Synthesizer
Platinum Member
- Feb 15, 2010
- 12,699
- 22,598
- Thread starter
-
- #21
Heee! Hilo sina habari nalo. Nchi hii bwana, inafikia wakati unatamani uipindue na kuwa-Samuel Doe watu waliofanya vitu hivi, kuanzia nyumba za serikali!Kila kitu kishauzwa, nyumba za TZR na viwanja kwenye maeneo karibia yote inakopita reli walishauziana kwa bei chee.
Halafu inaonekana kuna migogoro ya uongozi kwenye hili shirika ndio maana mambo hayaendi.
Uongo huu mkuu. Nimekaa Tunduma miaka 2 nikifanya kazi. Bandari ya Dar haina mbadala kwa Zambia mpaka sasa labda useme tu huduma ziboreshwe kutokana na changamoto kadha wa kadha.TAZARA haina hali nzuri. Na sababu kubwa ni kwamba utegemezi wa Zambia kwa TAZARA umepungua sana. Kwa sasa Zambia inaweza kupitisha mizigo yao sehemu nyingine zaidi ya Dar es Salaam, kutia ndaniMsumbiji na Afrika Kusini.
Mkuu mara nyingi watu waliokulia katika hali ya umasikini, wanapendezwa sana na vitu vikubwa vizuri ambavyo vinaweza kuwa sio muhimu wala kuwa na tija sana!Kama tumeshindwa kusimamia padogo tutaweza pakubwa? Tusifanye mambo ili tuonekane tunavyo, tufanye vituletee tija ya kweli
Uongo huu mkuu. Nimekaa Tunduma miaka 2 nikifanya kazi. Bandari ya Dar haina mbadala kwa Zambia mpaka sasa labda useme tu huduma ziboreshwe kutokana na changamoto kadha wa kadha.
Acha uongo Mkuu. Bandari ya Dar haina mbadala kwa Zambia, du! Kama huelewi vitu kwa nini uwaite watu waongo? Zambia watu wengi wanatumia bandari ya Beira Msumbiji kwa kuwa umbali wa Beira-Lusaka ni mfupi sana ukilinganisha na Dar - Lusaka. Mizigo mingi ya Zambia ambayo bado inatumia bandari ya Dar ni ile inayokwenda kaskazini mwa Zambia. Ukiwa Lusaka ni logical kupitisha Beira.Uongo huu mkuu. Nimekaa Tunduma miaka 2 nikifanya kazi. Bandari ya Dar haina mbadala kwa Zambia mpaka sasa labda useme tu huduma ziboreshwe kutokana na changamoto kadha wa kadha.
Mmmh!TAZARA haina hali nzuri. Na sababu kubwa ni kwamba utegemezi wa Zambia kwa TAZARA umepungua sana. Kwa sasa Zambia inaweza kupitisha mizigo yao sehemu nyingine zaidi ya Dar es Salaam, kutia ndaniMsumbiji na Afrika Kusini. Lazima tuseme ukweli Wazambia kwa sasa hawana shida sana na TAZARA, japo wao ndio wanatoa Mkurugenzi Mkuu, kosa tulilofanya huko nyuma.
Sasa ili kuinusuru TAZARA, jambo kubwa la kufanya ni kuiunganisha na Malawi kupitia Mbeya pale au Tunduma. Ukifanya hivyo TAZARA itakuwa na umuhimu mkubwa kwa Malawi na kuipa uhai mpya!
Kwa upande wa Malawi, tayari wanafikiria kujenga reli kati ya Central Region na Northern Region, na tayari wana wazo la kuunganisha hiyo reli na TAZARA kama Tanzania watakubali. Kwa hiyo wazo kwa Malawi lipo ni suala la Magufuli kukubaliana na Raisi wa Malawi mradi huo uanze mara moja.
Malawi wanataka sana kuunganishwa na TAZARA kwa sababu ya mradi wao wa makaa ya mawe wa Mchenga Coal Mine sehemu inaitwa Rumphi, mradi wa miti na mbao pale Chikangawana pia uranium pale Kayelekera. Na pia tusisahau suala la mafuta Ziwa Nyasa, yanayoweza kutoa umuhimu wa pekee kwa TAZARA .
