chochote unaanzia kwa kuvuta na kusambaza vizuri hewa safi mwilini na kuitoa iliyotumika nje ya mwili. Watanzania tunayo bahati kubwa ya kumpata mtu anayetuzibulia pua na mapafu ya nchi ili viungo vingine viweze kufanya kazi zake vizuri. Mpaka sasa Rais Magufuli hajakosea kitu chochote hasa kutokana na alivyoikuta nchi.

Nchi ilipokuwa imefikia kwa vyovyote vile ingehitaji mtu kama Rais Magufuli ambae angefufua nidhamu ya kazi, kuondoa mazoea, kufufua utendaji wa jeshi la polisi na watendaji, kufufua barabara, reli, umeme, viwanda, ndege na meli ambayo ndiyo pua, mapafu, moyo na mishipa ya damu ya taifa lolote.

Tumpe kura 2020 ili tumtume tena kuhakikisha kuwa anaboresha na kushuhulikia utawala wa sheria (mahakama, katiba, vyama vingi), uvuvi mkubwa, kilimo kikubwa, uchimbaji mkubwa, utalii, elimu ya kati na ya juu, na kipato cha watumishi wa umma (purchasing power).

Hata wakoloni walifanya hivi, wanafanya hivi na wataendelea kufanya hivyo.
 
Nchi ilishaharibika mno

Magufuli amekuja kuibadilisha Ndio maana Mafisadi na wauza madawa ya kulevya wanampinga sana
 
Mnapiga kelele sana mnamchanganya huyu Magufuli. Hamna Rais aliyepita ambaye alikuwa msafi wote walikuwa wabaya tena wabaya haswa.

Magufuli anajaribu kufanya vitu ili nchi iende mbele, tuongee ukweli jamaa anafanya kazi sana.

Hayo mambo ya haki za binadamu toka kipindi cha nyerere yalikuwepo. Watu walipotea na waandishi walidhibitiwa.

Kwa nini hawamu hii ya tano kila mtu anapiga kelele?

Mimi sio mwanasiasa ila naumia sana mnavyomkejeli Magufuli. Please acheni.
 
Tumwache magufuli afanye yake.
Ungekuwa familia ya mawazo
Ya lissu,Ya Ben saanane,ya mamia waliokufa rufiji,usingesema haki za binadamu hazina maana.Najaribu kuimagine ufahamu wako naona ni mdogo sana.Huwezi kupuuza haki za binadamu hata kama kuna udhaifu namna gani.

Kuna mambo mengi magufuli anafanya ni mabaya ambapo hata kwa haraka ukiweka mazuri na mabaya mabaya yanafuta mazuri yote maana mtu anayemrisha kuwafanyia ubaya wenzie huyo ni zaidi ya mbwa.Biblia yenyewe imesema tujihadhari na mbwa sasa kwa nini tusijihadhari na mbwa jiwe?
 
Afanye kazi kwa misingi ya katiba na shria sio kufanya kazi za nchi kama anafanya kazi za nyumbani kwake, kujimwambafy kwake na kupoteza watu na kuua afanye kwenye himaya yake na Janeth wake..
 
Kwani kazi ya rais ni ipi unayoijua
Siijuhi ambayo tumemzuia wakati tulimkabidhi kila kitu .Napata wasiwasi hata yeye hajui kazi yake.Ni kama urudi nyumbani uanze kukumbusha watu kuwa unajua mimi ndii baba mwenye nyumba haaa has very thing
 


WATANZANIA wametakiwa kuunga mkono harakati za maendeleo zinazotekelezwa na Rais John Magufuli huku wakifahamishwa kuwa ni mwendelezo wa ndoto za Baba wa Taifa, Mwalimu Julius Nyerere aliyokuwa nayo wakati wa uhai wake.

Mmoja wa wazee waliowahi kufanya kazi na Mwalimu Nyerere kabla na baada ya Uhuru wa Tanzania Bara Desemba 9, 1961 ambaye kwa sasa ni kati ya wanaounda Chama Cha Mapinduzi (CCM) - Veterani, Yahaya Ngoma amesema hayo akizungumzia miaka 58 ya Uhuru wa Tanzania Bara.

Mzee Ngoma alizungumza na gazeti hili kuhusu harakati za Mwalimu Nyerere katika mapambano yake ya kutafuta Uhuru wa iliyokuwa Tanganyika na baadaye Tanzania.

Mzee huyo ambaye alikuwa kati ya vijana waliofanya kazi kwa ukaribu na Mwalimu Nyerere tangu wakati wa chama cha TANU hadi ulipopatikana Uhuru na kisha kuundwa kwa CCM, alisema Mwalimu Nyerere alikuwa na ndoto kubwa nyingi ambazo hadi anakufa nyingine hazikutimia na sasa Rais Magufuli ndio anazitekeleza.

Amesema akiangalia mambo mazuri ambayo Rais Magufuli anayafanya kwa sasa mengine ni mwendelezo wa harakati zilizoanzishwa na Baba wa Taifa aliyeiongoza Tanzania tangu ilipopata Uhuru hadi alipong’atuka 1985. Amesema Mwalimu Nyerere alikuwa mzalendo ambaye hadi anaipatia nchi Uhuru ilikuwa haina vyanzo vingi vya mapato, wasomi wengi na hata hamasa ya maendeleo haikuwa kubwa kwa wananchi ikilinganishwa na ilivyo sasa.

Alisema Rais Magufuli ameichukua nchi ikiwa kwenye mikono ya wasomi ambapo kwa sasa wenye elimu ni wengi huku pia nchi ikiwa na vyanzo vingi vya mapato ambavyo asilimia kubwa vimevumbuliwa na Rais huyo.

Kuhusu mawazo ambayo alikuwa nayo Mwalimu Nyerere lakini hayakufanyiwa kazi ni pamoja na wazo la Mradi wa Kufua Umeme wa Maji katika Maporomoko ya Bonde la Mto Rufiji ambao tangu akiwa madarakani Baba wa Taifa alikuwa akipambana kuutekeleza bila ya mafanikio na Magufuli amemuenzi kwa kuuendeleza mradi huo.

Pia alibainisha kuwa wazo la kuhamia Dodoma kama Makao Makuu ya Nchi ni kati ya mawazo ambayo Mwalimu Nyerere aliyaasisi lakini yamekuja kutekelezwa na Rais Magufuli katika uongozi wake wa muhula wa kwanza. Alisema uimarishwaji wa Kampuni ya Ndege Tanzania (ATCL) ni kati ya mambo ambayo Mwalimu hadi anatoka madarakani alikuwa ameyaimarisha lakini yakaja kutetereka baadaye, ila Magufuli kwa miaka minne ya kwanza ya uongozi wake ameyatekeleza.
 
Magufuli amekuja wakati sahihi kuikomboa Tanzania iliyokuwa inatafunwa na mafisadi
 
inategemea ni ndoto ipi, ndoto imeotwa mwaka 1980 kuitekeleza 2019 - baada ya miaka 39 yaweza kuwa impractical vilevile.
 
Kongole kwa mwana Tanzania na muhitimu bora wa siasa za Mwalimu Nyerere.

Unatekeleza kwa vitendo na kasi yale aliyoyataka the late Julius Kambarage Nyerere.

Kuna wakati kama Watanzania wazalendo tuliichukia CCM kutokana na matendo ovu ya wana CCM mafisadi na tukatamani alternative ambayo bila kujua ilikuwa ni alternative ya kishetani.

Sasa tumeelewa kweli ya chama cha ukombozi Tanzania na Afrika na hatuna budi kuifuata, kuilinda na kuielezea.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…