Mafundisho mapya ya kuhusu miujiza (masuala ya kiroho) kutolewa na Kanisa leo: Kwa nini historia inajirudia leo kutoka mwaka 1978?

Yawezekana, weka link ya hiyo channel tuone
 
Yote hayo ni maarifa ya kibinadamu ambayo kama hauna KRISTO YESU moyoni hayana msaada kwako baada ya kutwaliwa hapa duniani.

Mariko 8:36​

Kwa kuwa itamfaidia mtu nini kuupata ulimwengu wote, akipata hasara ya nafsi yake?

Tuhimize watu wampokee Yesu mioyoni mwao, hayo ya siri yatabaki ya siri milele na yataeleweka kwa wachache, ila suala la kumkiri na kumpokea Yesu halihitaji akili kubwa wala maarifa mtambuka.

Yohana 17:3​

Na uzima wa milele ndio huu, Wakujue wewe, Mungu wa pekee wa kweli, na Yesu Kristo uliyemtuma.

Mbarikiwe
 
Sijakataa Mkuu na ninamkiri Kristo hakika ila msingi wa hoja yangu ipo kwenye kujifunza na kukubali kuwa yapo tusiyoyafahamu kabisa au tunayoyafahamu siyo yalivyo.
 
Ikumbukwe mafundisho yanayotolewa na Papa wa Kanisa Katoliki hayategemei kalenda ya kawaida au kalenda ya liturujia ya Kanisa. Mafundisho yanayotolewa na Papa yanategemea zaidi misingi ya imani ya Kikristo, mafundisho ya Kanisa, Maandiko Matakatifu (Biblia), na mamlaka ya kiinjili na kikanuni ambayo Papa anayo kama kiongozi wa Kanisa Katoliki.

Kalenda ya liturujia ya Kanisa inaonyesha sikukuu, matukio ya maisha ya Yesu, na sikukuu za watakatifu ambazo zinaweza kuathiri mafundisho yanayotolewa kwa waumini wakati wa sherehe hizo. Hata hivyo, mafundisho ya kimsingi yanabaki kuwa ya msingi wa imani na mafundisho ya Kanisa, na siyo kwa msingi wa kalenda ya liturujia au kalenda ya kawaida.

Kalenda ya kawaida inaweza kusaidia tu kwa kipindi au muktadha wa mafundisho fulani yanayotolewa na Papa, kama vile hotuba zake au barua za kitume, ambazo zinaweza kuhusisha matukio ya kijamii, kiroho, au ya kikatoliki yanayojitokeza kwa wakati fulani wa kalenda ya kawaida. Lakini msingi wa mafundisho hayo unatokana na mafundisho ya kikristo ya jumla zaidi.

Huenda sasa ukawa ndiyo muda sahihi zaidi kwao kufanya hivyo kutokana na kile wanachokielewa haswaa ambacjo wengi wetu hatukifahamu kabisa na hata kama tunakifahamu siyo katika namna kinavyopaswa kufahamika.
 
Kufahamu hayo ni jambo la heri, lakini ukiyafahamu halafu hauna WOKOVU yana msaada gani?.

Tutafute kwanza wokovu ambao hata bibi yangu ambaye hajui kusoma wala kuandika anaweza upata na akamuona Mungu baada ya kulala.

Mimi sipingi watu kutafuta maarifa na siri za dunia bali mkazo wangu ni WOKOVU kwanza halafu hayo mengine baadae.

Siku hizi makanisani mwetu kuna kasumba imemea na kuota mizizi ya kujiona dhehebu lenu ni bora na sahihi kuliko mengine, kitu ambacho si kweli maana utakatifu ni jambo binafsi.

Viongozi wanatilia mkazo taratibu za dhehemu badala ya wokovu ambao unaambatana na maisha matakatifu yanayojitenga na dhambi pamoja na vyanzo vyote vya uovu.

Zab 16:3​

Watakatifu waliopo duniani ndio Walio bora, Hao ndio niliopendezwa nao.
 
Naam,
Utafuteni kwanza Ufalme wa Mungu na haki yake na mengine yote mtazidishiwa.
 
Tarehe 17/5/2024 Dicasteria kwa Mafundisho ya Imani (DDF) imetoa "Kusikiliza Roho Anayefanya Kazi katika Watu wa Mungu wa Imani," seti mpya ya kanuni za kutambua madai ya matukio ya kimuujiza, kama vile maono, miujiza, na matukio mengine ya kimystika yanayodaiwa kuwa ya asili ya kimungu. Kanuni hizi zimeidhinishwa na Papa Francis, ambaye aliagiza zichapishwe. Zitachukua athari Jumapili ya Pentekoste, Mei 19, 2024, na zitabadilisha kabisa kanuni za awali, ambazo ziliidhinishwa mwaka 1978 na kuchapishwa rasmi na Vatican mwaka 2011.