Tukikataa kuunganisha TAZARA na Malawi, Malawi wanafikiria kutafuta namna ya kutumia mito Shire na Zambezi ili kufikia Bahari ya Hindi, kwenye mradi utakaoitwa Shire-Zambezi Waterway (SZW). Wakifanya hivyo wataacha kabisa kutumia bandari ya Dar es Salaam. Hivyo basi, ni vema Tanzania kuwafuata Malawi na kujadiliana nao juu ya kuunganisha reli zao na TAZARA
Tanzania inaweza pia kufikiria uwezekano wa kui-divert TAZARA ili ipitie Morogoro na Iringa mjini. Sijui tulitumia akili gani kuwakubalia Wachina wasipitishe TAZARA mjini kwenye mikoa hii. Ni gharama kubwa kufanya hivyo, lakini itakuwa investment itakayolipa sana tu, kama vile SGR!
Mkuu, Tanzania ilipotaka kujenga TAZARA ilienda kwa Uingereza na Germany. Hayo ndio majibu Nyerere aliyopewa, na kuambiwa itakuwa wakijenga TAZARA gharama yake ni kubwa mno Tanzania haitaweza kulipa hilo deni, kutokana na jiografia. Hata magazeti ya Ulaya yalichora katuni kuonyesha Tanzania inafikiria mradi wa reli ambapo treni inapanda mlima kama Kitonga kwa kutukebehi!Kwa Nini naona Ni ngumu Sana kutimiza hili, moja ni kwa sababu ya Jiografia ya nyanda za juu kusini, kupitisha Reli kwenda Malawi na milima ya Mbeya sijui Kama itawezekana, pia Reli hii ya Tazara inapaswa kuwekwa treni za kisasa, Kama Ile ya south Africa.
Kutoa reli kwenda Malawi labda kutoka pale Mpemba Hadi Ileje Kisha itoboze Malawi inaweza kuwa rahisi zaidi.
Walvis Bay ni option nyingine, ila ni karibu umbali sawa na Dar LusakaWalvis bay,Namibia
Chu En Lai akamwahidi Nyerere kwamba China wangesaidia kuijenga hiyo reli, kwa mkopo usio na riba, ndani ya miaka mitano! Nyerere akauliza kwa masharti gani? Akaambiwa wala sio mengi. Makubwa ni haya;
- Tutajenga reli kwa geji inayotumika China, na hivyo kwa miaka fulani mtakuwa mnaagiza vichwa na mabehewa kutoka China
TAZARA haina hali nzuri. Na sababu kubwa ni kwamba utegemezi wa Zambia kwa TAZARA umepungua sana. Kwa sasa Zambia inaweza kupitisha mizigo yao sehemu nyingine zaidi ya Dar es Salaam, kutia ndaniMsumbiji na Afrika Kusini. Lazima tuseme ukweli Wazambia kwa sasa hawana shida sana na TAZARA, japo wao ndio wanatoa Mkurugenzi Mkuu, kosa tulilofanya huko nyuma.
.......,
Tanzania inaweza pia kufikiria uwezekano wa kui-divert TAZARA ili ipitie Morogoro na Iringa mjini. Sijui tulitumia akili gani kuwakubalia Wachina wasipitishe TAZARA mjini kwenye mikoa hii. Ni gharama kubwa kufanya hivyo, lakini itakuwa investment itakayolipa sana tu, kama vile SGR!
Wewe una akili gani ya kuishauri serikali, kichwani huna akili bali unajifanya mjuaji.TAZARA haina hali nzuri. Na sababu kubwa ni kwamba utegemezi wa Zambia kwa TAZARA umepungua sana. Kwa sasa Zambia inaweza kupitisha mizigo yao sehemu nyingine zaidi ya Dar es Salaam, kutia ndaniMsumbiji na Afrika Kusini. Lazima tuseme ukweli Wazambia kwa sasa hawana shida sana na TAZARA, japo wao ndio wanatoa Mkurugenzi Mkuu, kosa tulilofanya huko nyuma.
Sasa ili kuinusuru TAZARA, jambo kubwa la kufanya ni kuiunganisha na Malawi kupitia Mbeya pale au Tunduma. Ukifanya hivyo TAZARA itakuwa na umuhimu mkubwa kwa Malawi na kuipa uhai mpya!
Kwa upande wa Malawi, tayari wanafikiria kujenga reli kati ya Central Region na Northern Region, na tayari wana wazo la kuunganisha hiyo reli na TAZARA kama Tanzania watakubali. Kwa hiyo wazo kwa Malawi lipo ni suala la Magufuli kukubaliana na Raisi wa Malawi mradi huo uanze mara moja.
Malawi wanataka sana kuunganishwa na TAZARA kwa sababu ya mradi wao wa makaa ya mawe wa Mchenga Coal Mine sehemu inaitwa Rumphi, mradi wa miti na mbao pale Chikangawana pia uranium pale Kayelekera. Na pia tusisahau suala la mafuta Ziwa Nyasa, yanayoweza kutoa umuhimu wa pekee kwa TAZARA .
