Magazeti ya leo Februari 15, 2022 yanatia kichefuchefu kuhusu Mbowe

Magazeti ya leo Februari 15, 2022 yanatia kichefuchefu kuhusu Mbowe

Nilitaka kuja na andiko kama lako uzuri umeniwahi Acha nichangie kwako.
"MBOWE ALIA NJAA" ni sentensi inayoonesha Mbowe amekosa chakula kutokana na kukosa uwezo kiuchumi wa kukipata. Wafanyakazi wanàpokosa kulipwa mshahara miezi 2 au 3 wanapolalamika tunasema wanalia njaa maana wamekosa uwezo wa kulisha familia zào. Lakini Kwa hili la Mbowe ni tofauti, nimesoma gazeti jingine limeandika "MBOWE ALALAMIKA KUTOPEWA CHAKULA MCHANA KWA MIEZI 5" angalau inaleta maana. Lakini lingine limepotosha zaidi Kwa kuandika "MBOWE AKOSA CHAKULA MIEZI 5" na nimeona hata baadhi ya watu mitandaoni Wenye milengo ya ovyo àmbao hawana kawaida ya kutafuta undani wa habari wameanza kumtukana Mbowe wakimwita mpuuzi na mzushi eti binadamu anawezaje kuishi miezi 5 bila kula? Waandishi na wahariri mna nafasi kubwa ya kuielekeza Jamii au kuipotosha. Kwa hili sehemu kubwa mmepotosha watu na kuwapa nafasi wasiojiweza kifikra kutukana watu bila sababu.
[emoji23] [emoji23] [emoji23] Bavicha bhana!

Si ndio uhuru wenyewe wa habari huu?
 
Ipo kwenye HAKI za Binadamu za kuishi.walipaswa walipe uzito kama haki ya mtu ya Msingi,kulia njaa hata mtaani tunalia njaa katika Mazingira mbalimbali,hata ukipata hela kidogo,ulitegemea zaidi,utasema unalia njaa.lakini ishu ya mtu kunyimwa chakula,maji sio kulia njaa.
Hata mheshimiwa mbowe analia njaa sio kwamba hapati chakula kweli. So argument yako inatokana na msukumo wa mawazo yako mwenyewe ambayo unataka wote tuyaamini.
 
..hii inaweza kuwa KASHFA kubwa kwa jeshi la magereza na mahakama.

..huenda mahabusu watuhumiwa wa kesi mbalimbali wanateseka kwa njaa wakati mashauri yao yakisikilizwa ktk mahakama zetu.

..Na Jaji Mkuu hajali. Waziri wa mambo ya ndani hajali. Mkuu wa magereza hajali. Dpp hajali.
 
Nimeona Magazeti Makubwa kama Mwananchi, Nipashe yamebeba kichwa Cha habari eti "MBOWE ALIA NJAA"

Alichokizungumza MBOWE ni Haki ya mtu kuvunjwa! Inakuweje iitwe kulia njaa? Pia issue hiyo sio ya kwake peke yake inaonyesha wafungwa wengi ni wahanga.

Kwanini hivi vipeperushi vimejaa njaa kichwani mpaka vinakosa angle ya habari?

Waandishi mtategemea ruzuku na bahasha za Serikali mpaka lini?!

Ishu za Haki za Mtu ziheshimiwe,ndio maana hata Mwandishi wenu Azory alivyo potezwa bado mkawa mnaleta mizaha.ni wakati wa kutoka kwenye boksi, hamjachelewa.

Sijaona kosa la mwandishi, ni kweli Mbowe kalia njaa, tatizo liko wapi?
 
Mkuu wangeandikaje labda?
"Magereza yavunja haki za binadamu"
Uwepo wa mitandao ya kijamii una pre-empty sana magazeti. magazeti yanatakiwa kuripoti habari ile ile lakini kwa engo tofauti. kuchambua vitu kwa kina na rejea badala ya juu juu kama ilivyo kwenye social media. Ndio maana mtu makini kama mimi siwezi kununua gazeti kwa sababu hakuna jipya.
 
Back
Top Bottom