Magari yaruhusiwa daraja la Wami. Ujenzi umekamillika 90%

Magari yaruhusiwa daraja la Wami. Ujenzi umekamillika 90%

CCM inazidi kutimiza ahadi zake.

Unadhani mkisema hivyo ndio watu wataipa kura CCM? Hizo ni kodi za wananchi, hata kama nchi ingekuwa imepinduliwa kwakuwa kodi zinakusanywa bado daraja kama hilo lingejengwa.
 
Unadhani mkisema hivyo ndio watu wataipa kura CCM? Hizo ni kodi za wananchi, hata kama nchi ingekuwa imepinduliwa kwakuwa kodi zinakusanywa bado daraja kama hilo lingejengwa.
Kodi za wananchi huwa zinaliwa kama michango ya wanaChadema inavyoliwa kama hakuna usimamizi thabiti.
 
Kuna kitu kinanishangaza kwenye ujenzi wetu. Ukiangalia hiyo picha ya daraja la Wami, utaona kuwa baada tu ya kuvuka daraja unaanza mpando na kona ya wastani kuelekea kulia na kona kali kuelekea kushoto mita kadhaa mbele.
Daraja la zamani hivyo hivyo, ukivuka tu daraja kuna mpando mkali, kona kulia kisha kushoto. Tofauti iliyopo kati ya daraja jipya na lile la zamani ni upana wa daraja jipya na kuinuliwa juu zaidi.
Najiuliza, kwa akili ya kawaida tu bila kuathiri taaluma za watu: Kwa nini hawakufikiria kutengeneza "Tunnel" iliyonyooka usawa na daraja ili iungane mbele na barabara mbele kwenye kona kali?
Kama "Tunnel ina gharama sana, kwa nini mpando usingechongwa pande mbili ili kupata barabara iliyonyooka kutoka kwenye daraja kwa kuzingatia usawa daraja lililojengwa.?

Nawaza tu kwa sauti, Wataalamu watatupa sababu kwa nini waliamua daraja liwe kama la zamani lakini jipya tu.
 
Itapendeza kama watumiaji watapita hapo kwa kulipia

Ova
 
Wewe uvccm ukaogopa kusema top ten kwa makusudi.

Kwa taarifa yako wachaga ndio wanaendesha uchumi kwenye hiyo mikoa ya top ten yote.

Ktk sekta ya biashara pato kubwa la Taifa linatoka kwenye viwanda sio wachuuzi wa bidhaa unaowataja wewe
 
Bado hawajalipatia jina? Madaraja yote makubwa yana majina, hili vipi?
 
afadhali kwa hili ila sitopasahau nilipata ajari kubwa sana january 23 2022 na kumpoteza mdogo wangu pale daraja la zamani
 
hilo daraja nimeliona ila mm nitaendelea kutumia lile la zamani
 
Back
Top Bottom