Mahakama ya Rufani: Maamuzi ya Rais kuhusu Wafanyakazi wa Umma ni ya mwisho

Mahakama ya Rufani: Maamuzi ya Rais kuhusu Wafanyakazi wa Umma ni ya mwisho

MAHAKAMA YA RUFANI: CMA HAINA MAMLAKA WAFANYAKAZI WA UMMA

Mahakama ya Rufani ya Tanzania imesema Tume ya Usuluhishi ya wafanyakazi (Commission for Mediation and Arbitration-CMA) haina mamlaka ya kusikiliza na kutolea maamuzi kesi zinazohusu migogoro ya wafanyakazi wa umma.

Kupitia kesi ya rufaa ya madai CIVIL APPEAL NO. 12 OF 2022 TANZANIA POSTS CORPORATION VERSUS DOMINIC A. KALANGI mahakama hiyo ya juu zaidi ya Tanzania imesema migogoro ya wafanyakazi wa umma inatakiwa kuishia ndani ya Serikali, pale mfanyakazi anapofukuzwa kazi na mkuu wa idara au shirika la Serikali anatakiwa kukata Rufaa kwenda Tume ya Utumishi wa Umma, na endapo mfanyakazi atakuwa hajaridhika na maamuzi ya Tume ya Utumishi wa Umma basi anatakiwa akate rufaa kwenda Kwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na maamuzi ya Rais yatakuwa ya mwisho, hii ni Kwa mujibu wa Kifungu Cha 25 Cha sheria ya utumishi wa umma Public Service Act (Cap 298 R.E. 2019)

Dominic A. Kalangi alikuwa mfanyakazi wa Shirika la Posta (Tanzania Posts Corporation), mwaka 2017 ajira yake ilisitishwa Kwa utovu wa nidhamu.

Dominic alipeleka malalamiko yake CMA ambapo alishindwa kesi akakata Rufaa Mahakama kuu Mtwara ambapo mahakama kuu ikaamuru Shirika la Posta limlipe fidia ya mishahara ya miezi sita Dominic A kalangi. Shirika la Posta likakata Rufaa Mahakama ya Rufani ya Tanzania

Kwa Mujibu wa sheria Shirika la Posta la Tanzania ni Mali ya umma linalomilikiwa na serikali hivyo wafanyakazi wake ni watumishi wa umma.

"Going by the wording of the above-quoted provision, it is unambiguously clear that all disciplinary matters or disputes involving public servants are exclusively within the domain of the Public Service Commission whose decision is appelable to the President. As correctly submitted by Ms. Kinyasi and as amply demonstrated above, the CMA has no jurisdiction to adjudicate upon such matters."

View attachment 2175700View attachment 2175702
Nini hii? Rais ndiyo muajiri mkuu na mfukuzaji mkuu, halafu uamuzi wake uwe wa mwisho?
Naona kama mahakama imejishusha hadhi!
Hebu wataalamu tusaidiane!
 
Mahakama ya Rufaa imejiongoza vibaya kutafsiri hivyo vifungu. Nina imani muda sio mrefu watafanya marejeo au watatoa hukumu nyingine itayorekebisha maamuzi waliyotoa katika Rufaa hii.

Discplinary Matters ni sahihi kupitia mchakato wa ndani kabla ya kwenda CMA au Mahakama Kuu kwa Judicial Review lakini sio sahihi kwa migogoro (disputes) isiyo ya kinidhamu, hii inatakiwa kwenda moja kwa moja CMA maana hakuna sheria inayoelekeza kuwa ishughulikiwe ndani ya taasisi husika au kwamba iende huko Tume ya utumishi wa umma nk. Tume ya utumishi wa umma uwezo wake ni kupokea Rufaa na sio kupokea migogoro iliyo fresh
Huu uamuzi binafsi nimeomba TLS iombe mapitio/marejeo kwa CA.
.
Wakuu wamejielekeza vibaya, they’ve open Pandora Box!.
.
That means all pending cases, judgment , execution is nullity
 
MAHAKAMA YA RUFANI: CMA HAINA MAMLAKA WAFANYAKAZI WA UMMA

Mahakama ya Rufani ya Tanzania imesema Tume ya Usuluhishi ya wafanyakazi (Commission for Mediation and Arbitration-CMA) haina mamlaka ya kusikiliza na kutolea maamuzi kesi zinazohusu migogoro ya wafanyakazi wa umma.

