Magufuli, CAG, Ndugai, Lissu, Makonda na Nape pitia hapa

Magufuli, CAG, Ndugai, Lissu, Makonda na Nape pitia hapa

Nilivyo elewa Mimi ni kwamba, ukitaka au ukiona haja ya kumsifia mtu basi msifie kwa watu atafurahi na mtajenga mahusiano mazuri, ila yule unaetaka kujenganae uhusiano mwema lakini unataka kumkosoa jambo ili uhusiano wenu udumu ndo mkosoe sirini. Haina mana kuwa hana hiyo sifa ,ila msifie tu hadharani au mwingine anafanya jambo baya una mshautia mbele za watu, hamtajenga mahusiano mema kwani hata badilika kutokana na kiburi cha macho ya watu.
Lakini haya yote na kwampenda amani na staha. Mfano kumtumbua mtu mkutanoni, kumuumbua mtu asiye weza kujitetea. Ni bora umuite faraghani kama muungwana atajirekebish.
Ila hapa petu TZ imefikia sasa tusipo waeleza watu ubaya wa mtu hadharani, huyo mtu ataendekea kupotisha watu kwani anafanya kusudi unafiki. Huyo anastahili kusutwa hadharani.
Umeelewa sana
 
Lissu anaingiaje hapa?
Lisu ni malaika

We think too small, like the frog at the bottom of the well. He thinks the sky is only as big as the top of the well. If he surfaced, he would have an entirely different view.
 
Hiyo 11 haijakaa sawa. Kumsifia mtu hadharani na kumpinga faraghani kwa lugha halisi huitwa: "Unafiki" Na misahafu inakemea tabia ya "Unafiki"
Hujaelewa.

We think too small, like the frog at the bottom of the well. He thinks the sky is only as big as the top of the well. If he surfaced, he would have an entirely different view.
 
Haimaanishi umsifie kwa kila kitu. Msifie kwa yale mazuri yake alafu yale mabaya au maovu unachonga naye chemba.
Hii ni rahisi kumbadilisha mtu kuliko kuongelea maovu yake hadharani maana anaweza kupanic ikawa hadithi nyingine.

Kwa uelewa wangu mdogo lakini
Hiyo 11 haijakaa sawa. Kumsifia mtu hadharani na kumpinga faraghani kwa lugha halisi huitwa: "Unafiki" Na misahafu inakemea tabia ya "Unafiki"
 
Acha uongo mkuu.


Sent using Jamii Forums mobile app
Uongo wangu uko wapi Hapa hatuzungumzii suala la urafiki Kama wengine wanavyotaka liwe. Hebu mchumulie Lisu. Alitamani Sana amshauri Rais Magufuli faraghani hasa alipokuwa Rais wa TLS, lakini Ni dhahiri Rais alifunga milango kwa sababu anazozijua yeye. Hivyo Lisu akaona njia muafaka ni kumkosoa hadharani. Angenyamaza ungekuwa ni unafiki.
 
Uongo wangu uko wapi Hapa hatuzungumzii suala la urafiki Kama wengine wanavyotaka liwe. Hebu mchumulie Lisu. Alitamani Sana amshauri Rais Magufuli faraghani hasa alipokuwa Rais wa TLS, lakini Ni dhahiri Rais alifunga milango kwa sababu anazozijua yeye. Hivyo Lisu akaona njia muafaka ni kumkosoa hadharani. Angenyamaza ungekuwa ni unafiki.
Na maelezo hayo ni katika mausiano yakawaida tu, sio kwenye siasa. Siasa INA husu watu hivyo kukosolewa au kusifiwa lazima iwe peupe hadharani.
 
Usinge weka hayo majina kwenye title hakika ningejua unanisema mimi

🤣🤣🤣🤣🤣
 
HII NAYO NI ADABU NJEMA

1. Usimpigie mtu kwa zaidi ya mara mbili mfululizo. Ukishaona simu yako haipokelewi basi elewa kuna sababu ya msingi acha subiri akupigie pindi atakapoona ulimtafuta.

2. Rejesha pesa ulizokopa bila kusubiri kukumbushwa na aliyekukopesha. Hiyo inaonesha uadilifu wako na tabia yako. Vivyo hivyo rejesha mwavuli, peni, kitabu au chochote ulichoazima hata kama kidogo usisubiri kukumbushwa.

3. Usiagize chakula cha gharama kubwa pale unapotolewa out na mtu. Ikiwezekana mwombe akuagizie mwenyewe au shauriana naye chakula gani unaweza kuagiza.

4. Usiulize maswali yenye ukakasi kama "Hee bado hujaolewa/hujaoa tu? Au " he! Hujapata mtoto tu?", "he! Hamjajenga tu? " Mwee bado tu hamjanujua gari?" Kwa kifupi ni kwamba hayakuhusu mhusika akipenda mjadili hilo ataanzisha mwenyewe.

5. Ikitokea unaingia mahali na kuna mtu anakuja nyuma yako ni vizuri ukamshikia mlango bila kujali umri au jinsia yake. Haikugharimu lolote kuonesha unajali.

6. Mkienda mahali na rafiki yako na akalipia usafiri au chakula basi jitahidi nawe kulipia zamu inayofuata usipende kupokea tu.

7. Kubaliana na mitazamo tofauti kumbuka 6 kwako inaweza kuwa 9 kwa aliyekaa upande mwingine. Mawazo ya ziada ni mbadala mzuri.

8. Usiwakatishe watu wanapokuwa kwenye mazungumzo yao mfano kwenye kundi kubwa la watu wao wamejitenga pembeni wawili wanaongea jambo fulani wewe unajiingiza kwenye mazungumzo bila samahani na bila kukaribishwa.

9. Ukimtania mtu akaonesha kutofurahia acha mara moja na usirudie tena kumtania.

10.Sema Asante mtu anapokusaidia jambo lolote.

11.Msifie Mtu hadharani, mpinge faraghani.

12. Unapokutana na mtu huna sababu ya kukosoa uzito wake "hee mbona umenenepa hivyo?" Au "Mbona umekonda sana?" Hayakuhusu akitaka kukueleza mwenyewe atakueleza wewe unatakiwa kusema tu "Umependeza"

13. Mtu anapokuonesha picha kwenye simu yake usianze kwenda kushoto au kulia ili kutazama picha zingine ishia hiyohiyo anayokuonesha huwezi jua picha gani inafuata.

14. Mtu anapokuambia anakwenda hospitali usianze kumuuliza " una tatizo gani?" Haikuhusu akitaka atakuambia mwenyewe.

15. Mheshimu mfagizi kama unavyomheshimu boss maana heshima ni kitu cha bure.

16. Ongea na mtu huku unamtazama machoni sio kuwa bize na simu yako au kutazama pembeni.

17. Usitoe ushauri wowote kama hujaombwa kufanya hivyo.

18. Mkikutana na mtu usianze kumuuliza umri wake au kipato chake labda akuambie mwenyewe.

19.Vua mawani yako (kama ya urembo mf. ya jua) unapoongea na mtu.

20. Usiongelee mambo ya utajiri wako au mafanikio yako kwa watu wasio na uwezo wala mambo ya watoto wako kwa watu ambao hawajajajaliwa watoto.
Sawa paid troll wa jiwe

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Lisu ni malaika

We think too small, like the frog at the bottom of the well. He thinks the sky is only as big as the top of the well. If he surfaced, he would have an entirely different view.
Swali halikusema Lissu ni malaika.
 
Back
Top Bottom