Mahakama yabatilisha makubaliano ya mgawanyo mirathi ya Mengi

Mahakama yabatilisha makubaliano ya mgawanyo mirathi ya Mengi

Kama Mzee wenu ameenda umri akiingiza nyumba ndogo tu mjiandae kisaikolojia maana mtifuano utakuwa kwenye mirathi.

Labda Mzee machale imcheze agawe kabla hajafa, nayo sio rahisi haswa ukikuta tayari ana Watoto wengi na wakubwa.
Kwa mfano watoto wa Mengi wangekuwa matajiri kama Mo dewji au Bakhressa wangeanza kusumbuana na Mjane kweli?
 
Ukijitoa katika nguvu za mihemko na ushabiki....unagundua kuwa huyo Binti ni tapeli kama walivyo matapeli wengine..... tofauti yake yeye na matapeli wengine ni kwamba yeye anataka kutumia maungo yake ya Siri kutapeli na kudhurumu........

Muendelezo wa haya matukio na harakati zake juu ya hiki anacho kipambania vinamuanika wazi kuwa ukaribu wake na marehemu haukuwa wa kimapenzi bali ni alikuwa kimkakati na hii vita ndio anataka kumalizia huo mkakati.........

Kwa Hali ilipofikia Sasa na sura ya hili jambo lilivyo ni kwamba kila upande umeshabadilika roho na ushetani umeshawavaa hao washindani......kila mmoja yupo tayari kwa lolote ili apate chochote au chote.........

Kwa hakika kila jicho la muungwana linamtazama kwa aibu huyu Binti kwa hiichi anachokipigania...... wakati mwingine haki utengenezwa kwa kufuata taratibu za kisheria lakini stahiki zinabakia moyoni.......Jacky ndani ya moyo wake anajua anachokifanya tangu anaanza mahusiano na marehemu.......

Yote kwa yote mwisho wa hili litaweka kumbu kumbu mbaya kwenye kichwa Cha huyu Binti mpaka anaingia kaburini iwe kashinda au kashindwa.........

Huu ni ukumbusho kwa tuliokuwa hai tusiruhusu ashki na tamaa kututawala na kufuta heshima tulizotumia miaka mingi kuijenga........

NB:
Ukiingia kwenye fikra na akili za watoto wa Mengi utaona ni jinsi gani inavyouma kuona kile mlichokuwa mnakipigania na kukijenga kwa miaka kinataka kuchukuliwa na kahaba mmoja kwa sababu ya kipande Cha karatasi na kulala na baba yenu kitanda kimoja na kumvulia nguo......ni kama mfano wa mtu aliyeshinda kamali......

Usiombe yakukute.....
 
Jack ana watu wazito nyuma yake. Yaani hata kama mtu haujasoma sheria unaona kabisa hapa kuna uwalakini.
Shida inakua ukishakua mtu mzima kuna vitu unakua unashindwa kufanya sababu ya uzee yakiwemo magonjwa nayo hayakuachi.

Utahitaji labda kuogeshwa au sijui kufidiwa etc ambavyo watoto wako hawawezi kufanya. Kidemu ulicho nacho kinakukazia kua kama hutaki kukakoa katasepa. Na we ndo hivyo ingawa kifedha uko vizuri lakini ki afya tia maji tia maji.
 
Ninapenda jinsi Jack anavyowatoa ulimi nje hao jamaa.

Asikubali wakamalizane nje ya mahakama na awe makini na nyendo zake tu.

Asingekuwa maarufu pengine kitambo angeshazimwa kama taa.
 
Kumekucha
IMG-20220827-WA0003.jpg
 
Ninapenda jinsi Jack anavyowatoa ulimi nje hao jamaa.

Asikubali wakamalizane nje ya mahakama na awe makini na nyendo zake tu.

Asingekuwa maarufu pengine kitambo angeshazimwa kama taa.
Hivi kwa nini Wachaga wanapenda kugombania Mali ambazo hata haziwahusu!? Maana kipindi Marehemu Yuko hai huwaoni,ila Marehemu akisha kufa tu hadi wababa wadogo wasiyojulikana watajitokeza na hata kufikia hatua ya kufungua mirathi ya Marehemu Baba yenu bila hata nyinyi Watoto wa Marehemu kujuwa kinachoendelea nyuma yenu! Dunia haada Ulimwengu Shujaa nakuambia!!
 
Shida inakua ukishakua mtu mzima kuna vitu unakua unashindwa kufanya sababu ya uzee yakiwemo magonjwa nayo hayakuachi.

Utahitaji labda kuogeshwa au sijui kufidiwa etc ambavyo watoto wako hawawezi kufanya. Kidemu ulicho nacho kinakukazia kua kama hutaki kukakoa katasepa. Na we ndo hivyo ingawa kifedha uko vizuri lakini ki afya tia maji tia maji.
Kuogeshwa si unaajiri nurse tu. Ulaya matajiri wanaajiri nurse tu. Kuliko kuoa gold digger.
 