Kupitia kesi ya rufaa ya madai CIVIL APPEAL NO. 12 OF 2022 TANZANIA POSTS CORPORATION VERSUS DOMINIC A. KALANGI mahakama hiyo ya juu zaidi ya Tanzania imesema migogoro ya wafanyakazi wa umma inatakiwa kuishia ndani ya Serikali, pale mfanyakazi anapofukuzwa kazi na mkuu wa idara au shirika la Serikali anatakiwa kukata Rufaa kwenda Tume ya Utumishi wa Umma, na endapo mfanyakazi atakuwa hajaridhika na maamuzi ya Tume ya Utumishi wa Umma basi anatakiwa akate rufaa kwenda Kwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na maamuzi ya Rais yatakuwa ya mwisho, hii ni Kwa mujibu wa Kifungu Cha 25 Cha sheria ya utumishi wa umma Public Service Act (Cap 298 R.E. 2019)

Dominic A. Kalangi alikuwa mfanyakazi wa Shirika la Posta (Tanzania Posts Corporation), mwaka 2017 ajira yake ilisitishwa Kwa utovu wa nidhamu.

Dominic alipeleka malalamiko yake CMA ambapo alishindwa kesi akakata Rufaa Mahakama kuu Mtwara ambapo mahakama kuu ikaamuru Shirika la Posta limlipe fidia ya mishahara ya miezi sita Dominic A kalangi. Shirika la Posta likakata Rufaa Mahakama ya Rufani ya Tanzania

Kwa Mujibu wa sheria Shirika la Posta la Tanzania ni Mali ya umma linalomilikiwa na serikali hivyo wafanyakazi wake ni watumishi wa umma.

"Going by the wording of the above-quoted provision, it is unambiguously clear that all disciplinary matters or disputes involving public servants are exclusively within the domain of the Public Service Commission whose decision is appelable to the President. As correctly submitted by Ms. Kinyasi and as amply demonstrated above, the CMA has no jurisdiction to adjudicate upon such matters."

View attachment 2175700View attachment 2175702
Hukumu iko sahihi kabisa, tatizo ni kwenye mfumo wetu wa utumishi ambapo civil service commission iko under control ya wizara, na hivyo moja kwa moja kuwa chini ya rais.
 
Huu uamuzi binafsi nimeomba TLS iombe mapitio/marejeo kwa CA.
.
Wakuu wamejielekeza vibaya, they’ve open Pandora Box!.
.
That means all pending cases, judgment , execution is nullity
Sure, zinakufa kibudu automatically
 
Hukumu iko sahihi kabisa, tatizo ni kwenye mfumo wetu wa utumishi ambapo civil service commission iko under control ya wizara, na hivyo moja kwa moja kuwa chini ya rais.
Hukumu haipo sahihi, sheria inayotoa haki za wafanyakazi ni sheria ya ajira na mahusiano kazini na sheria hiyo ndiyo iliyotoa tafsiri ya neno "dispute" (mgogoro). Kifungu cha 2 (1) cha Sheria ya Ajira na Mahusiano Kazini kimeeleza kuwa sheria hiyo inatumika kwa wafanyakazi wa sekta zote mpaka wa serikali (watumishi wa umma), na kifungu cha 14(1) cha sheria ya mahakama za kazi inaeleza kuwa migogoro ya kazi itapelekwa CMA. Sasa hukumu hii maana yake imetengua kifungu cha 2(1) cha Sheria ya Ajira na mahusiano kazini kuwa itatumika kwa wafanyakazi wasio wa serikali tu.

Kumbuka sheria ya utumishi wa umma haitoi wala kueleza haki za wafanyakazi bali inaeleza kazi za taasisi za serikali kwenye utendaji wa utumishi wa umma. Kwenye sheria ya utumishi wa umma, mkosaji ni mwajiriwa tu na sio mwajiri
 
Sure, zinakufa kibudu automatically
Haki Haihitaji Indoor Meetings.

