Mahakama ya Kimataifa ya ICC yatoa hati ya kukamatwa kwa Rais Vladmir Putin wa Urusi

Mahakama ya Kimataifa ya ICC yatoa hati ya kukamatwa kwa Rais Vladmir Putin wa Urusi

Messenger RNA

JF-Expert Member
Joined
Jul 24, 2022
Posts
1,411
Reaction score
3,712
Majaji wa mahakama ya kimataifa (ICC),imetoa hati ya kukamatwa popote atakapopatikana rais wa urusi Vladimir Putin.

=====

Katika uamuzi wake, ICC imemtuhumu Rais wa Russia kuhusika na uhalifu wa kivita kutokana na kufanya uvamizi na kutwaa ardhi Nchini Ukraine ingawa Moscow imesema hatua hiyo haina maana yoyote.

2A586B68-4C4F-4ADB-BC2F-D2C3F2C3F561.jpeg


Pia, Hati ya Mahakama ya ICC imeeleza kuwa Rais Vladimir Putin aliagiza mashambulizi yaliyosababisha Watoto kuhamishwa kinyume cha Sheria pamoja na uhamisho usio halali wa Raia kutoka eneo la Ukraine na kuingia Nchini Urusi.

Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje ya Urusi Maria Zakharova amesema "Maamuzi ya ICC hayana maana kwasababu Urusi haiko kwenye Mkataba wa Roma wa Mahakama ya Kimataifa ya Jinai, hivyo haiwajibiki chini yake."
 
Mahakama ya Kimataifa ya Uhalifu wa kivita (ICC) imetoa hati ya kukamatwa kwa Rais wa Urusi Vladimir Putin.

520BBBCB-F282-416D-8916-7B30EBA63838.jpeg

Mahakama ya ICC inadai kuwa anahusika na uhalifu wa kivita, ikiwa ni pamoja na kuwahamisha watoto kutoka Ukraine kwenda Urusi kinyume cha sheria.

Inasema uhalifu huo ulifanyika nchini Ukraine kuanzia tarehe 24 Februari 2022 - wakati Urusi ilipoanzisha uvamizi wake kamili.

Moscow imekanusha madai ya uhalifu wa kivita wakati wa uvamizi huo.

BBC
 
Vita part two wanawapa mwanya magenerali wa kirusi kupindua Russia kwa kumkamata kuwa wasipate shida wakimpindua kuwa wampeleke wapi ni the Hague

Hadi hilo tamko kutolewa ina maana assessment ya vita inaonyesha mwelekeo mzuri wa Putin kuchokwa ndani ya Russia kwenye inner circle za chama tawala na jeshi
 
Majaji wa mahakama ya kimataifa (ICC),imetoa hati ya kukamatwa popote atakapopatikana rais wa urusi Vladimir Putin.

=====

Mahakama ya Kimataifa ya Uhalifu wa kivita (ICC) imetoa hati ya kukamatwa kwa Rais wa Urusi Vladimir Putin.

520BBBCB-F282-416D-8916-7B30EBA63838.jpeg


Mahakama ya ICC inadai kuwa anahusika na uhalifu wa kivita, ikiwa ni pamoja na kuwahamisha watoto kutoka Ukraine kwenda Urusi kinyume cha sheria.

Inasema uhalifu huo ulifanyika nchini Ukraine kuanzia tarehe 24 Februari 2022 - wakati Urusi ilipoanzisha uvamizi wake kamili.

Moscow imekanusha madai ya uhalifu wa kivita wakati wa uvamizi huo.

BBC
USA 🇺🇸 pumbavu sana.
 
Back
Top Bottom