Hongera Makonda na Serikali ya JPM
Natoa pongezi zangu za dhati kwa rais wa Jamhuri yetu,Jeshi la polisi,Mkuu wa mkoa wa Dar es salaam,Baraza la mawaziri,bunge,mahakama kwa kazi nzuri mnayofanya ya kutuletea maendeleo.
Mnafanya jambo zuri sana katika kuwahamasiha wananchi washiriki katika maendeleo ya taiga lao.
Mmewatafutia madaktari ajira nje ya nchi na pia itakuwa vizuri mkiwatafutia na walimu na wengine wasokuwa na ajira.
Vile vile mnajenga maflyover dar es salaam
Mnasapoti wasanii kama vile diamond na shilawadu.Hongereni
Mmepiga vita watumishi hewa,vyeti fake,wala rushwa na kero nyingi
Mmesimamia haki katika mahakama na kuboresha huduma za jamii.
Madaktari wamejaa hospitali.wanafynzi wana walimu wa kutosha mikopo ya chuo inapatikana kwa urahisi na upesi.mishahara imeongezeka maradufu na mfumuko wa bei umepungua.
Rushwa imepungua na haki inatendeka.
Makahaba,mashoga na vibaka wameisha.
Ajita njenje kuanzia ofisini,mashambani na hata viwandani.
Viwanda vinaongezeka na tunazalisha asilimia 75 ya bidhaa tunazotumia kwa ajili ya uzalishaji.
Uwekezaji umekua maradufu.
Hongereni sana kwa kazi nzuri mnayofanya ya kufuta sheria kandamizi na kutunga sheria ambazo hazilindi watawala bali zina wawajibisha watawala.
Mheshimiwa rais serikali yako ina nguvu imejipanga inajielewa na haina walevi walevi.Wapiga dili wote mmewafunga.
Tunapenda sana viongozi wetu na tuna waomba mkaze buti zaidi kutuletea maendeleo.
Barabara za halmashauri zimetengenezwa vizuri,shule zimerekebishwa,mfuko wa maafa umefanya kazi vizuri kuwasaida wana kagera na wale waliopigwa na mafuriko...