Muhtasari wa mchakato
Kwa ujumla, mchakato mpya unamtaka askofu wa jimbo - mara tu anapojua kuhusu tukio linalodaiwa kuwa la kimuujiza katika eneo lake ambalo lina "dalili za ukweli" (II. B. Art. 7 § 1) - kuanzisha na kufanya uchunguzi wa madai hayo. Anafanya hivyo kwa kushirikiana na mkutano wa maaskofu wa taifa lake. Kisha anatayarisha hukumu yake (Votum) juu ya tukio hilo na kuituma kwa DDF pamoja na matokeo ya uchunguzi (cf. II. A. Art. 1). Baadaye, DDF inakagua matokeo ya uchunguzi na kutoa idhini au kukataa kwa hukumu ya askofu (cf. II. A. Art. 2).

Mara tu hukumu ya DDF inapofikiwa, wanatuma majibu yao kwa askofu wa jimbo ambaye ataarifu mkutano wa maaskofu wa taifa na "atawajulisha waziwazi Watu wa Mungu" uamuzi wa DDF (cf. II. B. Art. 21 § 1-2).

Huo ndio muhtasari wa msingi. Bila shaka, kanuni hizi zinatoa maelezo kuhusu jinsi uchunguzi unavyopaswa kufanywa na nani anapaswa kushiriki. Hati hiyo inazingatia hali mbalimbali, kama vile ushirikishwaji wa maaskofu na majimbo kadhaa. Pia inatoa mwongozo juu ya jinsi ya kushughulikia aina tofauti za matukio, kama vile vitu vinavyoweza kuhusishwa na miujiza au ujumbe unaoendelea kutoka kwa waonaji wanaodaiwa. Inamshauri askofu kuwa macho kuhusu tukio hilo wakati wa mchakato wa uchunguzi na tathmini. Inataja sehemu ambazo askofu, DDF, au papa wanaweza kuingilia kati.

Matokeo Yanayowezekana
Hapa ndipo hati hii inapojitofautisha sana na kanuni za awali. Hakuna tena hukumu juu ya asili ya kimuujiza ya matukio (constat de supernaturalitate, non constat de supernaturalitate, constat de non supernaturalitate) bali tathmini ya matunda ya kiroho yanayohusiana na tukio hilo. Kwa sababu hukumu za mwisho juu ya asili ya kimuujiza ya matukio haya ni nadra, matukio mengi hayaachwi bila tathmini wazi na Kanisa, jambo linalosababisha mkanganyiko miongoni mwa waumini. Njia mpya ilipendekezwa na DDF kwa papa:

Ili kuzuia ucheleweshaji zaidi katika utatuzi wa tukio maalum linalodaiwa kuwa na asili ya kimuujiza, Dicasteria ilipendekeza hivi karibuni kwa Baba Mtakatifu wazo la kumaliza mchakato wa utambuzi si kwa tamko la “de supernaturalitate” bali kwa “Nihil obstat,” ambalo litamruhusu Askofu kufaidika na tukio la kiroho kwa njia ya kichungaji. Wazo la kumalizia kwa tamko la “Nihil obstat” lilifikiwa baada ya kutathmini matunda mbalimbali ya kiroho na kichungaji ya tukio hilo na kuona hakuna vipengele vya kimsingi vibaya ndani yake. Baba Mtakatifu aliona pendekezo hili kuwa "suluhisho sahihi."

Sasa kuna matokeo sita yanayowezekana ya uchunguzi wa matukio kama hayo:

– Nihil Obstat: Bila kuelezea uhakika wowote kuhusu ukweli wa kimuujiza wa tukio lenyewe, dalili nyingi za kitendo cha Roho Mtakatifu zinatambuliwa. Askofu anahimizwa kuthamini thamani ya kichungaji na kukuza usambazaji wa tukio hilo, ikijumuisha hija;

– Prae oculis habeatur: Ingawa dalili muhimu za chanya zinatambulika, vipengele fulani vya mkanganyiko au hatari zinazoweza kutokea pia zinajulikana zinazomhitaji askofu wa jimbo kujihusisha na utambuzi wa makini na mazungumzo na wapokeaji wa uzoefu fulani wa kiroho. Ikiwa kulikuwa na maandishi au ujumbe, ufafanuzi wa mafundisho unaweza kuwa muhimu;

