Mafanikio ya Rais Magufuli: Viva Rais Magufuli, viva Tanzania

Sie tunachompongeza magufuli ni kutuonyesha thamani ya kodi yetu na kuisimamia.

Kupunguza kabla ya Magufuli serikali ilikuwa na akaunti zaidi ya 1500 hali iliyopelekea kupotea kwa mapato mengi na sasa ina akaunti moja. Ndio maana ukilipia huduma yoyote kwa serikali unapewa kumbukumbu namba.

Zamani tuliambiwa rais asiposafiri tutakufa njaa..tumeona ndani ya miaka mitano mushahara imeendelea kulipwa, usimamizi na ujenzi wa miradi mikubwa kama umeme, maji, vituo vya afya na hospitali za rufaa kama mara, mtwara na dodoma, elimu bure, kuongezeka kwa mikopo vyuo vikuu, ukarabati wa shule kongwe, ujenzi wa vyuo na shule, ujenzi na upanuzi wa barabara, bandari na viwanja vya ndege, ujenzi wa meli na ununuzi wa ndege, ufufuaji wa mazao kama mkonge, korosho, pamba na michikichi, ujenzi wa madaraja.
 
zaidi ya kugawa mapapai na kula mahindi barabarani, mradi wowote ni fedha za mikopo na mosaada toka nje, nyingine anazogawa kama njugu ni za serikali sema hazikaguliwi, tubaki tu kama wajinga
 
Hakuna hata mmoja zaidi ya kutuibia 1.5trilion.

Miradi yote ni ya kukopa na ufadhili wa mabeberu tu. Hata daraja alikopa.
 
zaidi ya kugawa mapapai na kula mahindi barabarani, mradi wowote ni fedha za mikopo na mosaada toka nje, nyingine anazogawa kama njugu ni za serikali sema hazikaguliwi, tubaki tu kama wajinga
Kumbe anakopa kwa mabeberu??
 
Ni mwaka 2015 tuu tuliomba sana Mungu atupe rais jasiri, chapakazi na mwenye maamuzi magumu na sahihi tukampata
Your browser is not able to display this video.


Sasa turudishe shukrani kwa Mungu
 
•Wasione vyaelea vyaundwa, ukishatengeneza barabara umerahisisha huduma za jamii, kama ni mtu anataka kwenda hospitali atawahi haraka, hata kama anataka kuwahi kwenda kuposa atamkuta binti anamsubiri kwa sababu barabara ni ya lami•
 
Mtu awahi hospitali halafu aambiwe akanunue dawa.
Tunywe tu miti shamba mkuu
Jengeni lami tarime kwenda Mugumu, kwani tumewakosea nini
Ukosefu wa barabara ya lami huku kunazuia utalii
 
Hivyo vinavyoundwa na kuelea vinaundwa kwa fedha zao za mfukoni au za wananchi? na kama ni fedha za wananchi lazima waunde wao tu?
 
halafu kuna hawa watu NHIF wametoa matibabu mengi sana ktk orodha ya kutibiwa kwa bima!
Sijui hawa watu wanatupeleka wapi!
halafu eti ukifikisha miaka 60 hakuna tena Bima, huu si udhalilishaji jamani?
Tupige kelele kupinga huu unyanyasaji uliopindukia!
 
Wanabodi,Kila kitu na wakati wake twende turudi JPM ni mchapa kazi na itabaki hivyo moyoni mwetu

Akiwa waziri Magufuli amepiga sana kazi wote tulimpenda sana

Tumuheshimu kwa uchapa kazi wake kwa Taifa hili,Alijitoa sana sana JPM

Tumkumbuke kwa mema yote aliyotenda akiwa waziri

Rais Magufuli anapiga kazi sana tangu akiwa waziri mpaka leo,

Rekodi yake itadumu daima kama mtu mwenye msimamo na asiyeyumba

Kila mtu na Mapungufu yake ingawa watu hupuuza mazuri

Ishu ya korona Magufuli ameshinda

Ishu ya kurudisha heshima maofisini Magufuli ameshinda

Tuongee na tubishane kuna mambo Magufuli ni special na unique

Hakika october tutashinda kwa mbinu za kisasa zaidi na zilizoboreshwa

Nipo na Magufuli wakati wote ,Tutashinda
Mambo ya heshima serikalini itabaki daima mioyoni yetu

Je? Chadema wanamuamini bado lowasa au Sumaye
 
Amefanya kazi kubwa sana ya kuua upinzani upinzani umekufa kabisa.
2.Amefanya kazi kubwa sana ya selikali yake kupiga wabunge risasi.
3.Amefanya kazi ya selikali yake kupoteza watu.
4.selikali yake imefanya kazi kubwa sana ya kuajiri vijana.
5.selikali yake imefanya kazi kubwa sana ya kuteka watu.

