Mahakama Kuu yatengua hukumu ya kuvuliwa Uwakili dhidi ya Fatuma Karume

Erythrocyte

JF-Expert Member
Joined
Nov 6, 2012
Posts
128,308
Reaction score
245,426
Hii ndio taarifa mpya iliyotufikia muda huu kutoka Mahakamani .

Taarifa hiyo inaeleza kwamba Mahakama kuu imeona kwamba Fatuma Karume alihukumiwa bila kupewa nafasi ya kujitetea mbele ya Kamati ya maadili ya Mawakili , hivyo imetengua hukumu yake na kuitaka Kamati hiyo kumaliza jambo hilo kwa haki

Ikumbukwe kwamba Mlalamikaji kwenye hili Sakata la Wakili Msomi Fatuma Karume lililojaa chuki, Wivu na uzandiki alikuwa Mwanasheria Mkuu wa Serikali , Je unadhani bado anafaa kukalia ofisi hiyo ?

 
Naona sikuhizi mahakama inanyoosha mikono kila kukicha, uonevu ulikuwa mkubwa sana.

Ila kuna huyu, Kigogo2014 na Maria Sarungi ni moto wa gesi unaochoma mioyo ya Mataga.
 
Huo ni ushindi kwa Dada,nawapenda haki wote
 

Maelekezo kutoka juu yalikwenda na aliyekwenda. Abakie huko huko.

Hiiiiii bagosha!
 
Sasa hivi Mihimili mingine imeanza kujiinua tena kutokea mavumbini. Ni muda sahihi sasa kurudi Mahakamani kufungua shauri la kupinga Halmashauri chini ya uongozi wa DEDs kusimamia chaguzi zote

Sisi Nchi tajiri sana hatushindwi kuweka key staff wa NEC Nchi nzima.
 
Naona sikuhizi mahakama inanyoosha mikono kila kukicha, uonevu ulikuwa mkubwa sana.

Ila kuna huyu, Kigogo2014 na Maria Sarungi ni moto wa gesi unaochoma mioyo ya Mataga.
Ili kuendana na upepo huu mpya ni dhahiri sasa Jaji Mkuu na Mwanasheria Mkuu waondolewe , tusimung'unye maneno , hawa walishiriki kila uchafu .
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…