Mahakama kuu imesema msanii Elizabeth Michael (Lulu) ana kesi ya kujibu

Mahakama kuu imesema msanii Elizabeth Michael (Lulu) ana kesi ya kujibu

Masikini Lulu. Wamsamehe tu.
Ningekuwa mimi ndo mama kanumba ningesamehe tu kwani hata akifungwa mwanae hawezi kurudi
Inaonesha una elimu ndogo juu ya maswala ya sheria mpenzi.

Kiufupi ni hivi katika aina ya makosa, kuna makosa ambayo yameainishwa kama ya jinai na makosa yasiyo ya jinai kama ya madai.

Sasa hapa kosa la Elizabeth Michael linaangukia katika jinai. Kwa maana kuua, kuiba, kutukana, kujeruhi, kutishia kuuwa au kujeruhi, kupiga, kubaka ama kulawiti mtoto mdogo, kutembea na mwanafunzi, kubaka mwanamke au mwanaume, kuendesha gari bila leseni, kukwepa kodi, kutapeli mali ya mtu, kujipatia pesa kwa njia ya udanganyifu, matumizi mabaya ya ofisi za uma, kuendesha gari haijakatiwa bima, kuuza bima feki, na mengineyo mengi ni aina ya makosa ya jinai kwa tafasiri ya kwamba sheria imeyaweka wazi kuwa ni kinyume cha utaratibu wa nchi.

Hivyo basi unapofanya kosa lolote la jinai, anayekukamata ni askari na ndiye anayepeleka mashitaka( kukusemea) kwenye vyombo vya sheria( mahakama) na huko utakwenda kusomewa tuhuma dhidi yako na pale utakapokutwa na hatia na ushahidi dhidi yako kubaini unahusika moja kwa moja na mashitaka husika then hainaga mjadala hiyo ni unakutwa na adhabu ile iliyoainishwa kwa mujibu wa sheria.

Mama kanumba hata akimsamehe hawezi kufanya chochote katika kuzuia huyu binti asipatwe na adhabu pale akikutwa na hatia kwa maana ametenda jinai na ni yeye dhidi ya serikali si dhidi ya mama kanumba. Binadamu tunaongozwa na hisia ila sheria ndizo zinazoongoza mahusiano yetu hapa duniani.

Kwa mfano mimi nikikukuta wewe na mumeo mnagombana na mumeo anakupiga na kukujeruhi ninaweza kwenda kumchukulia polisi.....wakamshika na kumuweka mahabusu, akafunguliwa kesi ya kushambulia na kudhalilisha mwanamke, akahukumiwa muda usiopungua miezi sita na faini si chini ya laki tano. Basi tu huwa tunakaushiana
 
Inakumbusha ile kesi ya mkimbiaji kilema msouth ambiwa anakesi ya kujibu mwisho akahukumia Kifungo lakini Mungu ampigianie.
 
Ata Manji alikuwa na kesi ya kujibu halafu mwishoni katusua .... mi sion km kuna ushahid wa kumfunga huyo lulu taking the fact walikuwa wawili chumban na hakuna mtu wa kutoa ushahid direct kwamba alimuona akimuua Kanumba .... nadhan kwake ni simple tu ushahid wa daktari na ushahid wake yy mwenyewe unamnasua .... by the way sitegemei kuwa Lulu alimuua Kanumba
Kesi gani?!
 
Ata Manji alikuwa na kesi ya kujibu halafu mwishoni katusua .... mi sion km kuna ushahid wa kumfunga huyo lulu taking the fact walikuwa wawili chumban na hakuna mtu wa kutoa ushahid direct kwamba alimuona akimuua Kanumba .... nadhan kwake ni simple tu ushahid wa daktari na ushahid wake yy mwenyewe unamnasua .... by the way sitegemei kuwa Lulu alimuua Kanumba
Kwahiyo aliamua kufa tu?!
 
Masikini Lulu. Wamsamehe tu.
Ningekuwa mimi ndo mama kanumba ningesamehe tu kwani hata akifungwa mwanae hawezi kurudi

Amsamehe vipi wakati yeye Lulu ana shine kila siku nguo mpya za gharama na mama ake ,wakati yeye mama Kanumba ananyauka na balimi kwa mwanae anayemtegemea kama mama Diamond kutolewa roho?

Chamsingi familia ya Lulu wangetafuta amani na familia ya Kanumba wayamalize kiutamaduni ,kama ng'ombe zichinjwe wale wasameheane. na Lulu achukue jukumu la kumlea huyo mama .