– Curatur: Vipengele mbalimbali au muhimu vya ukosoaji vinaonekana, lakini tukio hilo tayari limeenea sana, na matunda yanayothibitishwa ya kiroho yanahusiana nalo. Kwa hivyo, marufuku inayoweza kuwakera waumini haipendekeziwi, lakini askofu wa eneo anashauriwa kutochochea tukio hilo;

– Sub mandato: Masuala muhimu hayahusiani na tukio lenyewe bali na matumizi mabaya ya watu au vikundi, kama vile faida zisizo za haki au vitendo vya kimaadili. Vatican inamkabidhi askofu wa jimbo au mwakilishi uongozi wa kichungaji wa mahali fulani;

– Prohibetur et obstruatur [imezuiliwa na kusitishwa]: Licha ya vipengele mbalimbali vya chanya, masuala muhimu na hatari zinazohusiana na tukio hili zinaonekana kuwa nzito sana. Dicasteria inamwomba askofu wa eneo kutoa mafundisho ambayo yanaweza kusaidia waumini kuelewa sababu za uamuzi na kuelekeza upya wasiwasi wao halali wa kiroho;

– Declaratio de non supernaturalitate: Dicasteria ya Mafundisho ya Imani inamuidhinisha askofu wa eneo kutangaza kwamba tukio hilo limeonekana kuwa si la kimuujiza kulingana na ukweli halisi na ushahidi, kama vile kukiri kwa mwonaji anayedaiwa au ushahidi wa kuaminika wa kughushi tukio hilo.
 
Kila wakati mtakatifu, Bikira Maria, au Kristo mwenyewe anapojitokeza mbele ya mwanadamu duniani, inajulikana kama "onyesho".
Maria anajitokeza akitokea kuzimu au wapi? kwani yu hai au amekufa? au ungesema "mzimu wa bikira maria". fafanua.
 
Maria anajitokeza akitokea kuzimu au wapi? kwani yu hai au amekufa? au ungesema "mzimu wa bikira maria". fafanua.
Mkuu haya masuala ni ya kujifunza kutoka kwa wenyewe siyo kufafanua tu, Mimi pia ninajifunza na nina maswali mengi mno ila nilichojifunza ni kuwa:

Marian apparitions ni maonyesho ya kimuujiza ambayo inasemekana kuwa Bikira Maria, mama wa Yesu, anaonekana kwa watu. Katika maonyesho haya, Bikira Maria hutoa ujumbe maalum kwa wale wanaomuona. Hizi hutokea kwa kawaida katika mazingira ya kiroho na mara nyingi zinaambatana na wito wa toba, maombi, na imani.

Mifano maarufu ya Marian apparitions ni pamoja na maonyesho ya Lourdes nchini Ufaransa, ambapo Bikira Maria alimtokea msichana mdogo anayeitwa Bernadette Soubirous mnamo mwaka 1858, na maonyesho ya Fatima nchini Ureno, ambapo Bikira Maria alitokea kwa watoto watatu wachungaji mnamo mwaka 1917. Hizi apparitions zinaheshimiwa sana na Wakristo wa dhehebu Katoliki na zimekuwa sehemu muhimu ya ibada na mila zao.

Angalia na hii hapa:
Lucia dos Santos, Francisco Marto, na Jacinta Marto walikuwa watoto watatu wachungaji waliodai kumwona Bikira Maria katika kijiji cha Fatima, Ureno, mwaka 1917. Hizi maonyesho zinajulikana kama "Maonyesho ya Fatima."

Watoto hawa walisema waliona Bikira Maria kwa jumla ya mara sita kati ya Mei 13 na Oktoba 13, 1917. Wakati wa maonyesho haya, Bikira Maria aliwapa watoto hawa ujumbe unaohusu toba, kuomba kwa ajili ya wadhambi, na kusali Rozari kwa ajili ya amani duniani. Pia alitoa maono matatu maarufu yanayojulikana kama "Siri Tatu za Fatima."

Siri ya kwanza ilikuwa ni maono ya kuzimu. Siri ya pili ilitabiri Vita Kuu ya Pili ya Dunia na kuhitaji kugeuza maisha kwa toba na kujitoa kwa Moyo Safi wa Maria. Siri ya tatu ilibaki siri kwa muda mrefu kabla ya kutolewa hadharani na Kanisa Katoliki mwaka 2000, na inahusishwa na mateso ya Kanisa na jaribio la kumuua Papa.