Haki Inatakiwa Ionekane. Itachelewa Lakini Itaonekana.
.
Wamethibitisha Ufinyu wa Weledi Katika Kutekeleza Majukumu Yao.
.
HAKI YAKO NI MUHIMU KULIKO MAELEKEZO YAO.

[emoji375][emoji375]
 
Mahakama ya Rufaa imejiongoza vibaya kutafsiri hivyo vifungu. Nina imani muda sio mrefu watafanya marejeo au watatoa hukumu nyingine itayorekebisha maamuzi waliyotoa katika Rufaa hii.

Discplinary Matters ni sahihi kupitia mchakato wa ndani kabla ya kwenda CMA au Mahakama Kuu kwa Judicial Review lakini sio sahihi kwa migogoro (disputes) isiyo ya kinidhamu, hii inatakiwa kwenda moja kwa moja CMA maana hakuna sheria inayoelekeza kuwa ishughulikiwe ndani ya taasisi husika au kwamba iende huko Tume ya utumishi wa umma nk. Tume ya utumishi wa umma uwezo wake ni kupokea Rufaa na sio kupokea migogoro iliyo fresh
HV MTU AKIENDA CMA AKASHINDWA ANAWEZA KWENDA KWA RAISI?
 
Mahakama ya Rufaa imejiongoza vibaya kutafsiri hivyo vifungu. Nina imani muda sio mrefu watafanya marejeo au watatoa hukumu nyingine itayorekebisha maamuzi waliyotoa katika Rufaa hii.

Discplinary Matters ni sahihi kupitia mchakato wa ndani kabla ya kwenda CMA au Mahakama Kuu kwa Judicial Review lakini sio sahihi kwa migogoro (disputes) isiyo ya kinidhamu, hii inatakiwa kwenda moja kwa moja CMA maana hakuna sheria inayoelekeza kuwa ishughulikiwe ndani ya taasisi husika au kwamba iende huko Tume ya utumishi wa umma nk. Tume ya utumishi wa umma uwezo wake ni kupokea Rufaa na sio kupokea migogoro iliyo fresh
Inaelekea sheria unazijua au una elimu ya sheria. Asante kwa contribution nzuri. BTW kusema kuwa mambo yaishie kwa rais hakutafanya wafanyakazi kukosa haki hasa rais anapokuwa mtu zimezibuka kama Mwendazake? Naona ni kama kusema tajiri ndiye atakayekuwa na maamuzi ya mwisho kuhusu wafanyakazi wake na mahakama haiwezi kuingilia.
 
... sitaki kuamini Mahakama ya Rufani (Supreme Court of the land) imekuwa low kwa kiwango hiki.
 
anatakiwa akate rufaa kwenda Kwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na maamuzi ya Rais yatakuwa ya mwisho, hii ni Kwa mujibu wa Kifungu Cha 25 Cha sheria ya utumishi wa umma Public Service Act (Cap 298 R.E. 2019)
Hii sheria kama iko hivi ni hatari sana.... Rais ndie mkuu wa utumishi, halafu mfanyakazi ana kesi na utumishi; inakuwaje tena Rais awe mwamuzi wa mwisho? Au kuna kitu kimeachwa hapa? Hakuna nafasi ya mahakama hapa? Pascal Mayalla hebu tupe mwanga kidogo
 
Kwa sababu vyombo vinaripoti kwake. Tusimwangalie kama individual. Tumwangalie kama system au taasisi.
Ana rasilimali za kumtosha kufanya uamuzi sahihi.
Hebu tukumbushe ya Tozo ya shs 100 kwenye mafuta ilikuwaje?
 
