Magari ya gharama kubwa yamekuwa mengi mtaani, nini kipo nyuma ya pazia?

Magari ya gharama kubwa yamekuwa mengi mtaani, nini kipo nyuma ya pazia?

Kinumbo

JF-Expert Member
Joined
Dec 8, 2019
Posts
3,039
Reaction score
5,560
Aisee! Wakati baadhi ya watanzania kila uchwao wakilalamika ugumu wa maisha mtaani wakati huo huo kuna baadhi ya watanzania kila uchwao wananunua magari ya kifahari na gharama kubwa mno. Kama wewe ni mkazi wa Dar es Salaam utakubaliana nami, huko barabarani kwa sasa magari ya gharama ni mengi mno.

Magari kama Land Cruiser 300 series (GX-R, ZX), Range Rover Sport, Ford Endeavour, Cadillac Escalade na mengine mengi tu. Haya magari kwa sasa yamekuwa mengi sana hapa Tanzania, ni nini siri ya watu kununua haya magari kwa wingi?

Au ndio ile kauli ya kula kutokana na urefu wa kamba yako? Ila wakuu kuna watu wana hela sio poa, kuna hiyo Ford Endeavour nyeusi namba E imenipita hapa mpaka nikaanza kujiuliza maswali kichwani.

Kipi kipo nyuma ya pazia ni madili gani hayo wenzetu wanapiga mpaka wanamiliki vyuma kama hivyo?
 
Mbona simple tu, tafuta connection mkuu.
tapatalk_1716811998391.jpeg
 
Pesa ilizikwa, nyingine zilipata trip kwenda nje ya nchi wkt huo kila mtu alikuwa na wasiwasi.

Leo peaa zimeamua kurudi baada ya kuona huyu hana shida na sisi ila ana shida na nani amfunge kamba ya urefu wake, hivyo zimerudi.

Ukipata channeli ukapewa codes ni fasta tu wazo lako la kununua kiPaso au kiIST linakufa haraka sasa unaamia kwenye vinu vya CC1000 kupanda juu.
 
Mbona simple tu, tafuta connection mkuu. View attachment 3010239
Uongo uongo mimi ninazote hizo na namiliki zaidi ya hiyo.Miking money is another curriculum which does not require a As or degrees but a plan.Watu wasome msidanganyike the same probabilities ya wasiosoma au wenye F wanafanikiwa ,the same with As wanafanikiwa.Plan your life usiangalie mwingine.Sema wenye As Hawa shout kama wenye F kwa sababu ya inferiority complex na kujitutumua kuwa wameweza na kujitutumua.Guys whatever your doing fanya kwa bidii
 
Sawa Upopo
Uongo uongo mimi ninazote hizo na namiliki zaidi ya hiyo.Miking money is another curriculum which does not require a As or degrees but a plan.Watu wasome msidanganyike the same probabilities ya wasiosoma au wenye F wanafanikiwa ,the same with As wanafanikiwa.Plan your life usiangalie mwingine.Sema wenye As Hawa shout kama wenye F kwa sababu ya inferiority complex na kujitutumua kuwa wameweza na kujitutumua.Guys whatever your doing fanya kwa bidii
 
Dah! Hatari sana mkuu, kipindi kile hayo magari hayakuwa mengi kiasi hicho.
Pesa ilizikwa, nyingine zilipata trip kwenda nje ya nchi wkt huo kila mtu alikuwa na wasiwasi.

Leo peaa zimeamua kurudi baada ya kuona huyu hana shida na sisi ila ana shida na nani amfunge kamba ya urefu wake, hivyo zimerudi.

Ukipata channeli ukapewa codes ni fasta tu wazo lako la kununua kiPaso au kiIST linakufa haraka sasa unaamia kwenye vinu vya CC1000 kupanda juu.
 
Back
Top Bottom