Magufuli ili TAZARA isife, ongea na China ili iunganishwe na Malawi kupitia Mbeya au Tunduma, na pia ipitie Morogoro na Iringa mjini!

Kila kitu kishauzwa, nyumba za TZR na viwanja kwenye maeneo karibia yote inakopita reli walishauziana kwa bei chee.
Halafu inaonekana kuna migogoro ya uongozi kwenye hili shirika ndio maana mambo hayaendi.
Heee! Hilo sina habari nalo. Nchi hii bwana, inafikia wakati unatamani uipindue na kuwa-Samuel Doe watu waliofanya vitu hivi, kuanzia nyumba za serikali!

Hawa ni watu waliokuwa mawaziri na vigogo wanapigwa risasi baada ya Samuel Doe kupindua! Mara nyingine unashikwa na hasira za hivyo.

 
TAZARA haina hali nzuri. Na sababu kubwa ni kwamba utegemezi wa Zambia kwa TAZARA umepungua sana. Kwa sasa Zambia inaweza kupitisha mizigo yao sehemu nyingine zaidi ya Dar es Salaam, kutia ndaniMsumbiji na Afrika Kusini.
Uongo huu mkuu. Nimekaa Tunduma miaka 2 nikifanya kazi. Bandari ya Dar haina mbadala kwa Zambia mpaka sasa labda useme tu huduma ziboreshwe kutokana na changamoto kadha wa kadha.
 
Kama tumeshindwa kusimamia padogo tutaweza pakubwa? Tusifanye mambo ili tuonekane tunavyo, tufanye vituletee tija ya kweli
Mkuu mara nyingi watu waliokulia katika hali ya umasikini, wanapendezwa sana na vitu vikubwa vizuri ambavyo vinaweza kuwa sio muhimu wala kuwa na tija sana!
 
Kwa Nini naona Ni ngumu Sana kutimiza hili, moja ni kwa sababu ya Jiografia ya nyanda za juu kusini, kupitisha Reli kwenda Malawi na milima ya Mbeya sijui Kama itawezekana, pia Reli hii ya Tazara inapaswa kuwekwa treni za kisasa, Kama Ile ya south Africa.
Kutoa reli kwenda Malawi labda kutoka pale Mpemba Hadi Ileje Kisha itoboze Malawi inaweza kuwa rahisi zaidi.
 
Uongo huu mkuu. Nimekaa Tunduma miaka 2 nikifanya kazi. Bandari ya Dar haina mbadala kwa Zambia mpaka sasa labda useme tu huduma ziboreshwe kutokana na changamoto kadha wa kadha.
Acha uongo Mkuu. Bandari ya Dar haina mbadala kwa Zambia, du! Kama huelewi vitu kwa nini uwaite watu waongo? Zambia watu wengi wanatumia bandari ya Beira Msumbiji kwa kuwa umbali wa Beira-Lusaka ni mfupi sana ukilinganisha na Dar - Lusaka. Mizigo mingi ya Zambia ambayo bado inatumia bandari ya Dar ni ile inayokwenda kaskazini mwa Zambia. Ukiwa Lusaka ni logical kupitisha Beira.

Zambia hawakutumia Beira enzi za Makaburu kwa kuogopa hujuma ya mizigo inaposafirishwa kati ya Beira na Lusaka. Baada ya South Afrika kuwa huru basi waligeukia Beira na ndipo TAZARA ikaanza kusuasua.

Na bado kuna Wazambia wanapitisha mizingo bandari ya Durban, pamoja na magari, japo hayaruhusiwi kuendeshwa ndani ya South Africa lazima yapakiwe kwenye lori.

Angalia hapa chini uniambie ukiwa na akili timamu uko Lusaka utaingiza mzigo wako kupitia wapi, Dar au Beira?

Dar Lusaka 1933km
Lusaka - Beira - 850km

 
Mmmh!
 
Mkuu, Tanzania ilipotaka kujenga TAZARA ilienda kwa Uingereza na Germany. Hayo ndio majibu Nyerere aliyopewa, na kuambiwa itakuwa wakijenga TAZARA gharama yake ni kubwa mno Tanzania haitaweza kulipa hilo deni, kutokana na jiografia. Hata magazeti ya Ulaya yalichora katuni kuonyesha Tanzania inafikiria mradi wa reli ambapo treni inapanda mlima kama Kitonga kwa kutukebehi!

