Magufuli ili TAZARA isife, ongea na China ili iunganishwe na Malawi kupitia Mbeya au Tunduma, na pia ipitie Morogoro na Iringa mjini!

Magufuli ili TAZARA isife, ongea na China ili iunganishwe na Malawi kupitia Mbeya au Tunduma, na pia ipitie Morogoro na Iringa mjini!

Synthesizer

Platinum Member
Joined
Feb 15, 2010
Posts
12,699
Reaction score
22,598
TAZARA haina hali nzuri. Na sababu kubwa ni kwamba utegemezi wa Zambia kwa TAZARA umepungua sana. Kwa sasa Zambia inaweza kupitisha mizigo yao sehemu nyingine zaidi ya Dar es Salaam, kutia ndaniMsumbiji na Afrika Kusini. Lazima tuseme ukweli Wazambia kwa sasa hawana shida sana na TAZARA, japo wao ndio wanatoa Mkurugenzi Mkuu, kosa tulilofanya huko nyuma.

Sasa ili kuinusuru TAZARA, jambo kubwa la kufanya ni kuiunganisha na Malawi kupitia Mbeya pale au Tunduma. Ukifanya hivyo TAZARA itakuwa na umuhimu mkubwa kwa Malawi na kuipa uhai mpya!

Kwa upande wa Malawi, tayari wanafikiria kujenga reli kati ya Central Region na Northern Region, na tayari wana wazo la kuunganisha hiyo reli na TAZARA kama Tanzania watakubali. Kwa hiyo wazo kwa Malawi lipo ni suala la Magufuli kukubaliana na Raisi wa Malawi mradi huo uanze mara moja.

Malawi wanataka sana kuunganishwa na TAZARA kwa sababu ya mradi wao wa makaa ya mawe wa Mchenga Coal Mine sehemu inaitwa Rumphi, mradi wa miti na mbao pale Chikangawana pia uranium pale Kayelekera. Na pia tusisahau suala la mafuta Ziwa Nyasa, yanayoweza kutoa umuhimu wa pekee kwa TAZARA .

Tukikataa kuunganisha TAZARA na Malawi, Malawi wanafikiria kutafuta namna ya kutumia mito Shire na Zambezi ili kufikia Bahari ya Hindi, kwenye mradi utakaoitwa Shire-Zambezi Waterway (SZW). Wakifanya hivyo wataacha kabisa kutumia bandari ya Dar es Salaam. Hivyo basi, ni vema Tanzania kuwafuata Malawi na kujadiliana nao juu ya kuunganisha reli zao na TAZARA

Tanzania inaweza pia kufikiria uwezekano wa kui-divert TAZARA ili ipitie Morogoro na Iringa mjini. Sijui tulitumia akili gani kuwakubalia Wachina wasipitishe TAZARA mjini kwenye mikoa hii. Ni gharama kubwa kufanya hivyo, lakini itakuwa investment itakayolipa sana tu, kama vile SGR!
 
Kwny mambo ya ujenzi atakusikiliza,maana 24/7 hua anawaza tu mambo ya ujenzi ujenzi ujenzi,mambo mengine kama stahiki za wafanyakazi,ajira,mafao ya wastaafu hua hayamuumizi kichwa.

Nadhani huko kwny ujenzi kuna 10% za maana,ila huko kwingine hawafaidiki na chochote kile ndio maana hawana mpango napo.
 
Kwny mambo ya ujenzi atakusikiliza,maana 24/7 hua anawaza tu mambo ya ujenzi ujenzi ujenzi,mambo mengine kama stahiki za wafanyakazi,ajira,mafao ya wastaafu hua hayamuumizi kichwa.

Nadhani huko kwny ujenzi kuna 10% za maana,ila huko kwingine hawafaidiki na chochote kile ndio maana hawana mpango napo.
Hahaha! Itakuwa vema maana hili nina uhakika litasaidia sana kuirudisha TAZARA kwenye uhai. Wazambia si marafiki kama ilivyokuwa enzi za Kaunda, hawajali kabisa TAZARA.
 
Hiyo foleni ya magari ya mizigo iliyopo Tunduma,bora Wazambia watafute namna nyingine ya kujipatia MAISHA.
Tanzania tumeshindwa kabisa kucheza na fursa.
Pale kuna magari yanaishia Zambia na kunazo za kwenda Congo Lumbumbashi fursa ni nyingi ajabu.Sijui tunakwama wapi!
 
