Magufuli atengua uteuzi wa Mkurugenzi Mtendaji wa TANESCO, F. Mramba. Amteua Dkt. Mwinuka kukaimu

Magufuli atengua uteuzi wa Mkurugenzi Mtendaji wa TANESCO, F. Mramba. Amteua Dkt. Mwinuka kukaimu

Hii serikali mbona inafanya watu wote kama hatuna akili. kuhusu kupandisha kwa bei mbona EWURA waliweka kila kitu public?? Kwann serikali isiingilie kati toka wakati ule???. Yan Jan Mos imefika maamuzi ya mlipulipuko yanafanyika as if ndo serikali yote imejua jana kwamba bei ya umeme itapanda. Hapa ndipo serikali ya Mtukufu Rais inapopofanya siasa wakati ndugu zangu wa Upinzani wanapigwa mikwara kila leo. Hiz ni siasa uchwara.[HASHTAG]#SerikaliYaMilipuko[/HASHTAG].
Unafahamu process ya kupandisha umeme unakuwaje?
Yes hatua ya public hearing imefanyika, je waziri husika alipewa taarifa?
 
Huyu ndiye kabariki ongezeko la gharama kwa kushindwa kuikatalia Tanesco kwa masilahi ya wananchi.
 
Huoni kama serikali ya awamu ya 5 kuna tatizo la flow of information kati ya watendaji wa serikali hasa wakurugenzi wa mashirika na mawaziri/Raisi

Angalia hii mifano
1.Waziri wa afya vs NIMR -Hakuna Zika/Zika ipo
2.Waziri wa afya vs MSD-Akiba ya dawa chanjo imeisha/Hakuna upungufu wa dawa/chanjo
3.Raisi vs Hazina/BOT-TRA wamefungua FDA ili wachukue interest/kufungua FDA sio tatizo
4.RCs vs Raisi-Machinga/wachimbaji wadogo waondolewe/Wamachinga na wachimbaji wadogo wasiondolewe

Iko migongano mingi ikiwemo ya kuongeza na kushusha GPA kwa admission vyuoni.Huu ni mwaka wa 2 watendaji wa Raisi bado wanatofautiana.Kuna kipindi naona uamuzi wa JK kuwapeleka watendaji wake semina elekezi Ngurdoto ulikuwa uamuzi mzuri sana

Hapana, ni team Against Vs President, government na team yake.

Hawa team against wapo wameungana na ndiyo wanakosea katika timing zao katika kutoa taarifa yote ikiwa ni katika kutaka kumharibia raisi na serikali ili awe discredited.

Flow of information- nafikiri zipo njia mbili kulekea Ikulu kwa raisi mwenyewe na kwa kurugenzi ya mawasiliano na kuna aina tatu za haya mawasiliano- yaani kuna downward, upward or horizontally.

Halafu kuna barrier yaani vizuizi na hivi ndivyo raisi anajaribu kuviondoa ili apate kuwa na effective communication na watu walio chini yake au "subordinates".

Ila huwezi kuwa na mtitiriko mzuri wa taarifa kama hakuna nidhamu iwe kwenye timu nzima, vikozi kazi au kamati mbalimbali.

Hivyo raisi ananyoosha hii kitu aondpe vizuizi na awe na mawasiliano ya moja kwa moja na wasaidizi wake ambao wataelewa yeye anataka nini.
 
Rais Magufuli leo ametengua rasmi uteuzi wa Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la Umeme nchini(TANESCO), Eng. Felchesmi Mramba.

Aidha Rais amemteua Dkt. Tito Esau Mwinuka kukaimu nafasi hiyo. Kabla ya uteuzi huo Dkt. Mwinuka alikuwa mhadhiri wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam(UDSM).

Kwani tatzo la tanesco ni mramba au ni mzigo wa kulipa yale mabilioni ya fidia?
 
Nilimuona last year SABC kwenye Kongamano. Jamaa anaonekana yuko vizuri sana. Ni vigumu kupata vichwa vingi kama hivyo Tanzania. Kama umri haujaenda sana nafikiri anaweza kupata kazi somewhere nje!!

Kwenye hii tumbua tumbua sasa naamini kuna watu wazuri tunawapoteza pia!!
Vichwa vya kupandisha bei holela?
 
Ama kweli CCM ni ile ile. Kwa nini Rais anakwepa to address financial position ya Tanesco inayodidimizwa na wanasiasa wa CCM? Tanesco wanalipa mamilioni ya "dollars" kila siku kununua umeme wa IPTL etc kunufaisha wenye stake humo ambao ni wanasiasa na kupelekea Tanesco kupata tabu kujiendesha. Only way for Tanesco kujiweka Sawa ni raising tariffs na studies zote have maintained kwamba increased tariffs zipo reasonable due to uhalisia wa mambo. Kwanini serikali ilituingiza kwenye mikataba ya ovyo? That's the root cause, sio ewura au Tanesco. JPM mtumbua majipu, inakuwaje hili linamshinda?

CCM chini ya Chama kimoja ndio iliyosaini mkataba wa IPTL, huu ni mradi wa CCM moja kwa moja uliosainiwa Lumumba na ndio unaoitesa Tanesco.

Mramba ameonewa!
Kwahiyo wewe uko tayari kubeba zigo la mafisadi?...
 
Unafahamu process ya kupandisha umeme unakuwaje?
Yes hatua ya public hearing imefanyika, je waziri husika alipewa taarifa?
Je Serikal ndo imejua jana Kwamba bei ya Umeme itapanda???
 
Waliopandish
Vichwa vya kupandisha bei holela?
Waliopandisha bei ni Tanesco au EWURA!!?

Alikuwa anatafutiwa sababu tu!! Inge make a bit of sense kama waliwahusisha Ewura angetumbuliwa pia!
 
Ila kwa mauza uza ya Tanesco, huyu jamaa mi niliweka mzigo kama angekatiza mwaka, kajitahidi!
 
Barua haina tareh sahihi hakuna wala mhuri mmh
 
Yule jamaa wa EWURA aliekubaliana na ombi la Mramba la kupandisha bei ya Umeme anafanya nini ofisini mpaka leo??
Mramba ana makosa yake nae, lakini na yule jamaa nae angetimuliwa tu. Maana alichofanya yule M-Ewura ni sawasawa na Mwele wa NIMR, anapandisha bei bila kuwasiliana na Waziri husika
sio kila mtu rais anaweza mtengua otherwise atakuwa anavunja sheria.. CEO wa ewura anatenguliwa na bodi lkn baada ya kujiridhisha kupitia kamati maalumu iyakayoteuliwa...
 
Tatizo lipo kwenye kutangaza, mchakato wa kupata bei mpya hauna tatizo, baada ya kupata bei mpya kabla ya kutangaza walitakiwa kuwasiliana na serikali kama wanavyosema.
 
Back
Top Bottom