Mahakama Kuu Dar, imetupilia mbali kesi ya Kikatiba iliyofunguliwa dhidi ya Spika Ndugai kwa kumtambua Mwambe kama Mbunge baada ya Kujiuzulu

Mahakama Kuu Dar, imetupilia mbali kesi ya Kikatiba iliyofunguliwa dhidi ya Spika Ndugai kwa kumtambua Mwambe kama Mbunge baada ya Kujiuzulu

Namiomba sana Mungu hawa Majaji wanao amua kesi kwa maslahi ya amri za kutoka juu wewe hai hadi utakapo patikana uongozi wa nchi unao fuata sheria na kutii viapo vyao. Maana hivi sasa siamini kama kuna majaji/mahakimu wanao tafsri sheria.
Ati jaji anasema mahakama ina sumbukiwa?? Kweli?? Hivi wana thubutu kujiita majaji kweli?? Mungu yupo

Hawa sio Majaji baali ni Majizi tu!!!
Rais Magufuli tangu aingie Madarakani ameparaganyisha kabisa Mhimili wa Mahakama,Bunge na Serikali......Inasikitisha Sana!!!
Lakini dawa ya Marais Madikteta na wababe kama JIwe na kina Trump iko jikoni inachemka.....!!!Trump Kesha Anza kuinywa kwa lazima!
Ni swala la muda tu.
 
View attachment 1467675
Mahakama Kuu Kanda ya Dar es Salaam imetoa uamuzi na kutupilia mbali shauri la Kikatiba Na. 10 la mwaka 2020 lililofulinguliwa na Wakili wa Kujitegemea Revocatus Paul Kaunda kupinga Kauli ya Mhe. Spika aliyoitoa Bungeni kumtambua Mhe. Cecil Mwambe kuendelea kuwa Mbunge.

Mahakama Kuu kupitia Jopo la Majaji watatu ambao ni Mhe. Jaji Issa Maige, Stephen ,Mrimi Magoiga na Seif Mwinshehe Kulita, wametupilia mbali shauri hilo kwa uamuzi kuwa "SHAURI HILO HALINA MSINGI KISHERIA NA LENYE LENGO LA KUSABABISHA USUMBUFU KWA MAHAKAMA ". Mahakama imeona kuwa hoja zilizoletwa Mahakamani hapo zinahusu kuitaka Mahakama kutoa tafsiri iwapo Mhe. Mwambe ni Mbunge au sio mbunge. Hoja hiyo ingepaswa kuletwa kupitia shauri la Uchaguzi chini ya Ibara ya 83 ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na sio suala la Maombi ya Haki ya Kikatiba kama Mleta maombi hayo alivyofanya kupitia Ibara ya 26(2) ya Katiba. Mahakama imeona kuwa suala ambalo limejitokeza Bungeni kuhusu kukoma au kutokoma kwa Ubunge wa Mhe. Mwambe linahusu pia uamuzi wa Spika chini ya Kifungu cha 37 Cha Sheria ya

Katika shauri hilo Mleta Maombi waliwakilishwa na Wakili Daimu Halgfani, Steven Mwakibolwa, Fulgence Massawe. Mwambe aliwakilishwa na Wakili wa Kujitegemea Raphael na Upande wa Mhe Spika na Mwanasheria Mkuu wa Serikali wamewakilishwa na Bw. Vicent Tangoh (Wakili wa Serikali) Mkuu) , Bw. George Mandepo (Wakili wa Serikali Mkuu), Bibi Alesia Mbuta (Wakili wa Serikali Mkuu), Bw. Erigh Mrisha (Wakili wa Serikali) na NBibi Narindwa Sekimanga.

Mahakamani hapo leo pia, Mahakama ilitaja kesi inayofafana iliyofunguliwa na Arusha na kuhamishiwa Masijala ya Dar es Salaam. Kesi hiyo Na. 12 ya 2020 imefunguliwa na Asasi iliyo ya Kiserikali ya Civic and Legal Organisation ikipinga pia ubunge wa Mhe. Mwambe. Wadawa katika kesi hiyo ya kikatiba ni Mhe. Spika , Mwanasheria Mkuu wa Serikali na Cecil Mwambe.

Kesi hiyo itakuja kwa kutajwa tena Mahakamani hapo tarehe 11 Juni, 2020.

=====

Mahakama Kuu Kanda ya Dar es Salaam imetupilia mbali kesi ya Kikatiba iliyofunguliwa na wakili Paul Kaunda dhidi ya Spika wa Bunge, Job Ndugai akiomba mahakama hiyo kutengua amri ya Spika kumtambua Cecil Mwambe kama mbunge halali wa Ndada ikisema amekosea kufungua shauri hilo.

Mbali na Ndugai, walalamikiwa wengine katika shauri hilo ni aliyekuwa mbunge wa Ndanda, Cecil Mwambe na Mwanasheria Mkuu wa Serikali.
rasmi Tanzania sasa ishageuka kuwa lawless country.
kila mtu apambane na hali yake - ndiyo ujumbe kwa Watanzania chini ya awamu ya 5.
 
