Jamani huyu baba Mungu amuweke tu miaka mingi. Yaan kabla ya Magufuli hili taifa lilikuwa linatafunwa na kila mtu kuanzia wafagizi hadi mameneja na wakurugenzi kama shamba la bibi vile!!!
Ahsante sana kudhibiti rushwa, walau sasa hivi hakuna rushwa kila mahali, ingawa inasemekana kuna jipu anajiita 'Jiwe' na mwanae madereva wanatafuna bado hazina ya nchi yetu. Raisi wetu mpenzi Magufuli najua hujashindwa kudhibiti yote haya.
Ahsante kwa kutujali wakulima mhe baba jpm mpenzi wa watu na malaika!! Najua hii ya korosho ni mwanzo tu, mwakani utapanga bei ya mazao yote, na kama mfanyabiashara anaona haimlipi jesh litanunua nyanya, pilipili, mahindi, maharage, mchicha na kila zao kwa bei ya maslahi yako baba magufuli then watasaga mahindi hata kwa mabuti kudadadeki!!
Hakuna kama wewe mhe rais, mpemzi wa wanyonge. Ahsante kwa kutuletea ndege nzuri maana hata kama wengi wetu hatupandi, walau tunaondoa ushamba kwa kuziona zikipepea angani!!!
Ahsante kwa kufungia hela BOT Maana mabenk yalizidi utapeli, bora tu hela zipotee mzungukoni na matajiri waishi kama mashetani kama ulivyo sema rais wetu mzuri.
Yaani we mbaba ninavyo kupenda,
Mmmmwaaaaah!!!