Hii sheria kama iko hivi ni hatari sana.... Rais ndie mkuu wa utumishi, halafu mfanyakazi ana kesi na utumishi; inakuwaje tena Rais awe mwamuzi wa mwisho? Au kuna kitu kimeachwa hapa? Hakuna nafasi ya mahakama hapa? Pascal Mayalla hebu tupe mwanga kidogo
Watu wengi wanatafsiri vibaya, Sheria ya Utumishi wa Umma inataka watumishi wa Umma waexhaust all remedies kabla ya kwenda CMA au Mahakamani. Hivyo Mtumishi wa Umma (ambapo hata Mashirika ya Umma yanaangukia ndani ya Utumishi wa Umma) wanatakiwa wakiwa aggrieved na maamuzi ya mamlaka zao za ajira au nidhamu (hapa ni mambo yote disputes na nidhamu) wanatakiwa wakate rufaa Tume ya Utumishi wa Umma na wasiporidhika na uamuzi basi wakate rufaa kwa Rais, Rais akishatoa uamuzi wake ambapo ni highest kwenye Executive hapo sasa wanaweza kwenda Mahakamani.

Kilichokuwa kinafanyika ni watumishi wa umma kwenda CMA kabla hawajaexhaust all remedies kama Sheria ya Utumishi wa Umma Kifungu 32A kilivyotamka.
 
Watu wengi wanatafsiri vibaya, Sheria ya Utumishi wa Umma inataka watumishi wa Umma waexhaust all remedies kabla ya kwenda CMA au Mahakamani. Hivyo Mtumishi wa Umma (ambapo hata Mashirika ya Umma yanaangukia ndani ya Utumishi wa Umma) wanatakiwa wakiwa aggrieved na maamuzi ya mamlaka zao za ajira au nidhamu (hapa ni mambo yote disputes na nidhamu) wanatakiwa wakate rufaa Tume ya Utumishi wa Umma na wasiporidhika na uamuzi basi wakate rufaa kwa Rais, Rais akishatoa uamuzi wake ambapo ni highest kwenye Executive hapo sasa wanaweza kwenda Mahakamani.

Kilichokuwa kinafanyika ni watumishi wa umma kwenda CMA kabla hawajaexhaust all remedies kama Sheria ya Utumishi wa Umma Kifungu 32A kilivyotamka.
Wewe ni mmoja wa wanaotafsiri vibaya sheria ya utumishi wa umma hususani kifungu cha 32A. Hebu itafyte sheria hiyo na usome kifungu hicho halafu uone kama kinaeleza kuhusu watumishi wa umma wote (all public servants) au ni kifungu kwa kundi fulani tu la watumishi wa umma (operational service). Yaani usome na uone kama kifungu hicho kinatumika mpaka watumishi maofisa!!!

Halafu hilo neno dispute kama ulivyoliweka, umelitoa wapi mkuu, maana sheria ya utumishi wa umma haina tafsiri ya neno dispute bali sheria ya ajira na mahusiano kazini ndiyo yenye tafsiri ya neno dispute. Unavyosema dispute zinatakiwa kuamriwa ndani na wasiporidhika wakate rufaa utumishi wa umma, ni kifungu kipi cha sheria gani kinachoeleza hayo?
 
Hii sheria kama iko hivi ni hatari sana.... Rais ndie mkuu wa utumishi, halafu mfanyakazi ana kesi na utumishi; inakuwaje tena Rais awe mwamuzi wa mwisho? Au kuna kitu kimeachwa hapa? Hakuna nafasi ya mahakama hapa? Pascal Mayalla hebu tupe mwanga kidogo
Hicho kifungu cha 32A cha Sheria ya Utumishi wa umma, alikiweka mwendazake ili aweze kuwadhibiti wale walioitwa watumishi wa umma wenye vyeti feki. Hakutaka waende CMA, akaona njia ya kuwabana ni kwa kuongeza hicho kifungu cha 32A, hapo akawa amesahau kuwa kifungu hicho hakiwahusu maofisa (watumishi wa umma wenye shahada - degree), matokeo ni kuwa mawakili wa serikali wakaiongoza vibaya mahakama kuwa kifungu cha 32A kinawazuia watumishi wote wa umma kwenda CMA, na hapo Mahakama haikusoma kwa kina sheria ikajipiga piga mitama na kuwa na maamuzi tofauti tofauti (mahakama kuu) na sasa mahakama ya Rufaa ndio imetoa uamuzi wa mwisho ambao imejipotosha kabisa kuwa kutafsiri vibaya kifungu hichohicho.
 
Back
Top Bottom