Hakika JPM amslefanya kazi kubwa sana
 
Ndugu zangu naomba nianze kwa kunukuu kiapo cha Rais John Pombe Magufuli siku ile ya tarehe 05/11/2015 mbele ya Jaji Kiongozi Mh. Mohamed Chande Othman katika uwanja wa Uhuru baada ya kutangazwa mshindi wa Urais na Tume ya Uchaguzi chini ya Jaji mstaafu Damian Lubuva.


...

1. Mimi John Pombe Joseph Magufuli naapa kwamba nitakuwa mwaminifu kwa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na nitalinda na kuitetea Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ilivyowekwa kisheria. Ewe Mwenyezi Mungu nisaidie.
2. Mimi John Pombe Joseph Magufuli naapa nitatenda kazi zangu za Urais wa Jamhuri ya Tanzania kwa uaminifu kwa kutimiza wajibu wa kazi hizo kwa bidii na moyo mkunjufu na kwamba nitawatendea haki watu wote kwa mujibu wa sheria, mila na desturi za Jamhuri ya Muungano wa Tanzania bila woga, bila upendeleo, huba wala chuki. Ewe Mwenyezi Mungu nisaidie.
3. Mimi John Pombe Joseph Magufuli naapa katika kutekeleza madaraka niliyopewa kwa mujibu wa Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Ewe Mwenyezi Mungu nisaidie.

Sasa...

Pamoja na Rais John Pombe Magufuli katika awamu yake ya kwanza kushindwa kuilinda, kuitetea na kuiheshimu Katiba ya Jamhuri ya Tanzania kama alivyoapa, anapata wapi ujasiri wa kuwaangalia Watanzania kwa ujumla wao usoni na kuwaomba wamuongezee awamu nyingine? Ili iweje?

Ili azidi kuisigina Katiba kwa kutotenda haki kwa Watanzania wote kwa mujibu wa sheria, mila na desturi za Jamhuri ya Muungano wa Tanzania bila woga, bila upendeleo, huba wala chuki? Huu uthubutu anautoa wapi?

Pamoja na Rais John Pombe Magufuli katika awamu yake ya kwanza kuruhusu uwepo wa kikundi kinachodaiwa cha wasiojulikana kuwateka, kuwatesa na kuwapoteza raia wema wa taifa hili, anapata wapi ujasiri wa kuwaomba raia wenye hofu na usalama wao wamuongeze miaka mingine mitano? Ili iweje?

Ili wasiojulikana waendelee na vitendo vyao viovu dhidi ya raia wema wa nchi hii kwa kuwadhulumu haki yao ya msingi ya kuishi kwa uhuru, amani na usalama wao na mali zao bila hofu na woga? Huu uthubutu anautoa wapi?

Pamoja na kijana mwana harakati Ben Saanane kupotea na hadi leo haijulikani aliko katika awamu yake ya miaka mitano, Rais Magufuli anapata ujasiri wapi wa kuwatazama usoni familia yake, wazazi wake, ndugu zake, rafiki zake na Watanzania wenzake na kuwaomba wampe kipindi kingine? Ili iweje?

Ili azidi kuwatisha vijana kama Ben Saanane kwamba kwa kutumia uhuru wao wa maoni kikatiba katika kuikosoa serikali na kiongozi wake mkuu wanahatarisha maisha yao hivyo wawe tayari kupotezwa? Huu uthubutu anautoa wapi?

Pamoja na mwandishi wa habari Azory Gwanda kupotea katika mazingira tatanishi na juhudi kushindikana za kumpata, Rais Magufuli anapata wapi ujasiri wa kuwatazama usoni familia yake, jamaa zake, waandishi wenzake na Watanzania wenzake na kuwaomba wampe kura zao? Ili iweje?