Jaji steven magoiga aliwahi kugombea ubunge kwa ngazi ya kura za maoni za ccm (hakupita), akateuliwa kuwa mkurugenzi wa kishapu halafu akateuliwa kuwa Jaji wa high court
Tafakari.
 
"Huliza, post: 35580354, member: 431979"]Wanasiasa wanapotezea watu muda wa kufanya kazi
Suala hili limekupotezea vipi muda wako?
Kila mtu apambane na hali yake
Mwenye shauri alikuomba ushiriki?
Liwe Bunge au Mwambe kila mtu anaangalia familia yake
Nani alikuomba ushauri wa familia yake?
Kwa ufupi wananchi angalieni maisha yenu
Kwa ufupi unapambana na hali yako unalipa kodi kubwa sana inakwenda kuwalipa wenzako milioni 11 kwa mwezi. Unawapambania, hupambani na hali yako.

Nenda kapambane na hali yako kwa kuwalipia kodi wenzako. Watoto wako wanaishia VETA na wewe kila siku heri ya jana. kauli mbiu yao ''unapambana na hali yako'' ha ha ha ha !
Hao waliokwenda mahakamani hawana shida kama ulizo nazo! wanakupambania wewe mlipa kodi usiyeweza kurepea kandambili.

tindo JokaKuu
 
Tulitegemea hilo hakuna jipya ndiyo maana wananchi wanataka katiba mpya

Kwa hakika kabisa Katiba tuliyo nayo Sasa ni kwa ajili ya CCM tu na si Taifa la Tanzania. Watu wajiulize ni kwanini Magufuli hataki kuendeleza mchakato wa Katiba mpya?
CCM Wana hofu ya kupoteza madaraka ikiwa KATIBA MPYA itaanza kutumika! Ukweli mchungu!
 
Hukutegemea lakini ulishangilia kesi kupelekwa huko.

Toka mwanzo nilijua majibu yatakayotolewa na hizi mahakama, najua ni kwa kiasi gani utawala wa sheria umenajisiwa. Katika mazingira hayo kipi kingenifanya nishangilie? Nazidharau mno hizi mahakama zilizojiingiza kwenye siasa chafu.
 
Toka mwanzo nilijua majibu yatakayotolewa na hizi mahakama, najua ni kwa kiasi gani utawala wa sheria umenajisiwa. Katika mazingira hayo kipi kingenifanya nishangilie? Nazidharau mno hizi mahakama zilizojiingiza kwenye siasa chafu.
Ahahahahahah!
 
Tatizo wapinzani wanakurupuka bila kusoma sheria vizuri. Sheria ni msumeno, hao mnaowashitaki wapo pale sio kwa sababu ya kuwa pale tu. Hawafanyi kazi zao kwa kukurupuka wanafuata sheria, sasa Mahakama wanapowatafsiria sheria na nyinyi mnakataa maana yake ni kwamba uamuzi wowote ule utakaotolewa hamuwezi kuupenda, lakini mnaposhinda mnapayuka kama majuha vile. Kama mnafikiri hamjatendewa haki nafasi bado ipo ya kukata rufaa.
 
View attachment 1467675
Mahakama Kuu Kanda ya Dar es Salaam imetoa uamuzi na kutupilia mbali shauri la Kikatiba Na. 10 la mwaka 2020 lililofulinguliwa na Wakili wa Kujitegemea Revocatus Paul Kaunda kupinga Kauli ya Mhe. Spika aliyoitoa Bungeni kumtambua Mhe. Cecil Mwambe kuendelea kuwa Mbunge.

Mahakama Kuu kupitia Jopo la Majaji watatu ambao ni Mhe. Jaji Issa Maige, Stephen ,Mrimi Magoiga na Seif Mwinshehe Kulita, wametupilia mbali shauri hilo kwa uamuzi kuwa "SHAURI HILO HALINA MSINGI KISHERIA NA LENYE LENGO LA KUSABABISHA USUMBUFU KWA MAHAKAMA ". Mahakama imeona kuwa hoja zilizoletwa Mahakamani hapo zinahusu kuitaka Mahakama kutoa tafsiri iwapo Mhe. Mwambe ni Mbunge au sio mbunge. Hoja hiyo ingepaswa kuletwa kupitia shauri la Uchaguzi chini ya Ibara ya 83 ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na sio suala la Maombi ya Haki ya Kikatiba kama Mleta maombi hayo alivyofanya kupitia Ibara ya 26(2) ya Katiba. Mahakama imeona kuwa suala ambalo limejitokeza Bungeni kuhusu kukoma au kutokoma kwa Ubunge wa Mhe. Mwambe linahusu pia uamuzi wa Spika chini ya Kifungu cha 37 Cha Sheria ya

Katika shauri hilo Mleta Maombi waliwakilishwa na Wakili Daimu Halgfani, Steven Mwakibolwa, Fulgence Massawe. Mwambe aliwakilishwa na Wakili wa Kujitegemea Raphael na Upande wa Mhe Spika na Mwanasheria Mkuu wa Serikali wamewakilishwa na Bw. Vicent Tangoh (Wakili wa Serikali) Mkuu) , Bw. George Mandepo (Wakili wa Serikali Mkuu), Bibi Alesia Mbuta (Wakili wa Serikali Mkuu), Bw. Erigh Mrisha (Wakili wa Serikali) na NBibi Narindwa Sekimanga.