Tukikataa kuunganisha TAZARA na Malawi, Malawi wanafikiria kutafuta namna ya kutumia mito Shire na Zambezi ili kufikia Bahari ya Hindi, kwenye mradi utakaoitwa Shire-Zambezi Waterway (SZW). Wakifanya hivyo wataacha kabisa kutumia bandari ya Dar es Salaam. Hivyo basi, ni vema Tanzania kuwafuata Malawi na kujadiliana nao juu ya kuunganisha reli zao na TAZARA
Tanzania inaweza pia kufikiria uwezekano wa kui-divert TAZARA ili ipitie Morogoro na Iringa mjini. Sijui tulitumia akili gani kuwakubalia Wachina wasipitishe TAZARA mjini kwenye mikoa hii. Ni gharama kubwa kufanya hivyo, lakini itakuwa investment itakayolipa sana tu, kama vile SGR!
Mkuu uko sahihi kabisaa, TAZARA ilibidi wajikite vema kwenye abiria, pia mizigo IPO mingi sanaaa!Tazara,ijikite zaidi kusafirisha Abiria. Wana maeneo mazuri treni inapita na sehemu zingine watu hawana usafiri wa gari ni treni tu. hasa maeneo kuanzia mlimba mpaka makambako kwenye milima ya Udzungwa. wana maeneo mazuri ya utalii ikiwa selou game reserrve ambayo muheshimiwa ameibadilisha jina hata sikumbuki jina jipya na milima ya Udzungwa ingevutia zaidi watalii. wawe na treni maalum kwa ajili hiyo. kushindana na South Africa kwenye reli hatuwezi, Zambia wana uono wa mbali sana walishawahi kukiangusha chama tawala kule hatuwafakii hata kidogo
Mistari miwili ya mwisho ndo yenye uzito mkubwaTazara,ijikite zaidi kusafirisha Abiria. Wana maeneo mazuri treni inapita na sehemu zingine watu hawana usafiri wa gari ni treni tu. hasa maeneo kuanzia mlimba mpaka makambako kwenye milima ya Udzungwa. wana maeneo mazuri ya utalii ikiwa selou game reserrve ambayo muheshimiwa ameibadilisha jina hata sikumbuki jina jipya na milima ya Udzungwa ingevutia zaidi watalii. wawe na treni maalum kwa ajili hiyo. kushindana na South Africa kwenye reli hatuwezi, Zambia wana uono wa mbali sana walishawahi kukiangusha chama tawala kule hatuwafakii hata kidogo
Dar-Beira!!!? au Beira- Lusaka?Acha uongo Mkuu. Bandari ya Dar haina mbadala kwa Zambia, du! Kama huelewi vitu kwa nini uwaite watu waongo? Zambia watu wengi wanatumia bandari ya Beira Msumbiji kwa kuwa umbali wa Beira-Lusaka ni mfupi sana ukilinganisha na Dar - Lusaka. Mizigo mingi ya Zambia ambayo bado inatumia bandari ya Dar ni ile inayokwenda kaskazini mwa Zambia. Ukiwa Lusaka ni logical kupitisha Beira.
Zambia hawakutumia Beira enzi za Makaburu kwa kuogopa hujuma ya mizigo inaposafirishwa kati ya Beira na Lusaka. Baada ya South Afrika kuwa huru basi waligeukia Beira na ndipo TAZARA ikaanza kusuasua.
Na bado kuna Wazambia wanapitisha mizingo bandari ya Durban, pamoja na magari, japo hayaruhusiwi kuendeshwa ndani ya South Africa lazima yapakiwe kwenye lori.
Angalia hapa chini uniambie ukiwa na akili timamu uko Lusaka utaingiza mzigo wako kupitia wapi, Dar au Beira?
Dar Lusaka 1065km
Dar - Beira - 1933km
View attachment 1625509
Nimejichangamya Mkuu; Lusaka - Beira 950kmDar-Beira!!!? au Beira- Lusaka?