Ili ujumbe uwafikie Watanzania na waandishi wa habari popote walipo kwamba kuandika habari zisizoipendeza serikali hii na kionozi wake mkuu ni kuhatarisha maisha ya huyo mwandishi? Huu uthubutu anautoa wapi?

Pamoja na kituo cha utangazaji cha ClousFM kuvamiwa usiku wa manane na kiongozi wa mkoa akifuatana na askari wenye bunduki na kutaka kituo kiandike habari anazotaka yeye, Rais Magufuli anapata wapi ujasiri wa kuomba muhula mwingine wa vitendo vya aina hiyo kuendelea? Ili iweje?

Ili vituo vya habari popote vilipo, visitumike kwa namna yoyote kuwapasha wananchi habari ambazo serikali hii na kiongozi wake mkuu hawataki katakata wananchi wazipate kwa namna yoyote ile? Huu uthubutu anautoa wapi?

Pamoja na Mbunge Mh. Tundu Antiphas Lissu kumiminiwa risasi mchana kweupe na kunyimwa stahiki na haki yake ya kutibiwa kama Mbunge, Rais Magufuli anapata wapi ujasiri wa kuwaangalia wapiga kura jimboni kwa Lissu na bila kupepesa macho kuwaomba kura azidi kuwa Rais wao? Ili iweje?

Ili wakae wakijua kuwa yaliyompata Mh. Tundu Antiphas Lissu yataendelea kama wapiga kura wa jimbo hilo wataendelea kuwa wakaidi na kumchagua mwakilishi wanayempenda na si wanayeletewa? Huu uthubutu anautoa wapi?
  • Pamoja na mateso waliyopata wasanii kama Roma Mkatoliki wa kutekwa kuteswa na kudhalilishwa kote huko, bado Rais Magufuli ana ujasiri wa kipekee wa kuambatana na wasanii na wao kulazimika kumpigia kameni katika juhudi zake za kuomba kura aongezewe awamu nyingine, ili iweje? Hata sijui!
  • Pamoja na mateso waliyopata wakulima wa korosho mkoani Mtwara, Rais Magufuli anategemewa kufika huko na kwa ujasiri usio wa kawaida, ngeni na usioambatana na Utanzania wetu, na kuwataka wana Mtwara kumpa kura aweze kuwaongoza tena kwa muda wa miaka mitano, ili iweje? Hata sijui
  • Pamoja na mateso waliyopata wana Dar es Salaam kwa kuvunjiwa nyumba zao bila fidia na kulazimika kulala nje pamoja na watoto wao, Rais Magufuli anategemewa kuzuru eneo husika na kwa ujasiri usio wa kawaida kuwaomba wampigie kura katika uchaguzi ujao aendelee kuwa Rais wao, ili iweje? Hata sijui
  • Pamoja na dhulma uliombatana na unyang'anyi wa wazi waliofanyiwa wafanya biashara nchini hadi kufilisiwa katika awamu hii ya miaka mitano, Rais Magufuli anategemewa kuzunguka Mtwara hadi Kagera, Unguja hadi Kigoma na kwa ujasiri uso kifani, kuwaomba kura zao waendelee kukamuliwa! Ili iweje? Hata sijui
  • Pamoja na...ningeweza kujaza kitabu kizima.
Pamoja na pamoja yote hadi leo hatma ya Ben Saanane haijulikani, hatma ya Azory Gwanda haijulikani na hatma ya waliopotea haijulikani.
Pamoja na pamoja yote hadi leo waliomteka Roma hawajulikani, waliomteka MoDewji hawajulikani na waliommiminia Lissu risasi hawajulikani.
Pamoja na pamoja yote hatma ya wafanya biashara haijulikani, hatma ya wakulima (wa korosho) haijulikani na hatma ya wafanya kazi haijulikani
Pamoja na pamoja yote CCM ni ile ile, mgombea wa Urais kutoka CCM ni yule yule, Katiba ni ile ile na wasiojulikana bado hawajulikani.
Pamoja na pamoja yote Rais Magufuli anaomba kura na akichaguliwa ataapa tena kiapo kile kile. ...je Watanzania wenzangu tutapona?

Hakika uthubutu wa Rais John Pombe Magufuli si tu hauna mfano, ni ngeni na nakataa si wa Kitanzania.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…