Mahakamani hapo leo pia, Mahakama ilitaja kesi inayofafana iliyofunguliwa na Arusha na kuhamishiwa Masijala ya Dar es Salaam. Kesi hiyo Na. 12 ya 2020 imefunguliwa na Asasi iliyo ya Kiserikali ya Civic and Legal Organisation ikipinga pia ubunge wa Mhe. Mwambe. Wadawa katika kesi hiyo ya kikatiba ni Mhe. Spika , Mwanasheria Mkuu wa Serikali na Cecil Mwambe.

Kesi hiyo itakuja kwa kutajwa tena Mahakamani hapo tarehe 11 Juni, 2020.

=====

Mahakama Kuu Kanda ya Dar es Salaam imetupilia mbali kesi ya Kikatiba iliyofunguliwa na wakili Paul Kaunda dhidi ya Spika wa Bunge, Job Ndugai akiomba mahakama hiyo kutengua amri ya Spika kumtambua Cecil Mwambe kama mbunge halali wa Ndada ikisema amekosea kufungua shauri hilo.

Mbali na Ndugai, walalamikiwa wengine katika shauri hilo ni aliyekuwa mbunge wa Ndanda, Cecil Mwambe na Mwanasheria Mkuu wa Serikali.
Nilisema hakuna jaji wa ku handle kesi kama hiyo! hao wote ni UPE Judges. hakuna mwenye intellect wa kuhandle kesi kama hiyo! Kulita alikuwa Juzi Magistrates courts anatoa hukumu "mavi", leo awe na akili ya kufikiri kwa kitu kzito kama hicho!
 
Katiba ya nchi inataka mbunge kudhaminiwa na chama ,na Mara udhamini wake utakapo koma atapoteza ubunge wake ,tumeona hili likitokea kwa wabunge wengi.Sasa hii ya Ndugai kuwakingia kifua waliofukuzwa uanachama maana yake ni kuwa yeye ndio kawadhamini ambapo katiba haimtambui,hii Ni kuanzisha wabunge kundi la viti maalum vya spika kinyume na katiba cha ajabu na Mahakama Imebariki?.Awamu hi tutaona mengi ,hongera wabunge wa viti maalum vya spika.
 
Katiba ya nchi inataka mbunge kudhaminiwa na chama ,na Mara udhamini wake utakapo koma atapoteza ubunge wake ,tumeona hili likitokea kwa wabunge wengi.Sasa hii ya Ndugai kuwakingia kifua waliofukuzwa uanachama maana yake ni kuwa yeye ndio kawadhamini ambapo katiba haimtambui,hii Ni kuanzisha wabunge kundi la viti maalum vya spika kinyume na katiba cha ajabu na Mahakama Imebariki?.Awamu hi tutaona mengi ,hongera wabunge wa viti maalum vya spika.
wewe unashangaa hilo?

Kajionee namna sarikaki hii ya awmu ya tano, namna ilivyodhamiria kuupeleka muswada bungeni, ambapo itakuwa "marufuku" kwa mtu yeyote kupeleka shauri mahakamani linalohusu uvunjwaji wa Katika ya nchi, kwa viongozi wakuu wa nchi, ambao ni Rais, Makamu wake, Waziri mkuu, Spika wa Bunge na Jaji Mkuu!

Je kuna maana gani kwa viongozi hao wakuu wa nchi, kuapa kuitetea Katiba ya nchi kabla hawajakabidilhiwa madaraka hayo??
 
wewe unashangaa hilo?

Kajionee namna sarikaki hii ya awmu ya tano, namna ilivyodhamiria kuupeleka muswada bungeni, ambapo itakuwa "marufuku" kwa mtu yeyote kupeleka shauri mahakamani linalohusu uvunjwaji wa Katika ya nchi, kwa viongozi wakuu wa nchi, ambao ni Rais, Makamu wake, Waziri mkuu, Spika wa Bunge na Jaji Mkuu!

Je kuna maana gani kwa viongozi hao wakuu wa nchi, kuapa kuitetea Katiba ya nchi kabla hawajakabidilhiwa madaraka hayo??
yani maafrika hapana kwakweli
 
Tukisema nchi inaongozwa na washamba mlifikiri tulimaanisha nn?? Nchi hii sasa ni wazi itaongozwa kwa mawazo ya mtu na si kwa kufuata Sheria na Katiba ya nchi.
 
Back
Top Bottom