Mafirst born muishi maisha marefu

Mafirst born muishi maisha marefu

Etugrul Bey

JF-Expert Member
Joined
Aug 6, 2020
Posts
6,514
Reaction score
15,247
Screenshot_20250104_222316_Google.jpg


Kuwa wa kwanza kuzaliwa hakika ni mapambano makubwa sana,kwasababu moja kwa moja unajikuta majukumu yanakuandama kwa namna moja au nyingine

Hawa watu wanajitoa sana kuokoa jahazi lisizame katika familia,tena katika hizi familia zetu ambazo bado hazija jipata hakika mafirst born wanajitoa sana kwa kupenda au kwa kutokupenda,na watafanyaje angali wanategemewa wao

Ni mara nyingi unawakuta hawa watu wanashindwa kufanya mambo yao ya maendeleo kwasababu wapo pale kusapoti familia zao na wadogo zao,kwahiyo next time ukimuona first born hajajenga au kujiimarisha kiuchumi basi tambua ana mzigo mkubwa wa ndugu na jamaa wanamtegemea

Najua kuna baadhi mtasema hayo sio majukumu yake,bali majukumu yake ni kuangalia watoto wake na familia yake,nasema hivi kwa mtu ambaye anajitambua hawezi acha wazazi wake au ndugu ambao wanahitaji msaada kisha akawapuuza,hilo haliwezekani kwasababu hao ni jamaa zake na watu wake wa karibu

Kwao wao kuwaona ndugu zao wanaenda shule kwa msaada wao ni faraja kubwa sana,kuwaona ndugu zao wanapata mkate wao wa kila siku ni jambo lenye kuwapa faraja sana,kuiona familia inatabasamu ni jambo lenye kuwapa amani katika nyoyo zao

Mafirst born aluta continua kama mlivyoanza na ndio mtakavyo maliza,daima endeleeni kushow love kwa ndugu jamaa na marafiki,mmezaliwa wa kwanza kwakuwa mna mission hapa duniani,nyie ni viongozi,na sifa kubwa ya kiongozi ni kutatua shida za ndugu zake na jamaa zake

Kiongozi siku zote huwa baina ya shida za watu wake na kutafuta namna ya kuzitatua au kama sio kuzipunguza,haukuwa mzaliwa wa kwanza kwa bahati mbaya bali ili upambanie jamii yako

Nafahamu huwa mnajitoa sana kwa ajili ya ndugu hata wakati mwingine mnakosa yale ambayo mnayapenda katika nafsi,nawapa moyo kwamba,hakika mnabadilisha maisha ya watu wengi sana,huenda msipate nafasi ya kuambiwa hayo lkn mfahamu kwamba juhudi zenu haziendi bure

Endeleeni kupambana mpaka tone la mwisho la damu

Ni hayo tu!
 
Nilipata kazi kwa muongozo na ushauri wa bro angu wa kwanza bila kupiga simu wala kujitambulisha kwa mtu yoyote. Ilikua ni simu ya mazungumzo yasiyozidi dakika 15 ilitosha kutoa maelekezo ya nini kifanyike katika kila hatua sikua na notebook ila naiamini akili yangu kwa kunote vitu fasta.

Baada ya kupata kazi ananiunganisha na mtu wa kada kama yangu kutoka ofisini kwake kwa ajili ya maulizo kuhusiana na kazi, pamoja na hivyo bado hakuacha kujua maendeleo ya kazi na changamoto zake. Huyu jamaa huwa namuona kama baba mdogo namuheshimu kinoma. Kanikata miaka 9

First borns pokeeni maua yenu
 
Dah jioni hii kuna boda yeye kwao ndio wa Kwanza na ukiangalia ana miaka kama 24 hivi,amenibeba akanipa story mpk mwenyewe nikaona huluma.Yeye ndio wa Kwanza ana wadogo zake 2 ana Baba na mama wanaomtegemea kisha ana mke ambaye amepata stroke hao wote wanaomtegemea yeye na kazi yake ni kukesha,Ananiambia kwa mama anaacha elfu 7 kila siku sababu alimfungulia kiduka mama yake Baba akawa anachukua vitu mpk kimefilisika hivyo bado mzigo ni wake,bado Kwa mkewe angalau mke wake alikuwa na kazi kabla hajapata maswaibu aliyonayo , kiujumla nilimuonea huluma Sana mpk Sehemu ya Huku ikabidi niliache teni langu kama sadaka, sababu sote tumepitia misoto hiyo
 
Wazaliwa wa kwanza ni baba mbadala,Esau alizalau uzaliwa wake wa kwanza akamuuzia mdogo wake kwa chakula cha dengu akawa ndio ameuza baraka zote za uzaliwa wa kwanza,Yakobo ambaye ndiye mdogo wake Esau ndiye Israel wa leo taifa lenye nguvu duniani.
 
Nilipata kazi kwa muongozo na ushauri wa bro angu wa kwanza bila kupiga simu wala kujitambulisha kwa mtu yoyote. Ilikua ni simu ya mazungumzo yasiyozidi dakika 15 ilitosha kutoa maelekezo ya nini kifanyike katika kila hatua sikua na notebook ila naiamini akili yangu kwa kunote vitu fasta.

Baada ya kupata kazi ananiunganisha na mtu wa kada kama yangu kutoka ofisini kwake kwa ajili ya maulizo kuhusiana na kazi, pamoja na hivyo bado hakuacha kujua maendeleo ya kazi na changamoto zake. Huyu jamaa huwa namuona kama baba mdogo namuheshimu kinoma. Kanikata miaka 9

First borns pokeeni maua yenu
Nimeipenda hii
 
Dah jioni hii kuna boda yeye kwao ndio wa Kwanza na ukiangalia ana miaka kama 24 hivi,amenibeba akanipa story mpk mwenyewe nikaona huluma.Yeye ndio wa Kwanza ana wadogo zake 2 ana Baba na mama wanaomtegemea kisha ana mke ambaye amepata stroke hao wote wanaomtegemea yeye na kazi yake ni kukesha,Ananiambia kwa mama anaacha elfu 7 kila siku sababu alimfungulia kiduka mama yake Baba akawa anachukua vitu mpk kimefilisika hivyo bado mzigo ni wake,bado Kwa mkewe angalau mke wake alikuwa na kazi kabla hajapata maswaibu aliyonayo , kiujumla nilimuonea huluma Sana mpk Sehemu ya Huku ikabidi niliache teni langu kama sadaka, sababu sote tumepitia misoto hiyo
Huu ni ushuhuda tosha kwamba hawa watu ni watu na nusu hakika wanapambana sana

Duh huyu jamaa uliyemuelezea ana changamoto sana kwakweli,mungu amsimamie sana

Nimeboreka na tabia ya baba yake,mtu amemfungulia biashara mama yake halafu baba anaifilisi,hakika sio baba wote wana sifa ya kuwa baba
 
Back
Top Bottom