Sasa ili kuinusuru TAZARA, jambo kubwa la kufanya ni kuiunganisha na Malawi kupitia Mbeya pale au Tunduma. Ukifanya hivyo TAZARA itakuwa na umuhimu mkubwa kwa Malawi na kuipa uhai mpya!

Kwa upande wa Malawi, tayari wanafikiria kujenga reli kati ya Central Region na Northern Region, na tayari wana wazo la kuunganisha hiyo reli na TAZARA kama Tanzania watakubali. Kwa hiyo wazo kwa Malawi lipo ni suala la Magufuli kukubaliana na Raisi wa Malawi mradi huo uanze mara moja.


Kama tumeshindwa kusimamia padogo tutaweza pakubwa? Tusifanye mambo ili tuonekane tunavyo, tufanye vituletee tija ya kweli
 
Hiyo foleni ya magari ya mizigo iliyopo Tunduma,bora Wazambia watafute namna nyingine ya kujipatia MAISHA.
Tanzania tumeshindwa kabisa kucheza na fursa.
Pale kuna magari yanaishia Zambia na kunazo za kwenda Congo Lumbumbashi fursa ni nyingi ajabu.Sijui tunakwama wapi!
Japo kusafirisha mizigo kwa reli kwenda ambia kwa reli ni nafuu kuliko kutumia malori, bado watu wanapendelea kutumia malori. KUna risks za ajali sana kusafirisha mzigo kwa barabara. Kuna kitu TAZARA inakosea ndio maana watu wanaikwepa
 
Treni kusafirisha mizigo ya viwandani hapana kwakweli maana niwachafu sana hizo bidhaa zitajaa kunguni, mende, panya Sasa Nani aweke dukani vitu vichafu?
 
SGR ya Dar Moro mwaka wa nne huu unakwisha bado haina matarajio wewe unaleta tazara Tena? Wabunge wakienda kuikagua utasikia imeisha kwa asilimia sabini. Ilikua iishe November 2019 Leo hii Ni November 2020 ngoma bado mbichi kabisa.
Mradi wa awamu hii niliouona imeisha kwa mafanikio Ni
 
TAZARA haina hali nzuri. Na sababu kubwa ni kwamba utegemezi wa Zambia kwa TAZARA umepungua sana. Kwa sasa Zambia inaweza kupitisha mizigo yao sehemu nyingine zaidi ya Dar es Salaam, kutia ndaniMsumbiji na Afrika Kusini. Lazima tuseme ukweli Wazambia kwa sasa hawana shida sana na TAZARA, japo wao ndio wanatoa Mkurugenzi Mkuu, kosa tulilofanya huko nyuma.

Sasa ili kuinusuru TAZARA, jambo kubwa la kufanya ni kuiunganisha na Malawi kupitia Mbeya pale au Tunduma. Ukifanya hivyo TAZARA itakuwa na umuhimu mkubwa kwa Malawi na kuipa uhai mpya!

Kwa upande wa Malawi, tayari wanafikiria kujenga reli kati ya Central Region na Northern Region, na tayari wana wazo la kuunganisha hiyo reli na TAZARA kama Tanzania watakubali. Kwa hiyo wazo kwa Malawi lipo ni suala la Magufuli kukubaliana na Raisi wa Malawi mradi huo uanze mara moja.

Malawi wanataka sana kuunganishwa na TAZARA kwa sababu ya mradi wao wa makaa ya mawe wa Mchenga Coal Mine sehemu inaitwa Rumphi, mradi wa miti na mbao pale Chikangawana pia uranium pale Kayelekera. Na pia tusisahau suala la mafuta Ziwa Nyasa, yanayoweza kutoa umuhimu wa pekee kwa TAZARA .

Tukikataa kuunganisha TAZARA na Malawi, Malawi wanafikiria kutafuta namna ya kutumia mito Shire na Zambezi ili kufikia Bahari ya Hindi, kwenye mradi utakaoitwa Shire-Zambezi Waterway (SZW). Wakifanya hivyo wataacha kabisa kutumia bandari ya Dar es Salaam. Hivyo basi, ni vema Tanzania kuwafuata Malawi na kujadiliana nao juu ya kuunganisha reli zao na TAZARA

Tanzania inaweza pia kufikiria uwezekano wa kui-divert TAZARA ili ipitie Morogoro na Iringa mjini. Sijui tulitumia akili gani kuwakubalia Wachina wasipitishe TAZARA mjini kwenye mikoa hii. Ni gharama kubwa kufanya hivyo, lakini itakuwa investment itakayolipa sana tu, kama vile SGR!
Lengo la kujenga TAZARA ilikuwa kupitisha siraha kwa ajili ya ukombozi wa nchi za kusini mwa Africa, baada ya mabeberu kutubania! Haya mengine ni nsonsonso tu!
 