Japo hilo ni kosa la jinai na jamhuri ndo wahusika
 
Mungu saidia JUSTICE FOR KANUMBA.Eliza atuambie nini kilichotokea mule chumbani?Afungwe tu Lulu.
 
Alure KUNA KUNA KUUA KWA KUKUSUDIA NA KUTOKUSUDIA.

HAKUNA ANAYESEMA LULU ALIAMUA KUMWUA KWA MAKUSUDI KANUMBA ILA LAZIMA AWE NA KESI YA KUJIBU KWA KUWA YEYE NDYE ALIKUWA NA MAREHEMU MPK ANAKATA ROHO.

AKILETA MZAHA ATANYEA DEBE, DAMU YA MTU INAONGEA.

Hatofungwa maisha lakini kukaa jela hata miaka 7 syo nchezo nchezo
 
Duh! Pole zake. Sijui ni kesi ya kuua bila kukusudia au ni kesi ya kusababisha kifo!
 
Kutoa roho ya binaadamu mwenzako kisa mapenzi sio jambo la mchezo lazima sheria ifanye kazi yake.
Sheria no msumeno hakika unapaswa ukate bila kutazama sura, umaarufu, utajiri, umasikini wote wakatwe sawa na msumeno wa sheria.
 
Samcezar HONGERA KWA MAELEZO MAZURI

LAKINI MIMI NAJUA KUNA AINA TATU ZA KESI
1. KESI YA MADAI
2. KESI YA JINAI
3. KESI YA MAUAJI (MURDER CASE)

NAMBA 2 NA 3 ANAYESHTAKI NI JAMHURI

NAMBA MOJA, KUNA MDAI (MLALAMIKAJI) NA MDAIWA.
 
Masikini Lulu. Wamsamehe tu.
Ningekuwa mimi ndo mama kanumba ningesamehe tu kwani hata akifungwa mwanae hawezi kurudi

Elewa kuwa hapa si mama Kanumba ndo mshitaki , ni Jamhuri , hata akimsamehe kesi iko pale pale, kwani aliua Raia wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.
 
Inaonesha una elimu ndogo juu ya maswala ya sheria mpenzi.

Kiufupi ni hivi katika aina ya makosa, kuna makosa ambayo yameainishwa kama ya jinai na makosa yasiyo ya jinai kama ya madai.

Sasa hapa kosa la Elizabeth Michael linaangukia katika jinai. Kwa maana kuua, kuiba, kutukana, kujeruhi, kutishia kuuwa au kujeruhi, kupiga, kubaka ama kulawiti mtoto mdogo, kutembea na mwanafunzi, kubaka mwanamke au mwanaume, kuendesha gari bila leseni, kukwepa kodi, kutapeli mali ya mtu, kujipatia pesa kwa njia ya udanganyifu, matumizi mabaya ya ofisi za uma, kuendesha gari haijakatiwa bima, kuuza bima feki, na mengineyo mengi ni aina ya makosa ya jinai kwa tafasiri ya kwamba sheria imeyaweka wazi kuwa ni kinyume cha utaratibu wa nchi.

Hivyo basi unapofanya kosa lolote la jinai, anayekukamata ni askari na ndiye anayepeleka mashitaka( kukusemea) kwenye vyombo vya sheria( mahakama) na huko utakwenda kusomewa tuhuma dhidi yako na pale utakapokutwa na hatia na ushahidi dhidi yako kubaini unahusika moja kwa moja na mashitaka husika then hainaga mjadala hiyo ni unakutwa na adhabu ile iliyoainishwa kwa mujibu wa sheria.

Mama kanumba hata akimsamehe hawezi kufanya chochote katika kuzuia huyu binti asipatwe na adhabu pale akikutwa na hatia kwa maana ametenda jinai na ni yeye dhidi ya serikali si dhidi ya mama kanumba. Binadamu tunaongozwa na hisia ila sheria ndizo zinazoongoza mahusiano yetu hapa duniani.

Kwa mfano mimi nikikukuta wewe na mumeo mnagombana na mumeo anakupiga na kukujeruhi ninaweza kwenda kumchukulia polisi.....wakamshika na kumuweka mahabusu, akafunguliwa kesi ya kushambulia na kudhalilisha mwanamke, akahukumiwa muda usiopungua miezi sita na faini si chini ya laki tano. Basi tu huwa tunakaushiana
Safi sana ngosha umefumbua macho
 
Back
Top Bottom