Siku moja Chu En Lai, nadhani Nyerere akiwa ziarani China, akamuuliza Nyerere, vipi mpango wako wa kujenga TAZARA bado upo? Nyerere akajibu haiwezekani ni gharama sana. Chu En Lai akamwamwambia usiwasikilize Uingereza na Germany, wana ajenda nyingine kukukatalia - akiashiria kulikuwa na dimension ya makaburu kuzuia huo mradi.

Nyerere akauliza na ile milima? Akaambiwa kuna technology ya tunneling, kwa hiyo sehemu hizo tutachimba na kutoboa milima ili kupitisha reli, sio kusawazisha milima.

Chu En Lai akamwahidi Nyerere kwamba China wangesaidia kuijenga hiyo reli, kwa mkopo usio na riba, ndani ya miaka mitano! Nyerere akauliza kwa masharti gani? Akaambiwa wala sio mengi. Makubwa ni haya;
  1. Wakati wote tunajenga reli, kila bidhaa mnayoagiza nje iagizwe kutoka China - kuanzia penseli, raba, matoi ya watoto, soksi, sindano, pini, samaki wa kopo, dawa za miswaki nk hadi vifutio vya darasani!
  2. Wakati wa kujenga reli, mturuhusu udongo tutakaokuwa tukitoa tunapochimba mahandaki (tunnels) tuulete China
  3. Tutajenga reli kwa geji inayotumika China, na hivyo kwa miaka fulani mtakuwa mnaagiza vichwa na mabehewa kutoka China
Nyerere akasema yaani hapo sio tatizo, please come and build the rail! Hivyo kimsingi China wali-offer kujenga TAZARA bila sisi kuwaomba

Kumbuka kwamba hadi sasa China ndio wanaongoza duniani kwa umahiri wa kujenga reli
 

Mimi nafikiri tatizo ni kuwa either

tumebanwa sana na mkataba wa TAZARA hivyo wafanya maamuzi ya kitaifa wanaona ni bora kuipotezea au,

wafanya /mfanya - maamuzi ya kitaifa hawana interest na TAZARA kwasasa / milele -> basi tusubiri atakaye kua na interest ( Waliopita nafikiri walitaka kuwarudishia Wachina) au,

tuna wafanya maamuzi ambao wako vizuri sana kichwani na kimikakati na hivyo kuna jambo jema kitaifa wanalipika linalohitaji kuipotezea TAZARA kwasasa, iliije kushghulikiwa ipasavyo baadae, au etc

Vinginevyo ningeshahuri;

1. Ndoa ya TAZARA ivunjike au irekebishwe kwa makubaliano ili TZ imiliki na kuendesha reli upande wa TZ na Zambia wafanye upande wao ili kila nchi iwajibike kwa matendo yake.

2. Then itengenezwe dry port inayofaa pale Tunduma ili mzigo unaenda au kupitia Zambia usogezwe hapo kutoka Dar port bila kuwepo any unnecessary delays. Treni au malori ya mizigo ya Zambia/Tanzania/DRC yatachukua mizigo kutoka hapo. Abiria wa Zambia-Dar vice versa wata transit hapo mpakani baada ya kupitia immigration.

3. Vituo vya treni upande wa TZ vikarabatiwe na makaumpuni ya ndani chini ya usimamizi makini. Watu wasiohusika wasiruhusiwe kuingia vituoni badala yake kuwe na sehemu za kupokea abiria nje ya vituo.

4. Mabehewa ya abiria yaboreshwe, na daraja la chini kabisa liwe la kukaa bila kuzidi idadi ya viti. wafanyakazi wa ndani ya treni wawe na ujuzi na tabia inayotakiwa kuhudumia abiria.

5. Kuwe na vituo vya kuuza ticket zaidi ya vile vilivyopo katka vituo vya treni. Utatatibu uwe ni wa anayekuja kwanza anapata huduma kwanza. Mfumo wa kuuzia ticket uweze kuhudumia wauzaji wa ticketi nchi nzima bila kuchanganya. Hivyo iwezekane kununua ticket kwa mifumo kama ya Mobile money na katika tovuti.

6. Huduma ya mzigo ya ndani ya nchi iboreshwe kwa kuhakikisha mizigo haipotei na haichakachuliwi. kuwe na maenoeo ya kuchuliwa (pickup) na kufikishwa (delivery) katika maeneo mbali mbali ya miji - isiwe tu katika vituo vya treni. Bei za usafirishaji wa mizigo ziwe rafiki - lengo liwe kutoa huduma endelevu (sustainable) na sio kutengeneza super profit. shirika linaweza kwenda mbele zaidi na kuweka mfumo wa tracking ya mizigo kwakutumi technology kama ya RFID au nyinginezo.

