Mahakama ya ICSID: Professional bullying anayofanyiwa Profesa Mruma inafedhehesha jamii ya Wanazuoni

amedhalilishwa tena vya kutosha, tena na vibwamdogo tu vya kizungu ona huyo dogo hata 30 anaweza kuwa hajafika ila anamsumbua mtu anayejiita profesa wa kibongolala.
 
tunataka sikiu moja aende na mwigulu na phd yake ya open university tukamsikie anaongeaje. akimaliza huyo aende Jafo na Doto.
 
ndio maana maishani mwangu sijawahi kuheshimu profesa hata mmoja, naonaga wendawazimu tu waliochanganyikiwa na kitabu hata hawana uwezo kufanyia kazi elimu yao. ona sasa anadhalilishwa na vitoto vidogo havina hata masters.
 

Prof hapa alikuwa witness tu ndio nakubaliana na wewe, pamoja na prof kuwa witness pia kuna language barrier kati ya prof na hao majamaa wa winshear hawezi kabisa kutamka full sentence hata 1 tu akaeleweka. Huyu prof kingereza hajui hata kama vifungu vimekaa vibaya atleast tuone uwasilishaji wako wa hoja kama shahidi lakini yeye masikini anabaki kurusharusha mikono.
 
Ameyataka mwenyewe mtu wa geology ametoka wapi na wanasheriaa sipati picha Yule aliye kuwa mwanasheria wa jiwe bwana adeledurus kilangi jamaa alikuwa mweupe mno

Hyo Kaz angepewa Andrew chenge tungeshinda hyo kesi

Hapa mruma ameenda kama shahidi na si msimamizi au wakili wa kusimamia kesi.
Anaendaje chenge wakati hakuwepo kwenye cabinet iliyoundwa na magufuli kwenye hili suala.

Mwepesi kuhukumu halafu hata hujui kinachozungumziwa ni kipi.
Mruma kazingua hawezi kuongea kingereza tu, Yeye na mwenzake huyo wameenda as witnesses na si advocates.
 
Haya mambo hupikwa.....Kuna mwaka fulani kiongozi wetu mkubwa alidhalilishwa na kujikuta anaingia na suti SAUNA.
wengine walishawahi kukosa hotel Japan mpaka marehemu Mengi akaokoa jahazi.
 
Nasikia kwasasa wame restrict kuipata Tanzania lazima utumie VPN. Wanafikiri aibu ni hapa Tanzania kumbe ni huko nje ndio tunaonekana ni empty. Baba unakaa uchi nje alafu ndani kwako unajufunika! Ujinga ule ule na uwezo ule ule wa kufikiri.

Tumevuliwa nguo! Wasomi wetu wametuacha uchi dunia inatucheka!
 
Si sahihi kumtetea Pro. Mruma kuwa amevunjiwa heshima, kilichotokea ni udhaifu wa elimu yake. Pro. Mrema alionekana anaelekezwa kufungua kurasa! Pro. Mrema alijitetea kwa kusema eti hajisikii vizuri kwani hakuamka vizuri! Huu ni utetezi wa kitoto.
MKATABA MBOVU WAITIA KITANZI TANZANIA

Ndugu Watanzania!
Video hii ni sehemu ya Kesi ya Madini kati ya Tanzania na Kampuni ya Winshear Gold Corp. Mkataba wa Madini uliosainiwa mwaka 2014 na Waziri wa Nishati na Madini enzi hizo ndio unaobishaniwa hapa. Katika safu ya utetezi, Tanzania ilimpeleka Prof. Abdulkarim Mruma kuwa sehemu ya utetezi. Pamoja na umahiri na usomi wake, Prof. Mruma, hajafua dafu kwani vifungu vya mkataba vinaiumbua Serikali ya Tanzania.

Wakili msomi upande wa Winshear Gold Corp anamhoji Prof. Mruma kuwa inawezekanaje huo mchakato uliopita mikono ya wengi kama Mwanasheria Mkuu wa Serikali, Wizara ya Nishati na Madini, Wizara ya Sheria, Kituo cha Uwekezaji cha Tanzania na wasomi wabobezi wa madini kama Prof. Mruma hawakuyabaini hayo mapungufu ndani ya mkataba? Swali hilo alishindwa kujibu Prof. Mruma, hivyo akaishia 'kulenga shabaha mwituni'!

Tunachotaka kusema ni kuwa, kama serikali ikisaini mkataba mbovu, huko mbele ya safari hata ikipeleka wasomi 100 wenye uwezo kama wa Prof. PL Lumumba, Mhe. Tundu Lissu, Peter Kibatara, Dkt. Masumbuko Lamwai (RIP), Prof. Jwani Mwaikusa (RIP), Dkt. Sengondo Mvungi (RIP), nk itapigwa tu.

Tunapohoji na kuupinga Mkataba wa Bandari muwe mnatuelewa. Waambieni Dkt. Tulia, Prof. Mbarawa, Maulidi Kitenge, Cd. Chongolo, na Mwanasheria Mkuu wa Serikali waipitie vizuri video hii. Lakini tutamuomba Gerson Msigwa amuonyeshe Mhe. Rais Samia clip hii. Lakini majibu ya Prof. Mruma yanaonyesha wahusika walipitia mchakato wote. Swali linalojitokeza kwetu sote ni kwa nini serikali iliusaini? Kama ni hivyo, ni kwa nini Serikali iliuvunja baadaye?
Je, nini kimekushangaza? Je, nini maoni yako?