Kwa miaka mingi tulinunua locomotives na mabehewa ya TAZARA kutoka China tu. Sasa ina maana China walikuwa wanatengeneza kwa ajili ya TAZARA peke yake? MIaka ya hivi karibuni ndio tulianza kununua toka Germany
Asante mkuu umeeleza mambo mazuri sana. Kitu ambacho ningetaka kuongeza ni kama ulivyosema ushirikiano uliopo katika kuendesha huu mradi wa TAZARA hauna budi kuvunjwa. Hizi nchi mbili haziko pamoja tena kwa sababu kila nchi ina interest yake. Wazambia wana deal na wachina kwa sababu wamekwisha nunuliwa. Sisi bado na wala sitegemei kama watanzania tuko tayari kuiuza nchi yetu. Kwa hali hiyo huu mradi hauwezi ukaendeshwa kama ilivyo zoeleka.Nimesoma comment kuhusu Tazara humu,ila jambo kubwa ni uendeshaji wa Tazara hasa wa Zambia hawatoi hela hasa nadhani.Hata waziri Kamwele aliwahi kulalamikia hilo.Alipoingia raisi Lungu walikubaliana kutoa Bilion 10 kila upande ili kufufua Imjini zilizokuwa zimekufa.Tanzania kwa upande wao walitoa hizo fedha na kununua Motor ili kufufua injini 7 nadhani zitakuwa tayari maana hadi mwezi wa 7 mbili zilikuwa tayari.Pili nadhani ilikubaliwa baadhi ya vipengele vibadilishwe kwenye mkataba wa uanzishaji ili kila upande uweze kuhudumia sehemu ikiwa kwa mfano Tanzania ikinunua Injini,mabehewa ya abiria na mizigo inakuwa mali ya TZ kwa sasa uwezi fanya hivyo utakachonunua ni cha nchi 2 ndio shida.
Serikali haijaisahau Tazara maana hata mishahara inatoa ile migomo haipo toka JPM ameingia,Bado Tazara fursa nyingi zipo upande wa Tanzania Workshop kubwa Mbeya na Dar na ile Kongoro Quary ni kuna kokoto nyingi tuu.
Ishu kubwa ni Zambia kuwa na option nyingine kupata mizigo yao ndio shida.But kwa sasa baada ya mradi wa Nyerere kuanza wanapata mizigo mingi mpaka Fuga na kutoa Cement Mbeya mpaka Fuga.
Mi bado naamini serikali itainyanyua Tazara na itarudi mahali pake,ila ili la mkurugenzi atoke Zambia hadi m raisi alilalamika kwamba atafutwe mtu yeyote mwenye uwezo kufanya hiyo kazi.Maana alipokuwa anatoka kuweka jiwe la msingi la DAM aliwauliza wamefikia wapi kuhusu hayo makubaliano ya kubadili vipengele viongozi waka majibu hayaeleweki mara yapo kwa katibu mkuu miundombinu sijui nini.
Uko sahihi nalandana nawe!Nimesoma comment kuhusu Tazara humu,ila jambo kubwa ni uendeshaji wa Tazara hasa wa Zambia hawatoi hela hasa nadhani.Hata waziri Kamwele aliwahi kulalamikia hilo.Alipoingia raisi Lungu walikubaliana kutoa Bilion 10 kila upande ili kufufua Imjini zilizokuwa zimekufa.Tanzania kwa upande wao walitoa hizo fedha na kununua Motor ili kufufua injini 7 nadhani zitakuwa tayari maana hadi mwezi wa 7 mbili zilikuwa tayari.Pili nadhani ilikubaliwa baadhi ya vipengele vibadilishwe kwenye mkataba wa uanzishaji ili kila upande uweze kuhudumia sehemu ikiwa kwa mfano Tanzania ikinunua Injini,mabehewa ya abiria na mizigo inakuwa mali ya TZ kwa sasa uwezi fanya hivyo utakachonunua ni cha nchi 2 ndio shida.
Serikali haijaisahau Tazara maana hata mishahara inatoa ile migomo haipo toka JPM ameingia,Bado Tazara fursa nyingi zipo upande wa Tanzania Workshop kubwa Mbeya na Dar na ile Kongoro Quary ni kuna kokoto nyingi tuu.
Ishu kubwa ni Zambia kuwa na option nyingine kupata mizigo yao ndio shida.But kwa sasa baada ya mradi wa Nyerere kuanza wanapata mizigo mingi mpaka Fuga na kutoa Cement Mbeya mpaka Fuga.
Mi bado naamini serikali itainyanyua Tazara na itarudi mahali pake,ila ili la mkurugenzi atoke Zambia hadi m raisi alilalamika kwamba atafutwe mtu yeyote mwenye uwezo kufanya hiyo kazi.Maana alipokuwa anatoka kuweka jiwe la msingi la DAM aliwauliza wamefikia wapi kuhusu hayo makubaliano ya kubadili vipengele viongozi waka majibu hayaeleweki mara yapo kwa katibu mkuu miundombinu sijui nini.