Maonyesho haya ya Fatima yamekuwa na athari kubwa sana katika imani ya Wakatoliki na yamepelekea ujenzi wa madhabahu kubwa ya kidini huko Fatima, ambayo ni mahali pa hija kwa mamilioni ya waumini kila mwaka
 
Kanisa liruhusu ndoa ya mke zaidi ya mmoja kama ambavyo linapambana kuwapa uhuru wapenzi wa jinsia moja..
 
Kajifunze kuhusu mpasuko wa kanisa hadi kutokea kwa east and west church.
 
ndugu yangu, usije kudanganywa hata siku moja, mzimu ukikutokea ukasema ni Mungu. Maria alishakufa, Maria mwenyewe hata kabla hajafa alikuwa anafuata maelekezo ya Yesu, wewe ni nani ufuate maelekezo ya maria wakati maria mwenyewe alifuata ya Yesu?

mizimu mingi tu huwa inawatokea watu. shida ni uthibitisho kwamba hicho kilichotokea ni cha Kimungu au shetani? how we can prove it ni kwa kupitia Neno la Mungu. chochote kilicho kinyume na Neno la Mungu jua ni mpango wa shetani kukuondoa kwenye reli. Maria aliwatokea hao watu na kusema wasali rozali, wakati Yesu alisema yeye pekee ndiye njia na ndiye anayestahili kutajwa wakati wa maombi kwasababu alimwaga damu, alitoa kafara.

hata siku ya Mwisho, ni Yesu pekee kama mwanakondoo wa karafa anastahili kukifungua hata kile kitabu na zile muhuri kama ulishawhai kusoma kitabu cha Ufunuo. hakuna mwignine anayestahili, ila yeye tu, na sababu kuu ni kwamba, ni yeye pekee alitoa gharama ili Mungu atutambue,kwahiyo Mungu akamwadhimisha sana na kumwinua kuliko majina yoote yatajwayo, na ni kwa Jina la Yesu tu magonjwa, mapepo na mashetani yatakimbia.

ukitaka ujue umuhimu wa Jina la Yesu, mkute pepo, kifafa, au mshawi, halafu mwambia "kwa jina la maria mtakatifu, toka", utaona matokeo yake. litakudharau tu. ila ukisema kwa Jina la Yesu, lazima livurugwe. kwasababu ni Yesu tu alimshinda shetani, maria hakumshinda shetani.

Yesu alifanyika mwili, ila yeye ni Mungu yuleyule, hata hii dhana ya kuomba kwa baba alikuwa anaongea kwa vile amevaa mwili wa mwanadamu na baada ya kupaa aliketi MKono wa Kuume kwasababu tu ameshafanyika mwili ila ni Mungu yule yule. yeye na baba ni kitu kimoja,ni Mungu yuleyule mmoja. sasa inakuwaje wewe uanze kuomba kwa jina la mtu mwingine badala ya kuomba kwa JIna la huyu Mungu? unaipata point?
 
Kajifunze kuhusu mpasuko wa kanisa hadi kutokea kwa east and west church.
HIKI NDICHO TUNACHOONGEA

MATENDO 4:12
Wala hakuna wokovu katika mwingine awaye yote, kwa maana hapana jina jingine chini ya mbingu walilopewa wanadamu litupasalo sisi kuokolewa kwalo.

WAFILIPI 2:10 -11 ili kwa jina la Yesu kila goti lipigwe, la vitu vya mbinguni, na vya duniani, na vya chini ya nchi; 11na kila ulimi ukiri ya kuwa YESU KRISTO NI BWANA, kwa utukufu wa Mungu Baba.
YOHANA 14:6 Yesu akamwambia, Mimi ndimi njia, na kweli, na uzima; mtu haji kwa Baba, ila kwa njia ya mimi.

YOHANA 14:13 Nanyi mkiomba lo lote kwa jina langu, hilo nitalifanya, ili Baba atukuzwe ndani ya Mwana.

Wakolosai 3:17 “Na kila mfanyalo, kwa neno au kwa tendo, fanyeni yote katika jina la Bwana Yesu, mkimshukuru Mungu Baba kwa yeye”.

Matendo 2:37 “Walipoyasikia haya wakachomwa mioyo yao, wakamwambia Petro na mitume wengine, Tutendeje, ndugu zetu? 38 Petro akawaambia, Tubuni mkabatizwe kila mmoja kwa jina lake Yesu Kristo, mpate ondoleo la dhambi zenu, nanyi mtapokea kipawa cha Roho Mtakatifu”.
 
Leo ikiwa ni Jumapili ya pentekoste kanuni mpya zitatolewa makanisani tukienda tusikilize kwa upole.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…