chikambabatu
JF-Expert Member
- Dec 29, 2015
- 1,339
- 1,318
Ila ni hatari sana kutawaliwa na mtu mjinga, halafu wenye akili kiasi wanamshangilia, kabudi, yule mkurugenzi wa tbc, na wa kutunga sheria, Mungu ametusaidia, alisha tuzidi!Alitudanganya hadharani kwamba Gaddafi alikuwa Rais wa Kuwait!
Mabeberu Sasa yanatudhihaki lakini Mungu wetu mkuu, atanyanyua Tena mtetezi mwingine.
Nawaambia nyie mabeberu na makuwadi wenu hamtaitawala hii nchi milele.
Tanzania sio ya kwenu.
Huu ndiyo ukweli.Huwezi mtenganisha dikteta na propaganda
Alichozungumza hapa ni kweli, japo sio kipindi cha JK, lakini kuna wakati miaka ya 96 hivi walikuwa wanachelewa sana kupokea mshahara. Mfano wik iliyopita ndio unakuta wamepokea ya mwez uliopita. (Wa 5) ilikuwa kawaida.
Angeendelea miaka mitano tena, angebadili katiba na kuwa rais wa maisha.Ni lini mishahara ililipwa tarehe 15 au 20 ya mwezi unaofuata?
Mimi sikumbuki aisee kwenye utawala wa Kikwete sikumbuki nasisitiza kama kuna mtu anakumbuka aniambie.
View attachment 1831163
Aliposema nitawajengea flyover Dsm ni muongo! Aliposema nitajenga mji wa serikali Dodoma! Aliposema tutajenga mtambo wa umeme rufiji ni muongo! Alposema elimu bure ni muongo. Tusidhalilishe hayati haitusaidii sana kimaadili. Tuwe na kiasi kwenye kauli sote ni waja wake.Utapigana na marehemu mpaka lini? Je! Ukimshinda marehemu unataka zawadi gani?
Alisema pia nchi yetu haina corona na kuwa ata mapapai yameonekana na corona kwa mujibu wa vipimo vya maabaraKwenye medani ya uongo na uzandiki mbona hana mpinzani huyo. Anapita bila kupingwa wala hafanyi hata kampeni (CV yake inambeba kishenz).
● Alituambia tuwachange bukoba wahanga wa tetemeko waliovunjiwa nyumba zao. Tukajikaza kiaskari na kujibana watanzania kuwachangia. Waulize kama waliona hata Sh 100 ya ujenzi wa nyumba zao.
● Alituambia kila mwalimu atapewa Laptop. Waulize kama amepewa hata mmoja.
● Alituambia kila kijiji atawapa Millioni 50 kwaajili ya kufanya maendeleo na uchumi. Waulize kama waliiona hio hela.
● Alituambia wafanyakazi sekta za umma/walimu, wataongezewa mishahara na madaraja kabla hajaondoka. Waulize kama wameongezewa hizo nyongeza za mishahara na madaraja (Labda madaraja ya ubungo na mfugale ndio wameyaona).
● Alituambia tutalipwa hela ndefu kwenye fidia ya makinikia. Kila raia noah moja moja. Waulize kama mabeberu walitoa hio hela.
● Alituambia Tanzania tutatoa misaada kwa wazungu, sisi ni "DONA KANTRI". Hakuna cha donna wala sembe, ni mwendo wa hali ngumu mpaka skin tight kupwaya mitaani.
● Alituambia serikali yake kutakua hakuna wizi wala ufisadi, na atakefanya ufisadi wa hela basi zitamtokea tundu lolote. Mbona yeye na kina Ole Sabaaya na Makonda walifisadi nchi na kuiba.
● Kwenye kutupa idadi za samaki, watoto wa samaki pamoja na mayai yao kwenye Ziwa Victoria na Baharini. Wala tusipagusie kabisa, tuache hio issue siku ingine.
Yule mzee sio kabisa. Siku alivyofukiwa mpaka malaika watoa kichapo waliokua likizo, ilibidi waitwe kazini kwa dharura kumpokea.
Alishawahi kudanganya kuwa kuwa ndege zimeiingiza faida ya Bilion 128 na gawaio akapokea hadharani kumbe tumepigwa hasara ya Bilion 60Ilikuwa ni hobby yake
Nimesoma mpaka kwenye elimu bure nikaacha kusomaAliposema nitawajengea flyover Dsm ni muongo! Aliposema nitajenga mji wa serikali Dodoma! Aliposema tutajenga mtambo wa umeme rufiji ni muongo! Alposema elimu bure ni muongo. Tusidhalilishe hayati haitusaidii sana kimaadili. Tuwe na kiasi kwenye kauli sote ni waja wake.
Kwani kule kuzimu kuna kupumzika?Jamaa muacheni mzee wa watu apumzike kwa amani
Hahahaaah si tuliambiwa zitakuwa na rangi moja nchi nzima, nyeusi[emoji38][emoji38][emoji38]Ilo la makinikia nilichagua mpaka rangi ya Noah magu hapana aiseee
Hahaaah kumbe hakuna mapumziko.....Kwani kule kuzimu kuna kupumzika?
Aliposema tunajenga kwa fedha za ndani wakati anakopa kila uchwao alikuwa mkweli? Kama mkweli deni liketoka wapi?Aliposema nitawajengea flyover Dsm ni muongo! Aliposema nitajenga mji wa serikali Dodoma! Aliposema tutajenga mtambo wa umeme rufiji ni muongo! Alposema elimu bure ni muongo. Tusidhalilishe hayati haitusaidii sana kimaadili. Tuwe na kiasi kwenye kauli sote ni waja wake.