SGR ya Dar Moro mwaka wa nne huu unakwisha bado haina matarajio wewe unaleta tazara Tena? Wabunge wakienda kuikagua utasikia imeisha kwa asilimia sabini. Ilikua iishe November 2019 Leo hii Ni November 2020 ngoma bado mbichi kabisa.
Mradi wa awamu hii niliouona imeisha kwa mafanikio Ni
Wapinzani ndio walichelewesha hasa Zitto, heche ,Lema na Mbowe ila saivi wanamalizia mwezi wa 12, maana si wamebaki wenyewe?
 
TAZARA haina hali nzuri. Na sababu kubwa ni kwamba utegemezi wa Zambia kwa TAZARA umepungua sana. Kwa sasa Zambia inaweza kupitisha mizigo yao sehemu nyingine zaidi ya Dar es Salaam, kutia ndaniMsumbiji na Afrika Kusini. Lazima tuseme ukweli Wazambia kwa sasa hawana shida sana na TAZARA, japo wao ndio wanatoa Mkurugenzi Mkuu, kosa tulilofanya huko nyuma.

Sasa ili kuinusuru TAZARA, jambo kubwa la kufanya ni kuiunganisha na Malawi kupitia Mbeya pale au Tunduma. Ukifanya hivyo TAZARA itakuwa na umuhimu mkubwa kwa Malawi na kuipa uhai mpya!

Kwa upande wa Malawi, tayari wanafikiria kujenga reli kati ya Central Region na Northern Region, na tayari wana wazo la kuunganisha hiyo reli na TAZARA kama Tanzania watakubali. Kwa hiyo wazo kwa Malawi lipo ni suala la Magufuli kukubaliana na Raisi wa Malawi mradi huo uanze mara moja.

Malawi wanataka sana kuunganishwa na TAZARA kwa sababu ya mradi wao wa makaa ya mawe wa Mchenga Coal Mine sehemu inaitwa Rumphi, mradi wa miti na mbao pale Chikangawana pia uranium pale Kayelekera. Na pia tusisahau suala la mafuta Ziwa Nyasa, yanayoweza kutoa umuhimu wa pekee kwa TAZARA .

Tukikataa kuunganisha TAZARA na Malawi, Malawi wanafikiria kutafuta namna ya kutumia mito Shire na Zambezi ili kufikia Bahari ya Hindi, kwenye mradi utakaoitwa Shire-Zambezi Waterway (SZW). Wakifanya hivyo wataacha kabisa kutumia bandari ya Dar es Salaam. Hivyo basi, ni vema Tanzania kuwafuata Malawi na kujadiliana nao juu ya kuunganisha reli zao na TAZARA

Tanzania inaweza pia kufikiria uwezekano wa kui-divert TAZARA ili ipitie Morogoro na Iringa mjini. Sijui tulitumia akili gani kuwakubalia Wachina wasipitishe TAZARA mjini kwenye mikoa hii. Ni gharama kubwa kufanya hivyo, lakini itakuwa investment itakayolipa sana tu, kama vile SGR!
zama za kuongea na wachina zimepitwa na wakati ni kujenga wenyewe tu
 
Tazara,ijikite zaidi kusafirisha Abiria. Wana maeneo mazuri treni inapita na sehemu zingine watu hawana usafiri wa gari ni treni tu. hasa maeneo kuanzia mlimba mpaka makambako kwenye milima ya Udzungwa. wana maeneo mazuri ya utalii ikiwa selou game reserrve ambayo muheshimiwa ameibadilisha jina hata sikumbuki jina jipya na milima ya Udzungwa ingevutia zaidi watalii. wawe na treni maalum kwa ajili hiyo. kushindana na South Africa kwenye reli hatuwezi, Zambia wana uono wa mbali sana walishawahi kukiangusha chama tawala kule hatuwafakii hata kidogo
 
The railway line will die humbly...

