Mafanikio ya Rais Magufuli: Viva Rais Magufuli, viva Tanzania

Nampongeza sana Rais Magufuli kwa kutekeleza ahadi zake na hivyo kutufanya watu tulomchagua kutembea kifua mbele huku mtaani tukitamba dhidi ya wale walotubeza kuwa Magufuli hatoweza kuubadili mfumo ulomlea
Sasa nadhani wanaona haya. Viva Magufuli
Kabadili mfumo UPI ?
 
JPM anatupa matumaini katika nchi yetu hasa anavyoelekeza matumizi ya pesa kwenye mambo muhimu. Mungu ampe uzima na afya ya kuendelea kutupa matumaini ya kukua kwa uchumi wa nchi yetu hasa katika swala la ufufaji viwanda ili vijana wengi wapate ajira.
 
Tumbua tu majipu usiogope na Hakimu au jaji atakaye itaka serikali kulipa fidia kwa mafisadi wa sukari na wengineo naye atumbuliwe tu...nchi isonge mbele wananchi tumechoka.
 
Wacha niseme kutoka moyoni kabisa kuwa mimi CCM na Magufuli hawakupata kura yangu kwasababu ya kile kilichozoeleka kuwa ni watu wa kubebana na kulindana.
Lakini tangu Magufuli ameingia ameanza kunipa tumaini la TZ yangu niitakayo, na nilikuwa namtaka kiongozi ambaye akiingia atawabadilisha watu/watumishi kuwa walizonazo ni dhamana na si kuwa wao ni wafalme ila sisi ( wananchi) ndio mabosi wao.
Nchi ilifikia hatua mkuu wa mkoa/wilaya au wakurugenzi wa wilaya/mkoa ni kama miungu watu akosolewi na muda wote yeye yuko ofisini tu na mwendo wa kuiba tu na kujaza takwimu za uongo. Leo nadhani mnaona wakuu wa mikoa, wilaya,wakurugenzi na hata wakuu wa idara za serikali wanapiga kazi na wanatembelea sehemu za miradi au kusikiliza matatizo ya wananchi.
Leo hii wafanyabiahara walitaka waiendeleza tabia yao ( maana itakuwa hawajaianza leo wameshazoea) ya kuihadimisha bidhaa ili ipande thamani halafu apate faida kubwa sana wakati wananchi tunateketea kwa ukosefu wa sukari kisa eti yeye ana mtaji basi awatese wasiokuwa na uwezo huo.
 
SUKALI ILIOFICHWA IMESHAGAWIWA. ITAGAWIWA BURE?
HATA MIE NAPENDA RAIS HUYU KULIKO WALIOPITA LAKINI ANISHAWISHI NISIBADILIKE
 
Kuhusu viongozi wa nchi hii walijisahau sana... Japo yapo madhaifu kwa sasa ila naamini tutarekebisha taratibu
 
Hii inauma sana umeficha sukari tani 3000 halafu inakuja kutolewa bure watu wanagaiwa daaaah!!!umepoteza hela nyingi mno
 
Kuweka sawa hili swala kila mtu humu ndani ajue kuwa mahakama ya mafisadi inakuja ambapo DPP atapeleka Mashauri yote ytasikilizwa... Hakuna fisadi atapona amini hivo... Inaanza July

Hamtaamini mtakayosikia
 
Magufuli imeshakuwa dawa ya pressure, wala hauitaji dawa nyingine, Presida ni noma ,anatengeneza heshima, wazee wa michongo siku hizi wananyooka.
 
hahahahha mahaba niue, wacha wapambane yetu maombi ila future yake naona giza
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…