Mwana Kondoo Ameshinda! Tumfuate!
Askofu Emmaus Bandekile Mwamakula
Dar es Salaam, 24 Julai 2023; 15:40 pm.
 
Kweli alikuwa mkweli ,hasa aliposema miaka ya 2013-14 walikubali hiyo mikataba ya hovyo wakijua kabisa ,sema walikubali ili kuvutia uwekezaji.
Si unaona hapo, inamaana baadae walilazimishwa waikatae kwa visingizo kuwa walikuwa wanavutia uwekezaji.


Hilo ni neno ambalo limemshangaza hata yule mmwanasheria aliyekuwa namuuliza.

Dah, ni masikitiko makubwa sana. Mapaka akamuulzia, hili ndilo ulilofundishwa na wanasheria wako uliseme?

Yeye pale angejibu kuwa, hizo sheria za zamani na tulibadili namna ya uwekezaji kwa sheria mpya. Ili aje mwanasheria kujibu.


Inaonesha hakupata muongozo mzuri wa kujibu, yeye anaulizwa na mwanasheria ilitakiwa mwanasheria aweo pembeni yake kumpa muongozo wa namna ya kujibu.


Kiufupi ni utumbo mtupu. Hata ukweli hakuweza kuuelezea ipasavyo, nakubaliana na wanaoisema ni lugha.


Hivi Profesa kama huyu tutegemee wanafunzoimwake wawe vipi?

Ndiyo maana wenye uwezo wao hawawasomeshi watotozao Tanzania, ni waste of time tu.
 
Wale hawakujiandaa kabisa! Kesi za nchi wanaenda kienyeji kama wameenda vacation! Ndio maana kesi zote tunashindwa huko nje, mawakili kama wale wanaweza kutolewa jasho hata juniors tu.

Tumedhalilishwa sana!
 
Wale hawakujiandaa kabisa! Kesi za nchi wanaenda kienyeji kama wameenda vacation! Ndio maana kesi zote tunashindwa huko nje, mawakili kama wale wanaweza kutolewa jasho hata juniors tu.

Tumedhalilishwa sana!
Nimemaliza kusikiliza video ya pili ya siku ya kwanza, sasa nimeingia video ya kwanza ya siku ya pili. "ledi", mwanasheria huyo anamaanisha "ready". Sasa haelewi kuwa ledi ina sound kama "lady" yaani mwanamke, mpaka Madame Pesident alifikiri anaitwa yeye akatazama, kumbe mtu anasema yupo tayari.


Ni upumbavu mtupu tulioupeleka pale.
 
Embu andika ukaeleweka basi, unaandika kama unakimbizwa. Huyu ni Mruma yupi? Kesi inahusu nini? Against nani? Inafanyikia wapi? Lini?

Yaani unaandika kama vile ni muendelezo wakati inatakiwa iwe ni content inayojitosheleza
 
Una mawazo ya hovyo sana.

Kumbuka kukosea kwake taifa inalipa gharama kubwa. Tena billions
Kakosea wapi ? Wakati kesi tumeshindwa Kwa kuvunja mikataba ya hovyo.

Kwamba yeye alipanga kushindwa basi asingeenda kabisa,mbona una akili za kitoto sana .!!
Hajadhalilika hapo amewadhalilisha wazungu 🤣🤣🤣🤣😜
Kila kitu unaangukia kweny upande wa siasa ndo tatizo Bado akili haijakomaa.
 
Yani jamaa mdoga anavomuendesha mzee kilaza mruma alafu anaulizwa ndio unavowafundisha hapo UDSM.
Inaleta picha gani kwamba maprofa vilaza na phd za mchongo walizonazo hapa tz.

Aisee ccm mnawakati mgumu sana sema mnatumia nguvu kubaki madarakani.
Hakuna kesi tulizoshinda.
 
Ile video isifutwe ili iamshe ari ya watu kutimiza wajibu wao kwenye mashauri yanayolihusu Taifa kwa maslahi ya Taifa ! Kuifuta hiyo video ni kuficha ugonjwa ambao utakuja kuumbuliwa na kifo !

Uchunguzi mkubwa ufanyike kama kweli hawa wasomi wetu ni kweli vilivyomo kichwani ni sawa na vilivyomo kwenye vyeti vyao ???!!!

Inasikitisha sana !! Tena sana Kwakweli !
 

Prof..Abdulkarim Hamis Mruma​

Professor of Geology, currently serving as a Commissioner for the Mining Commission in Tanzania.
Mining Commission in Tanzania.

MADRASA MWENZENU NDUGU YENU HUYO BRO.
Huyo tena kafanya nzuri sana, kaenda kama shahidi na katowa ushahidi wake, kumbuka huyo hakwenda pale kama mwanasheria wa kumtetea yeyote. Siyo kazi yake.

Nadiriki kusema katika niliowaona mpaka sasa hivi, wote waliofanya kilchowapeleka pale basi ni yeye tu. Kaama ni shahidi kajibu alichoulizwa.


Nipo video ya tatu sasa HIVI, NNAWATAZAMA WANASHERIA WEYTU WALIVO BOGUS. Utumbo mtpu.

Natamani niifkie mwisho nione hukumu.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…