7. Waajiriwe wafanyakazi sahihi na Ratiba ya Treni ifwate wakati uliopangwa bila kukosa.

8. Naamini yakifayika marekebisho haya shirika litaanza kutengeneza pesa kuelekea kupata faida hivyo hata kulipia gharama za marekebisho haya wakati likiendelea kulipa mkopo kwa Wachina..

9. Ikianza kupatikana faida uanzishwe utaratibu wa Hisa ile sehemu ya kampuni imilikiwe na WATANZANIA binafsi wakati serikali ikishikiria kuwa majority share holder. Pesa zinazopatikana kutokana na uuzwaji wa share zitumike kimkakati ilikuongeza mapato zaidi ya kampuni.

10. Shirika liwe na utaratibu wa lazima wa ukarabati wa miuundo mbinu na treni zote bila kusubiri kuharibika. Shule ya msgundi wa treni Mbeya iboreshwe na ikiwezeka ishirikiiane na chuo cha Reli cha Tabora ilikutoa au kunoa wafanyakazi bora wa Shirika.

Mwisho, nilitegemea TAZARA na Reli ya Kati viwe ndio fundisho na/au chachu ya mradi wa Reli (SGR) mpya. Kwamba hapa tulikosea, turekebeshe ilituone matokeo au hapa tumefanya vizuri sasa tuongeze na kupanuka au tuwe wa kisasa zaidi. Lakini sijaliona hilo.

Je tumeshaelewa wapi tumekwama katika TAZARA na Reli ya kati? Je hatutarudia makosa?
 
Wewe una akili gani ya kuishauri serikali, kichwani huna akili bali unajifanya mjuaji.

Hivi unadhani Tazara ni mali ya wachina?
Sasa unataka JPM aongee nao kuhusu nini?

Serikali ya Ccm ipo makini, itajenga Sgr toka Mtwara mpaka Songea na kufika Mbamba Bay, pia itakuwa na matawi kwenda Liganga na Mchuchuma na hii ndio option nzuri ya kuunganisha Malawi na Zambia maana Bandari ya Mtwara ipo karibu. Tumia common sense acha kujifanya unajua.
 
Nimesoma comment kuhusu Tazara humu,ila jambo kubwa ni uendeshaji wa Tazara hasa wa Zambia hawatoi hela hasa nadhani.Hata waziri Kamwele aliwahi kulalamikia hilo.Alipoingia raisi Lungu walikubaliana kutoa Bilion 10 kila upande ili kufufua Imjini zilizokuwa zimekufa.Tanzania kwa upande wao walitoa hizo fedha na kununua Motor ili kufufua injini 7 nadhani zitakuwa tayari maana hadi mwezi wa 7 mbili zilikuwa tayari.Pili nadhani ilikubaliwa baadhi ya vipengele vibadilishwe kwenye mkataba wa uanzishaji ili kila upande uweze kuhudumia sehemu ikiwa kwa mfano Tanzania ikinunua Injini,mabehewa ya abiria na mizigo inakuwa mali ya TZ kwa sasa uwezi fanya hivyo utakachonunua ni cha nchi 2 ndio shida.
Serikali haijaisahau Tazara maana hata mishahara inatoa ile migomo haipo toka JPM ameingia,Bado Tazara fursa nyingi zipo upande wa Tanzania Workshop kubwa Mbeya na Dar na ile Kongoro Quary ni kuna kokoto nyingi tuu.
Ishu kubwa ni Zambia kuwa na option nyingine kupata mizigo yao ndio shida.But kwa sasa baada ya mradi wa Nyerere kuanza wanapata mizigo mingi mpaka Fuga na kutoa Cement Mbeya mpaka Fuga.
Mi bado naamini serikali itainyanyua Tazara na itarudi mahali pake,ila ili la mkurugenzi atoke Zambia hadi m raisi alilalamika kwamba atafutwe mtu yeyote mwenye uwezo kufanya hiyo kazi.Maana alipokuwa anatoka kuweka jiwe la msingi la DAM aliwauliza wamefikia wapi kuhusu hayo makubaliano ya kubadili vipengele viongozi waka majibu hayaeleweki mara yapo kwa katibu mkuu miundombinu sijui nini.
 
Mkuu uko sahihi kabisaa, TAZARA ilibidi wajikite vema kwenye abiria, pia mizigo IPO mingi sanaaa!