Serikali haina akili ya kufanya biashara,ila kwavile libwana mawe ni hewa,linadhani linaweza chochote...
Hahaha! Hapana Mkuu, tusikate tamaa. Na nakubaliana nawe 100% China ni mabeberu kuliko hata wazungu, kwa kuwa with China anakuja kama rafiki na hujui anakutega nini, baadaye ndio unagundua kakufanya kitu mbaya. Enzi za Mao na kina Chu En Lai waki-deal na Nyerere, those were genuine frieds, sio hawa Wachina wa siku hizi, always wanakuwa na hidden agenda na bado kuna watu wanawaamini kirahisi sana.

Hata hivyo, wazungu at least unachohitaji ni kuwa na akili ya kusoma vizuri mikataba yao between the lines, maana huwa at leat wanakuja kibiashara, japo wanataka ku-maximize profits.

Sasa these are the challenges we face as poor countries. WE cant run away from them, we cant say we will stop dealing with these beberus, we just need to be as smart as possible to meet them on a level business field.

Muhimu kwanza, ni sisi kuwa na mshikamano. Sielewi kwa nini tunasahau mambo ambayo tumeongea siku nyingi sana toka tukiwa watoto shuleni - umoja ni nguvu na utengano ni dhaifu. Sasa tunapokuwa na viongozi kama Magufuli ambao wanaamua tutengane kwa sababu tu za itikadi za kisiasa, huo ni upumbavu ambao utafanya tusifike popote. Whether watu wako CCM au upinzani, lengo ni kuendeleza Tanzania.

Kuna mawazo mazuri na mabaya sana yanatoka CCM na upinzani, sasa suala la msingi ni kujua jinsi ya kuishi pamoja huku tukikubali kushauriana na kukosoana. Mentality za watu kama kina Ndugai ni za kitoto sana kwa nchi hii, na it is very unfortunate kwamba raisi wetu Magufuli anakuwa anazichekea na kuzifurahia mentality za watu kama hao. Kwangu mimi inafanya nimuone kama a very poor national leader, no matter how many good intentions he has for this country
 
SGR ya Dar Moro mwaka wa nne huu unakwisha bado haina matarajio wewe unaleta tazara Tena? Wabunge wakienda kuikagua utasikia imeisha kwa asilimia sabini. Ilikua iishe November 2019 Leo hii Ni November 2020 ngoma bado mbichi kabisa.
Mradi wa awamu hii niliouona imeisha kwa mafanikio Ni
Naomba nimalizie sentensi......mradi wa awamu hii uliokamilika Ni " uwizi wa kula"
 
Kila kitu kishauzwa, nyumba za TZR na viwanja kwenye maeneo karibia yote inakopita reli walishauziana kwa bei chee.
Halafu inaonekana kuna migogoro ya uongozi kwenye hili shirika ndio maana mambo hayaendi.
 
Japo kusafirisha mizigo kwa reli kwenda ambia kwa reli ni nafuu kuliko kutumia malori, bado watu wanapendelea kutumia malori. KUna risks za ajali sana kusafirisha mzigo kwa barabara. Kuna kitu TAZARA inakosea ndio maana watu wanaikwepa
Kwa treni ya Tazara,kusafirisha mzigo ni ghali mno.Bora Kwa Lori na mzigo unafika hadi sehemu husika.Ndio sababu unaona watu bado wanatumia barabara.
 
Kwa treni ya Tazara,kusafirisha mzigo ni ghali mno.Bora Kwa Lori na mzigo unafika hadi sehemu husika.Ndio sababu unaona watu bado wanatumia barabara.
Hizo ndio changamoto TAZARA wanatakiwa wakabiliane nazo, ikiwezekana kuwa na contract na transporters wa malori wa kutoa mzigo kituo cha kushushia TAZARA na kupeleka hadi mlangoni kwa mteja. Hawawezi kuwa wanafanya kazi kwa kufuata traditions.
 
Kila kitu kishauzwa, nyumba za TZR na viwanja kwenye maeneo karibia yote inakopita reli walishauziana kwa bei chee.
Halafu inaonekana kuna migogoro ya uongozi kwenye hili shirika ndio maana mambo hayaendi.
Heee! Hilo sina habari nalo. Nchi hii bwana, inafikia wakati unatamani uipindue na kuwa-Samuel Doe watu waliofanya vitu hivi, kuanzia nyumba za serikali!
 
Back
Top Bottom