Hivi kwa nini Wachaga wanapenda kugombania Mali ambazo hata haziwahusu!? Maana kipindi Marehemu Yuko hai huwaoni,ila Marehemu akisha kufa tu hadi wababa wadogo wasiyojulikana watajitokeza na hata kufikia hatua ya kufungua mirathi ya Marehemu Baba yenu bila hata nyinyi Watoto wa Marehemu kujuwa kinachoendelea nyuma yenu! Dunia haada Ulimwengu Shujaa nakuambia!!
Haziwahusu kivipi na wameshiriki pamoja kuzichuma? Hao watoto si ndo walikua wakijazia wino kalamu za biki wakiwa wadogo wenzao wanacheza? Unasemaje haziwahusu? Ben hahusiki na amechangia katika utendaji?
 
Huyo huyo nurse,
Anakutega tega mwisho wa siku unajaa tu, unaingia King unaoa.
Nop nurse anakuwa professionnel .Chuoni wanasoma wanajua kutongonzwa kupo. Hivyo wanajua jinsi ya kureact kiprofession bila kumbugudhi mteja (patient)Client.
 
Hili la kukaa nje ya mahakama na kukubaliana ndilo la msingi.
Huko nyuma nilikuwa nawaambia Watu hili jambo si rahisi wanavyofikiria. Wengi walikuwa wanachangia kwa mihemko, kwamba Jack hakuchuma mali kwa hiyo akae kando Watoto wake watatunzwa na Watoto wakubwa wa Mengi.

1. Wanachosahau ni kuwa Jack ni mke halali wa Mengi (ndiyo maana katika mashauri yote hakuna mahali limepingwa)

2. Jack amezaa na Mengi watoto wawili. Watoto ambao ni haki yao kurithi mali za Baba yao ambaye ni Mzee Mengi

3. Na kwa kuwa Watoto wa Jack ni Watoto halali wa Mzee Mengi na hawajafikisha umri wa miaka 18 mnaweza kujua nani anastahili kusimamia haki zao.

Wosia uliodaiwa kuandikwa na Mengi ulitupiliwa mbali na mahakama. Kwa hiyo hapa mambo yanaanza upya ndiyo maana wakili wa Jack kaanza na kuhakikisha mali zote ambazo zilikuwa hazijagawanywa zinarudishwa pamoja halafu kesi ya mgao ianze upya. Hapa hata kama humpendi lakini huyo dada katumia mawakili wazuri.

Naona hapo la msingi wakae pamoja kwa kushirikiana na Wazee wenye busara na mgao ufanyike tu. Hata kama Jaclk hatapata kama ilivyosemwa kwenye ule wosia uliokataliwa, lakini obvious ataondoka na mgao mkubwa si haba.

Halafu sisi maskini humu JF acheni habari ya kuzungumzia kuhusu kuuliwa Jack.
Mzee Mengi hakuwa na historia ya aina hiyo. Wakati anamtongoza na kumuoa Jack, alifanya hayo yote akiwa na akili timamu na Mtu mzima. Tusitie kinyongo kwa mali zisizotuhusu.
Umeandika kwa busara sana. Una undugu na Hayati Nyerere?
 
Aisee tusije tukawadharau ma-slayqueens. Sio wote ni vilaza. Si mnaona Jack anavyowanyoosha wapalestina? Pia nadhani Jack alijifunza vitu vingi sana kutoka kwa akili kubwa Mengi. Ikumbukwe Mengi nae alikuwa balaa. Kuna kipindi alikuwa na taarifa za kiitelijensia kuhusu mwanae kubambikiwa madawa ya kulevya na kufanikiwa kulizima hilo tukio. Kwahiyo hata hizo mbinu za kimafia alumfundisha Jack. Mimi nashauri wapalestina wake kikao kule migombani na kulimaliza hili suala ili kulinda hadhi ya mapalestina.
 
Kuogeshwa si unaajiri nurse tu. Ulaya matajiri wanaajiri nurse tu. Kuliko kuoa gold digger.
Hapana ilikuwa trap unajua mzee na jack wanekutana wapi? Mzee aliwekewa mitego kibao huyo jack alishawai kukutana na mzee nje mara kibao huko south Africa mara marekani, ila finally walipokutana Dubai mzee aliingia king akamtongoza jack akakimbili ndoa ndo hapo
 
Hapana ilikuwa trap unajua mzee na jack wanekutana wapi? Mzee aliwekewa mitego kibao huyo jack alishawai kukutana na mzee nje mara kibao huko south Africa mara marekani, ila finally walipokutana Dubai mzee aliingia king akamtongoza jack akakimbili ndoa ndo hapo
Alikuwa na ndoto zake. Ndo maana hata alimforce Mengi aombe talaka kwa mkewe.
 
Back
Top Bottom