Pale Mlimba Kuna barabara imechingwa inaenda mafinga ( iringa) hivyo inaweza badili upepo wa abiria hasa wanaotaka kwenda iringa mjini!!
Lakini ukianzia mngeta,Chita,Mlimba,mpanga,uchindile Hadi makambako reli hii inahitaji maboresho Sana maana Mara kadhaa ajali hutokea hasa Treni ya mizigo!!

Ukija kuanzia mbingu, Ruipa, idete,Ifakara, kiberege, mang'ula, kisaki bado reli ni mbovu inahitaji maboresho Sana!
Zaidi ya yote TAZARA Ni msaada mkubwa Sana!
 
Mistari miwili ya mwisho ndo yenye uzito mkubwa
 
Dar-Beira!!!? au Beira- Lusaka?
 
Asante mkuu umeeleza mambo mazuri sana. Kitu ambacho ningetaka kuongeza ni kama ulivyosema ushirikiano uliopo katika kuendesha huu mradi wa TAZARA hauna budi kuvunjwa. Hizi nchi mbili haziko pamoja tena kwa sababu kila nchi ina interest yake. Wazambia wana deal na wachina kwa sababu wamekwisha nunuliwa. Sisi bado na wala sitegemei kama watanzania tuko tayari kuiuza nchi yetu. Kwa hali hiyo huu mradi hauwezi ukaendeshwa kama ilivyo zoeleka.

Kitu ambacho ninacho shauri ni kwamba let us do Business. Tunatakiwa huu mradi kuuboresha na kuweka kuwa mradi wa kisasa. Jamani ulimwengu umebadilika na ili sisi tuweze kwenda na wakati inabidi sasa tuanze kuwa na interests zetu. Kwa vile tuna potential kubwa sana ya kuwawekea wajukuu zetu mazingira bora ya biashara, kwa hivyo let us start now!

Huu mradi inabidi tuubadilishe na kuwa wa kisasa zaidi, yaani badala ya kutumia Locomotives tuuweke uwe wa High speed trains na SGR. Uwe wa speed ya 220km/h average. Hii inatosha kabisa na South Africa wala Zambia sidhani kama wana treni ambayo inaweza kimbia kwa mwendo huo.
Hapo tutakuwa tumewaacha nyuma.

You know inabidi tujikunje na hela zetu ili tuwe competative. Tukiendelea na treni za mizoga hizo hazita tufikisha mbali. Sisi lazima tuwaze mbali na sio kusubiri mpaka mzungu aanze nasi ndiyo tuige. No tunaweza kuwa Trend setter vile vile.

Ningemshauri Rais na serikali yake kuachana na dhamira yake ya kuwekeza kwenye mradi huu zaidi, badala yake ajenge SGR mpya ambayo ni competative kutoka Dar Port mpaka Tunduma. Vile vile kama ulivyo sema hatuna budi kuwa customer friendly kwa kuhamishia Bandari kavu Tunduma kiasi kwamba Wazambia wa kaskazini, wakongo wa Lubumbashi, Wamalawi wa kaskazini na wengineo watoe mizigo yao Tunduma kiurahisi.

Sisi tunaishusha mizigo yao kutoka kwenye meli Dar Port na kuwatoza hela ndogo za transport ya mizigo yao mpaka Tunduma. Hapo ndipo wao wenyewe wanafanya process zote za ku clear mizigo yao. Hiyo ni Business making na ajira vile vile kwa vijana wetu zitazalishwa.

Watanzania ndugu zangu tuwe wabunifu kidogo na sio kuogopa kuingia risks. Rais Magufuli hawezi akajua kila kitu nankutuambia sisi nini anataka. Ni lazima wale watu walio bahatika kuwa katika serikali yake, kumwelekeza kwa unyenyekevu kitu gani kingetakiwa kifanyike amnacho ni cha msingi na chenye tijaa kwa Taifa letu.

Najua kuwa yeye ni kichwa ngumu, lakini akiwa asured kuwa miradi ya namna hii inaleta ajira na maendeleo ya haraka kwa watanzania atakubali tu ifanyike.

Rais Magufuli amekuwa devoted kwenye kuleta maendeleo ya kweli kwa watanzania wote. Na nina uhakika ya kwamba akija kustaafu atafurahi sana na kuridhika moyoni kama atawaona watanazania wenzake wakiishi kwa raha na furaha kama wengine duniani.
 
Uko sahihi nalandana nawe!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…